Professor Shivji avunja Ukimya juu ya Maxence Melo

Professor Shivji avunja Ukimya juu ya Maxence Melo

Angeyasema haya live kwenye makongamano ningemuona muungwana kwelikweli lakini kuandika kwenye mitandao tena ambao wananchi wengi hawawezi pata ujumbe bado namuona walewale tu, [HASHTAG]#POPO[/HASHTAG].
Twitter ni social media inafaa kabisa kufikisha ujumbe. Wewe mbona maono yako madogo sana? Lengo la Shivji ni kufikia hadhira ya Watanzania na dunia pia. Twitter imefanikisha hili. Si umeona hata wewe umeshapata habari? Hilo ndiyo lengo kuu......si vinginevyo.
 
Angeyasema haya live kwenye makongamano ningemuona muungwana kwelikweli lakini kuandika kwenye mitandao tena ambao wananchi wengi hawawezi pata ujumbe bado namuona walewale tu, [HASHTAG]#POPO[/HASHTAG].
Kama hujui kitu uwe unapita kimya !! Unaelewa maana ya Hashtag aliyoweka na idadi ya watu watakaoiona. Kama uko katete huko kyela pita hivi.
[HASHTAG]#freemaxencemello[/HASHTAG]
 
Pasko alileta uzi kua alimhoji Shivji juu ya mwenendo wa nchi hii katika mlengo wa sheria (nadhani walikua kwenye kongamano).

Shivji hakujibu, alikaa kimya na kuonesha kua hataki kujibu.

Eti leo nimuamini? Hapana aisee.
Ahsante sana
Kila jambo lina wakati wake. Shivji alijua Pasco anataka nini, kutomjibu wakati ule haiondoi ukweli kuwa leo kasema hili. Ni uwezo wako tu wa kuchambua mambo ndio unakusumbua...
 
Shivji alitusaliti wakati wa mchakato wa katiba mpya. Aliyakana hata machapisho yake mwenyewe juu ya serikali 3.

Sina hamu na huyu mzee, usikute kaibuka kwa kuwa kafulia, wakimpoz
 
Bora kamtafsiria kabisa. Ila aangalie pensheni isipigwe stop.
 
Sasa hapo manyamela wanawaza jinsi,
Kumpata na kakosa hata kadogo,

Professor take care.
Hii ni serikali dharimu.
 
Huyo jamaa anakesha na kufikiri namna ya kudanganya akili za watu. Ni watu wenye maono makubwa Kama wakina Prof. Hawa ndio wanaweza kughamua nini kinaendelea.
 
Hehehe unajipa moyo eti the country is boiling... Unajua % ngapi wanakaa vijijini na maisha kwao yamekua vile vile kwa muda mrefu na bado hawajaona haja ya kubadilisha chama? Sana Sana wanasikia juhudi za Mkuu kupiga vita ubadhirifu wa vijisenti vyao vinavyokusanywa. Matatizo yako wewe kama mkazi wa mjini hayawezi kuleta mapinduzi yeyote the way unavyoongea na wenzako wachache kwenye vigenge vyenu vya pombe na kujihamasisha na kujiaminisha na upuuzi.
dunia imebadilika ujue,sasa hivi mpaka vijijin wanalalamika eti hela imepotea...
 
Kila jambo lina wakati wake. Shivji alijua Pasco anataka nini, kutomjibu wakati ule haiondoi ukweli kuwa leo kasema hili. Ni uwezo wako tu wa kuchambua mambo ndio unakusumbua...
Uwezo wangu unaniambia huu ni unafiki, kazi ni kwako kuchambua pia.
 
Laana za mababu ni nini? Mababu ni wakina nani? Laana zitashukaje sambamba na Malaika waliotumwa kufungia Mitandao ya kijamii? Wakianza kupaza sauti watu aina ya Prof Shivji basi ...
Huyu ni wale wale kama wasomi wengine, hakuna ninayemuamini Tanzania hii kuanzia Serikali, CCM, Upinzani. Wote ni wasanii tuu na wanafiki.
 
Uwezo wangu unaniambia huu ni unafiki, kazi ni kwako kuchambua pia.
100% Nakuunga mkono hawa wasomi wetu ni wanafiki maana wanauma na kupulizia wakitaka siku moja mkulu awaone na wao wapate keki ya Taifa. Wapi kina Palamagamba Kabudi, wapi Kina Mwakyembe, kaka mijitu hapa JF inatapeliwa kirahisi sana, angalia kina Sumaye wamewaminya wapinzani miaka yote lakini tangu mwaka jana wanaonekana makamanda. Huu ujinga wetu utaisha lini mimi sijui, tumekuwa zaidi ya Nyumbu. Maana nyumbu wanakumbuka wakati gani wahamie Masai mara kufuata malisho, sasa hivi ikitokea Mwigulu ama Maghembe akitoka CCM akaja upinzani wengi watashangilia hapa na kuwaita makamanda. Hata Muhongo taabu yetu ni kuona kuwa yeyote ambaye anahama ccm na kuja upinzani ni kamanda bila kujua lengo lake na nia yake.
 
Nimekusoma profesa.Loud and clear.
Message sent
 
Back
Top Bottom