Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,502
- 113,610
Wanabodi
Huu ni wito kwa Katibu Mwenezi mpya wa CCM, Comred Paul Makonda, kwanza kwa kumpongeza kwa kuifufua hamasa ya CCM kupendwa upya na kukubalika sana kupitia amsha amsha zake za Magufuli type (populist na populism) kila anapopita, tatizo lake ni moja tuu, anaipiga hii ngoma kwa nguvu mno, hivyo kuirindimisha kwa mlio mkubwa sana. Tatizo la ngoma inayovuma, ni ukiisikia ngoma inavuma sana, ujue inakaribia kupasuka!. Ili twende salama na kufika salama 2025, sisi watu wenye jicho la tatu, tunampa ushauri wa bure Mwenezi Makonda, twende taratibu mdogo mdogo ili tufike salama, kwa speed aliyoanza nayo, kama ataendelea kwa kasi hii, asije kushangaa hii ngoma ikampasukia njiani kabla hatujafika safari yetu!.
Rule No. 1. Never Outshine Your Boss
Mwenezi hawezi kumuagiza Waziri Mkuu na kuonya mawaziri, kwa kuwapa ultimatums!. Makonda aishie kwenye kusisitiza utekelezaji tuu wa ilani, na sio kutoa amri kuwaamuru na kuwaamrisha mawaziri!. Makonda hawezi kum summon Waziri Mkuu au mawaziri kwasababu yeye sio mamlaka yao ya uteuzi wala ya nidhamu. Mawaziri hawawajibiki kwa chama, wanawajibika kwa rais. iwapo kuna Waziri yoyote hajatekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM kikamilifu, chama kinamshitaki kwa rais ndie mamlaka pekee inayoweza kuwa summon na sio Mwenezi!. Waziri Mkuu wa JMT hawezi kupewa maelekezo ya chama na mwenezi kwasababu PM ni mjumbe wa CC ya CCM. Huwezi kuwapigia simu mawaziri na kuwapa maelekezo kwasababu wewe sio rais wa JMT. Magufuli alikuwa anafanya hivyo kwasababu yeye ndio bosi wao!, Makonda asijifanye Magufuli!, huku ni kumu outshine his boss!.
Enzi za Nyerere na Mwinyi, mfumo wa utawala wa taifa letu ulikuwa ni mfumo wa Party Supremacy, ambapo chama ndio kulikuwa kimeshika hatamu kuongoza serikali, hivyo viongozi wa serikali walikuwa na kofia mbili, wakuu wa mikoa ndio viongozi wa CCM wa mkoa na waliingia Bungeni. Kulikuwa mpaka kuna mkoa wa majeshi!, jeshi lilikuwa ni Idara ya chama na kulikuwa na ma kamisaa wa chama jeshini.
Mwaka 1992 tulipoingia mfumo wa vyama vingi, huo ndio ulikuwa mwisho wa party supremacy na kofia mbili, chama ni chama na serikali ni serikali, siasa ikaondolewa jeshini. Kofia mbili zilikuja kubaki kwa rais tuu wa JMT.
Tulianza mfumo wa Parliamentary Supremacy ambapo CCM kinatoa ilani ya uchaguzi kwa serikali kuitekeleza, Bunge ndio linaisimamia serikali.
Ufuatiliaji wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ndio kazi ya Mwenezi, lakini utaratibu wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa ilani ya CCM kwa serikali ni kwa mtindo wa "Eyes on Hands Off", kwa CCM kufuatia utekelezaji kwa eyes on, hivyo hiki anachokifanya Mwenezi Paul Makonda kufuatia utekelezaji wa ilani ndio kazi yake rasmi kwa kuona kwa macho na kuzungumza na wananchi, na watekelezaji wa ngazi ya chini, kuhusu kero zao mbalimbali.
Baada ya kuona na kusikia hatua za utekelezaji wa ilani, zinafuatiliwa kupitia vikao vya CCM kuanzia shina, tawi, kata, tarafa, wilaya, mkoa hadi taifa, mwenezi taifa anapaswa kupokea taarifa za waenezi wenzake toka chini, kuyaandika na kuyapeleka kwenye vikao vya rasmi vya chama kitataifa na kule ndipo chama kinajadili na kutoa maelekezo ambapo kazi ya Mwenezi ni kuyatangaza maamuzi na maelekezo ya chama kwa watendaji wa serikali na sio Mwenezi kutoa maagizo na ultimatum kwa watendaji wa serikali akiwemo Waziri Mkuu na mawaziri, hiyo sio jukumu la Mwenezi ni jukumu la mamlaka yao ya uteuzi na nidhamu ambayo ni Rais wa JMT.
