Ndugu raia Fulani, sisi wananchi tuliowachagua Wabunge (Waheshimiwa) ndio Wadharauliwa, hujabaini hili ndugu. Kama kweli hawatudharau wanafanya nini cha maana ili kutusaidia sisi???? Toka Bunge la kwanza hadi leo hakuna juhudi za waziwazi kumsaidia Mdharauliwa. Kama hawatudharau unafikiri kungekua na kauli kama "Hata mkila nyasi, Ndege ya Rais itanunuliwa." Leo umeleta hoja ya kulifuta jina la Mh. ambalo kimsingi lina wakweza bila sababu ya Msingi na kutufanya tulivae jila la Wadharauliwa. Ila mimi pia na leta hoja ya Kulifuta jina La Bunge TUKUFU. Lile Bunge letu lina UTUKUFU gani au labada mimi mafikirio yangu ni duni (ntakubali hili) kama kuna Mtu humu ndani na nje ya Jukwaa, atakapo kuja na kujaribu kuniaminisha UTUKUFU wa bunge letu. Sina uhakika, japo kuwa nilisha acha na kufuta imani yangu kwa dini za Kigeni, ila kama neno UTUKUFU, litaacha kama lilivyo then, ntaingiwa na mashaka makubwa sana na watu wanaohusishwa na neno hilo.