Rais Magufuli atahudhuria UN General Assembly Jumatatu?

Rais Magufuli atahudhuria UN General Assembly Jumatatu?

Sipendi upumbavu wa kuhusisha maamuzi magumu ya rais na hoja dhaifu ya lugha. Aliyewaambia UN hakuna wakalimani wa kiswahili ni nani? Hivi nyie wakuja mnajua lugha za UN ziko ngapi?

Hupenda we nani, nonsense
 
Mbona watanzania hamna jema kipindi cha JK mlisema anasafiri sana kipindi hiki cha JPM ametulia hasafiri ovyo bado mnalalamika kua hasafiri sijui watanzania mnataka nini acheni kulalama ovyo..

Come on, you have to strike the balance
 
Suala sio ngeli mkuu,
Marais Kama Putin wa Urusi huwa wanahutubia mikutano ya umoja wa mataifa kwa Lugha za nchi zao Na tafsiri inafanyika kwa wasioelewa.
Kwa nini sisi watanzania hatujithamini?
Inakera sana kuona watu wanashika bango humu kuwa rais hajui kiingereza, fikra za kitumwa kabisa!
Kiingereza ndio kitatuondolea umaskini?

Kiswahili kitatuondolea umasikini
 
Utapata kwani mimi nahisi kaka katumia muda huu wa majonzi ya Kagera kufanya rehearsal ya hotuba yake kwenye UN. Watu wanahoji kama ni lazima, mimi nadhani ni wajibu wa wakuu wa nchi kuhudhuria kwani ndicho kikao kikuu cha UN ambacho kila mkuu wa nchi anatoa lake la moyoni na kuelelzea kinachomkera. Kumbuka Mugabe ambavyo kila mwaka hakosi na kila mwaka ndo anapata mwanya wa kuwabeza watawala wa UK na US mpaka mara nyingi nchi nyingi huwa zinatoka. Kumbuka wakati wa Rais wa Venezuela alivyokuwa akitoa vigongo naye. Mwalimu alitumia kikao hiki hiki kwenye Senventees kumtetea China aingie kwenye UN na alikubaliwa at last.
Tunaomba kaka Pombe aende atoe ya moyoni, aelezee mikakati ya TZ kumaliza ufisadi na aongelee mifarakano ya Maziwa makuu inavyotuzalishia wakimbizi ili hali wakimbizi wanaoangaliwa ni wale wa Syria na kwingine wakati vita ya kongo na sintofahamu ya Burundi imefumbiwa macho. Awaelezee jinsi alivyoleta elimu ya bure na aseme alivyoanza na madawati na siyo madaftari, kalamu na vitabu vya kiada kwa kila mtoto. Naamini yupo busy na mazoezi na atapanda ndege yetu wenyewe kwenda na kutua JFK. Amina.

Amina
 
Watu kwa uchokozi? Mlitakaje labda, aende au asiende? Au mnataka kumpa barua zenu ampelekee Slaa kwni pale ni jirani na alipo na labda mmekosa stempu? Sasa akienda huko mnataka akawasemee huu ya jambo gani? Acheni uchokozi.
 
Kiswahili kitatuondolea umasikini
Hatuondolewi umaskini na utaalamu wa lugha iwe kiswahili ama lugha ya kigeni ......

JUHUDI/JITIHADA katika MAARIFA ulonayo ndo mambo mawili ya msingi
 
Me, a catalyst, never change at the end of chemical reaction but not put in the test tube, never ever kamwene mnogage! Uh sorry! English is a missed call.
Dah mkuu mpk hapo kwe kamwene wakalimani wataona vumbi
 
Kiingereza hakileti chakula. Kiingereza hakiondoi rushwa na ufisadi. Kiingereza hakiboreshi hali za maisha ya watanzania. Kwahyo hata kama Rais Magufuli angekuwa anaweza kuongea kiingereza bora kuliko binadam yeyote hapa duniani haimaanishi kuwa angefanya vizuri katika kutatua matatzo ya watanzania
Pia kujua kiingereza hakuzuii kufanya yote ulioyasema hapo juu....acha uvivu kijana hata marekan walipelekewa kiingereza na wanaongea mpk kesho...nchi za east africa zote wanaongea kuswahili plus lugha nyingne sa c watz tunataka kiswahili tuu!!!
 
Siku atayoenda na kuhutubia....watakufa mbafu zao...kwa kucheka jinsi atakavyokuwa ana pronounce
 
Tunamtakia kila ka kheri rais wetu ajenge ujasiri wa kukutana na marais wenzake, hali hii sio nzuri inawafanya watu waseme mengi sana. Najua akitoka mara moja atazoea tu. Tulisema lakini! urais sio lelemama na unahitaji uzoefu na uwezo.
 
UN General Assembly inaanza Jumatatu Sept 19 2016. Hivi ni lazima Rais aalikwe kuhudhuria mkutano huo au huwa wanaenda tu?..Rais wa Nigeria atahutubia na ameshawa taarifu wananchi wake nini atahutubia. Nakumbuka hata Rais Mstaafu Mwinyi niliwahi kumshuhudia akihutubia..Sijui Mheshimiwa Magufuli atahudhuria na kuhutubia? Nafikiri Msigwa atatuhabarisha.
Ndio maana kuna msemo unaosema; binadamu hawana jema.
Kikwete alikuwa anasafiri sana wakasema amezidi kusafiri akatungiwa majina mengi kiguu na njia mda wote anaruka angani Siku alizotumia kwa safari za nje ni nyingi kuliko alizotumia kukaa ofisini.

Kaja JPM asiyetaka kusafiri Mara kwa mara wanasema hajui kingereza,
Kweli nineamini upinzani wa tz una safari ndefu.
 
Back
Top Bottom