Sehemu ambapo Konda Boy anajichanganya ni kwa vile Rais Samia ndie Mwenyekiti wa CCM, na yeye ndie msemaji wa CCM, anatoa maagizo kwa viongozi wa serikali, akiwemo Waziri Mkuu na mawaziri ikiwemo kuwapa ultimatums kutoka kwa Rais Samia kama Mwenyekiti wa CCM, wakati Rais Samia anaweza kutoa maelekezo na ultimatums kwa watendaji wa serikali kama Rais wa JMT na sio Mwenezi kuivaa kofia ya rais wa JMT na ku summons mawaziri na kuwapa ultimatums akiwemo Waziri Mkuu!. That is wrong!. Huku ni ku overstepping over and above mamlaka yake, ni Rais wa JMT pekee ndie mwenye uwezo to summon ministers na kutoa ultimatums kwa Waziri Mkuu and not anyone else!. Hata Bunge haliwezi kum summon Waziri Mkuu na kumpa ultimatums bali linaweza kufanya hivyo kwa serikali.
Konda Boy ana overdo bila kujua!. Asioverdo ngoma ikipigwa sana, huwaga haichelewi kupasuka!.
Wito huu ni kwa wanaomtakia mema Paul Makonda na ili kulithibitisha kuwa tunamtakia mema, angalia tumeanza nae wapi.
Mimi nilianza nae hapa Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
Nikaja hapa Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni
Alipopitia misukosuko tukasimama nae kwanza kwa kutoa wito Ndugu, Jamaa na Marafiki, Njooni Tumtetee Makonda Dhidi ya Mapapa Wauza Unga Wanaomzushia... kisha tukamshauri Kumbe ni Uongo, Uzushi, Fitna, Majungu, Wivu na Kijicho Dhidi ya Mafanikio Yake!. Makonda Wapuuze! .
Kuna watu wenye roho za kwanini tukawaambia Wale mnaosubiri kwa hamu Makonda atumbuliwe, mtasubiri sana!. Ukiwa ni mpakwa mafuta, ni mpakwa mafuta!
Na mwisho nikapendekeza Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze...
Hivyo mheshimiwa sana Mwenezi Makonda, twende taratibu mdogo mdogo, hii duniani ni tambara bovu, tembea nayo taratibu!.
Wish you all the best
Kakayo
Paskali
Huu ni wito kwa Katibu Mwenezi mpya wa CCM, Comred Paul Makonda, kwanza kwa kumpongeza kwa kuifufua hamasa ya CCM kupendwa upya na kukubalika sana kupitia amsha amsha zake za Magufuli type (populist na populism) kila anapopita, tatizo lake ni moja tuu, anaipiga hii ngoma kwa nguvu mno, hivyo kuirindimisha kwa mlio mkubwa sana. Tatizo la ngoma inayovuma, ni ukiisikia ngoma inavuma sana, ujue inakaribia kupasuka!. Ili twende salama na kufika salama 2025, sisi watu wenye jicho la tatu, tunampa ushauri wa bure Mwenezi Makonda, twende taratibu mdogo mdogo ili tufike salama, kwa speed aliyoanza nayo, kama ataendelea kwa kasi hii, asije kushangaa hii ngoma ikampasukia njiani kabla hatujafika safari yetu!.
Rule No. 1. Never Outshine Your Boss
Mwenezi hawezi kumuagiza Waziri Mkuu na kuonya mawaziri, kwa kuwapa ultimatums!. Makonda aishie kwenye kusisitiza utekelezaji tuu wa ilani, na sio kutoa amri kuwaamuru na kuwaamrisha mawaziri!. Makonda hawezi kum summon Waziri Mkuu au mawaziri kwasababu yeye sio mamlaka yao ya uteuzi wala ya nidhamu. Mawaziri hawawajibiki kwa chama, wanawajibika kwa rais. iwapo kuna Waziri yoyote hajatekeleza ilani ya uchaguzi ya CCM kikamilifu, chama kinamshitaki kwa rais ndie mamlaka pekee inayoweza kuwa summon na sio Mwenezi!. Waziri Mkuu wa JMT hawezi kupewa maelekezo ya chama na mwenezi kwasababu PM ni mjumbe wa CC ya CCM. Huwezi kuwapigia simu mawaziri na kuwapa maelekezo kwasababu wewe sio rais wa JMT. Magufuli alikuwa anafanya hivyo kwasababu yeye ndio bosi wao!, Makonda asijifanye Magufuli!, huku ni kumu outshine his boss!.
Enzi za Nyerere na Mwinyi, mfumo wa utawala wa taifa letu ulikuwa ni mfumo wa Party Supremacy, ambapo chama ndio kulikuwa kimeshika hatamu kuongoza serikali, hivyo viongozi wa serikali walikuwa na kofia mbili, wakuu wa mikoa ndio viongozi wa CCM wa mkoa na waliingia Bungeni. Kulikuwa mpaka kuna mkoa wa majeshi!, jeshi lilikuwa ni Idara ya chama na kulikuwa na ma kamisaa wa chama jeshini.
