Rais Magufuli azindua Kanisa la Parokia ya Bikira Maria Emmakulata Chamwino, Dodoma. Achangisha fedha kanisani kuchangia ujenzi wa Msikiti

Misri katika ule mtaa mkuu kutoka uwanja wa ndege kuna msikiti upo karibu kabisa na kanisa na hali imekuwa hivyo miaka na miaka.

Mada yako imekosa mizania inayotokana na tafiti za kiulimwengu.

Msikiti kuwa karibu na kanisa siyo tatizo hata kidogo, ipo misikiti mingi tu duniani imejengwa na inapakana na makanisa

Tatizo ni Rais wa nchi, tena wa imani nyingine, kwenda katika nyumba yake ya ibada na kisha kutaka sadaka za waumini wenzie kanisani zikajenge msikiti.

Kama waislamu wenyewe wangemuomba aendeshe harambee ya kuchangia ujenzi wa msikiti wangeweza kumualika msikitini au kwenye uwanja wa wazi akapewa muongozo na waislamu wa namna ya kuendesha zoezi hilo!

La sivyo alivyofanya Magufuli ni kujivisha jambo ambalo si la dini yake kwa malengo yake binafsi (naamini ni ya kisiasa)
 
Kingine sina Hakika kama Mungu wa waislamu ndo Mungu wa Wakristo.

Hapa mtu unaweza ukajikuta unachuma dhambi bila kujua.

Sisi wakristo tunajua Mungu wetu ni Mungu mwenye wivu. Siwezi kuchangia ujenzi wa msikiti au ujenzi wa shaulin temple ili Mungu mwingine aka abudiwe. Kwa imani yangu iyo ni dhambi.
Ndio. allah sio Yehova. allah ni mmoja wa miungu tulioambiwa. " msiabudu miungu mingine ila Mimi."
 
Msikiti kuwa karibu na kanisa siyo tatizo hata kidogo, ipo misikiti mingi tu duniani imejengwa na inapakana na makanisa

Tatizo ni Rais wa nchi, tena wa imani nyingine, kwenda katika nyumba yake ya ibada na kisha kutaka sadaka za waumini wenzie kanisani zikajenge msikiti.

Kama waislamu wenyewe wangemuomba aendeshe harambee ya kuchangia ujenzi wa msikiti wangeweza kumualika msikitini au kwenye uwanja wa wazi akapewa muongozo na waislamu wenyewe amchangishe nani.

La sivyo alivyofanya Magufuli ni kujivisha jambo ambalo si la dini yake kwa malengo yake binafsi (naamini ni ya kisiasa)
Una ushahidi gani kama Rais hajaamua kufanya tukio lile kwa maombi ya hao hao waislam?.

Kwa taarifa yako wasaidizi muhimu wa Rais ni waislam, kazungukwa na waislam hivyo wanamwambia umuhimu wa Chamwino kuwa na msikiti.

Kumbuka kuwa Marehemu Mkapa na Nyerere hawakuwahi kuhudhuria zile shughuli za kuhifadhi Quran lakini JPM amehudhuria.
 
Hahaha mleta mada anasagau tu su anajisahaulisha, misikiti mingi sana imejengwa kwa kuchangiwa na waumiju wa madhehebu ya kikristo.

Faiza Foxy alisema eti ikulu ya magogoni ilijengwa na waislam, nikacheka sans.
Waislamu hawahawa wanaojengewa misikiti?!
 
Mnampaisha Tundu Lisu kwa lipi? Jamaa ni failure hata kabla ya uchaguzi kuanza rasmi.

Lissu ni Mwanaharakati makini, Ni Mwanasheria Nguli, ni Wakili Msomi, alikuwa ni Mbunge Machachari, Ni kiumbe jasiri! Hastahili kupaishwa na mtu yoyote yule! Anajipaisha mwenyewe.
 
