Rais Kikwete safarini Marekani

Rais Kikwete safarini Marekani

Kula bata JK watakuaje kwanza walikunyima kura ukachakachua watakukomaje.
 
Hivi ukiwa mwana ccm ni lazima uwe na akili ndogo kama pilitoni! Unaamua kujitoa ufahamu kwa kutetea huyo mbaba?

Ulitaka nimetete Mbowe anae-divert safari ya hawara yake kwa gharama za kodi yetu kwenda nae Dubai kula nae raha?
 
Kwahiyo Ritz unakiri JK nikama popo hewani muda wote.

Aiseee sijawahi kuona rais anayechambwa kiasi hiki! Hivi anasomaga hii maneno kweli? Kama upstairs kuko sawa lazima ujiuzulu mkulu! Ni aibu!
 
Aisee bibie Salma huwa yupo salama kweli akibaki au vijana washakamata fulsa?

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums

Cha kushangaza tunaambiwa mgonjwa lakini my wife wake yupo kitaa kama kawa, baba kaenda kutibiwa via Dubai!
 
Emekwenda na Mkewe au? au mkewe hatakiwi kupima afya yake? kama kamwacha akina mama fanyeni maandamano kwani huu ni unyanyasaji wa kijiisia!:sleepy:

Mkewe tumepishana naye mitaa ya peacock mida ya saa 8 mchana akiwa kwenye V8 nyeusi! Halafu tunaambiwa eti safari ya kucheck afya bila mke!!!! Majangaaa
 
Nyie pro-Chadema najua mna chuki sana na rais wetu JK hata kama anakwenda kutibiwa tatizo lipo wapi acheni unafiki basi, juzi hapa kiongozi wenu Dr.Slaa kaongozana na girlfriend wake Josephine kwenda Ujerumani kuangaliwa afya mlishangilia sana leo JK mnaanza kuponda acheni siasa za makengengeza.
Usiwe mjinga kila siku wewe,hivi Hospital alizofungua yeye kama Rais ni special kwa wananchi wengine na yeye hahusiki na kwa nini asicheki afya yake Muhimbili kama wengine??Usishabikie vitu vya kijinga
 
Haijakamilika! Tuwekee na pesa zilizoletwa na safari hizi, hapo utakuwa fair. Kinyume cha hapo CHUKI TU.
Watu kama wewe ndo mnaliweka taifa letu nyuma. Yaani wewe unaamini huyu mtu akisafiri kuna hela inaletwa ndani ya nchi? Kama wewe ni mzee, basi unasema hivyo kwa sababu ya uzee. Kama kijana, basi unaumwa na unastahili marafiki wa kukuchallenge na uwasikie kwa sababu una upungufu wa mawazo usio wa kawaida.

Ngoja tuojiane hapa. Juzi tu tulikuwa na sherehe za uhuru wa taifa letu uwanja wa taifa. JK alikuwepo peke yake (hapa naongelea viongozi wa nchi zilizotuzunguka). Hakuna aliyekuja. Ila baada ya hapo, Kenya wakafanya sherehe kama hiyo. Nakwambia JK aliwahi ile sherehe. Sasa nambie, huo ni urafiki gani? Yaani wewe unatembelea watu wasiokutembelea?

OK, turudi kwenye point yako kwamba akisafiri kuna pesa inaingia kwenye taifa letu. Kama kusafiri ni njia ya maendelea, tuangalie viongozi waliotuzunguka, Kenya, Uganda, Rwanda, Burundi, Congo. Au tafuta kiongozi yeyote Afrika. Akikosa tafuta duniani kote kiongozi anayesafiri kama JK. Si unatwambia kusafiri ni maendeleo? Kwa nini viongozi wote hawa wasiige mifano ya JK hili kuletea mataifa yao maendeleo?

Haya ni matumizi mabaya ya madaraka. Ni kutojari wananchi na kutumia dhamana aliyopewa kiongozi vibaya.

Tufanyeje?

Inabidi Katiba inayokuja ikemee tabia za namna hii. Safari zipangiwe badget. Ikiisha, basi. Tusipofanya hivyo, basi huu ni ufisadi mzuri na uliohararishwa. Yaani kiongozi anaweza kuwa tajiri wa maisha kwa safari tu kwa sababu analipwa posho, kwa JK itakuwa haipungui dollar 5000 kwa siku. Akipiga siku tatu ni dollar 15000 (mil.24). Hii ndo inamfanya anyatie safari kama Simba anavyomnyatia Swala. Yaani aende South Africa mara ya kwanza, arudi tena within a week, aende Kenya, then aende America.......who knows what next. Hizo elfu 5000 hazijumuishi maradhi na chakula na kina Michuzi na Camera zao.

Mwisho, tunahitaji viongozi waadirifu. Hawa hawatoki CCM hata wakija kwa style gani. Tunahitaji kuwa wapenzi wa taifa letu. Mataifa anayokimbilia kutembelea huyu JK, wao wanaheshimu misingi na maisha ya watu. Ndo maana hachoki kutembelea hayo mataifa.