Mwaka 1992 tulipoingia mfumo wa vyama vingi, huo ndio ulikuwa mwisho wa party supremacy na kofia mbili, chama ni chama na serikali ni serikali, siasa ikaondolewa jeshini. Kofia mbili zilikuja kubaki kwa rais tuu wa JMT.
Tulianza mfumo wa Parliamentary Supremacy ambapo CCM kinatoa ilani ya uchaguzi kwa serikali kuitekeleza, Bunge ndio linaisimamia serikali.
Ufuatiliaji wa utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM ndio kazi ya Mwenezi, lakini utaratibu wa ufuatiliaji wa utekelezaji wa ilani ya CCM kwa serikali ni kwa mtindo wa "Eyes on Hands Off", kwa CCM kufuatia utekelezaji kwa eyes on, hivyo hiki anachokifanya Mwenezi Paul Makonda kufuatia utekelezaji wa ilani ndio kazi yake rasmi kwa kuona kwa macho na kuzungumza na wananchi, na watekelezaji wa ngazi ya chini, kuhusu kero zao mbalimbali.
Baada ya kuona na kusikia hatua za utekelezaji wa ilani, zinafuatiliwa kupitia vikao vya CCM kuanzia shina, tawi, kata, tarafa, wilaya, mkoa hadi taifa, mwenezi taifa anapaswa kupokea taarifa za waenezi wenzake toka chini, kuyaandika na kuyapeleka kwenye vikao vya rasmi vya chama kitataifa na kule ndipo chama kinajadili na kutoa maelekezo ambapo kazi ya Mwenezi ni kuyatangaza maamuzi na maelekezo ya chama kwa watendaji wa serikali na sio Mwenezi kutoa maagizo na ultimatum kwa watendaji wa serikali akiwemo Waziri Mkuu na mawaziri, hiyo sio jukumu la Mwenezi ni jukumu la mamlaka yao ya uteuzi na nidhamu ambayo ni Rais wa JMT.
Sehemu ambapo Konda Boy anajichanganya ni kwa vile Rais Samia ndie Mwenyekiti wa CCM, na yeye ndie msemaji wa CCM, anatoa maagizo kwa viongozi wa serikali, akiwemo Waziri Mkuu na mawaziri ikiwemo kuwapa ultimatums kutoka kwa Rais Samia kama Mwenyekiti wa CCM, wakati Rais Samia anaweza kutoa maelekezo na ultimatums kwa watendaji wa serikali kama Rais wa JMT na sio Mwenezi kuivaa kofia ya rais wa JMT na ku summons mawaziri na kuwapa ultimatums akiwemo Waziri Mkuu!. That is wrong!. Huku ni ku overstepping over and above mamlaka yake, ni Rais wa JMT pekee ndie mwenye uwezo to summon ministers na kutoa ultimatums kwa Waziri Mkuu and not anyone else!. Hata Bunge haliwezi kum summon Waziri Mkuu na kumpa ultimatums bali linaweza kufanya hivyo kwa serikali.
Konda Boy ana overdo bila kujua!. Asioverdo ngoma ikipigwa sana, huwaga haichelewi kupasuka!.
Wito huu ni kwa wanaomtakia mema Paul Makonda na ili kulithibitisha kuwa tunamtakia mema, angalia tumeanza nae wapi.
Mimi nilianza nae hapa Nimemkubali Sana DC Makonda, anafaa kuwa Mkuu wa Mkoa Dar es Salaam
Nikaja hapa Mafanikio ya Makonda ni Uthibitisho Wa Jiwe walilolikataa Waashi litafanywa kuwa Jiwe Kuu la Pembeni
Alipopitia misukosuko tukasimama nae kwanza kwa kutoa wito Ndugu, Jamaa na Marafiki, Njooni Tumtetee Makonda Dhidi ya Mapapa Wauza Unga Wanaomzushia... kisha tukamshauri Kumbe ni Uongo, Uzushi, Fitna, Majungu, Wivu na Kijicho Dhidi ya Mafanikio Yake!. Makonda Wapuuze! .
Kuna watu wenye roho za kwanini tukawaambia Wale mnaosubiri kwa hamu Makonda atumbuliwe, mtasubiri sana!. Ukiwa ni mpakwa mafuta, ni mpakwa mafuta!
Na mwisho nikapendekeza Baada ya Magufuli, 2025 Makonda atatufaa sana, kwasababu ana uthubutu kuliko hata JPM!. Apunguze...
Hivyo mheshimiwa sana Mwenezi Makonda, twende taratibu mdogo mdogo, hii duniani ni tambara bovu, tembea nayo taratibu!.
Wish you all the best
Kakayo
Paskali