Zaidi ya Nusu ya Bajeti ya Wizara ya Ardhi itatumika kwenye Matumizi ya Kawaida

BARD AI

JF-Expert Member
Jul 24, 2018
3,518
8,456
DODOMA: Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi imewasilisha Bungeni Bajeti ya Tsh. Bilioni 171,372,508,000 kwaajili ya Matumizi yake kwa mwaka wa Fedha 2024/25 ambapo zaidi ya Nusu ya Bajeti (Tsh. 93,930,673,000) imeelekezwa katika Matumizi ya Kawaida

Pia, Wizara imeomba kiasi cha Tsh. 75,697,742,000 kwaajili ya Miradi ya Maendeleo ambapo Tsh. 15,642,989,000 kati ya Fedha kutoka Ndani ya Serikali na Tsh. 60,054,753,000 ni Fedha kutoka vyanzo vya Nje

============

HOTUBA YA WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI, MHESHIMIWA JERRY W. SILAA (MB.), AKIWASILISHA
BUNGENI MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI YA WIZARA KWA
MWAKA 2024/25


UTANGULIZI
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba, kutokana na taarifa iliyowasilishwa leo ndani ya Bunge lako Tukufu na Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii iliyochambua na kujadili Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi (Fungu 48) na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (Fungu 03); Bunge lako Tukufu lipokee na kujadili Taarifa za Utekelezaji wa Bajeti ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi (Fungu 48) na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (Fungu 03) kwa mwaka 2023/24. Aidha, naomba Bunge lako Tukufu lijadili na kupitisha Makadirio ya Mapato na Matumizi ya mafungu hayo mawili kwa mwaka 2024/25.
Mheshimiwa Spika, awali ya yote napenda kutumia fursa hii kumshukuru Mwenyezi Mungu mwingi wa rehema kwa kutujalia uhai na afya njema na kutuwezesha kushiriki Mkutano wa 15 wa Bunge la 12 ambao ni mahsusi kwa ajili ya kujadili Bajeti ya Serikali. Aidha, kwa heshima na taadhima naomba kutumia fursa hii kipekee kumshukuru Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuniamini na kuniteua kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi. Ninamuahidi kuwa nitaendelea kutekeleza majukumu aliyonikabidhi kwa juhudi, uadilifu na uweledi ili

kuleta ufanisi na kukuza ustawi na maendeleo ya wananchi kupitia sekta ya ardhi.
Salamu za Pongezi
Mheshimiwa Spika,
napenda kutumia fursa hii kumpongeza Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutimiza miaka mitatu tangu ashike madaraka ya kuongoza Taifa letu. Katika kipindi hiki cha uongozi wake, Sekta ya Ardhi imepata mafanikio mbalimbali ambayo yanajumuisha uboreshaji wa sera, sheria, taratibu na mifumo ya utoaji wa huduma; kuongezeka kwa kasi ya upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi; uendelezaji wa makazi; kurahisishwa kwa taratibu za upatikanaji wa haki za ardhi; utatuzi wa migogoro ya ardhi; na utoaji wa elimu kwa umma.
Mheshimiwa Spika, nawapongeza Mheshimiwa Dkt. Philip Isdor Mpango, Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mheshimiwa Dkt. Dotto Mashaka Biteko (Mb.), Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa umahiri wao katika kumsaidia Mheshimiwa Rais kusimamia na kuratibu shughuli za Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nawashukuru kwa maelekezo na ushauri wanaonipa ambao umeniwezesha kutekeleza

majukumu ya kuongoza sekta hii muhimu kwa maendeleo ya Taifa letu. Aidha, nampongeza Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa uongozi wake mahiri katika kusimamia maslahi na ustawi wa wananchi wa Zanzibar na kuendelea kudumisha Muungano wetu ambao umetimiza miaka 60.
Mheshimiwa Spika, kipekee nakupongeza wewe binafsi pamoja na Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb.), Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuongoza na kusimamia kwa umahiri shughuli za Bunge. Aidha, nawapongeza Mheshimiwa Najma Murtaza Giga (Mb.), kwa kuendelea kusimamia kwa ufanisi shughuli za Bunge kama Mwenyekiti wa Bunge. Vilevile, nawapongeza Mheshimiwa Dkt. Joseph Kizito Mhagama (Mb.) na Mheshimiwa Deodatus Philip Mwanyika (Mb.) kwa kuteuliwa kuwa Wenyeviti wa Bunge. Tunawaombea kwa Mwenyezi Mungu awajalie afya njema na hekima ili muweze kutekeleza majukumu ya kusimamia shughuli za Bunge kwa maslahi ya wananchi na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika, naomba kutumia fursa hii kumpongeza Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa (Mb.), Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwa Hotuba yake ya Bajeti ambayo imewasilisha utekelezaji wa malengo ya Serikali kwa mwaka 2023/24, pamoja na mwelekeo wa

shughuli za Serikali kwa mwaka 2024/25. Kwa hakika, hotuba hiyo imetoa mwelekeo wa utekelezaji wa majukumu ya sekta ya ardhi katika kuongeza kasi ya upangaji, upimaji na umilikishaji ardhi pamoja na upimaji na uhakiki wa mipaka ya vijiji kama njia mojawapo ya kudhibiti migogoro ya ardhi. Ninaahidi kuwa, Wizara itayafanyia kazi masuala yote yaliyoainishwa katika hotuba hiyo ili kufikia malengo ya Serikali yaliyokusudiwa.
Mheshimiwa Spika, natoa shukrani zangu za dhati kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii chini ya uongozi wa Mwenyekiti Mheshimiwa Timotheo Paul Mzava (Mb.) na Makamu Mwenyekiti Mheshimiwa Najma Murtaza Giga (Mb.) kwa utekelezaji wa majukumu ya usimamizi wa Sekta ya Ardhi. Maoni na ushauri ambao wamekuwa wakiutoa mara kwa mara umesaidia kuongeza tija na ufanisi katika utoaji wa huduma za sekta ya ardhi. Tunawaahidi kuendelea kuzingatia maoni na ushauri wao ili kutimiza azma ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuhakikisha kuwa sekta ya ardhi inachangia ipasavyo katika ukuaji wa uchumi wa nchi, kuimarisha usalama wa milki na kudhibiti migogoro ya ardhi.
Mheshimiwa Spika, nampongeza Mheshimiwa Dkt. Dotto Mashaka Biteko (Mb.) kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Waziri wa Nishati. Aidha, nawapongeza Mheshimiwa Deogratius John

Ndejembi, Mbunge wa Chamwino kwa kuteuliwa kuwa Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu); Mheshimiwa Daniel Baran Sillo, Mbunge wa Jimbo la Babati Vijijini kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi; Mheshimiwa Alexander Pastory Mnyeti, Mbunge wa Misungwi kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi; Mheshimiwa David Mwakiposa Kihenzile, Mbunge wa Mufindi Kusini kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Uchukuzi; na Mheshimiwa Zainab Athumani Katimba, Mbunge wa Viti Maalum kwa kuteuliwa kuwa Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais
- TAMISEMI. Vilevile, nampongeza Mheshimiwa Bahati Keneth Ndingo, kwa kuchaguliwa kuwa Mbunge wa Jimbo la Mbarali. Ninawatakia kila la heri katika utekelezaji wa majukumu yao.
Salamu za Pole
Mheshimiwa Spika
, naomba nitumie fursa hii kutoa pole kwa Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, wanafamilia wote, Bunge lako Tukufu, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania kwa ujumla kwa kuondokewa na kiongozi wetu mpendwa Hayati Ali Hassan Mwinyi aliyekuwa Raiswa Awamuya Piliwa Jamhuriya Muungano wa Tanzania. Hakika tutaendelea kumuenzi kwa kuleta mageuzi ya kiuchumi na kisiasa nchini.

Mheshimiwa Spika, mwezi Februari, 2024, Taifa letu lilipata msiba wa kuondokewa na aliyewahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Monduli na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Edward Ngoyai Lowassa. Nitumie fursa hii kumpa pole Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wanafamilia, ndugu, jamaa, marafiki na Watanzania wote kwa kumpoteza kiongozi huyo mahiri. Aidha, natoa pole kwa Mheshimiwa Fredrick Edward Lowassa, Mbunge wa Jimbo la Monduli kwa kuondokewa na Baba yake mpendwa.
Mheshimiwa Spika, natoa pole kwako wewe binafsi, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb.), Naibu Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Waheshimiwa Wabunge, Watumishi wa Ofisi ya Bunge, familia na Watanzania kwa ujumla kwa kuondokewa na Mheshimiwa Ahmed Yahya Abdulwakil, aliyekuwa Mbunge wa Kwahani, Zanzibar na Mheshimiwa Francis Leonard Mtega, aliyekuwa Mbunge wa Mbarali. Hakika michango yao itaendelea kukumbukwa.

Mheshimiwa Spika, nitumie fursa hii kuwapa pole Watanzania wote waliopoteza ndugu, jamaa na mali kutokana na maafa, ajali na majanga yaliyosababisha athari mbalimbali zikiwemo vifo, majeruhi, uharibifu wa mali na mazingira yaliyotokea katika maeneo mbalimbali nchini. Tunamwomba Mwenyezi Mungu awajalie uponyaji wa haraka watanzania wenzetu waliojeruhiwa ili waweze kupona na kurejea katika shughuli zao za kila siku za ujenzi wa Taifa. Aidha, tunamwomba Mwenyezi Mungu awalaze mahali pema peponi. Amina.
Mheshimiwa Spika, baada ya maelezo hayo ya utangulizi, naomba sasa nitoe taarifa kuhusu utekelezaji wa Mpango na Bajeti ya Wizara kwa mwaka 2023/24 pamoja na makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka 2024/25. Bajeti ya Wizara imeandaliwa kwa kuzingatia Dira ya Taifa ya Maendeleo (2025); Ilani ya Chama cha Mapinduzi ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020; Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano (2021/22–2025/26); Mpango Mkakati wa Wizara; Mikataba; Itifaki; Mipango na Makubaliano ya Kikanda na Kimataifa; Sera, Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo mbalimbali ya Sekta ya Ardhi; na maelekezo ya Viongozi Wakuu wa Serikali. Maeneo ya kipaumbele yatakayotiliwa mkazo na Wizara katika mwaka 2024/25 ni pamoja na:-

Kuongeza kasi ya upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi mijini na vijijini;
Kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro ya ardhi;
Kuimarisha mifumo ya TEHAMA katika utunzaji wa kumbukumbu, utoaji wa huduma na upatikanaji wa taarifa za ardhi;
Kuhakikisha uwepo wa nyumba bora, ukuaji wa sekta ya milki na maendeleo ya makazi kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii; na
Kuimarisha mipaka ya kimataifa.
MAPITIO YA UTEKELEZAJI WA BAJETI YA WIZARA KWA MWAKA 2023/24 NA MALENGO YA MWAKA 2024/25.
MAPATO NA MATUMIZI FUNGU 48
Mheshimiwa Spika
, katika mwaka 2023/24 Wizara iliidhinishiwa jumla ya shilingi bilioni 163.17 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 43.43 ziliidhinishwa kwa ajili ya Mishahara (PE); shilingi bilioni
37.61 kwa ajili ya Matumizi Mengineyo (OC) na shilingi bilioni 82.13 kwa ajili ya miradi ya maendeleo (DEV). Kati ya fedha za miradi ya maendeleo, shilingi bilioni 14.01 ni fedha za ndani na shilingi bilioni 68.12 ni fedha za nje. Aidha, Wizara iliongezewa bajeti ya shilingi bilioni 287.66 kwa ajili

ya kulipa madeni ya Wazabuni, Watumishi na Wakandarasi. Ongezeko hilo limefanya bajeti ya Wizara kufikia shilingi bilioni 450.83.
Mheshimiwa Spika, hadi tarehe 15 Mei, 2024, jumla ya shilingi bilioni 423.13 zilipokelewa, sawa na asilimia 93.86 ya bajeti ya shilingi bilioni
450.83. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 34.72 ni mishahara ya watumishi wa Wizara na Taasisi sawa na asilimia 79.94 ya bajeti husika; shilingi bilioni 21.94 ni matumizi mengineyo ya Wizara na Taasisi sawa na asilimia 56.24 ya bajeti husika na shilingi bilioni 366.47 ni miradi ya maendeleo sawa na asilimia 99.48. Kati ya fedha za miradi ya maendeleo zilizopokelewa, shilingi bilioni 309.53 ni fedha za ndani sawa na asilimia 99.52; na shilingi bilioni 56.94 ni fedha za nje sawa na asilimia
99.26. (Jedwali Na.1). Ukusanyaji wa Maduhuli
Mheshimiwa Spika,
ardhi ni miongoni mwa rasilimali muhimu ambazo zinachangia pato la Taifa kupitia ukusanyaji wa maduhuli yatokanayo na kodi ya pango la ardhi, ada na tozo nyingine za utoaji huduma za sekta ya ardhi. Katika mwaka 2023/24, Wizara kupitia Fungu 48 ilipanga kukusanya shilingi bilioni 300. Hadi kufikia tarehe 15 Mei, 2024, Wizara imekusanya shilingi bilioni 136 sawa na asilimia 45.3 ya lengo (Jedwali Na.2).

Mheshimiwa Spika, pamoja na jukumu la ukusanyaji wa maduhuli kuhamishiwa Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Wizara imeendelea kuwasiliana na Wizara ya Fedha kupendekeza jukumu la kukusanya kodi ya pango la ardhi liendelee kutekelezwa na Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi na iwezeshwe kwa kurudishiwa sehemu ya fedha (retention) kwa ajili ya makusanyo. Pendekezo hili linatokana na sababu mbalimbali zikiwemo: ukusanyaji wa kodi ya pango la Ardhi ni jukumu la kisheria lililoainishwa chini ya kifungu cha 25 na 33 cha Sheria ya Ardhi (Sura 113); ukusanyaji unahitaji wataalamu wa sekta ya ardhi ambao Wizara ndio mamlaka yao ya ajira na nidhamu; na mfumo wa TEHAMA wa Wizara unaotunza kumbukumbu za wamiliki umeunganishwa na shughuli kuu za kisekta za upangaji, upimaji, uthamini na umilikishaji ardhi na hivyo kupunguza changamoto za ukusanyaji zilizokuwepo hapo awali.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25, Wizara imekadiria kukusanya shilingi bilioni 250. Lengo hili litafikiwa kwa kuendelea kuimarisha mifumo ya TEHAMA kwa lengo la kurahisisha ukusanyaji wa maduhuli kidigitali; kuongeza kasi ya upangaji, upimaji na usajili wa ardhi; kuendelea kufuatilia madeni ya kodi ya pango la ardhi kutoka katika mashirika, taasisi za umma na wamiliki binafsi; na kutoa elimu kwa umma kuhusu umuhimu wa kulipa kodi ya pango la ardhi kwa wakati.

MAPATO NA MATUMIZI YA FUNGU 03
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24 Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (Fungu 03) iliidhinishiwa shilingi bilioni 8.19. Kati ya fedha hizo shilingi bilioni 2.49 ni Mishahara ya watumishi (PE); shilingi bilioni 2.29 ni fedha za Matumizi Mengineyo (OC); na shilingi bilioni 3.41 ni fedha za ndani kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya Maendeleo. Aidha, wakati wa utekelezaji wa Bajeti, Tume ilipata nyongeza ya bajeti ya mishahara kiasi cha shilingi milioni 627.12 kwa ajili ya mishahara kutokana na ongezeko la watumishi hivyo kufanya Bajeti ya Tume kufikia shilingi bilioni 8.82.
Mheshimiwa Spika, hadi tarehe 15 Mei, 2024, Tume imepokea jumla ya shilingi bilioni 7.33 kati ya bajeti ya shilingi bilioni 8.82 sawa na asilimia
83.11 ya bajeti iliyoidhinishwa. Kati ya fedha zilizopokelewa, shilingi bilioni 1.37 ni kwa ajili ya Matumizi Mengineyo (OC); shilingi bilioni 2.55 ni Mishahara; na shilingi bilioni 3.41 fedha za ndani kwa ajili ya utekelezaji wa mradi wa Maendeleo (Jedwali Na.3).

Ukusanyaji wa Maduhuli
Mheshimiwa Spika,
Wizara kupitia Tume imeendelea kutekeleza jukumu la kukusanya maduhuli kutoka katika vyanzo mbalimbali. Katika mwaka 2023/24, Tume ilipanga kukusanya shilingi Milioni 18 kutokana na kodi ya pango la nyumba zilizopo Tabora. Hadi, tarehe 15 Mei, 2024 shilingi Milioni 9.5 zimekusanywa sawa na asilimia
52.78 ya lengo. Aidha, Tume ilipanga kuhamasisha wadau kuchangia kiasi cha shilingi milioni 700 kwa ajili ya shughuli za upangaji wa Matumizi ya Ardhi. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 jumla ya shilingi bilioni 2.77 zilipokelewa kutoka kwa wadau mbalimbali sawa na asilimia 395.71 ya lengo (Jedwali Na.4). Ongezeko hili limetokana na mwitikio mkubwa wa wadau kuchangia kazi za upangaji wa matumizi ya ardhi.

