Jamaa wamegomea Kibomu kingine tu!
Akae atulie nyumbani kwake. Anaaga kwani anakufa? Ndio anatumia yale mabilioni yaliyotengwa kwajili ya hizi ziara za kij....
Mkuu lusungo, naomba rekebisha Kiswahili, Jee ni amezuiliwa au amekataliwa kuingia Denmark?!.Rais Wa Tanzania ndugu Jakaya Mrisho Kikwete amezuiliwa kuingia Denmark .....
Mkuu lusungo, naomba rekebisha Kiswahili, Jee ni amezuiliwa au amekataliwa kuingia Denmark?!.
Kuzuiliwa ni pale alipoamua kuingia bila ruhusa, halafu yeye na msafara wake ukazuiliwa kwenye entry point!.
Kukataliwa ni pale MFA ilipotuma NV (Note Verbale) kuomba JK aje kuaga, akakataliwa kistaarabu kutoka na uchaguzi!.
Which is which!, kuandika kuwa amezuiliwa is as if Rais Kikwete alitaka kuingia Denmark kama anaingia chooni na kukutana na zuio!. Tueleze which is which?!.
Pasco
Huu muda angeutumia kutatua changamoto kuliko kuupotezea hewani sijui mafaili ya watia nia atayapitia lini aisee....
CCM tayari ina muundo wake wa kuchaguwa watia nia na si lazima Rais ayapitie - Kumbuka hilo.
Hivi hizo shule huwa mnaenda kusomea ujinga?
Wazungu huwa wanatushangaa sana nafikiri wanashangaa zaidi rais wa nchi nyingine kupoteza muda kuaga wananchi wa nchi nyingine ambao hawakumpigia hata kura moja, kazi hii inatakiwa kufanywa na balozi zetu au kama ni lazima basi waziri wa mambo ya nje angewakilisha.Najiuliza na wao wakimaliza uongozi wanakujaga kuaga?