Huyu mama sijui na yeye amekua CCM masalia ametoka CCM asili (CCM ya Nyerere). wakati wa CCm ya Nyerere lazima uwe kichwa na sio ya sasa unatakiwa uwe na kichwa cha Nazi. Kinachonishangaza kwa huyu mama anasema sample ya Warioba Haikuwa stratified sio kweli. Kwanza Tume ilipokea maoni kutoka kwenye general public (huku kada zote walikuwepo) pili tume ilipokea maoni kutoka kwa makundi maalumu (wanasheria, wanataaluma, wanasiasa, viongozi wastaafu, viongozi wa dini, makundi ya walemavu vijana, mawaziri, n.k). Pia ieleweke wasomi wengi hawakupata nafasi ya kutoa maoni yao kwa kusema bali wengi waliandika email na machapisho mbali mbali na kuwakilisha tume. Tukisema kati ya 722,000 waliotoa maoni 10% (70,000) yao ni makundi maalum na kati yao waliozungumzia katiba ni 10% (7,000) na kati yao waliotaka muundo waserikali tatu ni 25% (1,750) je hawa si wengi kuliko bunge la katiba. Note nimetumia (10%) ambayo ni ndogo kuliko ilivyo kwenye vielelezo vya katiba kuhusu suala la Muungano na muundo wa serikali. Mama Tibaijuka sio kweli stratified sampling method haikutumika nilivyoonesha hapo juu hivyo hoja yako haina mashiko watu mia nne kasoro (maana ni 600 - wapinzani + baadhi ya 201) muone hoja za watu 17,000 hazifai