UANDAAJI WA HATIMILIKI NA USAJILI WA NYARAKA


Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuandaa, kusajili na kutoa nyaraka mbalimbali ikiwemo Hatimiliki na Hati za Hakimiliki za Kimila kwa wamiliki wa ardhi. Hati hizo huimarisha usalama wa miliki na hivyo kuwezesha udhibiti na kupunguza migogoro ya ardhi, kudhibiti umegaji wa ardhi kiholela, kuwezesha utambuzi wa maeneo katika zoezi la uwekaji wa Anwani za Makazi na kutumia ardhi kama dhamana katika Taasisi za fedha na vyombo vya sheria.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt Phillip Isdori Mpango akiwa pamoja na wananchi wa Makete aliowakabidhi Hati za Kimila mkoani Njombe Oktoba 2023.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kuandaa Hatimiliki 500,000, Hati za Hakimiliki za Kimila 520,000 na Hati za Sehemu ya Jengo 1,000. Aidha, Wizara iliahidi kusajili miamala ya hatimiliki na Nyaraka za Kisheria 100,000 na kutoa Vyeti vya Ardhi ya Kijiji 100. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara imeandaa na kusajili Hatimiliki 87,240 sawa na asilimia 17.4 ya lengo na Hati za Hakimiliki za Kimila 86,994 sawa na asilimia 16.73 ya lengo. Kwa upande wa Vyeti vya Ardhi ya Kijiji, jumla ya vyeti 362 vimeandaliwa sawa na asilimia 324 ya lengo, Hati za Sehemu ya Jengo 324 sawa na asilimia 32.4 ya lengo na miamala ya Hatimiliki na Nyaraka za Kisheria 95,456 sawa na asilimia
95.46 ya lengo zimesajiliwa (Jedwali Na.5).
Mheshimiwa Spika, zipo changamoto mbalimbali zilizosababisha kutofikia malengo ya uandaaji wa Hatimiliki. Changamoto hizo ni pamoja na uwepo wa madai ya fidia kwenye baadhi ya maeneo yaliyopangwa na kupimwa, uwepo wa migogoro ya ardhi kwenye baadhi ya maeneo, kutokamilishwa kwa malipo ya viwanja vilivyopangwa na kupimwa, wananchi wengi kutochangia gharama za urasimishaji na baadhi ya watumishi kutozingatia misingi ya haki, weledi na uadilifu.

Mheshimiwa Spika, ili kuongeza kasi ya umilikishaji, Wizara imeendelea kuchukua hatua mbalimbali zikiwemo utekelezaji wa Mradi wa Usalama wa Milki za Ardhi; Kushirikiana na sekta binafsi na Taasisi za Umma; Programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi; kuboresha mifumo ya TEHAMA katika utoaji wa huduma; na kuchukua hatua za kinidhamu kwa watumishi na kampuni zinazofanya kazi za urasimishaji zilizokiuka maadili. Aidha, Serikali kupitia Sheria ya Fedha ya mwaka 2023 ilichukua hatua ya kupunguza gharama za umilikishaji kwa zaidi ya asilimia 50. Hatua hizo zimeongeza kasi ya umilikishaji wa ardhi ambapo hati zilizomilikishwa zimeongezeka kutoka Hatimiliki 76,746 kwa kipindi cha Julai, 2022 hadi Mei, 2023 mpaka Hatimiliki 87,240 kwa kipindi cha Julai, 2023 mpaka Mei, 2024. Vilevile, utoaji wa hatimiliki umeongezeka kutoka Hatimiliki 67,331 mwaka 2020/21 hadi Hatimiliki 86,398 mwaka 2022/23 kutokana na huduma za ardhi kuanza kutolewa katika Ofisi za Ardhi za Mikoa. Nawahimiza wananchi kote nchini kuendelea kutumia Ofisi za Ardhi za Mikoa kupata huduma na fursa ya punguzo la tozo za umilikishaji kuhakikisha kuwa wanamilikishwa maeneo yao kwa mujibu wa sheria.
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2024/25, Wizara imepanga kuandaa na kutoa Hati za Hakimiliki za Kimila 520,000, Hatimiliki 500,000,

Vyeti vya Ardhi ya Kijiji 1,000 na Hati za Sehemu ya Jengo 1,000. Vilevile, miamala ya Hatimiliki na Nyaraka za kisheria 100,000 zitasajiliwa.
Usimamizi wa Masharti ya Umiliki
Mheshimiwa Spika,
wamiliki wa ardhi wana wajibu wa kuzingatia masharti yanayoainishwa katika nyaraka za umiliki ikiwemo kuendeleza ardhi husika kwa wakati. Ukiukaji wa masharti ya umiliki, umekuwa ukisababisha athari hasi kiuchumi na kijamii ikiwemo kuibuka kwa migogoro ya ardhi inayotokana na maeneo husika kuvamiwa. Katika kusimamia utekelezaji wa masharti ya uendelezaji hususani wa mashamba, mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kukagua mashamba na viwanja 230 ili kubaini uzingatiaji wa masharti ya umiliki. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, ukaguzi wa mashamba na viwanja 156 ulifanyika na kubaini kuwa viwanja na mashamba 124 hayajaendelezwa. Aidha, Wizara ilichukua hatua dhidi ya wamiliki waliokiuka masharti ya uendelezaji ambapo jumla ya milki za viwanja na mashamba 124 zimebatilishwa. Katika mwaka 2024/25, Wizara itakagua mashamba na viwanja 230 na kuchukua hatua kwa mujibu wa sheria kwa watakaobainika kukiuka masharti ya umiliki. Natoa rai kwa wamiliki wote wa ardhi kuhakikisha wanazingatia masharti ya umiliki kama yalivyoainishwa kwenye nyaraka zao za umiliki. Aidha, natoa muda wa siku 90 kwa wamiliki wa ardhi ambao

hawajaendeleza maeneo yao kwa mujibu wa sheria watekeleze wajibu wao, baada ya muda huo nitapendekeza ubatilisho wa milki zao.
Usimamizi wa Ardhi ya Uwekezaji
Mheshimiwa Spika,
Wizara inaratibu na kusimamia ardhi ya uwekezaji kwa kushirikiana na taasisi za uwekezaji nchini ili kuhakikisha ardhi kama rasilimali muhimu inaleta tija kiuchumi na kijamii. Usimamizi huu unahusisha ugawaji na usimamizi wa ardhi kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi kupitia Kamati ya Kitaifa ya Ugawaji Ardhi. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, maombi 216 ya ardhi ya uwekezaji yenye ukubwa wa hekta 11,292.14 yaliidhinishwa kwa ajili ya uwekezaji ambapo kati ya hayo maombi 65 ni ya raia wa Tanzania na 151 ni ya wawekezaji kutoka nje ya nchi. Uwekezaji wa nje una mtaji wenye thamani ya Dola za Marekani milioni 58.95 sawa na shilingi bilioni 152.98 (Jedwali Na.6).
Mheshimiwa Spika, Wizara imeshiriki katika Timu ya pamoja ya Wataalam wa Serikali inayoandaa Mwongozo wa Usimamizi wa Ardhi ya Uwekezaji na Wawekezaji. Lengo la Mwongozo huo ni kuhahikisha kuwa ardhi iliyotolewa kwa uwekezaji inaleta tija iliyotarajiwa kiuchumi na kijamii. Timu ya Wataalam inahusisha Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi; Ofisi ya Rais - Mipango na Uwekezaji; Ofisi ya Rais-

TAMISEMI; Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA); Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC) na Mamlaka ya Uzalishaji kwa Mauzo ya Nje (EPZA). Hadi tarehe 15 Mei, 2024 Timu hiyo imewatembelea wawekezaji 38 katika mikoa ya Dar es Salaam na Pwani kwa lengo la kuona hatua za uwekezaji wao na kupokea maoni yao yenye lengo la kuboresha mazingira ya kiuwekezaji. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kuratibu na kusimamia maeneo ya ardhi ya uwekezaji ikiwa ni pamoja na uhakiki wa matumizi ya ardhi iliyotolewa kwa wawekezaji na kuwa na vikao na wadau wa uwekezaji wakiwemo wawekezaji wenyewe ili kuhakikisha ardhi ya uwekezaji inaleta tija inayotarajiwa.
Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi Kiutawala
Mheshimiwa Spika,
Wizara imeendelea na utatuzi wa migogoro ya ardhi kiutawala kwa kutumia njia mbalimbali ikiwemo uendeshaji wa Kliniki za ardhi kwenye Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa, madawati ya kushughulikia kero na malalamiko, Timu na Kamati Maalum za Wataalam wa Serikali na ziara za viongozi wa Wizara katika maeneo mbalimbali nchini. Utatuzi huo unahusisha masuala ya fidia; utoaji wa viwanja mbadala; urekebishaji wa mipaka ya vijiji, viwanja au mashamba na utoaji elimu. Katika mwaka 2023/24 Wizara ilipanga kutatua migogoro 6,550 kiutawala ambapo hadi tarehe 15 Mei, 2024 migogoro 7,885 imetatuliwa (Jedwali Na.7).

Vilevile, rejista za migogoro katika Ofisi za Ardhi za Mikoa na Halmashauri zimeendelea kuhuishwa ili kuwa na kumbukumbu sahihi za migogoro ya ardhi nchini.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kushughulikia malalamiko na migogoro ya ardhi kupitia moduli ya mfumo wa kielektroniki wa ILMIS inayotarajiwa kuanza kutumika mwezi Julai, 2024. Aidha, Wizara kwa kushirikiana na wadau, itaendelea kupanga matumizi ya ardhi na kutoa elimu kwa umma kuhusu umiliki wa ardhi na madhara ya migogoro.
Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi Kupitia Kliniki za Ardhi
Mheshimiwa Spika
, kliniki za Ardhi ni mpango wa Wizara wenye lengo la kuhakikisha kuwa wananchi wote wenye kuhitaji huduma au wenye changamoto za ardhi wanapatiwa huduma karibu na maeneo wanayoishi kwa haraka na ufanisi unaotarajiwa na jamii. Kwa kutambua hilo, Wizara kwa kushirikiana na mamlaka nyingine za Serikali imekuwa ikiendesha zoezi la kliniki za ardhi kwenye Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa ambapo wataalam wa kada zote za ardhi wanakuwepo eneo moja kwa wakati mmoja hivyo kuwezesha upatikanaji wa huduma zote za ardhi papo kwa papo. Katika kipindi cha kuanzia Julai, 2023 hadi Mei, 2024 kliniki za ardhi zimefanyika

katika Mikoa na Mamlaka za Serikali za Mitaa chini ya Viongozi wa Wizara, Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya. Kwa kutambua umuhimu wa kliniki za ardhi na matokeo chanya yanayopatikana, Viongozi Wakuu wa Wizara wamefanya ziara kwenye majiji yote nchini na kushirikiana na viongozi wa maeneo hayo kushughulikia changamoto za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi. Majiji hayo ni Dar es Salaam, Arusha, Mwanza, Mbeya, Dodoma na Tanga. Napenda kutoa pongezi kwa Waheshimiwa Wakuu wa Mikoa na Wilaya kote nchini ambao wameshirikiana kwa karibu sana na Makamishna wa Ardhi Wasaidizi wa Mikoa na wataalamu wa sekta ya ardhi katika kuendesha na kusimamia Kliniki za ardhi katika maeneo yao.


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry William Silaa (Mb.) akiwasikiliza wananchi wakati wa Kliniki ya Ardhi tarehe 6 Novemba 2023 iliyofanyika jijini Dodoma.

Mheshimiwa Spika, kliniki za ardhi zimeonesha mafanikio kutokana na wananchi wengi kujitokeza kusikilizwa kwa uhuru na uwazi kisha changamoto zao kupatiwa ufumbuzi kwa haraka. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, wananchi 35,963 walihudumiwa katika mikoa 22 iliyoendesha kliniki za ardhi. Migogoro na malalamiko 7,444 yalipokelewa ambapo 4,565 imetatuliwa na 2,879 inaendelea kushughulikiwa. Aidha, Hatimiliki 17,553 zilikamilishwa na kukabidhiwa kwa wamiliki na maombi mapya ya hati 13,289 yalipokelewa. Katika kliniki hizo, jumla ya shilingi bilioni 3.03 zilikusanywa kama tozo na ada mbalimbali za kisheria.


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry Silaa (kushoto), Mwenyekiti wa Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii Mhe. Timotheo Mzava (wa pili kushoto) na wajumbe wa Kamati hiyo wakati wa Kliniki ya Ardhi Bunju jijini
Dar es Salaam.

Mheshimiwa Spika, kufuatia uendeshaji wa zoezi la Kliniki za Ardhi, Wizara imebaini vyanzo mbalimbali vya malalamiko na migogoro ya ardhi. Vyanzo hivyo ni pamoja na madai ya fidia, utolewaji wa milki pandikizi, uvamizi wa maeneo ya umma na binafsi, udanganyifu na utapeli kwa kutumia nyaraka za kughushi, ucheleweshaji wa huduma, mwingiliano wa mipaka, madai ya mali za urithi au wanandoa, utekelezaji wa miradi ya urasimishaji

na upimaji shirikishi na uelewa mdogo wa baadhi ya wananchi kuhusu masuala ya umiliki wa ardhi.
Mheshimiwa Spika, Wizara itaendelea kushirikiana na Taasisi nyingine za Serikali kuchukua hatua kwa wananchi wanaotumia nyaraka za kughushi au kuvamia viwanja vyenye umiliki kwa kuwafikisha mahakamani na kurejesha maeneo hayo kwa wamiliki halali. Aidha, Wizara imeanzisha Dawati Maalum katika Ofisi za Ardhi za Mikoa ili kuwezesha wananchi wenye migogoro ya ardhi hasa yenye sura ya jinai kuwasilisha malalamiko yao ili yapatiwe ufumbuzi. Natoa wito kwa Wananchi na wadau wote wa ardhi wenye changamoto zinazotokana na vitendo vya dhuluma kuendelea kujitokeza kutoa malalamiko yao ili kuiwezesha Wizara kuchukua hatua stahiki
Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi katika Vijiji 975
Mheshimiwa Spika, Wizara inaratibu utekelezaji wa Maelekezo ya Baraza la Mawaziri kuhusu utatuzi wa migogoro ya matumizi ya ardhi ya vijiji na Mitaa 975 nchini. Katika utekelezaji wa maamuzi haya, tathmini imebainisha kuwa vijiji na mitaa yenye migogoro ni 1,004 (vijiji 981 na mitaa 23) badala ya 975 kama ilivyokuwa imebainishwa hapo awali.

Mheshimiwa Spika, hadi tarehe 15 Mei, 2024 utekelezaji wa uamuzi katika vijiji 438 na mitaa 13 umekamilika na utekelezaji katika vijiji
543 na mitaa 10 unaendelea (Jedwali Na.8). Utekelezaji huo umewezesha ardhi yenye ukubwa wa ekari milioni 2.4 kumegwa na kurejeshwa kwa wananchi ikijumuisha ekari milioni 1.65 kutoka kwenye maeneo ya hifadhi, ranchi na mashamba ya Serikali; ekari 707,962 kutoka kwenye Mapori Tengefu 12 na ekari 46,715 kutoka kwenye Hifadhi za Misitu saba (7). Vilevile, maeneo 18 kati ya 20 yamefanyiwa uthamini na kiasi cha shilingi bilioni
178.57 kinahitajika kwa ajili ya kuhamisha wananchi kutoka kwenye maeneo ya Hifadhi na vyanzo vya maji. Kati ya maeneo yaliyothaminiwa, wananchi wa maeneo sita (6) wamelipwa fidia kiasi cha shilingi bilioni 20.07 (Jedwali Na.9 A&B)
Mheshimiwa Spika,
ili kuimarisha usimamizi wa mipaka ya Hifadhi, vigingi 32,838 vimesimikwa na mkuza kuchongwa kuzunguka maeneo ya Hifadhi za Taifa 21 na Mapori ya Akiba 29 na Hifadhi za Misitu 416. Pia, Serikali kupitia Tangazo la Serikali Na. 754 la tarehe 20/10/2023 imerekebisha mpaka wa Hifadhi ya Taifa ya Ruaha kwa kumega eneo lenye ukubwa wa kilometa za mraba 478 kwenda kwa wananchi. Utekelezaji wa maagizo ya Baraza la Mawaziri utakamilishwa kwa kumalizia kazi za uthamini na kulipa fidia; upimaji upya wa vijiji vinavyomegewa maeneo; kushughulikia maeneo yenye changamoto zaidi ambayo

yanahusisha baadhi ya vijiji vitakavyoondolewa katika maeneo ya hifadhi, vyanzo vya maji na maeneo muhimu kwa ajili ya ulinzi na usalama wa Nchi. Utekelezaji wa kazi hizo umepangwa kukamilika ifikapo Juni, 2024. Mwelekeo wa Wizara ni kuweka mifumo thabiti ya usimamizi na ufuatiliaji kwa kushirikiana na wadau wote muhimu ili kupunguza migogoro mikubwa kama hii kuendelea kujitokeza.
Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya
Mheshimiwa Spika,
Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya ni miongoni mwa vyombo vilivyoanzishwa kwa mujibu wa Sheria ya Mahakama za Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi, Sura 216 kwa ajili ya kushughulikia migogoro ya ardhi. Wizara imeendelea kuhakikisha kuwa Mabaraza haya yanaundwa na kufanya kazi katika Wilaya zote nchini. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 jumla ya Mabaraza 139 yameundwa ambapo kati ya hayo Mabaraza 104 yanatoa huduma. Napenda kutumia fursa hii kuzihimiza Sekretarieti za Mikoa pamoja na Ofisi za Wilaya kuwezesha upatikanaji wa majengo ya ofisi na wajumbe wa baraza ili Mabaraza 35 yaliyobaki yaweze kutoa huduma.
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kushughulikia mashauri 33,250. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 Wizara imeshughulikia mashauri 29,573 ambapo mashauri mapya ni

14,093 na mashauri ya zamani ni 15,480. Kati ya hayo, mashauri 15,550 yameshughulikiwa na kutolewa uamuzi na mashauri 14,023 yanaendelea kushughulikiwa. Aidha, Wizara imeendelea kufanya maboresho ya Mfumo wa Kielektroniki wa Kusimamia Mashauri katika Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya ili kuongeza ufanisi. Katika mwaka 2024/25 Wizara itashughulikia mashauri 14,023 yaliyobaki na mengine yatakayojitokeza.
UTHAMINI WA MALI
Mheshimiwa Spika,
Wizara pamoja na majukumu mengine ina jukumu la kuratibu, kusimamia na kutoa huduma za uthamini kwa madhumuni mbalimbali ikiwemo kuiwezesha Serikali na Taasisi nyingine katika ulipaji wa fidia, ukadiriaji tozo na kodi za Serikali, mizania ya hesabu, dhamana, rehani na mirathi. Katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kuratibu na kusimamia uandaaji na uidhinishaji wa taarifa za uthamini 54,000 ambapo kati ya hizo, taarifa za uthamini wa kawaida ni 20,000 na taarifa za fidia zenye wafidiwa 34,000 na kushughulikia malalamiko 30 ya uthamini wa fidia.
Mheshimiwa Spika, hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara imeidhinisha taarifa za uthamini 57,285 sawa na asilimia 111.66 ya lengo ambapo kati ya hizo, taarifa za uthamini wa kawaida ni 22,311 na taarifa za uthamini wa fidia 34,974.

