Prof. Anna Tibaijuka amkosoa Mh. David Kafulila

Prof. Anna Tibaijuka amkosoa Mh. David Kafulila

A.Tibaijuka ana kosoa kauli ya wao 600 kulinganisha na tume ilivyofanya. wao wameteuliwa kwa maana imetumika stratified sampling( kwa maana uteuzi wao ulicheck sifa fulani). lakini tume haikufanya stratified sampling.hivyo hoja ya A.tibaijuka iko sahihi kwenye ukosoaji wa hiyo scenario


Huyo mama mlevi tu,yan mchakato wa katiba ya watanzania ianze kuchagua watu wenye sifa kwa wananchi kutoa maon?
 
Unauliza kama walienda kila Mkoa, au unasema walitakiwa waende kila Mkoa?

NB: Tume ilipita kila mkoa. Lakini kitu ambacho sijasikia wakina Anna Tibaijuka wakitolea ufafanuzi ni je, ni wapi Tume ilikwenda kinyume na HADIDU REJEA (ToRs) katika ukusanyaji maoni? Na Anna Tibaijuka na genge lake walikuwa wapi muda wote ? Kwanini hawakuongea kuwa ukusanyaji wa maoni hauzingatii "stratified sampling? " mpaka kazi inamalizika ndio wanaanza kupiga kelele? Kumbuka rasimu iliyoko bungeni ni "edition" ya pili.

inawezekana kabisa mchakato ulikuwa ni mrefu kiasi cha Prof. Anna and the Company kuchanyikiwa au kusahau baadhi ya mambo.
anavyoliengelea hili utadhani utaratibu ulikuwa ni kupiga ngoma watu wanakusanyika toka pande zite na kuhojiwa, ni kama vile wamesahau kuwa kulikuwa pia kulikuwa na mabaraza.
 
Last edited by a moderator:
Sasa zogo la nini? Si wapitishe serikali 3 watuletee tuipigie kura utaona wananchi watavo kubali.
Nima uhakika serikali 2 hazipiti kwa kura ya raia
 
wadau nilikuwa naangalia habari,Prof. A Tibaijuka amesema Mh. Kafulila hakuwa sahihi alipokuwa anazungumzia kuhusu "samples" alisema,alichokisema kafulila siyo "stratified sampling" wala "non-stratified sampling" maana Tume ilikuwa inawahoji watu wa aina yoyote waliojitokeza mbele yao hivyo haikuwa inapanga iwafikie watu wa aina gani.

Haya mambo ya sampuli hayo,wataalamu mnasemaje?

Sasa huyu bibi kaongea nini? Hivi anazungumzia quantitave au qualitative study? Walioba alipata qualitative data ambayo data saturation inafikiwa hata na watu 30 wanaofata huwa yanajirudia.

Wanawachanganya watanzania kwa manufaa yao, ukiwa profesa ndani ya chama tawala huwa na uwezo wako wa kung'amua mambo unapungua unaendeshwa kama roboti tu.
 
Stratified or non stratified, mamlaka kamili ndio mpango mzima. I am Zanzibari and I approve this message.
 
A.Tibaijuka ana kosoa kauli ya wao 600 kulinganisha na tume ilivyofanya. wao wameteuliwa kwa maana imetumika stratified sampling( kwa maana uteuzi wao ulicheck sifa fulani). lakini tume haikufanya stratified sampling.hivyo hoja ya A.tibaijuka iko sahihi kwenye ukosoaji wa hiyo scenario

Bro usiwachanganye wasiojua, define stratified sample kwanza. Msifikiri kila mnayeongea naye ni mbumbumbu.
 
Alichosema JK ambacho ndio ukweli ni kwamba, katika watu laki 7 waliofikiwa na tume.. 0nly elf 47 ndio waliozungumzia juu ya muundo wa muungano... wengine wote hawakuona tatizo juu ya suala la muundo wa muungano.. kati ya hao elf 47.. watu elf 17 ndio waluotaka serikali 3..
Mkuu watu waliofikiwa ni laki 7; sio kuwa kila mmoja aliulizwa kuhusu muundo wa serikali ila waliojitokeza kuongelea muundo ni 47 elfu na 17 elfu kati yao walipendekeza serikali 3 na ambao hawakuona shida ya muundo wa serikali wako ktk 47 elfu humu.
Dhana ya kudai katika laki 7 ni elfu 17 tu walitaka serikali 3 ni kupotosha umma.
 
