Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,500
- 9,279
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Dodoma, Gilles Muroto, amesema kuwa kufeli kwa moyo na kukosa msaada wa haraka wa matibabu, ndiyo chanzo cha kifo cha Sheikh Rashid Bura, ambaye ni mmiliki wa shule za Zamzam mkoani humo.
Kamanda Muroto amebainisha hayo leo Disemba 27, 2019, na kusema kuwa mara baada ya kupata taarifa hiyo, Polisi walifika eneo la tukio na kwamba hawakukuta viashiria vyovyote vya mauaji, badala yake uchunguzi umebainika kuwa alifariki baada ya kukosa msaada kwa kuwa hali hiyo ilimkuta ofisini akiwa peke yake.
"Taarifa za kiuchunguzi za awali zinaonesha kifo chake kimetokana na kufeli kwa moyo na kwakuwa alikuwa ofisini kwake hakupata msaada na simu yake ilikuwa imezima ndugu zake walishindwa kumpata na ofisini tulikuta kupo salama na hakukuwa na wizi wowote uliofanyika" amesema Kamanda Muroto.
Kwa mujibu wa Kamanda Muroto, mwili wa Bura uligundulika siku ya Disemba 25, 2019, na kuwataka waandishi wa habari, kuacha kusambaza taarifa ambazo wanakuwa hawajazithibitisha kutoka kwenye vyanzo halisi likiwemo Jeshi la Polisi ama kwa Daktari
FAMILIA YATOFAUTIANA NA POLISI
Ali Rashid Bura (26), mtoto wa marehemu na msemaji wa familia ya marehemu, Abdillah Mboryo wamesema mwili wa marehemu ulikutwa ofisini kwake bila nguo huku ukiwa na makovu matatu mkono wa kushoto, kwenye paja na mgongoni.
Mtoto wa marehemu amesema baada ya kumtafuta baba yake maeneo mengine bila mafanikio, alikwenda ofisini kwake na kukuta mlango ukiwa umefungwa na alipoufungua kwa kuupiga teke ulifunguka.
“Ndipo nikauona mwili wa baba ukiwa umeharibika sana huku akiwa amekaa chini na nguo zote zikiwa pembeni,” anasema kijana huyo.
Naye Mboryo alisema: “Mwili wa marehemu ulikuwa na majeraha matatu; mkono wa kushoto, kwenye paja na mgongoni ambayo siwezi kuyazungumzia kwa sababu mimi si polisi lakini niliyaona.”
Habari zaidi, soma
Kamanda Muroto amebainisha hayo leo Disemba 27, 2019, na kusema kuwa mara baada ya kupata taarifa hiyo, Polisi walifika eneo la tukio na kwamba hawakukuta viashiria vyovyote vya mauaji, badala yake uchunguzi umebainika kuwa alifariki baada ya kukosa msaada kwa kuwa hali hiyo ilimkuta ofisini akiwa peke yake.
"Taarifa za kiuchunguzi za awali zinaonesha kifo chake kimetokana na kufeli kwa moyo na kwakuwa alikuwa ofisini kwake hakupata msaada na simu yake ilikuwa imezima ndugu zake walishindwa kumpata na ofisini tulikuta kupo salama na hakukuwa na wizi wowote uliofanyika" amesema Kamanda Muroto.
Kwa mujibu wa Kamanda Muroto, mwili wa Bura uligundulika siku ya Disemba 25, 2019, na kuwataka waandishi wa habari, kuacha kusambaza taarifa ambazo wanakuwa hawajazithibitisha kutoka kwenye vyanzo halisi likiwemo Jeshi la Polisi ama kwa Daktari
FAMILIA YATOFAUTIANA NA POLISI
Ali Rashid Bura (26), mtoto wa marehemu na msemaji wa familia ya marehemu, Abdillah Mboryo wamesema mwili wa marehemu ulikutwa ofisini kwake bila nguo huku ukiwa na makovu matatu mkono wa kushoto, kwenye paja na mgongoni.
Mtoto wa marehemu amesema baada ya kumtafuta baba yake maeneo mengine bila mafanikio, alikwenda ofisini kwake na kukuta mlango ukiwa umefungwa na alipoufungua kwa kuupiga teke ulifunguka.
“Ndipo nikauona mwili wa baba ukiwa umeharibika sana huku akiwa amekaa chini na nguo zote zikiwa pembeni,” anasema kijana huyo.
Naye Mboryo alisema: “Mwili wa marehemu ulikuwa na majeraha matatu; mkono wa kushoto, kwenye paja na mgongoni ambayo siwezi kuyazungumzia kwa sababu mimi si polisi lakini niliyaona.”
Habari zaidi, soma
Dodoma: Mmiliki wa Shule na Mkurugenzi Islamic Foundation akutwa ameuawa kinyama ofisini kwake
Ndugu Rashid Dalai, mmiliki wa shule ya kiislamu ya Zam zam iliyopo Dodoma na pia Mkurugenzi wa taasisi ya Islamic Foundation amekutwa amekufa ndani ya ofisi yake iliyopo ktk jengo moja na ofisi za Magazeti ya Serikali (Habari leo na Daily News) hapa Dodoma mjini maeneo ya Nyerere Square (karibu...
www.jamiiforums.com
Siasa za Kamanda Muroto na Kifo cha Sheikh Rashid Bura
Amani iwe ndugu zangu wa Jamii Forum. Nimeisikiliza kwa Makini taarifa ya RPC wa Dodoma Ndugu Muroto juu ya Kifo cha Ndugu yetu Mpendwa Marehemu Sheikh Rashid Bura ambaye pia alikuwa Mkurugenzi wa The Dalai Islamic Centre. Awali ya yote napenda Jamii ifahamu kuwa; a/ Sheikh Rashid Bura...
www.jamiiforums.com
RPC wa Dodoma, Afande Muroto aituhumu JamiiForums kwa kupotosha taarifa za kifo cha Sheikh Rashid Bura
Sheikh Bura alikutwa amekufa ndani ya ofisi yake. Afande Muroto anasema sababu ya kifo ni moyo wa Sheikh Bura " kufeli. " Taarifa za watu wengine zinadai mwili wa marehemu ulikutwa na majeraha matatu. Mkuu JokaKuu kuna msemo usemao '' ni bora kukaa kimya, unaweza kuongea na kuwatoa watu...
www.jamiiforums.com