Aidha, malalamiko 91 ya fidia yalipokelewa na kushughulikiwa. Sehemu ya utekelezaji huu umehusisha mazoezi mbalimbali ya uthamini kwa ajili ya fidia kwa wananchi wanaopisha miradi ya kimkakati na maeneo ya hifadhi (Jedwali Na.10). Vilevile, Wizara imeendelea kushirikiana na Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro kufanya uthamini wa mali za wananchi wa Ngorongoro wanaohama kwa hiari kupisha shughuli za uhifadhi. Uthamini umefanyika kwa awamu sita (6) katika kata 11 na vijiji 25 ambapo mali za kaya 650 zenye thamani ya shilingi bilioni 3.79 zimefanyiwa uthamini.
Mheshimiwa Spika, kumekuwa na changamoto ya uhalisia wa viwango vya thamani ya ardhi, hali inayoathiri ukadiriaji na ukusanyaji wa mapato ya sekta ya ardhi na utoaji wa huduma za uthamini. Kufuatia hali hii, Wizara imeanza kuandaa vitalu vya thamani ya ardhi vitakavyoakisi thamani halisi ya ardhi ili kuiwezesha Serikali kukusanya mapato stahiki yanayotokana na sekta ya ardhi. Aidha, vitalu vya thamani vitatumika kurahisisha kazi ya uthamini na hivyo kupunguza muda na gharama. Taarifa za vitalu hivyo zitatumika katika Mfumo Unganishi wa Taarifa za Ardhi (ILMISv3). Kazi ya kuandaa vitalu vya thamani ya ardhi kwa awamu ya kwanza imeanza katika Mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Mbeya, Mwanza, Tanga, Pwani, Tabora na Kigoma.

Mheshimiwa Spika, kumekuwepo malalamiko yanayohusu ulipaji wa fidia kutoka katika maeneo mbalimbali nchini. Malalamiko hayo yanatokana na wananchi kutofahamu kwa hakika wadau wanaohusika na ulipaji wa fidia; baadhi ya taasisi kufanya uthamini wa fidia bila kuwepo fedha kwa ajili ya malipo ya fidia; na kutozingatiwa kwa taratibu za uhakiki wa taarifa za uthamini wa fidia kwa mujibu wa Sheria ya Uthamini na Usajili wa Wathamini, Sura 138. Ili kuondoa malalamiko ambayo yamekuwa yakijitokeza mara kwa mara, Wizara imetoa Waraka wa Uthamini na Fidia Na. 1 wa Mwaka 2024 ambao pamoja na mambo mengine unaelekeza taratibu zinazopaswa kuzingatiwa wakati wa shughuli za uthamini, uhakiki wa taarifa za uthamini na ulipaji wa fidia. Naomba ifahamike kuwa, jukumu la Wizara ni kuratibu uthamini na wajibu wa kulipa fidia ni wa taasisi itakayonufaika na uthamini huo. Aidha, natoa wito kwa wadau wote wa uthamini kuhakikisha wanazingatia Waraka wa Uthamini na Fidia.
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2024/25, Wizara itaratibu na kusimamia uandaaji wa taarifa za uthamini 54,000. Kati ya hizo, taarifa za uthamini wa kawaida ni 20,000 na taarifa za uthamini wa fidia 34,000. Aidha, Wizara itaendelea kuratibu utekelezaji wa mazoezi mbalimbali ya uthamini wa mali na kushiriki katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na Serikali. Vilevile, malalamiko yatokanayo na uthamini wa fidia yataendelea

kushughulikiwa kadri yatakavyojitokeza.
UPANGAJI NA UENDELEZAJI WA MIJI NA MAKAZI
Mheshimiwa Spika,
Wizara imedhamiria kuboresha usimamizi na utekelezaji wa upangaji wa miji na makazi. Upangaji miji na makazi ni mojawapo ya majukumu ya msingi ya Wizara ambayo yanaratibiwa na kutekelezwa kwa mujibu wa sera, sheria, kanuni na taratibu za uendelezaji miji. Utekelezaji wa jukumu hili unalenga kuwa na makazi yaliyopangwa, kuhifadhi mazingira na kuwa na uhakika wa ardhi kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo uwekezaji.
Utangazaji wa Maeneo ya Upangaji Miji
Mheshimiwa Spika,
makazi ya vijiji ni miji ya baadaye. Baadhi ya makazi hayo yanakua kwa haraka katika sura ya kimji kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo ongezeko la idadi ya watu, shughuli za kiuchumi, mabadiliko ya mitazamo ya kimaisha, kuboreshwa kwa huduma za kijamii na miundombinu ya msingi mathalan; barabara, umeme, maji, shule, huduma za afya na uwekezaji wa miradi mikubwa ya kimkakati katika maeneo hayo. Kufuatia hali hiyo, Wizara imeendelea kutangaza katika Gazeti la Serikali maeneo ya vijiji yaliyoiva na kuwa na sifa ya kupangwa, kusimamiwa na kuendelezwa kimji kwa mujibu wa

Sheria ya Mipangomiji, Sura 355. Maeneo haya hutangazwa baada ya kupokea na kuridhia mapendekezo kutoka Mamlaka za Upangaji kwa kuzingatia vigezo vilivyowekwa. Aidha, makazi ya vijiji ambayo hayajakidhi vigezo vya kuendelezwa kimji, yataendelea kuendelezwa na kusimamiwa kwa kuzingatia Mwongozo wa Upangaji na Ujenzi wa Nyumba Bora Vijijini wa mwaka 2021.
Mheshimwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara iliendelea kushirikiana na Mamlaka za Upangaji kutambua na kutangaza maeneo yaliyoiva kwa ajili ya kupangwa, kusimamiwa na kuendelezwa kimji. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 jumla ya maombi ya maeneo 317 kutoka kwenye mamlaka za upangaji 49 yalipokelewa ambapo maombi 88 yalitangazwa katika Gazeti la Serikali na maombi 229 yapo katika hatua mbalimbali za utangazaji. Kati ya hayo, maombi 65 ni maeneo mapya na maombi 252 ni maeneo ya urasimishaji makazi (Jedwali Na.11). Nazihimiza Mamlaka za Upangaji nchini kuendelea kutambua na kuwasilisha mapendekezo ya maeneo yaliyoiva kupangwa, kusimamiwa na kuendelezwa kimji ili yatangazwe katika Gazeti la Serikali kuwa maeneo ya upangaji kwa mujibu wa Sheria.

Uandaaji wa Mipango Kabambe
Mheshimiwa Spika,
Mipango Kabambe hutoa dira ya matumizi ya jumla ya ardhi na hivyo kuzisaidia Mamlaka za upangaji (Majiji, Manispaa, Miji na Miji Midogo) katika udhibiti, usimamizi, ukuaji na uendelezaji wa miji. Mipango Kabambe ni dira ya utoaji wa huduma mbalimbali za kiuchumi, kijamii na kimazingira pamoja na usalama wa ustawi wa miji na watu wake. Mipango hii huandaliwa kwa mujibu wa Sheria ya Mipangomiji, Sura 355 ambapo Wizara ina jukumu la utoaji wa mwongozo wa uandaaji wa mipango kabambe, uidhinishaji wa mipango, ufuatiliaji wa utekelezaji, uidhinishaji wa marekebisho ya matumizi ya ardhi pamoja na uhuishaji wa mipango hiyo pindi utekelezaji wake unapofikia ukomo au kujitokeza kwa mahitaji ya ulazima.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu huo, Wizara katika mwaka 2023/24, iliahidi kuendelea kushirikiana na Mamlaka za Upangaji katika uandaaji na utekelezaji wa Mipango Kabambe kwa mujibu wa Sera, Sheria, Kanuni na Miongozo iliyopo. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 Mpango Kabambe wa Mji wa Bagamoyo umekamilika na kuidhinishwa. Mipango Kabambe mitatu (3) ya Miji ya Kahama na Mafinga na Jiji la Kibiashara la Kwala ipo katika hatua mbalimbali za uandaaji. Aidha, ufuatiliaji wa utekelezaji wa Mipango Kabambe ya Miji mitano (5) katika Halmashauri za Jiji la Arusha, Manispaa ya Iringa, Miji ya Babati, Tunduma na Njombe umefanyika.

Mheshimiwa Spika, ufuatiliaji huo ulibaini utekelezaji usioridhisha, ushirikishwaji duni wa wadau na wananchi, upungufu wa wataalam na vitendea kazi. Kutokana na changamoto hizo, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais - TAMISEMI imezielekeza Mamlaka za Upangaji kusimamia kikamilifu utekelezaji wa Mipango Kabambe na Mipangokina na kuendelea kutenga bajeti kwa ajili ya kuihuisha na kuifanyia marekebisho ya matumizi kadri ya mahitaji yanavyojitokeza.
Mheshimwa Spika, katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kushirikiana na Mamlaka za Upangaji kusimamia utekelezaji na uzingatiaji wa Mipango Kabambe katika Mamlaka za Upangaji minne (4) ambayo ni Jiji la Tanga, Manispaa ya Moshi na Halmashauri za Miji ya Korogwe na Kibaha. Vilevile, Wizara itasimamia ukamilishaji wa uandaaji wa Mipango Kabambe miwili (2) ya Halmashauri za Mji wa Mafinga na Manispaa ya Kahama. Pia, Wizara itaratibu uandaaji wa mipango ya uendelezaji wa maeneo matatu (3) yaliyochakaa katika Majiji ya Dar es Salaam, Mwanza na Arusha kwa lengo la kuyaboresha maeneo hayo ili yaendane na mahitaji ya kijamii na kiuwekezaji ya sasa na baadae.

Uandaaji wa Mipangokina
Mheshimiwa Spika,
Wizara ina jukumu la kuratibu uandaaji na uidhinishaji wa Mipangokina ili kuelekeza ukuaji, uboreshaji wa makazi, hifadhi ya mazingira, kuondoa ukinzani wa matumizi ya ardhi na kutoa uhakika wa upatikanaji wa maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali yakiwemo ya uwekezaji, makazi, biashara, miundombinu na huduma za jamii. Mipangokina huandaliwa kama sehemu ya utekelezaji wa mapendekezo ya matumizi ya ardhi yaliyomo katika mipango kabambe kupitia Mamlaka za Upangaji. Mipangokina inawezesha upimaji wa viwanja ardhini na uendelezaji wa maeneo ya huduma kama barabara, simu, umeme, mawasiliano na kurahisisha umilikishaji.



Mpango kina wa makazi Kijiji cha Kapanga kilichopo halmashauri ya wilaya ya Tanganyika mkoani Katavi

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kuidhinisha michoro ya Mipangokina 2,000 kutoka kwenye Mamlaka za Upangaji nchini. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 michoro ya Mipangokina 1,783 yenye jumla ya viwanja 244,519 vya matumizi mbalimbali imeidhinishwa sawa na asilimia 89.1 ya lengo. Katika mwaka 2024/25, Wizara inatarajia kuidhinisha Mipangokina 2,000 kutoka katika Mamlaka za Upangaji nchini.
Urasimishaji wa Makazi
Mheshimiwa Spika,
Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Makazi ya mwaka 2000 zinaelekeza kuwa maeneo ya makazi yaliyoendelezwa bila kupangwa yatarasimishwa. Katika kutekeleza matakwa ya sera hizi, Wizara imeendelea kuratibu urasimishaji wa makazi yaliyoendelezwa bila kupangwa kwa kuishirikisha jamii, asasi za kiraia na sekta binafsi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kurasimisha makazi 300,000. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, jumla ya makazi 237,424 sawa na asilimia 79.14 yamerasimishwa (Jedwali Na.12). Katika mwaka 2024/25 Wizara itarasimisha makazi 500,000. Aidha, Wizara itakamilisha tathmini ya utekelezaji wa Programu ya Kurasimisha Makazi na Kudhibiti Makazi yasiyopangwa Mijini (2013-2023) ili kubaini mafanikio, changamoto zilizojitokeza na matarajio ya baadaye. Pia, Wizara kwa

kushirikiana na Mamlaka za Upangaji na Sekta Binafsi inaendelea kufanya uhamasishaji kwa wananchi ambao bado makazi yao hayajarasimishwa ili kukamilisha zoezi hilo na kuendeleza kliniki za ardhi ili kukwamua urasimishaji katika maeneo ambayo hayajakamilisha miradi ya urasimishaji makazi yasiyopangwa.
Mheshimiwa Spika, Ili kufikia lengo la kurasimisha makazi 500,000 katika mwaka 2024/25, Wizara itaanza na kukwamua urasimishaji ambao ulikwama kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo uchangiaji hafifu wa wananchi na baadhi ya kampuni zilizofanya urasimishaji kutokamilisha kazi kwa wakati. Mathalan, katika mkoa wa Dar es Salaam urasimishaji haukukamilika katika mitaa 270. Ili kukwamua kazi hizo Wizara itaajiri wataalam wa muda wa mipangomiji na upimaji na kuhakikisha kazi hizo zinakamilika. Zoezi hili limeanza kutekelezwa katika mitaa 13 ya mkoa wa Dar es Salaam. Natoa Wito kwa wananchi ambao makazi yao hayajarasimishwa kujitokeza kurasimishiwa.
Udhibiti na Usimamizi wa Uendelezaji Miji (mabadiliko ya matumizi ya ardhi)
Mheshimiwa Spika
, kutokana na kuongezeka kwa shughuli za kiuchumi na kijamii kumekuwepo na ongezeko la ukuaji wa miji na kusababisha hitaji kubwa la kubadili matumizi ya ardhi, Wizara

imefanya marekebisho ya Kanuni za Viwango vya Kupanga Ukubwa wa Ardhi kwa matumizi mbalimbali ili kukidhi mahitaji ya sasa na ya baadaye. Pia, imeboresha Kanuni ya Makundi ya Matumizi na Madaraja ya Matumizi ili kuwezesha matumizi ya ardhi kushabihiana hivyo kuondoa migogoro ya matumizi ya ardhi. Vilevile, katika Kanuni hiyo mchakato wa mabadiliko ya matumizi ya ardhi umeboreshwa ambapo maombi yatajadiliwa katika ngazi ya mtaa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ndipo yajadiliwe na Kamati za Halmashauri ili kuimarisha ushirikishwaji wa wadau hivyo kupunguza migogoro ya ardhi.
Mheshimiwa Spika, maeneo ya wazi yanapaswa kusimamiwa, kutunzwa na kulindwa ili yatumike kwa maslahi mapana ya umma. Hata hivyo, maeneo hayo yamekuwa yakivamiwa na kubadilishwa matumizi au kutumiwa vinginevyo kutokana na sababu nyingi zikiwemo uvamizi wa makusudi, kutolipwa fidia kwa wamiliki wa asili, kutumika kama vyanzo vya mapato ya Halmashauri na usimamizi usioridhisha wa Mamlaka zilizopewa kusimamia maeneo hayo. Ili kukabiliana na matumizi holela ya maeneo hayo, matumizi ya maeneo ya wazi yamewekewa utaratibu wa kuidhinishwa na Wizara endapo yatahitajika kutumika kwa maslahi ya umma. Napenda kusisitiza kuwa maeneo ya wazi ni lazima yatunzwe, yalindwe na kudumishwa ili

yatumike kwa manufaa ya umma yakiwemo kufanyia mikutano ya hadhara, kupendezesha mandhari na mazingira ya mji, michezo kwa watoto katika mitaa, watu kupumzika, kufanyia chanjo kwa umma na kutumika kama hifadhi ya watu na misaada wakati wa maafa, majanga au dharura.
Mheshimiwa Spika
, katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kuratibu na kuidhinisha mabadiliko ya matumizi ya ardhi 500. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, jumla ya maombi 465 sawa na asilimia 93.2 ya mabadiliko ya matumizi ya ardhi yaliidhinishwa. Katika mwaka 2024/25 Wizara itaendelea kupokea na kuidhinisha maombi ya mabadiliko ya matumizi ya ardhi 500 kwa kuzingatia sheria na kanuni za mipangomiji.
Usimamizi na Uratibu wa Sekta ya Nyumba
Mheshimiwa Spika,
sekta ya nyumba imeendelea kuwa na mchango muhimu kiuchumi na kijamii kwa mtu mmoja mmoja na Taifa kwa ujumla. Upatikanaji wa nyumba ni mojawapo ya kiashiria cha kukua kwa uchumi wa nchi na kupungua kwa umasikini wa kipato. Wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali imeendelea kuweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa huduma za uendelezaji nyumba ikiwemo upatikanaji wa mikopo ya nyumba yenye masharti nafuu. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 Serikali kupitia Tanzania

