Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Kitu muhimu cha kukumbuka ni kua wabunge tumewatuma bungeni kutetea haki zetu na sio kwenda kubishana kuhusu posho zao. Ndugu Zitto inadhaniwa kua umefika mbali kidogo, kosa alilofanya muheshimiwa halionekani kua anatakiwa kujiunzulu ispokua anaweza kuwekwa sawa tu. Kosa sio kosa kosa ni kurudia kosa
 
Najiaandaaa kuelekea mkoani kwa ajili ya kutimiza majukumu ya kikazi,bahasha kubwa iko tayari hapa mezani kwangu,naambiwa niende kwa mhasibu kusaini upokeaji wa posho na masurufu mengine.Nimekataa kuchukua posho hii,mwajiri ananiona kama kichaa vile,ana wasiwasi kazi minayoenda kuifanya haitafanyika,namwakikishia niko makini,naendelea kumweleza hapa nilipo ndo sehemu ya kuonesha uzalendo,na siku nikishika ofisi ya umma,utakuwa mwendo mdundo.Sitaki posho!!!

Hapo kwenye red mimi nina wasiwasi. Usije kukataa na posho za kujikimu ukafika huko safarini ukakwama na kutafuta 'njia mbadala'. Wenzio wanatenganisha posho, kwanza wanakubali zile za kujikimu, ndipo wanakataa zile za vikao. Wewe hujatenganisha nini unakataa na kipi unakubali. Je, utaziacha hapo hapo kwa cashier au utaelekeza zipelekwe kwenye taasisi yako binafsi?
 
"............Vijana tunasema ni lazima mtashinda lengo lengo lenu la ujamaa lazima mtashinda................"
 
Kwa wafuatiliaji wa siasa za Tz tunaufahamu vizuri msimamo wa Dr(PhD). Slaa. Amekuwa mtu wa kwanza kulalamikia ukubwa wa malipo na posho za wabunge tangu akiwa Mbunge. It is very clear kwamba hakubaliani na hizo posho.
kwa nini alikuwa akizipokea siku zote? mbona hata sasa hivi nasikia analipwa mamilioni ya hela za kodi zetu bila hata ya kukatwa kodi?
siungi mkono suala la posho hasa zisizo za lazima kama siting allowances za wabunge etc.
 
Hapo kwenye red mimi nina wasiwasi. Usije kukataa na posho za kujikimu ukafika huko safarini ukakwama na kutafuta 'njia mbadala'. Wenzio wanatenganisha posho, kwanza wanakubali zile za kujikimu, ndipo wanakataa zile za vikao. Wewe hujatenganisha nini unakataa na kipi unakubali. Je, utaziacha hapo hapo kwa cashier au utaelekeza zipelekwe kwenye taasisi yako binafsi?

Nimeelekeza waongezewe mishahara wafanyakazi wa chini.
 
Labda ingekuwa lugha ya kichangga hapo sina ujanja, kiingereza ata mbwa wangu nyumbani anajua, wewe ndio acha ushabiki kwa hiyo mpaka sasa bado utaki kukubali kama wabunge wako kina Mbowe wamekopa benki, labda nikuulize kwa nini Ofisi ya katibu wa bunge imewadhamini kwenye benki?

Acha ushabiki
 
Haya bana, wasaidie wapo wenye shida wengi, huenda MUNGU akakukumbuka hata katika ufalme wake.
 
Inawezekana watu walikopa au walitumia mtaji mkubwa wa fedha zao ili kufanikisha kuupata ubunge, hivyo wanaamini bila posho hawawezi kurudisha mtaji waliotumia
 
ritz ana akili za kiNepi Nepi, bila shaka ni 'Nepi Nayeye'
 
serekali inawapa fedha. wizara inapewa bajeti. katoliki wamevunga mkataba na gov. mapesa za wazungu. afya hospital zimeguzwa za wilaya. huu ni utap[eli tu kufutiwa kodi

Ruzuku inayotolewa na serikali kwa hospitali hizi si kwa ajili ya ujenzi, hizi hospitali zinakuwa zimeshajengwa, ila serikali inachangua gharama za huduma na kuhudumia watumishi wake iliowapeleka huku kusaidia kwa kuwa yenyewe imeshindwa kujenga hospitali zake za wilaya na rufaa...Ndo zile zinaitwa teule... Mfano Bunda, Rubya, Biharamulo, Bombo, KCMC, Bugando nk. Wanaolalamikia suala hili (watazamani) ni wale ambao ama madhehebu yao au yale wanayoshabikia yameshindwa kujenga hospitali ambazo serikali inaweza kusapoti.
 
