Pinda: Wanaopinga kodi ya simu hawana jema

Pinda: Wanaopinga kodi ya simu hawana jema

Waziri mkuu Mizengo Pinda amesema tozo hiyo si ya kuwaumiza wananchi bali mapato yake yatakwenda moja kwa moja kusaidia kueneza umeme vijijini.

Alisema hayo alipozungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Songea juzi, katika ziara yake ya wiki moja mkoani Ruvuma.
Pinda '' ni kama vile tozo iliyoongezwa kwenye mafuta ya petrol, ambayo imetupa fedha nyingi katika mfuko wa barabara, za kuunganisha miji na mikoa''.

Aliongeza '' Nani asiyetaka vijiji vipate umeme kama miji, ili usaidie kuondoa giza, uendeshe viwanda vidogo vidogo na usaidie kukuza uchumi? Wanaopinga tozo hii, hawatutakii mema'' alisema Pinda.

source: Habari leo

mkuu molemo, mi nadhani tuachane na huo uenyekiti wa uvinza. tujipange kwa uchaguzi ujao ili tuje iongoza hiyo council sisi kama sisi. hayo mafungamano na huyo aliepewa viti maalum na jk siyaafiki kabisa mkuu.
 
Kweli alishasema"wapigwe tu maana tumewachoka" na sisi tunapigwa tu huku tukihamaki tusijue cha kufanya.
 
Shenzy kabisa huyo,watu wa vijijin hata chakula hawajui watapata wapi wanatoza kodi ya simucard ili wawape umeme wapi na wapi??
Nani kawaambia wao wanashida hiyo,na kama wanaona wana shida hiyo kwanin wasiwapelekee kwa gharama ya kodi zingine?lazima wawalimbikizie kodi zingine ili wawape umeme??kwan ndio makubaliano na hao walalahoi??upuuzi kabisa hawa viongoz wasio na mbele wala nyuma

Mkuu wangu acha tu yaani, tunahitaji mabadiliko ya as soon as possible aiseee,excuse ya kijinga sana eti wanataka kuwapelekea watu umeme vijijini bila hata aibu, vyakula vyenyewe hawana.

Yani hai make sense kabisaaaa hata chembe, kuna namna nyingi sanaaa za kuweza kuwasaidia ila sio kwa namna hii wanayofanya, serikali ndio mwisho wake hapo kufatilia na kuwasaidia wananchi wak, inahuzunisha sana
 
Mbona km kodi tnlipa wakat wa knnua vocha, ukpewa salario wankata, uknunua chochote kile wankata sasa itafkia mahal hata uraia utalpiwa
 
Viongozi wetu wanajisahau saana! Si mnamuona PM mstaafu mwingine i.e. mzee wa ukitaka mafanikio njoo CCM! Sasa yuko upande wa walalahoi! Huyu sijui atakuwa upande gani baada ya miaka miwili ijayo!
 
Sio hawana jema tu, Walipishwe tu, na wakipinga wadaiwe, wasipo lipa wafuatwe hadi mtaani wanapoishi walipe tuu!
 
Huyu mtoto wa 'Mpagazi' ni mtu mmoja very useless person. Uwaziri wake Mkuu hauna maana wala msaada wowote kwa WaTanzania. Ni bora awe anafunga bakuli lake tu kuliko kumwaga upup*u kila mara. Ati naye huyu anajiita 'mtoto wa mkulima'....sssshhh arrgggg...mkulima my foot!
 
Waziri mkuu Mizengo Pinda amesema tozo hiyo si ya kuwaumiza wananchi bali mapato yake yatakwenda moja kwa moja kusaidia kueneza umeme vijijini.

Alisema hayo alipozungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Songea juzi, katika ziara yake ya wiki moja mkoani Ruvuma.
Pinda '' ni kama vile tozo iliyoongezwa kwenye mafuta ya petrol, ambayo imetupa fedha nyingi katika mfuko wa barabara, za kuunganisha miji na mikoa''.

Aliongeza '' Nani asiyetaka vijiji vipate umeme kama miji, ili usaidie kuondoa giza, uendeshe viwanda vidogo vidogo na usaidie kukuza uchumi? Wanaopinga tozo hii, hawatutakii mema'' alisema Pinda.

source: Habari leo

Wapigwe tu, tena me nasema wapigwe tu maana tumechoka!
Liwalo na liwe!
 
wanaopinga hiyo tozo na wapigwe, wawapige hasa!Mwalimu alisema, cahama dhaifu kitazaa serikali dhaifu! Nasi tukadhani hiyo serikali itaishia kufilisitu nchi kumbe hatukujua kuwa watatupiga na kutupiga haswa. Hadi kwa mabomu, risasi za moto na hata kung'oa kucha. Sasa tukumbuke kutafakali kila tunapoambiwa mbali na hapo tutaendelea kupigwa tu.

