Dr Adam Francis
JF-Expert Member
- Aug 12, 2011
- 719
- 1,173
Hakuna jambo linafurahisha kama kuona mtanzania mwenzetu anapata mafanikio makubwa kimataifa. Sisi watanzania wazalendo tumeupokea taarifa za kuchaguliwa kwako kuwa mkurugenzi wa WHO Afrika matumaini makubwa.
Nafasi aliyoipata Prof. Janabi ni ushindi wetu watanzania kama Taifa. Katika hili hatutakuwa waugwana kama tusipotambua mchango wa Rais Samia katika mafanikio haya. Bila shaka haya ni matokeo ya kazi nzuri ya kuimarisha diplomasia.
Jambo kama hili lina faida nyingi. Ukiacha ukweli kuwa mnapokuwa na mwakilishi mfanya maamuzi kwenye chombo kikubwa kama WHO, maswala yetu kama nchi yanapata mtetezi wakutumainiwa, kubwa lingine ni hamasa inayojengwa kwa wanataaluma na vijana wengine wa kitanzania kuwa mambo makubwa na mazuri yanawezekana.
Mm binafsi nakupongeza na kukutakia kila la kheri katika majukumu yako mapya.
Pia soma: News Alert: - Prof. Mohamed Janabi achaguliwa kuongoza WHO AFRO
Nafasi aliyoipata Prof. Janabi ni ushindi wetu watanzania kama Taifa. Katika hili hatutakuwa waugwana kama tusipotambua mchango wa Rais Samia katika mafanikio haya. Bila shaka haya ni matokeo ya kazi nzuri ya kuimarisha diplomasia.
Jambo kama hili lina faida nyingi. Ukiacha ukweli kuwa mnapokuwa na mwakilishi mfanya maamuzi kwenye chombo kikubwa kama WHO, maswala yetu kama nchi yanapata mtetezi wakutumainiwa, kubwa lingine ni hamasa inayojengwa kwa wanataaluma na vijana wengine wa kitanzania kuwa mambo makubwa na mazuri yanawezekana.
Mm binafsi nakupongeza na kukutakia kila la kheri katika majukumu yako mapya.
Pia soma: News Alert: - Prof. Mohamed Janabi achaguliwa kuongoza WHO AFRO