Usikimbilie kutoa matusi kabla ya kujiuliza kwanini fedha hizo walizokopa kopa na wanazoendellea kukopa hawazipeleki majimboni kwao ilkwahayo waharakishe maendeleo? au fedha hizo wanakwenda kufanyia nini isipokuwa kujilimbikizia mali? if that yhe case,huruma kwa wananchi hapo uko wapui isipokuwa unafiki? hayo ndiyo maswali ya kujiuliza kabla ya hoja zako za nguvu.
 
Najiaandaaa kuelekea mkoani kwa ajili ya kutimiza majukumu ya kikazi,bahasha kubwa iko tayari hapa mezani kwangu,naambiwa niende kwa mhasibu kusaini upokeaji wa posho na masurufu mengine.Nimekataa kuchukua posho hii,mwajiri ananiona kama kichaa vile,ana wasiwasi kazi minayoenda kuifanya haitafanyika,namwakikishia niko makini,naendelea kumweleza hapa nilipo ndo sehemu ya kuonesha uzalendo,na siku nikishika ofisi ya umma,utakuwa mwendo mdundo.Sitaki posho!!!

Hongera. Huko utajikimu vipi? Au na huko unapewa posho kwa hiyo umekataa ya ofisini ili ukachukue ya huko. Naona wewe umekataa posho mbili!!
 
Hongera Zitto. Wapenda haki na watetezi wa wanyonge wanakuombea kwa Mwenyenzi Mungu. Hivyo vita ni vikubwa na wanaoguswa wako samaki wakubwa, sasa je umejipanga kiasi cha kuwashinda kwa hoja kwani wao wana nguvu ya dola? Vile vile ndani ya chama chenu, je hakuna wasaliti? Jipe moyo mkuu nguvu ya uma iko juu.
 
Sichochei wala sina mtimanyongo na mtu yeyote. Sipingi posho za vikao kuondolewa kwa wabunge na wafanyakazi wengine wa serikali. Ila sasa kusema kweli wafanyakazi wengi wa serikali wananufaika sana na hizi posho za vikao. Kuna viongozi (wakubwa), kuna wahudumu na kuna wataalamu (sekretariat) wote hawa kukiwa na vikao nao wanapata posho kusupliment mishahara yao. Pia kuna meal allowance na extra duty (siyo overtime) allowance; sijui kuna mtu anajua zinalipwalipwaje. Wafanyakazi kwa sasa wana chuki na mtu aliyeanzisha hili suala kabla ya kuhakikisha kuwa mishahara yao inapanda kabla ya kuondoa posho za vikao ambazo wanasema huenda zikafuatiwa na kuondolewa kwa posho zingine kama meal allowance na extra duty allowance.
 
wamesema ni posho zisizo za lazima tuuuuuuuuuuuu........

utakuwa umetumwa na wanamagamba!!!!

[h=3]Askofu KKKT ajitosa mjadala wa posho[/h]
*Ataka wabunge wanaozikataa waungwe mkono
*Mbowe azifananisha na wizi wa kutisha


Na Martha Fataely, Hai

ASKOFU wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi Kaskazini, Dkt. Martin Shao, ameunga mkono hoja ya
wanaotaka kufutwa kwa posho zisizokuwa za msingi kwa watumishi wote wa umma na wabunge kwa maslahi ya taifa.

Msimamo huo ulitolewa mjini hapa juzi ikiwa ni siku chache tangu Kambi ya Upinzani Bungeni iwasilishe mapendekezo ya kutaka posho zisizo za lazima kwa watumishi na wabunge ziondolewe kwa kuwa ni mzigo kwa taifa.

Asjkofu Shao alitangaza msimamo huo wakati wa mahafali ya 40 ya Chuo cha Uganga Machame kinachomilikiwa na kanisa hilo, ambapo wanafunzi 48 walihitimu masomo ya stashahada ya utabibu.