Mortgage Refinancing Company (TMRC) imewezesha taasisi za fedha 31 kutoa mikopo ya nyumba yenye riba nafuu kiasi cha shilingi bilioni 587.
Mfuko wa Mikopo ya Nyumba kwa Watumishi wa Serikali
Mheshimiwa Spika,
Mfuko wa Mikopo ya Nyumba kwa Watumishi wa Serikali unalenga kuongeza upatikanaji wa makazi bora kwa watumishi wa Serikali, kuwawezesha kukarabati, kukamilisha au kujenga nyumba mpya. Katika mwaka 2023/24, Wizara kupitia Mfuko ilipanga kukopesha watumishi 100. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 mfuko umewezesha watumishi 87 kupata mikopo ya nyumba yenye thamani ya shilingi Billioni 1.06 hivyo kufanya watumishi waliopata mikopo kufikia 1,706 ikiwa na thamani ya shilingi bilioni 10.75. Katika mwaka 2024/25 watumishi wa Serikali 100 watawezeshwa kupata mikopo ya nyumba yenye thamani ya shilingi billioni 2.2.
Ushirikiano na Taasisi za Kimataifa katika Uendelezaji wa Makazi
Mheshimiwa Spika,
Wizara imeendelea kushirikiana na taasisi mbalimbali za kimataifa ikiwemo Shirika la Makazi Duniani (UN-Habitat) katika masuala ya uendelezaji makazi nchini. Ushirikiano huo, licha ya kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia baina ya nchi yetu na nchi nyingine

Duniani, umekuwa ni jukwaa la kujifunza na kupata uzoefu katika kutekeleza Ajenda Mpya ya Makazi Duniani ambayo inatekelezwa na nchi zote wanachama wa umoja wa mataifa.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo ya makazi iliandaa maadhimisho ya Siku ya Makazi Duniani yaliyofanyika tarehe 02 Oktoba, 2023 Jijini Dodoma yakiongozwa na kauli mbiu ya “Resilient Urban Economies - Cities as Drivers of Growth and Recovery" ikimaanisha “Uchumi Himilivu wa Miji - Miji Kichocheo cha Ukuaji na Ufufuaji wa Uchumi. Maadhimisho haya yalitolewa kwa njia ya mjadala na mafunzo ambapo wawakilishi 150 kutoka Wizara, Taasisi za elimu, Jiji la Dodoma, Taasisi zinazotoa huduma, NHC na WHC walishiriki. Katika mkutano huo, wadau walijadili namna ya kufanya miji kuwa kichocheo cha ukuaji na ufufuaji wa uchumi hasa baada ya janga la UVIKO 19 na namna ya kujipanga na majanga yajayo.
Mheshimiwa Spika, Wizara ilishiriki Mkutano wa Umoja wa Mataifa kuhusu Malengo ya Maendeleo Endelevu uliofanyika mwezi Julai, 2023 Jijini New York, Marekani. Mkutano huo ulilenga kuwasilisha taarifa ya utekelezaji wa hiari wa Malengo ya Mendeleo Endelevu (SDGs) ya Umoja wa Mataifa ambayo kwa hapa nchini, malengo hayo huratibiwa na Wizara ya Fedha. Katika wasilisho

hilo, Wizara sambamba na Wizara nyingine, imehusika kitaalamu na Lengo Na. 11 kati ya malengo 5 yaliyokuwa yanatolewa taarifa katika mkutano huo kuhusu kufanya “Majiji na Makazi kuwa Jumuishi, Salama, Stahimilivu na Endelevu”. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kuimarisha uhusiano na taasisi hizo za kimataifa katika masuala ya maendeleo ya makazi.
USIMAMIZI WA SEKTA YA MILKI
Mheshimiwa Spika,
pamoja na majukumu mengine, Wizara ina jukumu la kusimamia Sekta ya Milki nchini. Sekta ya Milki inajumuisha ardhi iliyopangwa na kupimwa kwa kujengwa nyumba za makazi, majengo ya biashara, viwanda, maeneo ya burudani na majengo ya matumizi maalum. Wadau wa Sekta ya Milki wanajumuisha wawekezaji, wamiliki wa majengo, wapangaji, taasisi za fedha, mawakala, wanunuzi wa nyumba na viwanja na watafiti wa soko la nyumba. Sekta hii imeendelea kukua na kuvutia wadau wengi zaidi kutokana na fursa za uwekezaji katika nyanja mbalimbali ikiwemo soko la fedha na nyumba za kupangisha.
Mheshimiwa Spika, ili kuimarisha usimamizi wa sekta hii, katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kukamilisha uandaaji wa Sheria na kanuni za kusimamia Sekta ya Milki, kutoa elimu kwa wadau na kuandaa kanzidata ya Waendelezaji Milki pamoja na mawakala wa Milki. Napenda kulitaarifu Bunge lako Tukufu kuwa Mapendekezo ya Kutunga

Sheria ya Milki yameandaliwa na kuwasilishwa kwenye mamlaka ya uamuzi. Mapendekezo hayo pamoja na mambo mengine yanalenga kuanzisha Mamlaka ya Kusimamia Sekta ya Milki ‘Real Estate Regulatory Authority’ ili kuongeza tija na ufanisi katika usimamizi na uratibu wa sekta hii muhimu kwa uchumi wa nchi.
Mheshimiwa Spika, Wizara iliratibu Mkutano wa wadau wa Sekta ya Milki uliofanyika tarehe 19 – 20 Januari, 2024 jijini Dar es Salaam ukiwa na lengo la kuwatambua mawakala na kujadili namna bora ya utekelezaji wa shughuli zao. Kauli mbiu ya Mkutano huo ilikuwa ni “Urasimishaji wa Shughuli za Mawakala wa Milki kwa Maendeleo ya Taifa”. Mkutano huo ulihudhuriwa na wawakilishi kutoka kampuni za uendelezaji milki; mawakala wa milki; na taasisi za umma na binafsi. Aidha, kupitia mkutano huu Wizara imeweza kuboresha taarifa za kanzidata ya mawakala na wadau mbalimbali wa sekta ya milki.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25, Wizara imepanga kuanzisha kanzidata kwa ajili ya usajili wa miradi ya uendelezaji milki. Aidha, Wizara itaendelea kutoa elimu kwa wadau kuhusu shughuli za sekta ya milki ikiwa ni pamoja na kuwashirikisha katika kuboresha mazingira ya kuvutia uwekezaji na biashara katika Sekta ya Milki. Natoa wito kwa wadau wote wa sekta ya milki kuhakikisha wanajitokeza ili shughuli

zao ziweze kutambuliwa na Serikali.
UPIMAJI NA RAMANI
Mheshimiwa Spika,
Wizara ina jukumu la kusimamia na kuratibu shughuli za upimaji ardhi wa nchi kavu na ndani ya maji; utayarishaji wa ramani kwa ajili ya utekelezaji wa mipango mbalimbali ya Serikali; na kutoa miongozo, kanuni na taratibu zinazohusu upimaji ardhi kulingana na mabadiliko ya teknolojia na mahitaji.
Uwekaji wa Alama za Msingi za Upimaji Ardhi
Mheshimiwa Spika,
alama za msingi ni miongoni mwa miundombinu muhimu katika kazi za upimaji ardhi. Wizara inaendelea kuratibu na kuongeza alama za msingi za upimaji ili kuwezesha na kurahisisha kazi, kupunguza muda pamoja na gharama za upimaji ardhi. Katika mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kuweka alama mpya za msingi 267 katika maeneo mbalimbali nchini. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 alama za msingi za upimaji 378 zimewekwa katika mikoa ya Dodoma (47), Manyara (13), Tanga (40), Tabora (22), Singida (10), Iringa
(26), Pwani (27), Mara (14), Kigoma (12), Geita (24),
Kagera (12), Kilimanjaro (10) na Shinyanga (47) na hivyo kuwa na jumla ya Alama za Msingi za Upimaji 1,423. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaweka alama mpya za msingi 150 katika Halmashauri mbalimbali nchini. Lengo la Wizara ni kuwekeza

zaidi kwenye usimikaji wa Vituo vya Kielektroniki vya Upimaji (Continuously Operating Reference Station- CORS) ambavyo vitawezesha kazi za upimaji kufanyika kwa ufanisi zaidi.


Alama za Msingi za upimaji wa ramani.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kuanza hatua za awali za ujenzi wa vituo 22 vya kielektroniki vya upimaji (Continuously Operating Reference Station - CORS) katika makao makuu ya mikoa 22. Vituo hivyo ni maalum kwa ajili ya kutuma taarifa za upimaji (GNSS signals) kwa wapima ardhi. Mkandarasi atakayefanya kazi ya kusimika vituo hivyo amepatikana, makubaliano yamefanyika na kazi ya usimikaji wa

vituo hivyo itafanyika katika mwaka 2024/25.
Upimaji wa viwanja na mashamba
Mheshimiwa Spika
, katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kuratibu, kusimamia na kuidhinisha viwanja 500,000 na mashamba 500. Hadi tarehe
15 Mei, 2024, viwanja 249,340 na mashamba 7,559 yamepimwa na kuidhinishwa sawa na asilimia 49.87 ya lengo la viwanja na asilimia 1,511.8 ya lengo la mashamba (Jedwali Na.13). Ongezeko kubwa la mashamba yaliyopimwa na kuidhinishwa linatokana na mpango wa Serikali wa kuhamisha wananchi kutoka katika eneo la hifadhi ya Ngorongoro kwenda Msomera na Saunyi mkoani Tanga. Katika mwaka 2024/25, Wizara itasimamia upimaji na uidhinishwaji wa viwanja 500,000 na mashamba 500.
Utayarishaji wa Ramani
Mheshimiwa Spika,
Ramani ni zao la kazi za upimaji ardhi, ambalo huweza kupatikana katika mfumo wa nakala ngumu au nakala tete. Ramani huzalishwa kutokana na taarifa za msingi za kijiografia. Ramani zinazotayarishwa zinajumuisha za viwanja, mashamba, mipaka ya kiutawala na kimataifa na Hifadhi za Taifa. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, ramani za mipaka ya kiutawala ya Wilaya 17 katika Mikoa ya Dar es Salaam (5), Kagera (7), Dodoma (2), Tanga (1), Arusha (1) na Mbeya (1)

zimeandaliwa. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kuandaa ramani za mipaka ya kiutawala ya Wilaya
25. Mwelekeo wa Wizara ni kuwa na Ramani za kidigitali ili kurahisisha upatikanaji wa ramani.
Mheshimiwa Spika, kumekuwepo na changamoto ya uandaaji wa ramani unaofanywa na baadhi ya taasisi na sekta binafsi bila kuzingatia sheria na ubora hali inayosababisha kuwepo kwa tafsiri zisizo sahihi za mipaka ya kimataifa na kiutawala. Matokeo yake ni kuwepo kwa migogoro ambayo ingeweza kuzuilika endapo taratibu za uandaaji wa ramani zingezingatiwa kwa mujibu wa Sheria ya Upimaji, Sura 324. Naelekeza taasisi zote za umma na binafsi zizingatie takwa la kisheria linalompa mamlaka Mkurungenzi wa Upimaji na Ramani kuandaa na kuidhinisha ramani zote zikiwemo za mipaka ya kiutawala na kimataifa.
Upimaji wa Mipaka ya Vijiji
Mheshimiwa Spika
, Wizara ina jukumu la kuratibu na kupima mipaka ya vijiji ambapo katika mwaka 2023/24 ilipanga kuhakiki na kupima mipaka ya vijiji 100. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, jumla ya vijiji 742 vimehakikiwa na kupimwa mipaka. Kati ya hivyo, vijiji 475 vimehakikiwa mipaka na vijiji 267 vimepimwa (Jedwali Na.14). Aidha, migogoro ya mipaka ya vijiji vitano (5) vya Bangalala, Mwembe, Makanya, Mgwasi na Nasuro katika Wilaya ya Same imetatuliwa. Vilevile, mgogoro wa

mipaka kati ya shamba la Malonje (Efatha) na vijiji vitano (5) vya Sikaungu, Msandamuungano “A”, Msandamuungano “B”, Songambele Azimio na Malonje katika Wilaya ya Sumbawanga umetatuliwa. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kushirikiana na Ofisi ya Rais-TAMISEMI kuhakiki na kupima mipaka ya vijiji 1,000 nchini. Natoa rai kwa mamlaka za Serikali za Mitaa na Sekretarieti za Mikoa kuhakikisha kuwa Vijiji vinavyoanzishwa vinapimwa mipaka yake kabla ya kutangazwa katika gazeti la Serikali.
Tafsiri na Uhakiki wa Mipaka ya Kiutawala na Hifadhi
Mheshimiwa Spika,
Wizara ina jukumu la kutafsiri ardhini Matangazo ya Serikali (GNs) ya mipaka ya utawala na hifadhi kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Wizara za kisekta na Mamlaka mbalimbali ili kutatua changamoto za mipaka. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, matangazo ya mipaka ya kiutawala saba (7) yametafsiriwa katika Wilaya za Sumbawanga na Momba (2), Wanging’ombe na Makete (2), Shinyanga na Nyang’hwale (2), Kilindi na Kiteto (1). Vilevile, Tangazo la Serikali namba 235 la mwaka 1968 la Hifadhi ya Taifa ya Serengeti limetafsiriwa na kuwezesha utatuzi wa mgogoro wa mpaka wa vijiji saba (7) vya Nyambuli, Machochwe, Mbalibali, Bisarara, Bonchugu, Nyamakendo na Merenga katika Wilaya ya Serengeti.

Upangaji na Upimaji wa Viwanja Mbadala vya Waathirika wa Maporomoko ya Mlima Hanang’
Mheshimiwa Spika,
nchi yetu imekumbwa na maafa yaliyotokana na mvua nyingi ambazo zimeendelea kunyesha katika maeneo mbalimbali nchini. Miongoni mwa maeneo yaliyokumbwa na maafa hayo ni Wilaya ya Hanang’. Kufuatia maafa yaliyotokea katika Wilaya ya Hanang’ kutokana na kuporomoka kwa sehemu ya Mlima Hanang’, Wizara kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais- TAMISEMI imepanga na kupima viwanja mbadala vya waathirika wa maporomoko hayo. Viwanja hivi vimepimwa kutoka katika eneo la ekari 100 zilizomegwa kutoka shamba la Jeshi la Magereza lililopo katika kijiji cha Gidagamowd, Wilaya ya Hanang’. Jumla ya viwanja 269 vimepimwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo makazi (235), makazi na biashara (15), biashara (7) na huduma za jamii (12). Aidha, waathirika wote 108 wamepatiwa viwanja kwa ajili ya makazi.
Upangaji na Upimaji wa Viwanja na Mashamba kwa Ajili ya Wananchi Wanaohama kwa Hiari Kutoka Katika Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro
Mheshimiwa Spika,
Wizara kwa kushirikiana na Wizara ya Maliasili na Utalii (Mamlaka ya Hifadhi ya Eneo la Ngorongoro) inaendelea na upimaji wa viwanja na mashamba kwa ajili ya makazi, kilimo na ufugaji. Kazi hii inafanyika

katika vijiji vya Msomera (Handeni) na Saunyi (Kilindi) katika Mkoa wa Tanga ambapo lengo ni kupima viwanja 10,000 na mashamba 8,500.
Hadi tarehe 15 Mei, 2024, viwanja 5,031 vya makazi vyenye wastani wa ukubwa wa ekari 2.5 na mashamba 7,897 yenye ukubwa wa wastani wa ekari 5 yamepimwa. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa, pamoja na changamoto zilizojitokeza katika utekelezaji ikiwemo mvua kubwa zilizonyesha, Wizara imejipanga kukamilisha upimaji wa mashamba ifikapo Juni, 2024.


Muonekano wa mpango wa matumizi ya ardhi katika eneo la Msomera wilayani Handeni mkoa wa Tanga.