Mkuu watu waliofikiwa ni laki 7; sio kuwa kila mmoja aliulizwa kuhusu muundo wa serikali ila waliojitokeza kuongelea muundo ni 47 elfu na 17 elfu kati yao walipendekeza serikali 3 na ambao hawakuona shida ya muundo wa serikali wako ktk 47 elfu humu.
Dhana ya kudai katika laki 7 ni elfu 17 tu walitaka serikali 3 ni kupotosha umma.

Tatizo kubwa la takwimu za Tume haliko katika wingi wa waliohojiwa. Hata swala la stratified sample au la si muhimu hapa. Swala muhimu ni method of sampling. TUME haikuwa na sample. Imesikiliza yeyote aliye tayari kutoa maoni. Hilo ni jambo zuri kwao, na linawafanya waliotoa maoni wajisikie vizuri, lakini maoni hayo hayawezi kuwa representative, hata kama yangetoka kwa watu 10,000 badala ya 17,000 kwa vile sample (kama ingekuwepo) ni non-probability mahali ambapo kwa kanuni zote za ukusanyaji wa maoni wakilishi palitakiwa probability sampling, hasa simple random. Hayo ya stratified ni maneno watu wanayasema tu, kwa sababu hata accuracy ya stratified sample inahitaji probability sampling
 
Huyu mama nilimdharau tangu atumie ndege ya serikali kwenda Bukoba na kurudi Dar akiwa pekeyake! Ni walewale tu mchumia tumbo kama wengine!
 
Nasikia wapiga kura wake wa jimbo la Muleba Kusini wanasikitika kutomchagua Mhe Balozi Wilson Masilingi!
 
Prof yupo sahihi, ni vizuri watu warudi kujikumbusha statistics. Ile tume ilihoji watu takriban 350,000 kwa maana ndiyo sample inayowakilisha watanzania. Hivyo 17,000 walioongelea muungano ni asilimia 5 tu ya sample na ndiyo asilimia ya watanzania. Ukija kwa bunge la katiba wapo 600 ndiyo sample ya wawakilishi wa watanzania hivyo asilimia itatokea hapo (idadi ya wajumbe / jumla ya wajumbe)

Ulitakiwa kwenda mbali zaidi, kutuambia hao watu 350,000 walihojiwa na tume juu ya muundo wa muungano. Vinginevyo ni kutulisha upepo!
 
Tume tuliinunulia magari ya kifahari ilipoleta taarifa tulipokea kwa furaha kila mtu akawa anashangilia ni shetani gani aliyekuja kati kuharibu raha za watu jamani
 
Watanzania wengi wanataka serikali tatu, kupinga uhalali wa hii hoja ni ku-force mambo na kuonyesha jinsi usivyokuwa attached to regular wanananchi mitaani.
However, kufananisha wabunge walivychaguliwa na maoni yalivyosikilizwa ni sampling methods mbili tofauti. Wabunge walikuwa stratified based on groups wanazowakilisha while rasimu haiku-stratify watoaji wa mapendekezo (kama stratification ilifanyika ni znz vs bara tu). Kwa hiyo ni kweli kaflila alikosea kutoa mfano huo.

Stratification imefanyika vile vile kati ya wanawake na wanaume; na wakazi wa mjini na wa vijijini, kalagabaho!!! Karejee jedwali la Tume.
 
A.Tibaijuka ana kosoa kauli ya wao 600 kulinganisha na tume ilivyofanya. wao wameteuliwa kwa maana imetumika stratified sampling( kwa maana uteuzi wao ulicheck sifa fulani). lakini tume haikufanya stratified sampling.hivyo hoja ya A.tibaijuka iko sahihi kwenye ukosoaji wa hiyo scenario

Elewa tu maana ya stratum kwanza kabla ya ku argue unknowingly.....

Mabaraza ya katiba yalikuwa kitu gani kama siyo strata?

