Prof. Mohamed Janabi achaguliwa kuongoza WHO AFRO
Nami natamani kujua, kama nchi kuna faida gani inapatikana kuwa na kiongozi ngazi hiyo huko WHO? Maana nakumbuka Migiro alikuwa UN, Salim Ahmed nae AU ila sidhani kama kuna tija yoyote kwa taifa.
Umeona mkuu hapo umeongea sasa
 
Hii ni taarifa ya hivi punde.
Prof. Mohamed Janabi ambaye pia ni Mkurugenzi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili amechaguliwa kuongoza Shirika la Afya Duniani ukanda wa Africa.

Pongezi nyingi kwake na watanzania.
===============
Profesa Mohamed Janabi, Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH), amechaguliwa kuwa Mkurugenzi wa Kanda ya Afrika wa Shirika la Afya Duniani (WHO). Uchaguzi huo umefanyika leo, Jumapili Mei 18, 2025, huko Geneva, Uswisi.

Prof. Janabi anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Dk. Faustine Ndugulile, aliyekuwa Mkurugenzi Mteule wa Kanda hiyo na Waziri wa zamani wa Afya wa Tanzania, aliyefariki dunia Novemba 2024.

Katika nafasi hii mpya, Prof. Janabi atahudumu kwa kipindi cha miaka mitano, akiwa na fursa ya kuchaguliwa tena kwa muhula mmoja zaidi. Kazi yake kuu itakuwa ni kuongoza juhudi za kuunda sera za afya, kuratibu huduma za dharura za afya, pamoja na kushinikiza suluhu bunifu kwa changamoto za kiafya barani Afrika.

Wagombea wengine walioshiriki katika uchaguzi huo lakini hawakufanikiwa ni pamoja na:

  • Moustafa Mijiyawa (Togo)
  • Dk. N’Da Konan Michel Yao (Ivory Coast)
  • Mohamed Lamine Dramé (Guinea)

View attachment 3338251
Nilijua tu atashinda! Na ningeshangaa sana kama asingeshinda pamoja na usomi wake na kampeni kubwa iliyofanywa kuhakikisha anashinda.
HONGERA SANA PROFESSOR MOHAMED YAKUB JANABI.
 
Imekuwa gumzo kwa sababu kuna watu walikuwa wanaombea ashindwe, na wakawa wanaapiza kwamba hawezi kushinda! Kwahiyo, kabla ya kuhoji kwani TZ itanufaika na nini tulitakiwa kwanza tuhoji wale waliokuwa wanaombea ashindwe kwani walihofia Tanzania ingedhurika na nini kwa ushindi wake?
Sawa turudi kwenye swali sasa, kwa hiyo ushindi wake una manufaa gani kwa Tanzania?
 
Duh, kuna wakati CHADEMA tunakuwa hatujui tunachokitafuta! Sasa Janabi naye tulikuwa tunamchukia kwa lipi hasa? Sasa tumeumbuka mchana kweupe!
Binafsi mm sio chadema wala sio CCM, ila chadema wanazingua Sana, sasa hv wamebadili gia wanasema hicho cheo kina faida gn kwa nchi 😂
 
Back
Top Bottom