HUDUMA ZA TEHAMA
Mheshimiwa Spika,
mpango wa Wizara ni kuifanya TEHAMA kuwa nyenzo muhimu ya kuendesha shughuli za sekta ya ardhi. Lengo la hatua hiyo ni kuongeza uwazi, ufanisi, uwajibikaji na kupunguza gharama na muda wa utoaji huduma. Wizara imekamilisha usanikishaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Huduma za Ardhi kwa kutumia watalaam wa ndani. Hatua inayoendelea ni kuhamisha taarifa kutoka kwenye mifumo ya zamani na majalada kwa awamu kwenda kwenye Mfumo ulioboreshwa. Aidha, mfumo utaanza kutumika kwa awamu ya kwanza katika Mikoa ya Arusha, Tanga, Mbeya, Mwanza na Dodoma ifikapo Juni, 2024. Manufaa ya mfumo huu ni pamoja na: -
Kuwezesha wananchi kuomba huduma bila kulazimika kwenda Ofisi za Ardhi;
Kufahamu muda ambao huduma inayoombwa itakamilika. Hii itawapa wananchi uwezo wa kutoa taarifa endapo watacheleweshewa huduma;
Kuondoa changamoto ya upotevu wa nyaraka zinazowasilishwa na wananchi kwani zitakuwa zinawasilishwa kupitia mfumo (online);
Kuongeza uwazi na uwajibikaji katika ngazi zote za utendaji kazi kwa kuwa viongozi wataweza kufuatilia mwenendo wa utekelezaji wa majukumu unavyoendelea;

  • Kuunganishwa na mifumo mingine ya Serikali ili kurahisisha utoaji wa huduma; na
  • Kuondoa changamoto ya miliki pandikizi na hivyo kudhibiti migogoro ya ardhi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kusimika na kusambaza miundombinu wezeshi ya TEHAMA katika Ofisi za Ardhi za Mikoa 25 na Halmashauri 132. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, usimikaji wa miundombinu wezeshi ya TEHAMA katika Halmashauri 44 imekamilika na kazi ya usimikaji wa miundombinu hiyo inaendelea katika Halmashauri 41. Pamoja na huduma nyingine, miundombinu hii itatumika katika utoaji wa huduma za ardhi kupitia Mfumo wa Usimamizi wa Huduma za Ardhi.
Mheshimiwa Spika, Wizara pia, iliahidi kuanzisha wavuti ya wateja (Self-Service Web Portal) kwa lengo la kuwawezesha wananchi kupata huduma kupitia wavuti hiyo bila kulazimika kwenda ofisi za ardhi na hivyo kupunguza gharama na muda wa kupata huduma. Napenda kuliarifu Bunge lako tukufu kwamba usanikishaji wa Wavuti hiyo pamoja na Mobile App umekamilika na huduma zimeanza kutolewa kupitia wavuti hiyo. Katika mwaka 2024/25, Wizara itakamilisha usambazaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Huduma za Ardhi katika Mikoa iliyobaki hatua kwa hatua. Pia, itawajengea uwezo watumiaji wa Mfumo huo

katika ngazi ya Wizara, Mikoa na Halmashauri. Vilevile, wananchi watajengewa uwezo kuhusu matumizi ya Mfumo kwa njia mbalimbali ikiwemo vipeperushi, mitandao ya kijamii, vyombo vya habari, mabango na kwa njia ya video zitakazopatikana kwenye Mfumo.
MAPITIO YA SERA NA SHERIA
Mheshimiwa Spika,
Wizara imeendelea kuhakikisha kuwa, Sera, Sheria na Kanuni za Sekta ya Ardhi zinafanyiwa marekebisho ili kukidhi mahitaji. Katika kutekeleza azma hiyo, Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 na Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Makazi ya mwaka 2000 zimeendelea kufanyiwa marekebisho ambapo Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995 (Toleo la mwaka 2023) imeidhinishwa. Hatua inayofuata ni kutoa elimu kwa umma, kufanya marekebisho ya sheria mbalimbali na kuanza utekelezaji wa mkakati wa kutekeleza Sera. Aidha, Sera ya Taifa ya Maendeleo ya Makazi ya mwaka 2000 inaendelea kufanyiwa marekebisho ambapo pamoja na kuhuisha masuala ya makazi, itajumuisha masuala mahsusi ya usimamizi wa sekta ya nyumba ili kuongeza tija na ustawi wa wananchi na Taifa kwa ujumla.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kukamilisha taratibu za kutunga na kurekebisha sheria mbalimbali za sekta ya ardhi. Napenda kuliarifu Bunge lako

Tukufu kuwa Mapendekezo ya Kutunga Sheria ya Chuo cha Ardhi, Sheria Mpya ya Upimaji na Usajili wa Wapima Ardhi na Sheria ya Milki yameandaliwa na yapo katika hatua za ukamilishaji. Aidha, marekebisho ya Sheria ya Usajili wa Wataalam wa Mipangomiji, Sura 426 yamefanyika ili pamoja na masuala mengine, kuainisha na kuongeza wigo wa madaraja ya Wataalam wa Mipangomiji na sifa za usajili kwa kila daraja.
Mheshimiwa Spika, ili kuboresha utaratibu wa utekelezaji wa shughuli za Madalali na Wasambaza Nyaraka wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya, Kanuni za Uteuzi, Malipo na Nidhamu kwa Madalali wa Baraza na Wasambaza Nyaraka zimefanyiwa marekebisho na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 61 la tarehe 26 Januari, 2024. Aidha, Kanuni za Ada kwa Huduma za Uthamini na Ushauri wa Kitaalam za mwaka 2023 zimetungwa na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 548 la tarehe 4 Agosti, 2023. Kanuni hizi zinalenga kuboresha huduma za uthamini na zitatumika kwa Wathamini waliosajiliwa na kutoa huduma za uthamini na ushauri wa kitaalam kwa sekta binafsi. Vilevile, Kanuni za Uthamini na Usajili wa Wathamini (Mafunzo na Mitihani) za mwaka 2023 zimefanyiwa marekebisho na kutangazwa kwenye Gazeti la Serikali Na. 450 la tarehe 7 Julai, 2023.

Mheshimiwa Spika, Wizara imetunga upya Kanuni mbili (2) za Sheria ya Mipangomiji, Sura
355. Kanuni hizo ni Kanuni ya Viwango vya Kupanga Maeneo kwa Matumizi Mbalimbali ya Ardhi na Kanuni ya Makundi ya Matumizi na Madaraja ya Matumizi. Madhumuni ya kutunga upya kanuni hizi ni kujumuisha matumizi mapya ambayo hayakuzingatiwa katika kanuni zilizokuwepo; baadhi ya vigezo na viwango vya upangaji kutokidhi mahitaji; mabadiliko ya miji yaliyoainishwa katika taarifa ya Sensa ya Watu na Makazi ya Mwaka 2022 pamoja na Sensa ya Majengo ya Mwaka 2022 yanayohitaji kufanyika kwa mabadiliko ya kanuni; kukidhi mahitaji ya kila matumizi ya ardhi; na mabadiliko ya kiuchumi na sura za miji kuhitaji mwongozo mpya wa kikanuni. Taratibu za kukamilisha utungaji wa kanuni hizo zinaendelea.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25 Wizara itakamilisha marekebisho ya Sera ya Maendeleo ya Makazi pamoja na kufanya marekebisho ya sheria na kanuni mbalimbali za sekta ya ardhi kadri itakavyohitajika.

MIRADI YA MAENDELEO
Programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24 Wizara iliidhinishiwa shilingi bilioni 4.5 kwa ajili ya kuendelea na utekelezaji wa Programu ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha ardhi. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara imepokea shilingi bilioni 3.6 kwa ajili ya utekelezaji wa Programu sawa na asilimia 80. Katika kipindi hicho, viwanja 10,463 vimepangwa, viwanja 9,463 vimepimwa na viwanja 8,177 vimemilikishwa kwenye Halmashauri 14.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2021/22 Wizara ilizikopesha Mamlaka za Serikali za Mitaa 57, Ofisi ya Ardhi Mkoa wa Iringa, Chuo Kikuu Ardhi na Vyuo vya Ardhi vya Morogoro (ARIMO) na Tabora (ARITA) shilingi bilioni 50 kwa ajili ya kuongeza kasi ya kupanga, kupima na kumilikisha ardhi. Wizara imeendelea kufuatilia marejesho ya fedha hizo kwa kushirikiana na Ofisi ya Rais – TAMISEMI. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, shilingi billioni 23.71 zimerejeshwa na Halmashauri 55 ambapo Halmashauri 13 zimerejesha mikopo yao kwa asilimia 100; Halmashauri 42 zimerejesha sehemu ya fedha; na Halmashauri mbili (2) za Manispaa ya Shinyanga na Wilaya ya Musoma hazijarejesha kabisa (Jedwali Na.15). Napenda kuzipongeza Halmashauri ya Jiji la Mwanza;

Manispaa za Morogoro, Ilemela na Kigamboni; Halmashauri za Moshi, Meru, Kilosa, Geita, Kaliua, Mbozi; na Halmashauri za Miji ya Tunduma na Bariadi zilizotekeleza wajibu wa kurejesha fedha kwa mujibu wa makubaliano. Naungana na Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, kuzitaka Halmashauri na Taasisi ambazo hazijarejesha au hazijakamilisha marejesho, kurejesha fedha wanazodaiwa ifikapo Juni, 2024 ili kuziwezesha Halmashauri nyingine kunufaika na fedha hizo. Kwa halmashauri ambazo hazitatekeleza agizo hilo, fedha hizo zitakatwa moja kwa moja kutoka kwenye ruzuku zao.
Mheshimiwa Spika,
ili kuepuka changamoto zilizojitokeza kwenye utaratibu wa utoaji wa mikopo kwa awamu ya kwanza, Wizara imefanya maboresho katika utaratibu huo. Maboresho yaliyofanyika yanahusisha fedha kutolewa kupitia Ofisi za Ardhi za Mikoa; fedha kutolewa kwa awamu kwa kuzingatia hatua ya kazi iliyofikiwa; na fedha za mauzo ya viwanja kuwekwa kwenye akaunti maalum ya Mfuko wa Maendeleo ya Ardhi.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara imebuni na kusanifu Mradi wa Msalato Satellite City katika Jiji la Dodoma utakaokidhi mahitaji ya watu zaidi ya 14,776. Mradi huo utawezesha ujenzi wa makazi bora yenye miundombinu na huduma muhimu za jamii na

biashara za aina mbalimbali hivyo kupunguza msongamano wa wananchi wanaofuata mahitaji katikati ya mji. Katika mwaka 2024/25, Wizara imepanga kubuni na kusanifu miji ya Satelaiti miwili (2) katika majiji ya Dodoma (Msalato) na Arusha (AFCON City) ili kuwa na miji nadhifu na kudhibiti makazi holela. Aidha, Wizara itaendelea kusimamia kikamilifu matumizi ya fedha za mfuko ili kuwezesha halmashauri kupanga na kupima miradi iliyoandaliwa.


Muonekano wa Mradi wa Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi wa Msalato Satellite City jijini Dodoma

Mheshimiwa Spika, Wizara imeandaa mpango wa uendelezaji wa maeneo ya mijini yenye thamani kubwa yaliyochakaa ambayo hayatumiki kwa tija. Utekelezaji wa mpango huu utawezesha uboreshaji mandhari ya miji, kuchochea shughuli za kiuwekezaji na kuongeza thamani ya ardhi katika maeneo hayo. Ili kuwezesha utekelezaji, Wizara imeandaa Mwongozo wa Upangaji na Uendelezaji Upya wa Maeneo Yaliyochakaa unaoweka utaratibu wa utekelezaji ambao utasambazwa kwenye Mamlaka za Upangaji ili uweze kutumika. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaanza utekelezaji wa Mpango wa Uendelezaji Upya wa Maeneo Yaliyochakaa katika majiji ya Mbeya na Dar es Salaam.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25 Wizara kupitia Programu ya KKK itapanga, kupima na kumilikisha viwanja 100,000 kwa ajili ya matumizi mbalimbali kwa kushirikiana na Mamlaka za Upangaji pamoja na sekta binafsi. Aidha, Wizara itaandaa mipango ya uendelezaji upya wa maeneo kongwe katika mikoa ya Dar es Salaam, Mwanza na Arusha. Vilevile, utafanyika uhakiki wa matumizi ya ardhi katika Majiji matano
(5) ya Dodoma, Mbeya, Mwanza, Arusha na Tanga na Manispaa tatu (3) za Kahama, Morogoro na Kigoma.

Mfuko wa Maendeleo ya Ardhi
Mheshimiwa Spika;
mwaka 1991/92, Serikali ilianzisha Mfuko Maalum wa Kupima Viwanja (Plot Development Revolving Fund – PDRF) ambao ulilenga kuwezesha upangaji, upimaji na umilikishaji viwanja. Hata hivyo, mwaka 2016 Serikali ilisitisha matumizi ya akaunti za mifuko mbalimbali nchini ikiwemo akaunti ya Mfuko huu. Kusitishwa kwa matumizi ya akaunti kuliikosesha Wizara chanzo cha uhakika cha fedha za upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi.
Mheshimiwa Spika, kwa kuzingatia umuhimu wa upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi nchini, Serikali imeridhia kurejeshwa kwa matumizi ya akaunti ya Mfuko wa Maendeleo ya Ardhi. Kwa kuanzia, Serikali imetoa mtaji wenye thamani ya shilingi bilioni 15.4 na imeridhia marejesho ya fedha kiasi cha shilingi bilioni 50 za Kupanga, Kupima na Kumilikisha zinazodaiwa kwenye mikopo ya Halmashauri ziingizwe kwenye Mfuko huu. Ili kuwezesha uendelevu wa mfuko na ufanisi katika utekelezaji, Mwongozo wa Uratibu na Usimamizi wa Mfuko umeandaliwa. Wizara inatoa shukrani za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kurejesha matumizi ya akaunti ya mfuko.

Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP)
Mheshimiwa Spika,
Wizara imeendelea kutekeleza Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP). Mradi huu unatekelezwa kwa miaka mitano (5) (2022/23 – 2026/27) katika mikoa yote 26 na unalenga kutatua changamoto mbalimbali zinazoikabili Sekta ya Ardhi ikiwemo uboreshaji wa miundombinu ili kurahisisha utoaji huduma za kupanga, kupima, kumilikisha ardhi, uthamini na maboresho ya sera na sheria mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, Wizara ilipokea na kutekeleza maelekezo ya Bunge ya kufanya mapitio ya mpango wa utekelezaji wa Mradi wa LTIP ili kuongeza mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, Wizara ilifanya mapitio ya mpango wa utekelezaji wa Mradi na kuongeza mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji kutoka mpango wa awali wa vijiji 250 hadi kufikia vijiji 1,667.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara kupitia Mradi huu ilipanga kupima mipaka ya vijiji 700; kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi na mipangokina ya vijiji 700; kuandaa na kuidhinisha Hati za Hakimiliki za Kimila 200,000 na kukarabati ofisi za ardhi za Halmashauri 41. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, jumla ya mipaka ya vijiji

407 imepimwa na kuhakikiwa, vyeti vya ardhi ya kijiji 320 vimetolewa na mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji 843 imeandaliwa katika Halmashauri
21 (Jedwali Na.16). Mipango hii imewezesha kupangwa kwa ardhi yenye ukubwa wa jumla ya Hekta 5,013,087 kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo malisho (564,691), makazi (267,595), hifadhi za misitu (363,935), makazi na kilimo (1,230,898), kilimo (2,538,750), huduma za kijamii (44,476) na ardhi ya akiba (2,742). Aidha, vipande vya ardhi 381,509 vimetambuliwa kwa ajili ya kutoa Hati za Hakimiliki za Kimila katika Wilaya sita (6) za Tanganyika (69,216), Maswa (85,182), Mbinga (56,547), Mufindi (72,991),
Songwe (77,514) na Chamwino (20,059).
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24 jumla ya makazi 500,000 yalipangwa kurasimishwa katika Halmashauri 23; kuanza kusimika vituo 22 vya upimaji na kuweka alama za msingi za upimaji
276. Hadi tarehe 15 Mei 2024, vipande vya ardhi 62,200 vimerasimishwa katika Halmashauri za Jiji la Dodoma (7,545), Wilaya ya Chalinze (12,112), Manispaa ya Kigoma (6,171), Mji wa Nzega (11,796), Manispaa ya Kahama (10,860) na Manispaa ya Shinyanga (13,716); na Alama za Msingi za Upimaji 327 zimewekwa katika Halmashauri 26 sawa na asilimia 118 ya lengo. Aidha, zabuni kwa ajili ya urasimishaji makazi 400,000 imetangazwa Vilevile, Mkandarasi kwa ajili ya ujenzi wa vituo 22 vya upimaji amepatikana na kazi ya ujenzi itaanza katika mwaka 2024/25.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, Wizara ilipanga kuanza ujenzi wa majengo 25 ya Ofisi za Ardhi za Mikoa na kujenga kumbi za mihadhara nne (4) katika vyuo vya ardhi vya Tabora na Morogoro. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 washauri elekezi wa ujenzi wa majengo 25 ya Ofisi za Ardhi za Mikoa na kumbi nne (4) za mihadhara za Vyuo vya Tabora na Morogoro wamepatikana na wamekamilisha rasimu za ubunifu wa majengo. Washauri elekezi waliopatikana ni wataalam wa ndani. Hii ni katika kuendeleza azma ya Awamu ya Sita ya kuimarisha sekta binafsi nchini.
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kuwajengea uelewa wananchi kuhusu utekelezaji wa mradi katika ngazi za Mitaa, Kata na Wilaya katika maeneo ya mradi. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 wananchi 282,593 wamejengewa uelewa kuhusu sheria za ardhi na utekelezaji wa Mradi ambapo wanaume walikuwa 158,118 na wanawake 124,475. Vilevile, katika kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro, Mradi umewezesha kumaliza mashauri
496 katika mabaraza matano (5) ya Bagamoyo, Musoma, Tarime, Tabora na Ifakara na hivyo kupunguza mlundikano wa kesi katika mabaraza hayo. Vilevile, mradi umeboresha mazingira ya kufanyia kazi kwa kuwezesha ununuzi wa samani za ofisi, vitendeakazi na magari 18. Aidha, taratibu za ununuzi wa magari mengine 52 zinaendelea na zinatarajiwa kukamilika mwaka 2024/25. Hatua hii itapunguza changamoto ya usafiri iliyopo katika sekta ya Ardhi.


Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Jerry William Silaa, akimkabidhi magari Katibu Mkuu Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi. Anthony Damian Sanga kwa ajili ya utekelezaji wa Mradi wa LTIP.