Tena sampling ya wajumbe wakatiba iko biased kwani is composed of big proportion na CCM ambayo kwa takwimu yao ni only 4% (if at all wanachama wao wanafika 5M kama wanavyodai) ya watanzania wote walio jiandikisha kupiga kura 2010 ambao ni 20M. Ebu fikiria eti wanajiita majority kwa kigezo gani cha statistics? Kama ni kura then watambue waliokataa kwenda kupiga tunaweza kusema hawana interest na chama chochote maana kwakutumia rationality theory then willingness inaonyesha preference; implying were not willing!

Ndiyo kusema Mh. Warioba alitumia purposive sampling, baada ya ku stratify raia wote wa Tanzania ndiyo maana hata aliweza kuonyesha maoni ya ofisi ya waziri mkuu miongoni mwa trata zingine alizozichagua purposeful.

Tabia ya wasomi kupindisha mambo kukidhi self desires ni hatari kuliko ugonjwa wa Ebola!

Ukitaka justifications basi bora u siki other avenue siyo kutumia academics ina shusha credibility ya wasomi wote!
 
wadau nilikuwa naangalia habari,Prof. A Tibaijuka amesema Mh. Kafulila hakuwa sahihi alipokuwa anazungumzia kuhusu "samples" alisema,alichokisema kafulila siyo "stratified sampling" wala "non-stratified sampling" maana Tume ilikuwa inawahoji watu wa aina yoyote waliojitokeza mbele yao hivyo haikuwa inapanga iwafikie watu wa aina gani.

Haya mambo ya sampuli hayo,wataalamu mnasemaje?

Mimi pia nilimsikia huyu Anna Kajumulo akijisifu kuwa yeye ni msomi na hivyo anaona Kafulila hakuwa mkweli alipozungumzia mambo ya sampling!!! Yeye huyu mama amesomea mambo ya Agricultural economics na sampling Theory ni sehemu ndogo tu aliyofundishwa ukimlinganisha na watu waliosomea STATISTICS. Amesahau kuwa katika kufanya utafiti the important thing unachotakiwa kuzingatia ni kuwa sample yako iwe Representative; hayo mambo ya stratified na non-stratified sampling anawachanganya magamba wenzie ambao ni mbumbumbu kwani hayo yote yanakuwa yameangaliwa kama sample yako ni REPRESENTATIVE ambayo ndio aina ya sample iliyotumiwa na tume ya Warioba. Hawa mburula wa Magamba hata kama wana shahada wakiingia siasa akili zao zinadata shauri ya njaa hata kama wamefanya kazi United Nations!!
 
Tatizo kubwa la takwimu za Tume haliko katika wingi wa waliohojiwa. Hata swala la stratified sample au la si muhimu hapa. Swala muhimu ni method of sampling. TUME haikuwa na sample. Imesikiliza yeyote aliye tayari kutoa maoni. Hilo ni jambo zuri kwao, na linawafanya waliotoa maoni wajisikie vizuri, lakini maoni hayo hayawezi kuwa representative, hata kama yangetoka kwa watu 10,000 badala ya 17,000 kwa vile sample (kama ingekuwepo) ni non-probability mahali ambapo kwa kanuni zote za ukusanyaji wa maoni wakilishi palitakiwa probability sampling, hasa simple random. Hayo ya stratified ni maneno watu wanayasema tu, kwa sababu hata accuracy ya stratified sample inahitaji probability sampling

Kabla ya ku disqualify method ni vizuri ukajua njia za kukusanya opinions......

Tuache creming bila kujali context; Warioba was not doing academic research..... Alikuwa ana search for public opinion ambayo hamzuii kufanya judgemental conclusions na kutumia njia zinazofaa ku analyze information aliyo gather to suit objectives alizokuwa nazo.

Amefanya triangulation ya kutosha kuja na conclusion ambayo wengi walio na open mind tunakubaliana nazo.


Kama una argue ya Tume ya maoni je ni ambie composition ya wajumbe wa katiba una i justify vipi?

Warioba na wajumbe wenzake ni watu wenye experience kubwa na wana institutional memory ya tangu uhuru hivyo kwa hadi yao tunategemea wana social capital kubwa kiasi ambacho hawawezi danganya na wameonyesha jinsi walivyo wafikia watu wa hali na jinsi zote.

Wametoa matangazo kwenye media, wameenda kuwafuata watu katika makundi mbalimbali na kuwaita katika mabaraza yao mnataka takwimu gani yenye diversity kiasi cha hicho walichokifanya?
 
Back
Top Bottom