Liwalo na liwe!
 
Hapo ndo siwaelewi CCM kabisaaaa... hebu cheki
1. Makamba anadai alizidiwa nguvu mpaka tozo ya line ya simu ikaingia bungeni...
2. Wabunge wa CCM wasema NDIYOOOOOOO ipite, na ikapita....
3. Ilipoanza kulalamikiwa, NAPE akaema CCM inapinga uwepo wa tozo hiyo......
4. Makamba akarudi kwa Mnyika na mkumwambia aache unafiki wa mitandanoni.... na akaonyesha kama vile tozo hii itasitishwa...
5. Pinda naye anakuja na maneno yanayoonyesha kuwa tozo hiyo ipo na itatozwa kama kawaida

MASWALI...
1. Hivi, kwa nini Pinda, Makamba na Nape hawana kauli moja juu ya hili...??
2. Aliyemfanya Makamba ashindwe wakati anapinga tozo hii hadi ikaingia bungeni... NI PINDA..???
3. Hawana vikao vya kiserikali ili kutoa kauli moja..???
4. Nani msemaji wa jambo hili..??? Kwamba akitoa taarifa yeye ndo tuiamini..??

Ukweli umenena, tusubiri waliotajwa wajibu....si ajabu kila mmoja wao atakuja na majibu mengine tofauti...watch.
 
Kwa motto ambaye amabahatika kuzaliwa leo na kukua le oleo anaweza akaamini kuwa mpango huu wa serikali wa kutaka kumaliza matatizo ya Umeme, Maji, Barabara na mamabo mengine ya maendeleo ni wa kweli!!.



Lakini kabla sijaanza kubonyeza hivi vitufe nimejiuliza sana, hivi tangu tupate uhuru, Tanzania imepata misaada mingapi kwa ajili ya sekta hizi na imefanikiwa kiasi gani ukiacha hii tunayoipata kupitia mnada giza wa kuiuza Tanzania yetu?!!



Tanzania ni moja kati ya Nchi chacvhe duniani zinazoongoza kupata misaada mingi yenye riba nafuu au mingine isiyokuwa na masharti, lakini ukiangalia kile tunachokipata na kile kinachotumika katika jamii, havina uwiano kabisa!! Sasa tujiulize kama tumeshindwa kufikia malengo kwa matirilioni ya pesa taslimu, Je, tutaweza kumaliza hili kwa kodi hii ya shiulingi 1000 ya kadi ya simu?!

TAFAKARI
 
simu ninunue mimi, line ninunue mimi vocha ninunue mimi na vyote ninalipia kodi wakati wa kununua. Sasa hii tozo ya 1000 kila mwezi ya nini? Mbona majanga
 
Siku 3 za Vitendo: Julai 29 tunagomea (Voda), Julai 30 (Airtel), Julai 31 (Tigo na laini nyingine zote). Tumia nguvu yako ya fedha kulazimisha mabadiliko ya sera. Chomoa SIM Card siku hizo kugomea Kodi hiyo kwa mwezi kutumia line.Gomea Kodi ya SIM CARD: Huu ni mgomo wa mwanzo: Sambaza kwa angalau watu 10!!
 
Hapo ndo siwaelewi CCM kabisaaaa... hebu cheki
1. Makamba anadai alizidiwa nguvu mpaka tozo ya line ya simu ikaingia bungeni...
2. Wabunge wa CCM wasema NDIYOOOOOOO ipite, na ikapita....
3. Ilipoanza kulalamikiwa, NAPE akaema CCM inapinga uwepo wa tozo hiyo......
4. Makamba akarudi kwa Mnyika na mkumwambia aache unafiki wa mitandanoni.... na akaonyesha kama vile tozo hii itasitishwa...
5. Pinda naye anakuja na maneno yanayoonyesha kuwa tozo hiyo ipo na itatozwa kama kawaida

MASWALI...
1. Hivi, kwa nini Pinda, Makamba na Nape hawana kauli moja juu ya hili...??
2. Aliyemfanya Makamba ashindwe wakati anapinga tozo hii hadi ikaingia bungeni... NI PINDA..???
3. Hawana vikao vya kiserikali ili kutoa kauli moja..???
4. Nani msemaji wa jambo hili..??? Kwamba akitoa taarifa yeye ndo tuiamini..??

Mkuu hivi Pinda NI NANI KATIKA TANZANIA?
 
Back
Top Bottom