Ni kwa waliopungukiwa maarifa tu ndo wanaoweza kuunga mkono hoja hii ya hovyo. Ka una maarifa timamu huwezi kuleta hoja hii ukafikiri ndo jambo jema kwa nchi na kwamba tulishabikie hapa JF. Sisi kama watu waungwana yatupasa kumuunga mkono mheshimiwa raisi kuhakikisha nchi inakaa kwenye mstari na inakuwa na maendeleo chanya na si kumdhihaki na kuonyesha juhudi zake ni bure na kwamba nchi iendelee kuendeshwa hovyohovyo kwa kuendekeza wahujumu uchumi, wauza madawa ya kulevya, mafisadi na majanga mengineyo ktk nchi.
MTanzania anaemuunga mkono Magu akili yake itakuwa sio nzuri huyo,watanzania tulikuwa na furaha awamu ya nne ya utawala wa CCM,awamu hii ya tano watanzania wamegubikwa na ukungu mzito wa majonzi,maisha ya mtanzania yamekuwa hayana uhakika wa kesho..
Mimi ni mmoja katika watanzania waliokuwa wakimfagilia Magufuli,lakini baada ya kuona vipi anafanya kila juhudi kuwanjima haki za msingi watanzania hapo nikamuona hana maana hata kidogo..
Katika historia Tanzania haijawahi kutokea watanzania kuwa na woga kama awamu hii,Nchi yoyote yenye raia wenye woga wa maisha haiwezi kupata maendeleo ya aina yoyote,nidhamu ya woga ni moja katika kitu kinacholeta umasikini kwa mwanadamu...
Watanzania ni watu wa kujituma,watu wa kujaribu mbinu tafauti katika kuleta maendeleo katika maisha yao,sijui humu ndani ya JF kama kuna anaefahamu hili neno
Bongo limekujaje au nani kalibuni,kama mtataka kujua nitakufamisheni lakini kwasababu hii mada hausiano na hilo jina basi tupotezee tu..
Magufuli ilikuwa haina haja ya yeye kama raisi kuanza kubaguwa anaowatala,ilikuwa haina haja ya kuwanyanyasa watanzania walikuwa wana mawazo tafauti na yeye,yeye alikuwa anatakiwa akumbuke kuwa ni raisi wa watanzania wote,walio na mawazo kama yake na wasio na mawazo kama yake..
Ukianza kuwafanya unao watawala
wabaguane,huwezi kuleta maendeleo katika nchi, kama raia hawalewani,leo hii raisi anafika hadi kusema "hawa msiwavunjie ni wapiga kura wangu",Je raisi wetu ana tawala kwa visasi...,Mh Zitto ameshawahi kuwa Tanzania ina tawaliwa na washamba,hii ni kweli raisi wetu ni mshamba..
Mwalim Nyerere wakati wa utawala wake alikuwa anasisitiza sana
utani miongoni mwa makabila ya watanzani,
utani ni moja katika mila na jadi za waTanzania,utani unaleta maelewano katika jamii...
Raisi wetu Magu hataniwi
ukimtania anakufunga,ukimwambia
ukweli anakufunga,
ukimkosoa anakufunga,raisi haambiliki,anaona anaowatawala ni wajinga mwerevu yeye peke yake,hivi sasa waTanzania
hawataniani tena,waTanzania wameanza kuzungumza
ukabila na udini...
Huyu raisi hafai kututawala watu wapole na wastarabu kama waTanzania
.....,tutafutieni mwengine