Tujifunze kuwa wapenzi wa taifa letu. Tuache kuongwa kofia na kanga tukauza utu wetu. Mimi binafsi nikipewa nichague kati ya mtu anayeiba meno ya tembo na kubeba wanyama kwenye ndege (majangiri) na mtu anayesafiri kila siku na kulipwa mamillion akiwa safarini, bado mshahara wake, ntachagua yule anayeua Tembo. Wote wanafanya maovu kwa taifa lakini wa Tembo anaiba kidogo ukilinganisha na msafiri (wenye ubongo wamenielewa).

Inabidi lianzishwe somo la ethics mashuleni. Watoto wajifunze kwamba kuiba ni kubaya. Akiingia kiongozi mwingine, kigezo kimojawapo kiwe kuweka wazi gharama alizotumia JK safarini. Nakuhakikishia watu wakijua, atakuwa the most hated guy nchini mwetu.

Then, we need rule of law. Sheria ifanye kazi yake. Pasiwepo mtu aliyeko juu au chini ya sheria. Sheria mbovu ndo zinafanya mambo yanayoendelea nchini. Mpaka leo hakuna mtu wa kuuliza safari zinalipwa na nani? Zina tija gani na nchi yetu. Inabidi watu waende jela kwanza ndo tutajifunza discipline.

Watanzania tujue kuwa kupiga kura ni homework na si mchezo. Hii ni sawa sawa na kupanda mazao. Ukipanda mahindi, utavuna mahindi. Ukipanda maharagwe, utavuna maharagwe. Ukipanda magamba, utavuna magamba. Siamini kama hiki chama kinaweza kutoa mtu akalikomboa taifa letu. Mfumo wa wizi wao ni kujuana. Niwape mfano mmoja. JK anachagua mawaziri. Baadae anajua kwamba baadhi yao si watendaji wazuri, badala ya kuwafukuza, anahitisha kikao hili kujadili. Kumbuka hicho kikao watu wanakaa na kulipwa tena pesa ya walala hoi. Huu ni udhaifu na ni uzembe.

Mfano mwingine, mnakumbuka kuvua magamba? Magamba ni neno tu linalosimama badala ya wizi, utoa rushwa, ugawaji rushwa, mauaji nk. Sasa nani kavua gamba?

Hiyo mifano inatosha sasa kuonesha kuwa hawa watu sio tu hawako serious na taifa letu bali hawalipendi taifa letu. Tuwekeze sasa kwa mtu ambaye atakuwa si rafiki yao. Akiingia tu rafiki yao, basi tutakuwa ni watu wa kulalamika na kuishia mitandaoni.

Habari njema tulionayo ni kwamba, wao wanaweza kutuibia, kutuma polisi wakatuwekea vyuma sehemu za siri, wakatutesa, wakatupiga, wakaua watoto wetu ila kuna kitu hawawezi kutunyanganya, HAKI YA KUPIGA KURA. Tumia vema nafasi hii mtanzania. bado tunao muda wa kuwaondoa hawa wezi.

Nawasilisha.
 
Kijitonyama nakupongeza kwa uandishi na mawazo yako ktk ujenzi wa taifa letu. Magamba wanajua haki iliyosalia kwa mtanzania ni KUPIGA KURA. Soma nyuzi za hii mada uone magamba wanavyochezea akili ya watanzania.

Sitaki kukukatisha tamaa ila jukumu langu mimi na wewe ni kuendelea kuwafundisha wajue uzito wa haki hiyo iliyosalia kwao. Bila kujua uzito huo, magamba watachukua haki hiyo kirahisi sana- tena kupitia tume ya uchaguzi.
 
Ngoja tuojiane hapa. Juzi tu tulikuwa na sherehe za uhuru wa taifa letu uwanja wa taifa. JK alikuwepo peke yake (hapa naongelea viongozi wa nchi zilizotuzunguka). Hakuna aliyekuja. Ila baada ya hapo, Kenya wakafanya sherehe kama hiyo. Nakwambia JK aliwahi ile sherehe. Sasa nambie, huo ni urafiki gani? Yaani wewe unatembelea watu wasiokutembelea?.
Unataka kusema wakati wa sherehe za uhuru 9 December hakuna rais yoyote aliekuja kutoka Africa?
 
Rais Kikwete amewasili Dubai usiku jana akiwa njiani kwenda marekani kwa ajili ya matibabu na kufanya check up ya afya yake.

Maafisa wa ikulu wamethibitisha kuwa safari hii ni kwa ajili ya matibabu tu ingawa haijasemwa anasumbuliwa na nini

Ni maombi yangu kwa MUNGU apone na apate afya njema.
Sikubaliani na mwenendo wa serikali yake na chama chake.
Ila kwa kuwa ni kiongozi wa nchi yangu, namtakia afya njema, hekima na busara.
 
kijitonyama wewe ni mmoja wa wazalendo wachache tulio nao.

Ahsante sana!
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom