Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Wabunge na viongozi wa serikali huitana waheshimiwa, hivyo kutulazimu kuwaita hivyo. Ni waheshimiwa kwa lipi? Kuna tofauti gani kati ya raia huyo aliyekuwa anagombea ubunge mwaka jana na mwaka huu yupo mjengoni (kariakoo)? Ana kipya kipi cha kumzidi yule ambaye aligombea nae ama yule raia aliyempigia kura? Au ni hizo posho na hiyo mikopo na mishahara minono? Hakuna tofauti. Ifike muda sasa wabunge na viongozi serikalini, pawe na sera ya kuitana NDUGU
 
big up ndugu, kumbuka juzijuzi kuna mwanajamii mmoja alisema kuwa, kama kuna WAHESHIMIWA basi automatically kuna WADHARAULIWA
ni jambo la msingi na hilo
 
Ni kweli ndugu,hata mimi hapa jf nshaanza zamani,huwa ktk post zangu natumia neno ndugu,kwa kuwa linabeba uzito stahiki. Ueshimiwa upo kwa kila raia,si mpaka uwe mbunge ndo ueshimiwe! Nlishawai kumshangaa mbunge bungen 2007 akipinga eti mtu asiye mbunge asiitwe mheshimiwa! Ajabt wabunge wetu wanapenda kutukuzwa!
 
Neno ndugu lina uzito sana, na kama alivyosema, ndugu hapo juu, mheshimiwa kinyume chake ni mdharauliwa. Nani mdharauliwa sasa?
 
Raia Fulani umenena, enzi za Mwalimu (watanzania wote tulikuwa sawa sawa) tuliitana 'Ndugu'. Neno mheshimiwa ilikuwa mahakamani tu.
 
Neno ndugu lina uzito sana, na kama alivyosema, ndugu hapo juu, mheshimiwa kinyume chake ni mdharauliwa. Nani mdharauliwa sasa?
Huyohuyo Mheshimiwa akienda wrong anakuwa mdharauliwa
 
Umenifurahisha ndugu,kwa mfano pale Marekani rais anaitwa Mr.President,sasa sijuhi huku J.K atachukuliaje akiitwa hivyo? Mbona Baba wa Taifa aliitwa hivyo na alipenda kuitwa 'Ndugu' ...tatizo ni kwa hawa viongozi masrahi
 
its a total package ( compulsory posho + uheshimiwa na mazagazaga yake) huwezi kukataa kuitwa mheshimiwa.Hata ukikataa wananchi wanalazimika kukuita hivyo - ( agizo la kikatiba?)
 
tunataka katiba mpya itakayoweka usawa kati ya mpiga kura na kiongozi, kuwaita waheshimiwa kunaweka madaraja kati ya watawala na watawaliwa, ng wanapofanya madudu uheshimiwa unakuwa kinga ya kuwadiscipline. pumbavu zao
 
Duh! Its a compulsory to be called muheshimiwa. Ukikataa unapewa adhabu
 
Kuitana mhe.au ndugu ina tija gani kwa taifa?

Kuitana ndugu kuna umuhimu kwasababu dhana ya usawa itachukua mkondo wake. Hatutabaguana, hatutachukiana, hatutatendeana matendo mabaya hivyo tutakua na uzalendo na utaifa zaidi.

Lakini sasa hivi kwasababu kuna waheshimiwa na wadharauliwa, mheshimiwa akifisidi basi sie tuseme tuu hewala bawana ...
 
Sio suala la kupunguza ufisadi ni kuleta heshima kwa kila binadamu.Utu wa mtu haupimwi kwa cheo alichonacho. ndio maana ni vizuri tuitane ndugu kwa heshima ya utu wetu
 
Kuitana mhe.au ndugu ina tija gani kwa taifa?
haina tija yeyote ila ni namna moja ya kujipendekeza kwa wapenda mijisifa ubwanyenye,etc.Muheshimiwa,baron,mustahiki,earl,first lady,prince,sahib,sultan,lord,sir, monsieur,count,duke,baroness,etc are social titles.Napoleon Bonaparte once said men adore titles(hata kama kimsingi haina tija).kujumuisha napendekeza honorific titles kwa viongozi wetu upinzani.Sijui hii imekaa vipi?Grand Duke SlaaEarl of kigoma Zitto Kabwe.Baroness Halima MdeeCount LissuEsquire Lyatonga Mrema. Unakumbuka titleLast king Scotland,conquerer of British Empire ?
 
big up ndugu, kumbuka juzijuzi kuna mwanajamii mmoja alisema kuwa, kama kuna WAHESHIMIWA basi automatically kuna WADHARAULIWA
ni jambo la msingi na hilo

Kuitana "Ndugu" imetulia na huu ndo utamaduni wa Mwafrika, kuitana "Mheshimiwa na Mtukufu", ni utamaduni wa waarabu na wazungu wa enzi hizo za utumwa na ukoloni! Hawa wanao ng'ang'ania kuitwa waheshimiwa ni "makoloni meusi" sawa na makaburu tu!
 
UNACHOKIZUNGUMZA KINA UKWELI,
NAKUMBUKA WAKATI WA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA KWANZA NA AWAMU YA PILI MARAIS WALIKUWA WANAITWA
'WATUKUFU':bange:
LAKINI ALIPOKUJA KAKA BENI AKAKATAA KUITWA MTUKUFU NDIPO LIKAANZA
'MHESHIMIWA' :israel:

KWA UPANDE WA RAIS.
HIVYO HATA KWA WABUNGE INAWEZEKANA TU, MBONA KWA RAIS IMEWEZAKANA?
NA IWE HIVYO
 
Back
Top Bottom