Mheshimiwa Spika, kazi zilizopangwa kutekelezwa katika mwaka 2024/25 kupitia Mradi wa Uboreshaji Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) ni: -
  • Kuhakiki na kupima mipaka ya vijiji na kutoa vyeti vya vijiji 1,000;
  • Kuandaa mipango ya matumizi ya ardhi ya vijiji 1,000;

Kuandaa Mipangokina ya vijiji 100 na kuandaa Hati za Hakimiliki za Kimila 300,000;
Kurasimisha vipande vya ardhi 100,000 kupitia wataalam wa Serikali na vipande 400,000 kupitia kampuni zinazofanya kazi za urasimishaji;
Kubadilisha Nyaraka za ardhi (Data conversion) 1,921,758 kutoka analojia kwenda kidijitali;
Kuwezesha upatikanaji wa miundombinu kwa ajili ya usambazaji wa mfumo wa ILMIS kwa Ofisi za Ardhi 67;
Kusanifu na kusimika Vituo vya Kieletroniki vya Upimaji (CORs) 22;
Kujenga mfumo wa kidigitali wa Vitalu vya Thamani ya Ardhi nchini;
Kujenga Ofisi za Ardhi za Mikoa 25;
Kujenga kumbi za mihadhara katika Vyuo vya Ardhi vya Tabora - ARITA (2) na Morogoro
- ARIMO (2);
Kuwezesha ubunifu na ujenzi wa Jengo la Taifa la Kuhifadhi Kumbukumbu za Ardhi;
Kukarabati Ofisi za ardhi katika Halmashauri 34;
Kununua vifaa, kuhuisha mitaala na kuwezesha ukuzaji wa ujuzi wa watumishi wa Vyuo vya Ardhi Tabora na Morogoro;
Kuboresha utendaji kazi wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya 30; na

  • Kuandaa na kuboresha sera, sheria na miongozo mbalimbali.
Mradi wa Uimarishaji wa Miundombinu ya Upimaji na Ramani (Land Data Infrastructure – LDI)
Mheshimiwa Spika
, mradi wa Uimarishaji wa Miundombinu ya Upimaji na Ramani una thamani ya Dola za Kimarekani milioni 65 na unalenga kuweka miundombinu ya upimaji na ramani ambayo itaongeza kasi ya upangaji, upimaji ardhi na uandaaji wa ramani kwa matumizi mbalimbali. Pamoja na shughuli nyingine, Mradi utawezesha ujenzi wa Vituo vya Kielektroniki vya Upimaji (CORs) 30, ununuzi wa vifaa vya kisasa vya upimaji na uandaaji wa ramani ikiwemo ndege moja (1) yenye rubani na ndege 17 zisizo na rubani (drones) na vifaa vya kisasa vya kielektroniki vya kuchakata ramani. Utaratibu wa kumpata mshauri mwelekezi wa mradi umekamilika na mkataba kati ya Wizara na Mshauri Mwelekezi uliwekwa saini tarehe 9 Mei, 2024. Kazi atakazofanya ni usanifu wa mradi, kuandaa viwango na miongozo ya upimaji na uandaaji wa ramani za kidigitali pamoja na kusimamia utekelezaji wa mradi kwa kushirikiana na wataalam wa ndani.
Mheshimiwa Spika, katika hatua za awali za utekelezaji wa mradi wa LDI, Wizara imeanzisha Kituo cha Mafunzo na Ubunifu (TNGC) kitakachotumika kuwajengea uwezo watumishi

katika matumizi ya teknolojia ya mifumo ya taarifa za kijiografia na kumbukumbu za ardhi. Aidha, Kituo hicho kitaongeza uwezo wa wataalamu wa ndani kutekeleza miradi ya ardhi na hivyo kuokoa matumizi ya fedha za kigeni zinazotumika kuajiri wataalam kutoka nje ya nchi. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 watalaam 10 wamepata mafunzo ya ukufunzi nchini Tanzania na Korea Kusini.


Mtaalamu wa kurusha Ndege isiyo na Rubani akijiandaa kurusha ndege.

Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea na utekelezaji wa mradi kwa kukamilisha ununuzi wa vifaa na

kuandaa ramani za msingi za uwiano wa 1:2,500 kwa miji mikuu ya mikoa na uwiano wa 1:25,000 kwa nchi nzima.
Mradi wa Uimarishaji wa Mipaka ya Kimataifa
Mheshimiwa Spika
, Wizara imeendelea kuimarisha mipaka ya kimataifa kwa kujenga na kuongeza alama, kuzipima, kukarabati zilizoharibika, kuandaa ramani za mipaka na kuandaa mikataba ya mipaka. Katika mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kuimarisha sehemu ya mpaka wa kimataifa kati ya Tanzania na Kenya yenye urefu wa kilomita 80 pamoja na mpaka wa Tanzania na Burundi yenye urefu wa kilomita 100. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara iliendelea na uimarishaji wa mpaka wa Tanzania na Kenya kwenye kipande cha kilomita 110 kutoka Namanga hadi Tarakea ambapo kazi hiyo imekamilika. Kazi ya uimarishaji wa sehemu ya mpaka wa Tanzania na Kenya yenye urefu wa kilomita 100 kutoka Tarakea mpaka Ziwa Jipe inaendelea na itakamilika katika mwaka 2024/25. Aidha, ramani 65 za sehemu ya mpaka wa Tanzania na Kenya kutoka Ziwa Viktoria (Rorya) hadi Tarakea (Rombo) yenye urefu wa kilomita 238 kati ya kilometa 458 zilizoimarishwa zimekamilika. Katika mwaka 2024/25, Wizara itakamilisha uimarishaji wa sehemu ya mpaka wa Tanzania na Burundi yenye urefu wa kilomita 100 pamoja na kuendelea na uandaaji wa ramani za mipaka ya kimataifa.


Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. Geophrey Pinda (wa nne kushoto) akiwa na wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi Maliasili na Utalii wakikagua mpaka wa Tanzania na Kenya eneo la Namanga mkoani Arusha.

USHIRIKI WA WIZARA KATIKA MIRADI YA KIMKAKATI
Mradi wa Ujenzi wa Bomba la Mafuta
Mheshimiwa Spika,
Wizara ilifanya kazi ya upimaji wa mkuza wa Bomba la Mafuta Ghafi la Afrika Mashariki (EACOP) katika upande wa Tanzania wenye urefu wa Kilomita 1,146. Mkuza uliopimwa unaanzia Mtukula (Kagera) hadi Chongoleani (Tanga). Ramani za mkuza huo unaopita katika mikoa nane (8) na Halmashauri 28

zimeandaliwa na kuidhinishwa. Aidha, Wizara imeshiriki katika kukamilisha utwaaji wa ardhi ya nyongeza ya hekta 12.75 iliyopo katika vijiji vya Mwighanji (Singida), Serya (Kondoa) na Kelema Mashariki (Chemba).
Mheshimiwa Spika, katika kuhakikisha kunakuwepo na usalama wa milki kwenye njia ya Mradi, Wizara imekamilisha uandaaji na usajili wa Hatimiliki kwa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) katika Halmashauri 28 za mikoa nane (8) inayopitiwa na bomba hilo. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kushirikiana na Taasisi zote za utekelezaji wa mradi huu na miradi mingine ya kimkakati kuhakikisha inakuwa na milki salama kwa kadri itakavyotakiwa.
TAASISI NA BODI ZILIZO CHINI YA WIZARA SHIRIKA LA NYUMBA LA TAIFA (NHC)
Mheshimiwa Spika,
Shirika la Nyumba la Taifa lina jukumu la kujenga nyumba za makazi na majengo mengine kwa ajili ya kuuza na kupangisha; kujenga majengo kulingana na mipango iliyoidhinishwa na Serikali; kuzalisha na kuwezesha uzalishaji wa vifaa vya ujenzi; kusimamia milki za majengo; kufanya ukarabati; kukusanya kodi ya pango; kutoa huduma ya ushauri elekezi, upangaji wa maeneo na ukandarasi wa majengo. Majukumu hayo yanatekelezwa kupitia Mpango Mkakati wa Shirika wa miaka 11 (2015/16 – 2025/26).

Ujenzi wa Nyumba za Makazi na Majengo Mengine kwa ajili ya Kuuza na Kupangisha
  • Mradi wa Kawe 711, Golden Premier Residence na Morocco Square
Mheshimiwa Spika; katika mwaka 2023/2024 Shirika lilipanga kukamilisha ujenzi wa miradi mikubwa ikiwemo mradi wa nyumba 422 wa Kawe 711 wenye thamani ya shilingi bilioni 169 na nyumba 196 wa Golden Premier Residence wenye thamani ya shilingi bilioni 71 iliyokuwa imesimama tangu mwaka 2018. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa, ujenzi wa Mradi wa Kawe 711 unaendelea na umefikia asilimia 35 na unatarajiwa kukamilika mwezi Aprili 2026. Aidha, mradi wa Golden Premier Residence (GPR) bado umesimama na majadiliano kati ya Shirika na mkandarasi yanaendelea.
Mheshimiwa Spika; Shirika limeendelea na uuzaji na upangishaji wa majengo katika Mradi uliokamilika wa Morocco Square, ambapo katika jengo lenye nyumba za makazi 100, tayari nyumba 71 zimeshauzwa na mauzo ya nyumba zilizobakia yanaendelea. Aidha, upangishaji wa Hoteli yenye vyumba 81 umefanyika kwa asilimia 100, Maduka (Retail Mall) asilimia 94 na ofisi asilimia 42.


Hotel ya King Jada ni moja ya majengo ya Mradi wa Morocco Square jijini Dar es salaam

  • Mradi wa Samia Housing Scheme
Mheshimiwa Spika; katika mwaka 2023/24 Shirika lilipanga kutekeleza mradi wa ujenzi wa nyumba 560 uliopo Kawe Jijini Dar es Salaam na nyumba 500 katika Jiji la Dodoma maeneo ya Njedengwa, Iyumbu na Medeli. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, ujenzi wa nyumba 560 awamu ya kwanza katika eneo la Kawe Jijini Dar es Salaam umefikia asilimia 60 na unatarajiwa kukamilika mwaka 2024/25.

Ujenzi wa Majengo ya Biashara
Mheshimiwa Spika;
katika mwaka 2023/24 Shirika lilipanga kuendelea na ujenzi wa majengo ya biashara katika Mikoa ya Kagera (Bukoba), Mwanza, Dodoma, Shinyanga (Kahama), Morogoro, Mtwara (Masasi) na Lindi. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 ujenzi wa majengo ya maduka 50 katika Mji wa Kahama umefikia asilimia 14 na ujenzi wa jengo la biashara katika mji wa Masasi umeanza.
Utekelezaji wa Sera ya Ubia ya Shirika
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24 Shirika lilipanga kutekeleza miradi 24 ya ubia yenye thamani ya shilingi bilioni 340 kupitia Sera yake ya Ubia ambapo hadi tarehe 15 Mei, 2024, Shirika limeidhinisha na kusaini mikataba ya miradi 21 yenye thamani ya shilingi bilioni 271. Miradi hii itatekelezwa kwa muda wa miezi 24 ambapo utekelezaji umeanza Januari, 2024 katika Mikoa ya Dar es Salaam (17), Mwanza (3) na Iringa (1).
Mheshimiwa spika, kupitia miradi hii, Shirika linatarajia kupata manufaa mbalimbali ikiwemo kuongeza idadi ya nafasi za upangaji, mathalan katika eneo la Kariakoo nafasi za upangishaji zitaongezeka kutoka 324 hadi 2,691. Hivyo, mapato, thamani ya mali za Shirika na faida ya uwekezaji kwa kuzingatia eneo (Return on Investments) itaongezeka.

  • Ukarabati wa Nyumba za Shirika
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24 Shirika limekamilisha ukarabati wa majengo 181 ambayo yana nyumba 3,111 katika mikoa 23 ya Shirika. Aidha, jumla ya majengo 83 ambayo yana nyumba 451 yaliyopo katika mikoa mbalimbali ya Shirika yanaendelea kufanyiwa ukarabati (Jedwali Na. 17).
  • Ukusanyaji wa Mapato ya Shirika
Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2023/24, Shirika lilipanga kukusanya shilingi bilioni 274 kutokana na vyanzo mbalimbali ambavyo ni kodi ya pango shilingi bilioni 105, ukandarasi shilingi bilioni 99 na shilingi bilioni 70 kutokana na mauzo ya nyumba na viwanja. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, Shirika limekusanya jumla ya Shilingi bilioni 208.5 sawa na asilimia 76.1 ya lengo. Kati ya fedha hizo, shilingi bilioni 90.4 ni makusanyo ya kodi ya pango, makusanyo ya mauzo ya nyumba na viwanja ni shilingi bilioni
50.8 na shilingi bilioni 60.9 ni mapato yanayotokana na miradi ya ukandarasi pamoja na ushauri elekezi na shilingi bilioni 6.4 ni mapato mengineyo.

  • Ukusanyaji wa Madeni ya Shirika
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2023/24, shirika limekusanya shilingi bilioni 7.2 ambapo kiasi cha shilingi bilioni 4.1 ni deni la pango la nyumba, shilingi bilioni 2.7 kutoka kwenye miradi ya ukandarasi na shilingi milioni 400 ni madeni mengineyo ikiwemo ya uuzaji wa nyumba. Madeni hayo yamepungua kutoka shilingi bilioni 25.7 Julai, 2023 hadi shilingi bilioni 18.5 Mei, 2024 sawa na asilimia 28. Hata hivyo, Shirika bado linakabiliwa na changamoto ya wadaiwa sugu wa kodi ya pango; miradi ya ukandarasi na wanunuzi wa nyumba kutokukamilisha malipo yao kwa wakati. Hivyo, Shirika limeweka mikakati ifuatayo ili kukabiliana na changamoto hizo;
Kuingia mikataba na wapangaji ili kuwaruhusu kulipa madeni yao kwa awamu;
Kuvunja mikataba ya upangaji kwa wapangaji waliokaidi kulipa madeni yao na kuwaondoa kwenye nyumba na kukamata mali zao kwa ajili ya kuuza ili kufidia madeni yao;
Kuwatangaza wadaiwa sugu katika vyombo vya habari;
Kuhakikisha kuwa, kila mpangaji mpya anayepangishwa analipa amana ya pango ya miezi mitatu (security deposit); na

Kuingia makubaliano na Credit Information Reference Bureau ili kusajili majina ya wadaiwa sugu na kuwanyima fursa ya kupata mikopo katika taasisi za fedha.
Kuingia mikataba na wapangaji ili kuwaruhusu kulipa madeni yao kwa awamu;
Kuvunja mikataba ya upangaji kwa wapangaji waliokaidi kulipa madeni yao na kuwaondoa kwenye nyumba na kukamata mali zao kwa ajili ya kuuza ili kufidia madeni yao;
viii).Kuwatangaza wadaiwa sugu katika vyombo vya habari;
Kuhakikisha kuwa, kila mpangaji mpya anayepangishwa analipa amana ya pango ya miezi mitatu (security deposit); na
Kuingia makubaliano na Credit Information Reference Bureau ili kusajili majina ya wadaiwa sugu na kuwanyima fursa ya kupata mikopo katika taasisi za fedha.

Natoa wito kwa wapangaji kulipa ankara zao kwa wakati na wadaiwa wote kulipa madeni yao mapema kabla hatua zaidi hazijachukuliwa kwa ukiukaji wa mikataba.
  • Ujenzi wa Miradi ya Ukandarasi
Mheshimiwa Spika, Katika mwaka 2023/24 Shirika limendelea na utekelezaji wa miradi ya ukandarasi ikiwemo ujenzi wa Majengo ya Ofisi za Wizara nane (8) Jijini Dodoma, ujenzi wa Jengo la Shule ya Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Ujenzi wa majengo manne (4) ya Wakala wa Huduma za Ununuzi Serikalini (GPSA), Kituo cha biashara ya madini ya Tanzanite Mirerani, ujenzi wa Jengo la Kitengo cha Moyo cha Jakaya Kikwete (JKCI) ambapo hadi tarehe 15 Mei, 2024, utekelezaji wake ni kama ifutavyo:-
Ujenzi wa majengo ya Ofisi za Wizara nane (8) yenye thamani ya shilingi bilioni 194 Katika Mji wa Serikali Mtumba umefikia wastani wa asilimia 81;
Ujenzi wa jengo la Shule ya Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam wenye thamani ya shilingi bilioni 9.8 umefikia asilimia 75;
Ujenzi wa majengo manne (4) ya Wakala wa Ununuzi wa Serikali (GPSA) katika mikoa ya Simiyu, Songwe, Dodoma na Pwani yenye

thamani ya shilingi bilioni 2.8 umekamilika kwa asilimia 100;
Ujenzi wa Kituo cha biashara ya madini ya Tanzanite wenye thamani ya shilingi bilioni
5.5 katika mji wa Mirerani Mkoa wa Manyara umefikia asilimia 85; na
Ujenzi wa jengo la Kitengo cha Moyo cha Jakaya Kikwete (JKCI) wenye thamani ya shilingi bilioni 3.1 Jijini Dar Es Salaam umefika asilimia 99.
Mpango wa Utekelezaji wa Shughuli za Shirika kwa mwaka 2024/25
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2024/25, shirika limepanga kutekeleza kazi zifuatazo: -
Kuendelea na ujenzi wa nyumba 422 katika mradi wa Kawe 711 ambapo unatarajiwa kufikia asilimia 75 ya utekelezaji ifikapo Juni, 2025. Lengo ni kukamilisha ujenzi ifikapo Aprili, 2026;
Kuendelea na ujenzi wa nyumba 196 katika mradi wa Golden Premier Residence (GPR) ifikapo Juni, 2025;
Kuanza ujenzi wa nyumba 560 za Mradi wa Samia Housing Scheme (SHS) awamu ya pili katika eneo la Kawe Jijini Dar es Salaam;