Misri katika ule mtaa mkuu kutoka uwanja wa ndege kuna msikiti upo karibu kabisa na kanisa na hali imekuwa hivyo miaka na miaka.

Mada yako imekosa mizania inayotokana na tafiti za kiulimwengu.
Mkuu katika hili umesoma vizuri? Au mimi kuna sentensi sikuziona? Sijaona akizungumzia suala la kanisa kuwa karibu na msikiti. Hii ipo hata Daslama pale Magomeni ambapo upande wa pili kuna kanisa. Nilichokiona anzungumzia Magufuli, rais wa jamhuri, kuwaombea waislamu mchango wa kujenga msikiti. Maombi yenyewe yaliyofanywa kwa wakristo ndani au katika maeneo ya nyumba yao ya ibada na zaidi wakati huu tunaelekea kwenye uchaguzi mkuu.
 
Hahaha mleta mada anasagau tu su anajisahaulisha, misikiti mingi sana imejengwa kwa kuchangiwa na waumiju wa madhehebu ya kikristo.

Faiza Foxy alisema eti ikulu ya magogoni ilijengwa na waislam, nikacheka sans.
Waislamu hawahawa wanaojengewa misikiti?!

Msikiti upi hapa nchini ulijengwa kwa michango ya wakiristo ukiachilia mbali huu ambao Magufuli anataka kiki za kisiasa?
 
Ni kweli hata wakristo wanawaita waislamu ni wapagani kwamba hawana dini.
Kila dini inajiona wao ndo wako sawa,,iwe walokole,budha,hindu etc,,wala haipaswi kuwa mjadala,kwasisi tunaoabudu imani za jadi,huwa tunawachora tu na kubaki kuwasikitikia jinsi mnavyopoteza mda.
 
Msaidizi wake ni Alhaj na kiubinadamu anajisikia vibaya kuwa na waislam kadhaa kanisani halafu wasiwe na msikiti katika eneo lao la kazi.

Samia Suluhu, Kassim Majaliwa na wengine wasaidizi wa karibu ni waislam hivyo mkumbuke umuhimu wao kwake kimaisha.

Msiongozwe na chuki mpaka mkapoteza uwezo wa kuyatafakari masuala ya kawaida kabisa ya kiubinadamu.

Hapo Chamwino ni sehemu ya Dodoma na ni makao makuu kutakuwa na ongezeko la waislam miaka ijayo.
Kama mnakosoa harambee iliyofanyika baada ya mkuu wa nchi kuona kuna hitaji hilo, mbona pia alishafanya harambee kwa kumuomba mfalme wa Morocco kujenga msikiti mkubwa Afrika Mashariki na msikiti unaendelea kujenga na kama sikosei mwaka huu unafunguliwa?? Acheni roho za kichadema muwe wakweli msiwe wanafiki. Waislamu hawana tatizo na hilo isipokuwa wale wenye chuki binafsi na jemedali JPM. Yaani ni hivi hamtashinda kwa uovu huu
 
Kwani hicho chuo kabla ya kupewa waislamu kilikuwa ni taasisi ya dini gani?
Tanesco Morogoro, achana na hii dhana ya kibaguzi JPM hajaanza jana wala juzi kuwa karibu na waislam.

Bashiru Ali Kakurwa
Kassim Majaliwa
Samia Suluhu Hassan

Hao ni wasaidizi wake tena wa karibu sana, ni lazima nafsi imsukume ili na wao wakiwa Chamwino wawezwe kuswali.

Miaka ile ya Mwalimu Nyerere pengine halikuwepo wazo la kujenga msikiti lakini kumbuka ni miaka ya 1970 na 80 leo ni karne tofauti kabisa.
 
