Professor Shivji avunja Ukimya juu ya Maxence Melo

Professor Shivji avunja Ukimya juu ya Maxence Melo

Watanzania tulianza kupigania haki tangu enzi za mababu zetu akina Mkwawa, Isike, Chabruma, Mirambo, n.k. Wakati huo hakukuwa na mikataba ya kuheshimu haki ya kimataifa, hakukuwa na simu, hakukuwa na radio, internet wala TV lakini watu walijua wanatakiwa kuwa huru, hata kama uhuru huo haukuwa kwa tafsiri ya leo, lakini walijua kuwa walistahili uhuru na haki.

Akaja Mwalimu na wenzake, Mwinyi, Mkapa, na kisha Kikwete. Wakati wote huo tumeendelea kujenga Taifa ambalo tunataka liwe na huru kamili, demokrasia kamili, haki kamili, n.k. Hatujafika huko lakini tumekuwa tunapiga hatua. Kinashangaza sasa hivi badala ya kuzidi kupiga hatua kwenda mbele, tayari tunarudi nyuma.

Binadamu ni mtu huru ndiyo maana Mungu kamwumba kila mmoja na kichwa chake chenye ubongo unaojitegemea. Mtu yeyote anayetaka watu wote watumie ubongo wake kwa kila kitu, hawezi kufanikiwa, badala yake atasababisha matatizo makubwa.
Kweli mkuu
 
Huwezi kuamini mtu yule bwana alitumia mitandao kufanya campaign then anaichukia kiasi hiki halafu ukifika tena muda wa campaign atataka kuitumia tena.
 
Bado tutazuia makongamano yanayofanyika chuo kikuu cha Dar wakifanya tutasimamisha ujenzi wa mabweni.Wajaribu waone.
 
Pasko alileta uzi kua alimhoji Shivji juu ya mwenendo wa nchi hii katika mlengo wa sheria (nadhani walikua kwenye kongamano).

Shivji hakujibu, alikaa kimya na kuonesha kua hataki kujibu.

Eti leo nimuamini? Hapana aisee.
Ahsante sana
 
Alivyo tugeuka kwenye katiba yetu iliyo pendekezwa na wananchi basii namchukukia kama prof lipumba tuu.!.
 
Jitihada zote ziwe za kisheria tafadhali, hivi huyo muhindi hafahamu kuna sheria ya makosa ya mtandao na kwamba hapo imekiukwa?

Aliyeandika ni mwanasheria,anaelewa wapi serikali inakosea.
 
Angeyasema haya live kwenye makongamano ningemuona muungwana kwelikweli lakini kuandika kwenye mitandao tena ambao wananchi wengi hawawezi pata ujumbe bado namuona walewale tu, [HASHTAG]#POPO[/HASHTAG].

Wewe uliupataje! Unajua maana ya mawasilianao? Unajua anachokitetea Max? Basi timiza wajibu wako!
 
Back
Top Bottom