Kuendelea na ujenzi wa nyumba 150 za Samia Housing Scheme katika eneo la Medeli na Iyumbu Jijini Dodoma kwa ajili ya kuuzia wananchi;
Kukamilisha ujenzi wa majengo ya biashara katika mkoa wa Shinyanga (Kahama) na kuanza ujenzi katika mji wa Masasi (Mtwara);
Kuanza ujenzi wa majengo ya biashara katika miji ya Moshi, Arusha, Tanga, Tabora, Lindi, Morogoro, Bukoba na Dar es Salaam;
Kuendelea na ujenzi na kusimamia miradi 21 ya ubia yenye thamani ya shilingi billioni 271 na kukaribisha wawekezaji wengine kutoka sekta binafsi ili kufanya uendelezaji wa majengo ya biashara na makazi kupitia sera ya ubia;
Kuendelea kukusanya mapato ikiwemo madeni ya kodi ya nyumba, miradi ya ukandarasi, uuzaji wa nyumba, viwanja na madeni mengineyo ambapo mikakati madhubuti imewekwa ili kukusanya madeni hayo;
Kuendelea kutekeleza mpango wa matengenezo kwa kukarabati majengo 250;
Kuendelea na utekelezaji wa miradi ya ukandarasi ikiwemo kukamilisha ujenzi wa jengo la Shule ya Uchumi ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kituo cha biashara ya madini ya Tanzanite Mirerani na miradi mingine itakayojitokeza;

Kuendelea kutekeleza shughuli za utaalam elekezi/ushauri katika miradi mbalimbali nchini;
Kuendelea na ujenzi wa mradi wa jengo la Ofisi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Mawasiliano Tanzania (TCRA) Jijini Dodoma na Zanzibar;
Kukamilisha uandaaji wa Mpango Kabambe wa matumizi ya ardhi katika maeneo ya Mwashiwawala – Mbeya, Kwala – Pwani na kufanya mapitio ya mpango wa Kitovu cha Mji eneo la Kawe; na
Kufanya utafiti kuhusu teknolojia sahihi katika ujenzi wa nyumba za gharama nafuu.
TUME YA TAIFA YA MIPANGO YA MATUMIZI YA ARDHI
Mheshimiwa Spika,
Wizara ina jukumu la kusimamia shughuli za Upangaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kupitia Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi. Aidha, Tume hii, ina jukumu la kuandaa, kuratibu, kuwezesha na kusimamia utekelezaji wa mipango ya matumizi ya ardhi nchini, Kufanya Ufuatiliaji, Tathmini, Uzingativu wa Mipango pamoja na kufanya tafiti za Matumizi ya Ardhi zinazohusiana na ardhi. Utekelezaji wa majukumu hayo unazingatia Mpango Mkakati wa Tume (2021/22-2025/26).
Mheshimiwa Spika, Mipango ya matumizi ya ardhi huwezesha kutenga maeneo kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo maeneo ya malisho,

kilimo, makazi, uwekezaji, miundombinu ya barabara, huduma za jamii, hifadhi za misitu na mapitio ya wanyamapori (shoroba). Upangaji huu huleta tija katika uzalishaji, kuimarisha usalama wa milki na kudhibiti migogoro baina ya watumiaji wa ardhi. Mipango hii huandaliwa katika ngazi ya Vijiji, Wilaya, Mkoa, Kanda na Taifa.
Uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Wilaya na Vijiji
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24, Wizara kupitia Tume ilipanga kuandaa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Wilaya tano (5) na Vijiji 210 katika Halmashauri mbalimbali nchini. Mipango hii huandaliwa kwa njia shirikishi na kwa kushirikiana na Mamlaka za Upangaji na wadau. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara kupitia Tume imewezesha uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 339 katika wilaya 30 sawa na asilimia 161.4 ya lengo la mwaka (Jedwali Na.18). Ongezeko la vijiji vilivyoandaliwa mipango ya matumizi ya ardhi linatokana na utekelezaji wa Mradi wa Uimarishaji Usalama wa Milki za Ardhi na mwitikio wa wadau wa ndani na nje ya nchi kuchangia uandaaji wa mipango ya matumizi ya ardhi. Uandaaji wa Mipango hii umefanya kuwa na jumla ya Vijiji 4,126 vilivyoandaliwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kati ya vijiji 12,318 vilivyopo nchini.


Wananchi wa Kijiji cha Kibuye, kilichopo katika Kata ya Bukuba, Wilayani Buhigwe wakimsikiliza Bw. Emmanuel Mbula, mtaalamu kutoka Tume ya Matumizi ya Ardhi akitoa
elimu juu ya Sheria za Usimamizi Rasilimali Ardhi ikiwa ni maandalizi ya upangaji matumizi ya ardhi
ya Kijiji hicho

Mheshimiwa Spika, Mipango ya Matumizi ya Ardhi iliyoandaliwa kwa mwaka 2023/24 imewezesha kupangwa maeneo ya matumizi ya ardhi katika Vijiji vya Halmashauri za Wilaya mbalimbali nchini. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 jumla ya hekta 1,287,534.46 zimepangwa kwa ajili ya matumizi mbalimbali ikiwemo uwekezaji (12,167.27), malisho (91,611.28), hifadhi za misitu (150,377.92),
misitu ya uvunaji (24,394.10), makazi (107,426.30)
kilimo na makazi (229,767.75), kilimo (608,586.81),

huduma za jamii (15,494.13), miundombinu (12,866.02) na hifadhi za vyanzo vya maji (34,842.88). Katika mwaka 2024/25, Wizara kupitia Tume itaendelea kuratibu na kuwezesha uandaaji wa mipango ya matumizi ya Ardhi ya Vijiji 422 kwa kushirikiana na Mamlaka za Upangaji na wadau wa kimkakati katika maeneo mbalimbali ya miradi ya kimkakati, migogoro, mpakani na yenye uzalishaji mkubwa wa mazao.
Mheshimiwa Spika, pamoja na uandaaji wa Mipango ya Vijiji, Wizara kupitia Tume ilipanga kuandaa Mpango wa Matumizi ya Ardhi wa Wilaya moja katika mwaka fedha 2023/24. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 Tume imewezesha uandaaji wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi wa Wilaya katika Halmashauri ya Bukombe Mkoani Geita. Aidha, katika mwaka wa fedha 2024/25, Tume itaendelea kuandaa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Wilaya tano (5). Natoa wito kwa Halmashauri za Wilaya zote nchini kutoa kipaumbele katika kutenga fedha za uandaaji na utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ili kuongeza kasi ya uaandaji wa mipango ya matumizi ya ardhi.

Uandaaji wa Mipangokina ya Vijiji Katika Makazi na Mashamba
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24, Tume ilipanga kuandaa mipango kina ya makazi na mashamba katika vijiji vitano (5) itakayowezesha utoaji wa Hati za Hakimiliki za Kimila 5,200. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, jumla ya mipangokina ya makazi na mashamba katika vijiji 66 imeandaliwa katika Halmashauri za Wilaya 19 na kufikisha jumla ya Vijiji 88 vilivyoandaliwa Mpangokina nchini. Aidha, mipango hii imewezesha uwekaji wa miundombinu ya huduma za jamii na utoaji wa Hati za Hakimilki za Kimila 18,125 katika Halmashauri za Wilaya 17. Hati hizi zimewawezesha wananchi kuwa na milki salama na kuwawezesha asilimia 15 ya wananchi kuzitumia kama dhamana kupata mikopo kutoka Taasisi za Fedha.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka wa Fedha 2024/25, Tume itaendelea kuwezesha uandaaji wa mipangokina 40 katika maeneo yanayotengwa kwa matumizi ya makazi, mashamba, misitu na hivyo kuwezesha utoaji wa Hati za Hakimilki za Kimila 8,200. Hii itawawezesha wananchi kiuchumi na kuimarisha usalama wa milki.

Uwezeshaji wa Mamlaka za Upangaji
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka wa fedha 2023/24 Tume ilipanga kuzijengea uwezo timu shirikishi za upangaji 255 katika Mamlaka za Upangaji za Wilaya na Vijiji na kutoa elimu kwa umma. Elimu iliyopangwa kutolewa ilihusu Sheria za Ardhi, Miongozo na Taratibu za uandaaji, utekelezaji na usimamizi wa mipango ya matumizi ya ardhi, usuluhishi wa migogoro, uhifadhi wa mazingira, wanyamapori, vyanzo vya maji na uzingatiaji wa mipango na mabadiliko ya tabianchi.
Mheshimiwa Spika, hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara kupitia Tume imezijengea uwezo Mamlaka za upangaji za Vijiji 339 na Halmashauri za Wilaya 30 kuhusu uandaaji, usimamizi na utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi. Jumla ya wajumbe 16,090 wakiwemo wajumbe
241 wa Halmashauri za Wilaya 30, Wajumbe 7,797 wa Halmashauri za Vijiji (VC) ikiwemo Wajumbe 2,712 wa Kamati za Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi za Vijiji (VLUM); Wajumbe 2,373 wa Mabaraza ya Ardhi ya Vijiji (VLC); Wajumbe 594 wa Kamati ya Uhakiki wa Maslahi ya Ardhi (VLAC) na wajumbe 2,373 wa Kamati za Uhakiki wa Mipaka walijengewa uwezo katika Halmashauri mbalimbali nchini. Aidha, katika mwaka 2024/25 Tume itaendelea kuzijengea uwezo Mamlaka za Upangaji 420.


Katibu Mkuu wa Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhandisi Antony Sanga (aliyesimama) akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Kigala, mkoa wa Njombe wakati wa zoezi la uandaji wa mpango wa matumizi ya ardhi ya Kijiji hicho.

Elimu kwa Umma
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka wa fedha 2023/24 Tume ilipanga kurusha vipindi 30 vya elimu kwa umma kuhusu upangaji wa matumizi ya ardhi. Hadi tarehe 15 Mei 2024, vipindi 102 vimerushwa kupitia runinga, redio, tovuti na mitandao ya kijamii. Aidha, Tume iliendesha mikutano mbalimbali uwandani yenye lengo la uelimishaji Jamii kuhusu majukumu na kazi zinazotekelezwa na Tume. Katika mwaka

2024/25, Tume itaendelea kuziwezesha Mamlaka za upangaji na kutoa elimu kwa umma kwa vipindi 40 kuhusu sheria za ardhi, miongozo na taratibu za upangaji, usimamizi na utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi nchini.
Uhuishaji na uhakiki wa Mipaka ya Vijiji
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24, Tume imewezesha uhuishaji na uhakiki wa mipaka ya kiutawala ya vijiji 194 katika Halmashauri za Wilaya 20. Aidha, migogoro ya Ardhi ya vijiji 183 imetatuliwa katika Halmashauri za Wilaya 20 (Jedwali Na.19). Vilevile, Vyeti vya Ardhi ya Vijiji 46 vimeandaliwa na kutolewa kwa kushirikiana na wadau katika Halmashauri za Wilaya Saba (7) za Tunduru (11), Makete (1), Ruangwa (1), Liwale (5),
Butiama (23), Morogoro (2), Mpimbwe (3). Katika mwaka 2024/25, Tume itaendelea kuhakiki na kuhuisha mipaka ya vijiji wakati wa uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi, kushirikiana na Mamlaka za Upangaji kutoa vyeti vya ardhi vya vijiji na kuimarisha mipaka ya kiutawala ya vijiji.


Wapima Ardhi wa Wizara wakishirikiana na wananchi katika zoezi la kupima mipaka ya vijiji katika halmashauri ya Ushetu Septemba, 2023.

Tafiti
Mheshimiwa Spika,
Wizara kupitia Tume imeendelea kufanya tafiti mbalimbali zinazohusiana na Sekta ya Ardhi na upangaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi. Tafiti hizi husaidia kujenga uelewa kwa wadau na kuhuisha Sheria na Miongozo mbalimbali ndani ya Sekta ya Ardhi. Katika mwaka 2023/24, Tume ilipanga kufanya tafiti mbili (2) zinazohusu matumizi ya Ardhi na Maendeleo ya Vijiji katika Halmashauri mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Spika, Tume imekamilisha kufanya tafiti mbili zinazohusiana na matumizi ya Ardhi kuhusu changamoto na fursa za upangaji wa matumizi ya ardhi na matokeo yake katika kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi. Tafiti zilifanyika katika vijiji saba (7) vya Mgaraganza, Mkongoro, Mwamgongo katika Mkoa wa Kigoma; Vijiji vya Kizerui, Mbomole na Sakale katika Mkoa wa Tanga na Makuka katika Mkoa wa Iringa. Tafiti hizi zililenga katika kubaini masuala chanya au hasi yanayoweza kuathiri uandaaji na utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi na athari zinazoweza kujitokeza ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi kwa maeneo yenye umuhimu kwa uhifadhi nchini.
Mheshimiwa Spika, matokeo ya tafiti hizi yamebainisha kuwa kuandaliwa kwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kumepunguza migogoro kati ya wakulima na wafugaji, shughuli za kibinadamu na uhifadhi katika maeneo. Mipango ya Matumizi ya Ardhi imesaidia kuhifadhi vyanzo vya maji na misitu na kusababisha kuboreshwa kwa hali ya uzalishaji wa mazao ya kilimo na upatikanaji wa maji katika maeneo yao. Vilevile, Mipango ya Matumizi ya Ardhi imesaidia kutengwa kwa maeneo ya misitu ambayo imechangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa hali joto na kuongezeka kwa mvua na upatikanaji wa maji. Serikali itaendelea kuimarisha mbinu shirikishi za uandaaji, utekelezaji na usimamizi wa uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi nchini. Aidha,

mikakati endelevu itaendelea kuwekwa ili kuwezesha wananchi kumilikishwa maeneo yao na kuendelea kupewa elimu inayolenga kutunza maeneo yao na kusimamia utekelezaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa kuzingatia kanuni ndogo. Katika mwaka 2024/25, Wizara kupitia Tume itafanya tafiti mbili (2) zinazohusiana na upangaji na Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi.
Uimarishaji wa Mfumo wa Taarifa na Utunzaji wa Kumbukumbu za Mipango ya Matumizi ya Ardhi
Mheshimiwa Spika,
Wizara kupitia Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi imeendelea kuboresha na kusimamia Mfumo wa Taarifa na Utunzaji wa Kumbukumbu za Mipango ya Matumizi ya Ardhi (NLUIS). Mfumo huu unawezesha kuandaa na kuhifadhi kumbukumbu za Mipango ya Matumizi ya Ardhi ili kurahisisha upatikanaji wa taarifa za Mipango ya Matumizi ya Ardhi. Aidha, katika mwaka 2024/25 Tume itaendelea kuboresha Mfumo wa Taarifa na Utunzaji wa Kumbukumbu za Mipango ya Matumizi ya Ardhi, kusambaza katika Halmashauri za Wilaya na kuwezesha utumiaji wa mfumo.
Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2023/24, Wizara kupitia Tume ilipanga kuhifadhi Mipango ya Matumizi ya Ardhi 810 katika Mfumo wa Taifa wa Utunzaji wa Taarifa na Kumbukumbu

za Mipango ya Matumizi ya Ardhi pamoja na kuendelea kuboresha mfumo huu. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, jumla ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 534 imehifadhiwa hivyo kuwa na mipango iliyohifadhiwa kufikia 1,252 kati ya Mipango 3,283 iliyoandaliwa na Tume na wadau mbalimbali. Aidha, katika mwaka 2024/25, Wizara kupitia Tume itaendelea kuhifadhi taarifa za Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 850 na Wilaya 10 katika mfumo.
Ufuatiliaji na Tathmini ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi
Mheshimiwa Spika,
kwa mwaka 2023/24 Tume imeendelea kufanya Ufuatiliaji na Tathmini ya uzingatiaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 62 katika maeneo yaliyopitiwa na Miradi ya Kimkakati katika Halmashauri za Bahi, Chemba, Singida, Bunda, Makete, Sumbawanga, Igunga, Kibaha, Tarime, Chamwino, Ngorongoro, Kilombero, na Misungwi. Ufuatiliaji na Tathmini umebaini kuwa, Mipango ya Matumizi ya Ardhi inayoandaliwa haizingatiwi ipasavyo. Sababu ya kutokuzingatiwa ni pamoja na changamoto ya kimuundo kati ya Kamati za Halmashauri za vijiji hususan Kamati ndogo za huduma za jamii na Kamati ya Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi (VLUM). Hii inatokana na Mwongozo wa Ushirikishwaji wa Uaandaji wa Mpango wa Matumizi ya Ardhi kuzuia wajumbe wa Halmashauri ya Kijiji kuteuliwa kuwa wajumbe wa Kamati ya Usimamizi wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji

(VLUM) hali inayosababisha mgongano katika utekelezaji wa majukumu na hatimae kuacha ombwe katika usimamizi wa utekelezaji wa mipango ya Matumizi ya Ardhi.
Mheshimiwa Spika, kutokana na changamoto hiyo, Wizara kupitia Tume imeanza kufanya marekebisho ya mwongozo wa uaandaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa kushirikisha wadau mbalimbali wa masuala ya Ardhi ili kuwianisha majukumu ya Kamati ya Huduma za Jamii na VLUM.
BODI ZA KITAALAM
Mheshimiwa Spika,
Wizara ina jukumu la kusimamia Bodi za Wataalam wa Sekta ya Ardhi. Bodi hizo ni Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipangomiji; Bodi ya Usajili wa Wathamini; na Baraza la Taifa la Wapima Ardhi. Majukumu ya Bodi hizi yanajumuisha kusajili wataalam wa sekta na kampuni za kitaalam, kusimamia weledi na maadili ya kitaaluma.
Bodi ya Usajili wa Wataalam wa Mipangomiji
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24, Wataalam 39 na kampuni 11 za Mipangomiji zimesajiliwa, hivyo kuwa na jumla ya Wataalam 499 na kampuni 101 zilizosajiliwa. Aidha, Wataalam wawili (2) wamefutiwa usajili na Bodi kwa

ukiukwaji wa sheria na maadili katika utendaji kazi. Pia, Bodi inaendelea kufanya uchunguzi kuhusu tuhuma za ukiukaji wa maadili ya utendaji kazi dhidi ya wataalam saba (7) na Kampuni sita (6) za mipangomiji katika mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Lindi na Songwe.
Mheshimiwa Spika, Bodi imefanya ufuatiliaji wa utendaji kazi na uzingatiaji Sheria za Mipangomiji katika Mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Mwanza, Shinyanga, Geita na Dodoma, na kufanya ukaguzi wa jumla ya michoro ya mipangomiji 935 pamoja na kutoa ushauri wa kitaalam katika Ofisi za Ardhi za Mikoa hiyo.
Mheshimiwa Spika, Bodi kwa kushirikiana na Mamlaka ya Serikali Mtandao (e-GA) imeandaa mfumo wa kielektroniki kwa ajili ya kusajili miradi inayofanywa na wataalam na kampuni za mipangomiji na wataalam wa mipangomiji. Mfumo huu utarahisisha upatikanaji wa taarifa zinazohusiana na miradi na wataalam wa mipangomiji na kuimarisha ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25, Bodi itaendelea kusajili Wataalam na kampuni za mipangomiji zitakazokidhi vigezo ili kuimarisha utendaji kazi. Aidha, usimamizi na ufuatiliaji wa utendaji kazi na uzingatiaji wa sheria za mipangomiji utaendelea kufanyika ili kuimarisha ustawi wa sekta ya mipangomiji.