Kweny Uislam Sadaka haimtazami mtoaji bali dhamira na uhalali wa umiliki kile ulichotoa

Hata uwe Sheikh au Mufti kama Sadaka yako ina malengo labda ya kisiasa au kuleta zahma kwny Jamii au mali hiyo ya sadaka imetokana na dhulma basi sadaka hiyo ni Void

Wakati wa Bwana Mtume kuna Msikiti uliamriwa uvunjwe baada ya kujengwa kwa kuwa tu dhamira haikuwa njema ya Wajenzi

So kwny Uislam hata unapotoa Sadaka kwa Asie Muislam kwa dhamira safi ya kumsaidia kuondokana na shida zake unapata thawabu
Kwahiyo asiye muislamu kuchangia msikiti ni dhambi bwashee?
 
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, au wanafanya kwa kufuata taratibu za dini yao, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu Rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
Mi naona rais hajakosea kitu maana anapofanya harambee za ghafla iwe kumsaidia kwa mfano yule mama kilema pale ubungo flyover kila msaidizi wake anachangia. Akichangisha kanisani wote wasaidizi wake bila kujali dini wanatoa. Kama rais amejihusisha kujengwa kanisa eneo la ikulu hivyohivyo amejihusisha kuchangisha kwa msikiti wa eneo la ikulu. Utamaduni wa watanzania kuchangiana kwa ujenzi nyumba za ibada umeanza siku nyingi na hii ni moja ya sifa za watanzania.
 
Ndugu rais, wewe ni Rais siyo sheikh, wewe ni Mkiristu siyo Muislamu, mambo ya Waislamu waachie Waislamu wenyewe!

Una haki ya kuchangisha fedha kwa ajili ya matendo ya imani yako lakini huna haki ya kusimama ndani ya nyumba ya imani yako kudictate kipi kifanywe kwa niaba ya watu wa imani nyingine.

Waislamu wana taratibu zao za kujenga nyumba za Ibada zao, wanachangia wao wenyewe au wanatafuta mfadhili wa imani yao wao wenyewe, kisha wanajenga msikiti wao!

Umewahi kusikia wapi Waislamu nchini wameendesha harambee makanisani kwa ajili ya kupata pesa kwa ajili ya kujenga misikiti yao? Au unafikiri Waislamu hawana marafiki Wakiristo wakiwemo maaskofu na mapadre ambao wangeweza kuwaomba wawafanyie harambee wajenge hizo nyumba?

Au lini umewahi kusikia maaskofu na mapadre wameomba michango kupitia misikitini ili Waislamu wachangie ujenzi wa makanisa?

Kuna mambo ni boundary ya kuheshimiana kiimani, nayo ni kutokuingiliana katika namna kila imani inavyoendesha mambo yake!

Najua pengine kibinadamu uliona aibu kutokana na mihela mirefu unayoimwaga makanisani siku hizi kwa jina la sadaka, ukahisi labda umma wa Waislamu utakuona kama mtu anayetumia mafungu yale ya urais yasiyokaguliwa na yeyote kwa ajili ya sadaka hizo, mimi nasema usihofu, maadamu wewe ni Mkatoliki na Mkiristu basi usiuonee haya Ukiristo wako wewe toa tu, Waislamu wanajiweza, wanaweza kujenga misikiti yao wao wenyewe na infact misikiti nchi hii ni mingi kwelikweli na imejengwa na Waislamu wao wenyewe!

Kuhusu misikiti iliyojengwa na Wafalme na marais, hiyo Waislamu tunajua huwa wanatafuta hao wafadhili wao wenyewe, ila sasa kwa kuwa Kiprotokali jambo linalofanywa na mfalme au rais wa Taifa moja katika jingine lazima mfalme au rais wa taifa husika awe na taarifa ndiyo maana taasisi za dini zinaweza kukujulisha ili usaidie kunyoosha mambo! Hii ni tofauti na kwenda kanisani ukaanzisha harambee ya kujenga misikiti! Ndugu Rais ulitumwa au kuombwa na Muislamu gani kutaka kujenga msikiti kupitia fedha za kanisani?