Alisema hoja hiyo ni ya msingi hasa kwa kuzingatia kuwa Tanzania ni nchi maskini, ambayo inahitaji uangalizi wa fedha, na siyo kila mmoja kuangalia maslahi yake binafsi.

"Taifa limekuwa likikumbwa na matukio ya wizi, ubadhirifu na ufisadi wa kutisha, hivyo wanapotokea watu wachache ambao wanaonekana kutafuta kupunguza matumizi yasiyo ya lazima, sisi kama taifa tunapaswa kuwaunga mkono na kukemea pale inapobidi," alisema Askofu Shao na kuongeza kuwa;

"Nchi hii kuna uozo wa watu kuangalia maslahi yao, yaani wao kwanza, tabia hii twapaswa kuiepuka, kila mtu asiangalie mambo yake mwenyewe, bali aangalie na ya wengine," alisema.

Kwa mujibu wa askofu huyo, baadhi ya watumishi wamekuwa wakilipwa posho ambazo zingeweza kusaidia kuboresha huduma za afya kwa kuwapa motisha wale wanaofanyakazi katika mazingira magumu ili wananchi wanaoishi katika maeneo hayo waweze kupata huduma bora.

Alisema ni vyema kwa serikali kuona umuhimu wa kubadili sera hizo ili kuwawezesha watumishi wake kuongezewa mishahara na kupata kipato kutokana na mishahara yao halali na siyo kujilundikia posho.

Askofu Shao alitoa mwito kwa serikali kuona umuhimu wa kuboresha huduma maeneo ya vijijini, hasa kwa upande wa sekta ya afya na kutilia mkazo utaratibu wa kuwapangia vituo vya kazi wataalamu kuanzia ngazi ya zahanati, vituo vya afya na hospitali

Alisema zaidi ya asilimia 80 ya wakazi nchini wanaishi vijijini na hukumbwa na tatizo la upungufu wa huduma hizo, lakini serikali imekuwa ikitoa asilimia 60 ya huduma hizo huku ikichangiwa na mashirika ya dini kwa asilimia 40.

Dk. Shao alisema kanisa limekuwa likijikita zaidi kutoa huduma hizo vijijini, hivyo serikali inapaswa kuunga mkono jitihada hizo kwa lengo kuwaondolea wananchi kero ya kutumia gharama kubwa kupata matibabu.

Awali, akizungumza wakati wa mahafali hayo, Mbunge wa Jimbo la Hai, Bw. Freeman Mbowe alielezea masikitiko yake juu ya taarifa mbalimbali zinazotolewa na vyombo vya habari zikipotosha ukweli wa suala la posho.

Bw. Mbowe alisema anashangazwa na vyombo vya habari kuripoti kuwa ugomvi wa posho ni miongoni mwa wabunge, jambo ambalo alisema siyo kweli, kwani wamekuwa wakipinga posho zisizokuwa na umuhimu kwa watumishi wa kada za manejimeti na wabunge.

Alisema kambi ya upinzani imekuwa ikipinga posho nyingi zinazotolewa au kuchukuliwa na baadhi ya watumishi wa kada za juu ambao kwa siku huweza kuandikiwa au kujiandikia posho zaidi ya mara tatu.

"Jamani nilichokuwa napinga ni hiki, unakuta mbunge analipwa posho ya kujikimu yaani malazi, chakula na mawasiliano sh. 80,000, hii hatuna ugomvi nayo, lakini akihudhuria bungeni hata kama anaumwa yaani hatakaa siku nzima, analipwa pesa ya kukaa sh. 70,000, jamani huu ni wizi wa kutisha," alisema Bw. Mbowe.

Alisema kwa upande wa menejimenti za utumishi wa umma, pia kuna posho zisizohesabika kwani kila mwezi hujikuta wanalipwa mshahara sh. milioni moja na posho sh. milioni tano. - NI UKWELI KABISA

"Watu ambao wamekuwa wakifaidi posho hizi ni wale mawaziri, makatibu wakuu, wakurugenzi, wakuu wa idara lakini wale wafanyakazi wa kawaida wala hawapati chochote na ndiyo maana kunakuwa na tofauti kubwa kati ya walionacho na wale wasiokuwa nacho ilihali wote wanalipwa mshahara," alisema.- NA HIZI POST NI KWA AJILI YA WANAMAGAMBA TUUUUU

"Unakuta mtu haonekani ofisini, kazi yake ni kuvizia vikao vya posho, anaingia cha kwanza anasaini na kuondoka, vile vile kama ni ofisa elimu anakwenda kukagua miradi ya elimu analipwa posho na wakati huo ametumia gari la serikali lenye mafuta lakini pia mshahara upo pale pale," alisema.

