Wala mimi siko huko isipokuwa hizi habari za kumchagua rais kwa sababu ni Kijana/Mzee au Mkristu/Muislaam inanipa mashaka sana na akili zetu.
Kiongozi kama rais ana sifa zake. Ni kiongozi ambaye anatambua tofauti zetu na umuhimu wa nila na tamaduni ambazo zimetuweka sisi kuwa wamoja kwa miaka 50 na Taifa gani tunataka kulijenga. Sasa unapopongeza utukufu unaotazama mtengano wa kiimani hizo tamaduni kuwa kigezo hapo ndipo naposhindwa kuelewa. Na ujue fika kwamba kuna tofauti baina ya Leadership na Management iwe kwa sifa ama malengo.
Hakuna adui mkubwa wa umoja wa watu kama kuendeleza tofauti zao na ndiomaana Nyerere alisisitiza kufuta Ukabila. Na pengine niseme tukitoka katika Ukristu kesho Hao hao wakristu watadai tunahitaji rais Lutherani au Protestant kwa sababu kila rais aliyepita alikuwa Mkatoliki, Na Shia nao watakuja na lao kuhusu Sunni, Bniani na kadhalika. Yanayotokea Iraq na nchi za Kiarabu leo sii ya bahati mbaya, hawa watu kabila zao sina define Imani zao, ni watu waloshindwa kuelewa mila na tamaduni zilizowaweka pamoja badala yake wakaweka imani zao kuwa msingi wa jamii.
Hata huko India vile vile kabila ndizo zinajenga imani zao za dini na ndio maana wameishi kwa matabaka miaka yote. Pakistan, India na Bangladesh kugawanyika ilitokana na ubaguzi wa Kikabila = Dini. Hivyo nasi kuiga vitu kama hivi wakati tunaona athari zake ni kuonyesha wazi kwamba tunashindwa kusoma wakati. Kwa wenzetu wazungu Uislaam na dini nyinginezo ni wageni kwao hivyo mgeni analazimika kufuata mila na tamaduni zao japo wao ni wa makabila tofauti na imani tofauti ndani ya Ukristu.
ndio maana sisi wengine tunamwona Nyerere kama Genius kwa sababu alijaribu kuondoa Ukabila na Udini kutokana na mifano aloiona Ulaya. Mrusi aliyehamia Marekani leo anajisikia ni Mmarekani kuliko Mwafrika alozaliwa Marekani. Na ajabu Mrusi huyo huyo siku kuna mashindano baina ya Urusi na Marekani utamwona akibeba bendera vya Urusi. Tazama World cup hii jinsi Waamerika wenyewe walivyokuwa nyuma ya timu yao japo ikicheza na nchi ya asili yake anarudi kwao. Hakuna mtu alomshikia bango mwenzake wala uadui kwa sababu wanaelewa nini maana na haki za Uraia pamoja na fursa zake.
maendeleo ya watu hawa hayakuja kwa bahati mbaya bali ni kuelewa ruksa na fursa za Uraia. Kuelewa kwamba hakuna Ukabila ndani ya Marekani ila kuna taifa jipya lenye mkusanyiko wa Mataifa yote duniani na wenye vipaji na fursa ya kufikia ndoto ulokuwa nayo. Na tuseme ukweli bila woga Ujio wa Obama (sii mweusi tu bali ana asili ya Kenya, Afrika) ni ishara tosha ya Taifa waloweza kulijenga maana katoka ktk kundi la watu wachache na wanaodharauliwa kuliko mataifa yote.
Tuachane na fikra hizi za Ujana na Udini zitatupeleka pabaya zaidi..