Wakati mwingine naangalia haya mambo na kuona kuwa yamekaa kisiasa. Hata hivyo mambo ya dini ni sensitive sana si vizuri kuchanganya dini na siasa! Mwalimu alionya sana kuhusu mambo haya!

Ipo namna mtu asiye muislamu anavyoweza kuguswa na kuamua kujenga msikiti, kwa mfano, Mwalimu aliguswa moyoni mwake baada ya kustaafu uraisi akaamua kutafuta fedha za kujenga Msikiti Butiama, Mwalimu alikuwa na connection za Vatican, Makanisa makubwa makubwa lakini hakwenda kutafuta fedha makanisani ili ajenge msikiti, Mwalimu alikwenda kwa Ghadafi ndiye aliyempa pesa za kujenga Msikiti huko Butiama!

Nimkumbushe tu Ndugu Magufuli kuwa, dini ya Kiislamu pia imeweka misingi ya aina gani ya misikiti inafaa kuswaliwa ndani yake, Quran inasema ile misikiti iliyojengwa kwa dhamira safi ndiyo misikiti ya Mungu na ndiyo inayofaa kuswaliwa bali ile iliyojengwa kwa dhamira isiyo njema, yenye malengomalengo fulani hivi hiyo haina baraka za Mungu na haifai kuswaliwa ndani yake!

Nashauri Ndugu rais awe makini sana na haya mambo ya dini, haya ni mazito sana, akiyakosea yataiweka heshima nzima ya taasisi ya urais rehani halafu kuja kurekebisha taswira hiyo inaweza kutumia gharama kubwa.

MAMBO YA WAISLAMU WAACHIWE WAISLAMU WENYEWE. NDUGU RAIS FANYA YALE YA IMANI YAKO AU YALE UTAKAYOOMBWA UFANYE KAMA UKIPENDA!
Ukisoma between lines - mwandishi - Ana chuki isiyopimika dhidi ya wakatoliki.
Mwandishi anaumia sana kumuona Rais anatoa sadaka kanisani.

Hili la kuchangiana si hoja yake ya msingi. Ila imempa upenyo tu kuventi chuki yake dhidi ya wakatoliki.

Rais ni kiongozi wa nchi. Anaongoza wakristo, waislam na hata wasio na dini.
Ana jukumu la kuwaunganisha wote waishi kindugu, kuthaminiana, kuheshimiana na kusaidiana.

Mwandishi asingetumia chuki yake dhidi ya ukatoliki angeweza kuiona dhamira njema ya Rais kutuunganisha na kutufanya tuishi kitanzania - tukipendana na kushirikiana bila kujali tofauti zetu kiimani, kikabila nk.
Sisi ni WATANZANIA na ni NDUGU.
 
Ndugu zangu, Amani iwe juu yenu pamekuwepo na madai na majitapo mengi kutoka kwa baadhi ya political laymen tangu jana baada ya baba mwenye nyumba kutembeza bakuli kanisani kuomba fedhwa za kujenga msikiti.

Hapo nina maswali mawili matatu.

Moja, Baba mwenye nyumba alitumwa na masheikh kuwaombea michango kanisani, bila shaka mamlaka za waislamu zitatujulisha.

Pili, Je ni upendo wa baba mwenye nyumba kwa wapangaji wake kutaka kuonesha religious equilibrium katika kipindi hiki cha kutafuta political pasture?, sina hakika sana kama iko hivyo.

Tatu, Ni uumini na uchamungu wa kiwango cha juu cha baba mwenye nyumba?, nadhani hili ni jibu sahihi.

Nne, Ni ipi hukumu ya kisheria katika dini ya uislamu kujenga msikiti kwa fedhwa ambazo yakinani zimetokea kanisani bila wasiwasi wowote?

Hapo maulama watatusaidia

Tano, Je hili halina athari yoyote kisiasa khasa wakati huu wa uchaguzi?

Sita, Ni lini msikiti wa mfalme wa Moroko utazinduliwa nao waislamu wachangie kanisa?
 
Back
Top Bottom