Bw. Mbowe aliwataka Watanzania kuwaombea kwa kukataa posho kwani kuna hatari ya wao kutolewa roho, kwa kuwa wamegusa maslahi ya wakubwa zaidi. Hata hivyo alisema hawahofii hilo.

Alisema matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi ni makubwa. Alitoa mfano akisema wabunge wanapotaka kusafiri badala ya kutumia usafiri wenye nafuu kwa manufaa ya taifa, wanatumia gharama kubwa bila msingi.

"Kwa mfano, ukishakuwa mbunge tu ujue umeula, kwani kwenye ndege ukipanda unakaa First Class (daraja la kwanza) kwenda Marekani nauli yake ni dola 8,000 (sh milioni 12) wakati ndege hiyo hiyo, ina vipengele vya Business Class dola 5,000 (sh milioni 7.5) na Economy Class sh. milioni 1.8, haya ni matumizi mabaya," alisema.

Alisema kutokana na hali ya umaskini hapa nchini viongozi wanapaswa kuona umuhimu wa kupunguza matumizi yasiyokuwa ya lazima ili kutatua kero mbalimbali zinazowakabili wananchi wake. WEWE UNASEMAJE??

Awali Kaimu Mkurugenzi wa Hospitali ya Machame, Dkt. Elisinya Masawe aliwashukuru washirika wa maendeleo wa hospitali hiyo kutoa shirika la Alegent Health la Marekani hususani mwakilishi wake, Bw. Robert Cassworn kwa moyo wa kujitolea kuisadia hospitali hiyo.
 
Hivi huyu editor wa DN anataka kunihakikishia kuwa kwa hii posho ninayopata ofisini kwangu ninaweza kupata mkopo! Wahariri wengine ni majuha sana, mwanahabari anapaswa kujiridhisha na kila anachotaka kukichapa (hasa kama anatoka katika gazeti makini), yaani ameshindwa kutofautisha posho na mshahara ambao ki mantiki unaweza kumfanya mbunge kupata mkopo. DN task ya head guyz and not ya tummies
 
itawachukua mda kuelewa mantiki ya kufuta hizo posho. naamini CCM wataitumia hiyo km nguzo yao ya kutetea posho.
 
Tumekwishaaa watz! kwa hili sioni uhalali wa CCM kuwepo Tz, yani mi sioni umhimu wa kuwaacha waishi dunia hii, yani wapo pale kutetea na kuunga hoja mkono suala la kumuibia mtu mnyonge na maskini wa Tz, Shame on you CCem, vionee! nyoooooo! yan nina hasira. Shangingi moja ni sawa na Zahanati mbili nzuri tena zenye ubora! jamani.
 
Kweleakwelea mimi siwezi kutumwa na mtu yeyote najituma mimi mwenyewe na nasema ambacho nikiona na kukisikia. Unaona sasa hapo kwenye post yako yanongelewa mambo mengi ikiwepo usafiri wa ndege. Kwa hiyo suala la posho linatakiwa liangaliwe kwa ujumla wake. Nakuambia zaidi ya posho za vikao kuna meal allowance na extra duty allowance; hizi zina umuhimu gani? Ukiziondoa hizi bila kuongeza mishahara kwa wafanyakazi wa serikali utaelewana nao kweli? Najua posho ni zinalipwa kwa discretion ya mwajiri na siyo statutory kama ulivyo mshahara na posho hazichangii kwenye terminal benefits. Hapa wafanyakazi wana enjoy posho lakini uzeeni kiinua migongo hakitakuwa kizuri. Tatizo ni kwamba ukizigusa bila kuongeza mishahara yao kweli nakuambia wafanyakazi wa serikali watakuchukia. Nimewasikia wenyewe wakisema siyo wawili wala watatu ni makumi!
 
Back
Top Bottom