Hapo naona Prof. Tibaijuka kateleza au hakuelewa alichokizungumza. Anaposema Kafulila hakuwa sahihi alipokuwa anazungumzia kuhusu "samples" kuwa alichokisema kafulila siyo "stratified sampling" wala "non-stratified sampling". Napata tabu kidogo juu ya alivyojichanganya Prof.
Msingi wa hoja yangu ni kama ifuatavyo;
Ikumbukwe kuwa Sampuli Sample inaweza kuwa wakilishi au isiwe wakilishi kutokana na target area of interest, say population ya watu, wadudu etc.
Sampuli isiyo wakilishi :
Mfano, Kipima joto (ITV), let say kuwa umewahoji watu 4, then kati ya hao wawili wakasema ndiyo na wawili wakasema hapana. Kwa aina hii ya sampuli huwezi sema(Ku-generalize) kuwa asilimia 50 ya watanzania/ wakazi wa Dar wamesema ndiyo. Bali utasema asilimia 50 ya watu WALIOHOJIWA wamesema ndiyo, na asilimia iliyobaki wamesema hapana.
Sampuli wakilishi:
Kimsingi, hii hufanyiwa mahesabu kutokana na ukubwa wa population yako, hapa namaanisha kwamba ni lazima kwanza ujue ukubwa (size) wa population of interest from which the sample is drawn, then yanafanyika mahesabu ambayo kwayo unapata namba ambayo ni ndogo kuliko ukubwa wa population yako LAKINI ni namba ambayo ni wakilishi na hapo ndipo unapoweza kufanya GENERALIZATION.
Sasa basi, ili kupata sampuli ambayo ni wakilishi au isiyo wakilishi kuna aina mbali mbali za sampling ambazo ni, Simple random sampling (SRS), Systematic sampling, Stratified sampling, Cluster sampling, Multi stage sampling (ambayo ni muunganiko wa kuanzia aina mbili za sampling).
Kwa maana ya aina za sampuli nilizozielezea hapo juu na kwa maana ya alichokisema Prof. Tibaijuka, ni kuwa "non-stratified sampling" ni aina nyingine za sampling kwa maana ya SRS, Systematic sampling, Cluster sampling na Multi stage sampling na siyo stratified sampling
Kwa kifupi unapozungumzia "stratified sampling" ni aina ya sampuli ambayo unaifanya kiasi kwamba elements zake zinakuwa zimegawanywa kimakundi ambapo element katika ndani ya kundi moja zinakuwa hazifanani/tofauti na elements ndani ya kundi jingine. Mfano: kundi la wavulana pekee yao, na kundi jingine la wasichana peke yao, au watu wa vijijini kundi moja na watu wa mijini kundi lao/jingine.
Itakumbukwa kuwa Tume ya Warioba walizunguka nchi nzima, ambapo watu wa mkoa mmoja unaweza sema ni kundi moja, na watu wa mkoa mwingine ni kundi jingine na kadhalika. So kwa maana hiyo hiyo watu waliotoa maoni wanaweza wakawa stratified KI-MIKOA.
Ukija kwenye muundo wa wajumbe 201 wa Bunge la Katiba waliochaguliwa, wajumbe hawa wanaweza wakawa stratified kwa makundi wanayowawakilisha. Mfano kundi la wafugaji, kundi la walemavu, kundi la waganga wa jadi, kundi la vyama vya siasa, wawakilishi wa madhehebu etc. Hawa wote ni Stratified sampling.
Ukija kwa wajumbe waliosalia ambao ni wabunge wa Bunge la Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, kimsingi hawa walichaguliwa na wananchi lakini hawa nao pia unaweza kuwa Statify kimikoa wanayotoka, mfano wabunge wote wa kutokea mkoa wa Iringa watakuwa kundi moja, wa mkoa wa Mara watakuwa kundi jningine etc, hivyo hawa wote nao ni Stratified.
Kwa ujumla alichoongea Kafulila ni aina Stratified Sampling.
Hoja aliyoisema Prof. Tibaijuka kuwa Tume ilikuwa inawahoji watu wa aina yoyote waliojitokeza mbele yao hivyo haikuwa inapanga iwafikie watu wa aina gani haina mashiko, kwa sababu hao wote waliojitokeza mbele ya tume ni watanzania haijalishi wapo vipi. Hii ni sawa na jinsi wajumbe 201 walivyochaguliwa, haijalishi ni wa umri upi, au wawe wamesomea kutunga katiba, au wawe na kimo cha futi fulani etc, cha msingi ni watanzania.
Swali ambalo Prof angohoji ni kama idadi ya watu (sampuli) waliohojiwa na Tume ya Warioba ni wakilishi kwa watanzania wote? Na je sampuli ya wajumbe 601 ni wakilishi kwa watanzania wote? Na sio kusema ni Stratified au Non stratified!
Karibuni kwa mjadala.