Posho na Mishahara ya wabunge...

Posho na Mishahara ya wabunge...

Utasikia Mheshimiwa mchungaji Dr. Flani...kupotezeana muda tu, nakumbuka mbunge Lucas Selelii ye alikuwa anapenda kutumia "Mheshimiwa bwana spika.."
 
Aulizwe AHM raisi pandikizi toka jirani, yeye ndiye alibadilisha kanuni yetu ya kuitana ndugu. Alianzisha waheshimiwa na yeye alikuwa juu ya waheshimiwa, aliitwa MTUKUFU raisi wa JMT. Ndo athali za kuendekeza uswahili na umwinyi yaani kujipa misifa kwa mbele sana
 
Jana tulifanikiwa kunasa taarifa za uzushi/uongo zinazopikwa pale magogoni chini ya uratibu wa rais Kikwete na vipemba wake kwa ajili ya kuhujumu juhudi za wanamageuzi wa cdm za kupambana na ufisadi hasa suala la posho,bahati nzuri wahariri wengi wameanza kufunguka kutoka ktk mkono wa chuma ccm hawakuiandika habari hiyo! Chakushangaza nikuwa mhariri wa habari leo kaitoa tena front page!

Haya ni maajabu taaluma imekwenda likizo na ubambucha umechukua nafasi yake, hii ni hatari katika dunia ya dot com!!
 
Pia hii salamu shikamoo ina utata mtupu. Maana yake halisi nakushika mguu na hilo ni jambo la kiutumwa halikubaliki enzi ya dotcom. Pili inabidi ukisie umri wa msalimiwa,amekuzidi ua mdogo wako.Ukikosea tu ushazuwa balaa .
 
Wabunge na viongozi wa serikali huitana waheshimiwa, hivyo kutulazimu kuwaita hivyo. Ni waheshimiwa kwa lipi? Kuna tofauti gani kati ya raia huyo aliyekuwa anagombea ubunge mwaka jana na mwaka huu yupo mjengoni (kariakoo)? Ana kipya kipi cha kumzidi yule ambaye aligombea nae ama yule raia aliyempigia kura? Au ni hizo posho na hiyo mikopo na mishahara minono? Hakuna tofauti. Ifike muda sasa wabunge na viongozi serikalini, pawe na sera ya kuitana NDUGU

Anne M'kinda amesema pale ni kariakoo. KAA LIA KOO, kwa koo lake anakula. Hana jipya.
 
acha wajikaange wenyewe kwa mtu mwenye busara ashajua mwisho wa sumu ya nyoka umewadia.wananchi wa leo sii wale wa kudanganywa tena.viva wanamageuziii..
 
ikishindikana kabisa kuondoa posho, CDM wachukue posho lakini zisinufaishe familia zao waanzishe clubs shule za msingi,sekondari na vyuoni kushughulikia matatizo yanayokabili makundi haya na ipendekeze cku ya jumapili au jumamosi kama siku ya kukutana na kupeana changamoto za kielimu kwa kuwashindanisha kwa mitihani na kuwafundisha haki za binnadamu,mwanafunzi;kisiasa kwa kuwajengea uwezo wa kujenga hoja na kutetea,michezo kwa kurefresh
 
Ok wazo zuri tuuuu.................wasirudi nyuma wawaache wazee wa magamba wakimung'unya maneno na kufikiria tu jinsi ya kuliibia taifa hili masikini la akili lakini tajiri la rasilimali
 
ikishindikana kabisa kuondoa posho, CDM wachukue posho lakini zisinufaishe familia zao waanzishe clubs shule za msingi,sekondari na vyuoni kushughulikia matatizo yanayokabili makundi haya
Tuanze na poso ya katibu mkuu wetu.
 
*****&&&&&%%%%$$$$########## zao..................napata hasira sana mimi jamani
 
Hakyanani wewe kama ni kijana basi ukiwa mzee lazima utakuwa mwanga hivi hizo posho ndo limekuwa jambo la kushangaza sana au? Isije ikawa janja ya magamba hasa wewe ulieleta hii thread kutusahaulisha mambo yenye maana na kung'ang'ania posho posho kila kukicha upuuzi mtupu.kuwa bwana acha ujinga wewe.leta mambo mapya acha utoto.Hivi unajua mitambo ya symbion pale ubungo huwa inalipiwa na serekel kodi ya pango kiasi cha sh 50 milion kwa siku na bado uzalishaji haujaanza??
 
Tuanze na poso ya katibu mkuu wetu.
ccm haimpi mtu cheo kupitia JF kwa kutetea upuuzi ila endelea na jitihada za kutetea yawezekana nape akakuona ukamsaidia kutetea ulaji wa kundi flani
 
Chadema kweli kama wapo makini kwenye hili swala la posho, ni vizuri wangeanzia Ndani ya chama chao, waanze na A loser Dk Slaa, nadhani huwo utakuwa mfano mzuri kwa jamii yetu watanzania
 
ccm haimpi mtu cheo kupitia JF kwa kutetea upuuzi ila endelea na jitihada za kutetea yawezekana nape akakuona ukamsaidia kutetea ulaji wa kundi flani
Mbona hiyo posho ya katibu mkuu unaitetea sana?? Au unaona ni sahii yeye kuipata?
 
Back
Top Bottom