Mvaa Tai
JF-Expert Member
- Aug 11, 2009
- 6,157
- 4,454
Waziri mkuu Mizengo Pinda amesema tozo hiyo si ya kuwaumiza wananchi bali mapato yake yatakwenda moja kwa moja kusaidia kueneza umeme vijijini.
Alisema hayo alipozungumza kwenye mkutano wa hadhara mjini Songea juzi, katika ziara yake ya wiki moja mkoani Ruvuma.
Pinda '' ni kama vile tozo iliyoongezwa kwenye mafuta ya petrol, ambayo imetupa fedha nyingi katika mfuko wa barabara, za kuunganisha miji na mikoa''.
Aliongeza '' Nani asiyetaka vijiji vipate umeme kama miji, ili usaidie kuondoa giza, uendeshe viwanda vidogo vidogo na usaidie kukuza uchumi? Wanaopinga tozo hii, hawatutakii mema'' alisema Pinda.
source: Habari leo
Mimi na Pinda kifedha tunaweza kuwa sawa tu hivyo hii kodi haituumizi, tatizo ni wale watu wa chini ambao hiyo tozo ya elfu moja inaweza ikafanana kabisa na pesa anayotumia kununua vocha kwa mwezi, amesahau kwamba kuna watu wamenunua simu ili imsaidie kubeep tu akiwa na shida. Mimi kuna mtu namfaham amepanga chumba analipa Tshs3000 kwa mwezi pale ngudu nadhani unapata picha hii tozo ya elfu1 kwa mwezi ni mzigo kiasi gani kwake, na ana simu kila wakati ipo hewani kazi yake kubwa ni vibarua vya mashambani ile simu ipo ili apigiwe tu.