Bodi ya Usajili wa Wathamini
Mheshimiwa spika,
hadi tarehe 15 Mei, 2024 jumla ya Wathamini 94 wamesajiliwa katika ngazi ya Usajili Kamili, Wathamini 84 katika ngazi ya Usajili wa Awali, Wathamini Wasaidizi 52 wameorodheshwa na Kampuni za Uthamini nane (8) zimesajiliwa. Idadi hii inafanya jumla ya Wathamini 389 wenye Usajili Kamili, Wathamini 775 wenye Usajili wa Awali, Kampuni za Uthamini 75 na Wathamini Wasaidizi 162. Bodi pia inashughulika na masuala ya kinidhamu na kimaadili ambapo wathamini 28 na kampuni 16 zimetolewa taarifa kuhusu masuala ya kinidhamu na hatua kuanza kuchukuliwa. Hivyo, kufanya jumla ya Wathamini ambao wamechukuliwa hatua kufikia 41 na kampuni 36; kati ya masuala haya ya kinidhamu, masuala yanayohusu wathamini 27 na kampuni 29 yamekamilishwa na kufungwa.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25, Bodi imepanga kuendelea kusajili wathamini 150 katika ngazi zote, kutengeneza Mfumo wa TEHAMA kwa ajili ya usajili wa wathamini, kufanya mapitio ya mitaala ya mafunzo ya kujiandaa na mitihani ya Usajili Kamili, kufanya kaguzi za kitaalam, kuendesha mafunzo endelevu kwa wathamini na kufanya Mkutano Mkuu wa Mwaka. Aidha, Bodi imepanga kukusanya kiasi cha shilingi milioni
740.55 kutoka kwenye vyanzo vyake vya mapato ya ndani.

Baraza la Taifa la Wapima Ardhi
Mheshimiwa Spika,
katika mwaka 2023/24, Baraza lilipokea maombi 98 kwa ajili ya usajili wa wapima ardhi na maombi ya leseni za kampuni. Kati ya maombi yaliyowasilishwa, wapima ardhi 74 wamesajiliwa na kampuni 24 zilipewa leseni hivyo, kufanya jumla ya wapima ardhi waliosajiliwa nchini kuwa 793 na kampuni zenye leseni 119. Katika mwaka 2024/25, Baraza litasajili wapima ardhi 80 na kutoa leseni kwa Kampuni 30. Aidha, Baraza litaendelea kuchukua hatua kwa wapima ardhi na kampuni zitakazokiuka taaluma ya maadili ya kazi za upimaji kwa kusitisha leseni ya upimaji.
Vyuo vya Ardhi vya Morogoro na Tabora
Mheshimiwa Spika
, Vyuo vya Ardhi Morogoro (ARIMO) na Tabora (ARITA) vimeendelea kutekeleza majukumu ikiwemo kufanya utafiti, kutoa mafunzo ya muda mrefu katika ya fani za mipangomiji, upimaji ardhi, urasimu ramani, ubunifu na uchapishaji, usimamizi wa ardhi, uthamini na usajili. Katika mwaka 2023/24, Wizara kupitia vyuo hivyo iliahidi kudahili wanafunzi 2,000 (ARITA 1,500 na ARIMO 500).
Napenda kuliarifu Bunge lako tukufu kuwa jumla ya wanafunzi 1,744 walidahiliwa ambapo Chuo Ardhi Tabora kilidahili wanafunzi 1,256 na Chuo cha Ardhi Morogoro kilidahili wanafunzi 488 katika

mafunzo ya Astashahada na Stashahada. Aidha, wanafunzi 1,602 wamehitimu mafunzo yao. Aidha, Chuo cha Ardhi Morogoro kimeongeza miundombinu ya Madarasa kwa kujenga vyumba vitatu (3) vya mihadhara. Vilevile, Wizara iliahidi kukamilisha ujenzi wa Maktaba ya Chuo cha Ardhi Tabora ifikapo Juni, 2024. Napenda kuliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, ujenzi wa Maktaba hiyo unaendelea na utakamilika kama ilivyopangwa.
Mheshimiwa Spika, katika mwaka 2024/25 Wizara kupitia vyuo vyake inatarajia kudahili wanafunzi 2,670 (ARITA 1,580 na ARIMO 1,090).
Aidha, kutokana na ongezeko la mahitaji ya wataalam wa sekta ya ardhi, Chuo cha Ardhi Morogoro kitaongeza udahili wa wanafunzi kutoka wanafunzi 489 hadi 1,090. Vilevile, Wizara itakamilisha ujenzi wa vyumba viwili (2) vya madarasa ya Chuo cha Ardhi Morogoro.


Naibu Waziri wa Ardhi Mhe. Geophrey Pinda (kushoto) akipata maelezo kutoka kwa mwanafunzi wa Chuo cha Ardhi Morogoro (ARIMO) wakati wa mahafali Novemba 2023

MASUALA MTAMBUKA
Utawala na Rasilimali Watu
Mheshimiwa Spika,
Utawala na Rasilimali Watu ni sehemu muhimu katika usimamizi na utekelezaji wa majukumu ya Wizara. Hadi tarehe 15 Mei, 2024 Wizara ina jumla ya watumishi 2,395 kati ya hao wanaume 1,679 na wanawake 716. Aidha, katika kipindi hicho Wizara ilipata kibali cha kuajiri Watumishi 98 wa fani za Upimaji wa Ardhi,

Uthamini na Utawala wa Ardhi. Kwa kuzingatia muundo na majukumu ya Wizara, idadi halisi ya mahitaji ya watumishi ni 5,028 na hivyo kuwa na upungufu wa watumishi 2,633 (Jedwali Na.20). Katika kukabiliana na upungufu huo, Wizara imeendelea kuwasiliana na Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora ili kupatiwa watumishi kwa idadi inayokidhi mahitaji. Aidha, watumishi 347 wamepandishwa vyeo na watumishi 37 wamebadilishwa kada. Watumishi 1,166 watapandishwa vyeo katika mwaka 2024/2025.
Mheshimiwa Spika, Wizara imeendelea kusimamia nidhamu na uadilifu katika utoaji wa huduma za Sekta ya Ardhi nchini. Katika kusimamia nidhamu za watumishi, hatua mbalimbali kwa watumishi waliotuhumiwa kwa makosa mbalimbali zilichukuliwa ambapo watumishi 22 wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi wa tuhuma za ukosefu wa maadili ya utendaji kazi katika Utumishi wa Umma; Watumishi saba (7) waliachishwa kazi na watumishi wawili (2) walipewa onyo na kuwekwa chini ya uangalizi.
Kuwajengea Uwezo Watumishi
Mheshimiwa Spika,
Wizara imeendelea kuwajengea uwezo watumishi kwa kuwawezesha kushiriki katika mafunzo ya muda mrefu na mfupi kwa lengo la kuwaongezea utaalam, ujuzi na maadili ili kuhakikisha wanakuwa na weledi zaidi

katika utoaji wa huduma bora kwa wananchi. Katika mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kuwawezesha watumishi 215 kupata mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa kuzingatia mahitaji na Mpango wa Mafunzo wa Wizara. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara imewezesha mafunzo ya muda mfupi na mrefu kwa watumishi 330. Katika mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kuwawezesha watumishi kushiriki mafunzo kwa kuzingatia Mpango wa Mafunzo wa Wizara.
Habari na Elimu kwa Umma
Mheshimiwa Spika
, katika mwaka 2023/24, Wizara iliahidi kuendelea kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala mbalimbali ya Sekta ya Ardhi. Hadi tarehe 15 Mei, 2024, Wizara imetoa elimu kwa umma kuhusu masuala ya sekta ya ardhi kupitia vipeperushi, majarida, mitandao ya kijamii, makala za magazeti, kliniki za ardhi, mikutano ya hadhara na vipindi vya redio na luninga. Aidha, Wizara ilifanya mkutano mmoja (1) na wahariri wa vyombo vya habari pamoja na mikutano 11 ya waandishi wa habari kuhusu masuala ya Sekta ya Ardhi. Vilevile, elimu kwa umma imetolewa kupitia tovuti ya Wizara (www.lands.go.tz) na maonesho mbalimbali. Pia, elimu kwa umma imeendelea kutolewa kupitia kipindi cha Televisheni cha ‘Maisha ni Nyumba’ kinachoratibiwa na Shirika la Nyumba la Taifa.

Mheshimiwa Spika, kwa mwaka 2024/25, Wizara itaendelea kutoa elimu kwa umma kwa njia mbalimbali ikiwemo vyombo vya habari, mitandao ya kijamii, mikutano ya hadhara na maonesho mbalimbali.
SHUKRANI
Mheshimiwa Spika,
kipekee nawashukuru Mhe. Geophrey Mizengo Pinda (Mb), Naibu Waziri; Mhandisi Anthony Damian Sanga, Katibu Mkuu; na Bi. Lucy Dominico Kabyemera, Naibu Katibu Mkuu; kwa kunisaidia kutekeleza majukumu ya kusimamia sekta hii muhimu. Aidha, nawashukuru Bw. Nathaniel Mathew Nhonge, Kamishna wa Ardhi; Bw. Hamad Abdallah Hamad, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Nyumba la Taifa; Prof. Wakuru Magigi Maseka, Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi; Bi. Evelyne Mugasha, Mthamini Mkuu wa Serikali; na Bi. Stella Tullo, Msajili wa Mabaraza ya Ardhi na Nyumba ya Wilaya. Pia, nawashukuru Wakuu wa Idara na Vitengo, Wenyeviti wa Bodi; na watumishi wote wa Wizara na Taasisi kwa kutekeleza majukumu yao kwa bidii na maarifa na hivyo kuleta ufanisi katika kufikia malengo ya Wizara.
Mheshimiwa Spika, naomba nitumie fursa hii kuwashukuru Washirika wa Maendeleo ambao Serikali imekuwa ikishirikiana nao katika utekelezaji wa shughuli za maendeleo zinazohusiana na Sekta ya

Ardhi. Washirika hao ni pamoja na Benki ya Dunia, Benki ya EXIM ya Korea Kusini, UN-HABITAT, Shelter Afrique, African Union Boarder Program, Regional Centre for Mapping of Resources Development (RCMRD), Benki ya Maendeleo Afrika, Benki Kuu ya Tanzania (BOT), Tanzania Mortgage Refinancing Company (TMRC), Watumishi Housing Company Limited, taasisi za fedha za ndani, Asasi za Kiraia, Sekta Binafsi na wananchi kwa michango yao katika utekelezaji wa majukumu ya sekta ya ardhi.
Mheshimiwa Spika, napenda kutoa shukrani kwa vyombo vya habari kwa ushirikiano mkubwa waliotupatia katika kutoa elimu na hamasa kwa umma kuhusu masuala ya sekta ya ardhi. Kwa hakika wanahabari wameiwezesha Wizara kuwafikia wadau wengi zaidi kwa namna mbalimbali.
Mheshimiwa Spika, mwisho lakini si kwa umuhimu, napenda kuishukuru familia yangu hususan mke wangu Bi Mariam Bakari Silaa na mwanangu Simba William Silaa kwa uvumilivu na kunitia moyo katika utekelezaji wa majukumu yangu.
HITIMISHO
Mheshimiwa Spika,
napenda kuhitimisha hotuba yangu kwa kuliarifu Bunge lako Tukufu kuwa, Wizara katika mwaka 2024/25, itaendelea kuimarisha uratibu na usimamizi wa maendeleo ya

Sekta ya Ardhi kwa kuboresha huduma zinazotolewa. Ili kutekeleza azma hiyo, Wizara itazingatia vipaumbele vilivyoainishwa awali ambavyo ni:-
Kuongeza kasi ya upangaji, upimaji na umilikishaji wa ardhi mijini na vijijini;
Kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro ya ardhi;
Kuimarisha mifumo ya TEHAMA katika utunzaji wa kumbukumbu, utoaji wa huduma na upatikanaji wa taarifa za ardhi;
Kuhakikisha uwepo wa nyumba bora, ukuaji wa sekta ya milki na maendeleo ya makazi kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii; na
Kuimarisha mipaka ya kimataifa.

MAKADIRIO YA MAPATO NA MATUMIZI KWA MWAKA 2024/25
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu lijadili na kuidhinisha
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi (Fungu 48) na Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi (Fungu 03) kama ifuatavyo: -

Fungu 48: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi

Na
Maelezo
Aina
Makisio ya Bajeti
A​
Mapato ya
250,000,000,000.00​
Makisio ya Matumizi

B

Matumizi ya Kawaida
Mishahara (PE)
48,435,318,000​
Taasisi (PE)
1,720,210,000​
Jumla ya
50,155,528,000
Matumizi
35,399,978,250​
Taasisi (OC)
1,243,068,750​
Jumla ya Matumizi Mengineyo
36,643,047,000
Jumla ya matumizi ya Kawaida
86,798,575,000
CMatumizi ya
Maendeleo
Ndani
10,601,757,000​
Nje
60,054,753,000​
Jumla ya Miradi ya Maendeleo
70,656,510,000
Jumla Kuu
157,455,085,000
Jumla ya Matumizi ya Kawaida na Maendeleo kwa Fungu 48 ni shilingi 157,455,085,000.00.
Fungu 03: Tume ya Taifa ya Mipango ya Matumizi ya Ardhi.

AINAAINA YA MATUMIZI
SHILINGI
A
Mapato
Mapato ya Serikali
18,000,000
B
Matumizi ya Kawaida;
Mishahara
3,887,780,000​
Matumizi Mengineyo
3,244,318,000​
Jumla Ndogo
7,132,098,000
C
Matumizi ya Maendeleo
Fedha za ndani
5,041,232,000​
Jumla Ndogo
5,041,232,000
JUMLA KUU (B+C)
12,173,330,000

Mheshimiwa Spika, jumla kuu ya fedha zinazoombwa na Wizara (Fungu 48 na Fungu 03) ili Bunge liweze kujadili na kuidhinisha ni shilingi 171,372,508,000.00.
Mheshimiwa Spika, naomba kuhitimisha hotuba yangu kwa kutoa shukrani zangu za dhati kwako binafsi pamoja na Waheshimiwa Wabunge kwa kunisikiliza. Hotuba imeambatana na majedwali yanayoainisha kwa ufasaha takwimu zinazohusiana na shughuli zilizotekelezwa na Wizara. Aidha, hotuba hii inapatikana pia kwenye tovuti ya Wizara ambayo ni www.lands.go.tz.
  • Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.

VIAMBATISHO
Jedwali Na. 1: Mchanganuo wa Fedha za Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo zilizopokelewa na kutumika hadi 15 Mei, 2024



Aina ya Bajeti
Kiasi kilichoidhinishwa kwa mwaka 2023/24
ikijumuisha
Uhamisho (Reallocation)
Kiasi cha fedha kilichopokelewa hadi 15 Mei 2024
Asilimia (%) ya kiasi kilichopokelewa vs kilichoidhinishwa.
1​
Matumizi ya KawaidaMishahara (Wizara + Taasisi)
43,428,651,000​
34,717,391,508.40
79.94​
Jumla ya Mishahara43,428,651,000
34,717,391,508.40
79.94
Matumizi Mengineyo
(OC) -(Wizara+Taasisi)
39,013,249,859​
21,941,760,775.50​
56.24​
Jumla ya Matumizi
mengineyo (OC)
39,013,249,859
21,941,760,775.50
56.24
Jumla ya Matumizi
ya Kawaida
82,441,900,859
56,659,152,283.90
68.73
2​
Miradi ya
Maendeleo
Ndani
311,013,639,000​
309,527,884,044.20
99.52​
Nje
57,370,439,214​
56,943,395,682.60
99.26​
Jumla ya Fedha za Maendeleo
368,384,078,214
366,471,279,726.80
99.48
Jumla Fungu 48
450,825,979,072
423,130,432,010.70
93.86
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 2: Maduhuli Yatokanayo na Kodi ya Ardhi Yaliyokusanywa kuanzia Julai, 2023 hadi 15 Mei 2024
Na.
Mkoa
Makisio
Makusanyo
Asilimia %
1​
Arusha
16,790,000,000​
6,807,617,905.70​
40.55
2​
Dar es Salaam
92,575,000,000​
59,579,518,853.19​
64.13
3​
Dodoma
23,000,000,000​
13,118,598,939.12​
57.00
4​
Geita
4,830,000,000​
1,068,926,791.18​
22.13
5​
Iringa
5,060,000,000​
2,403,471,650.14​
47.50
6​
Kagera
4,715,000,000​
1,315,630,478.73​
27.90
7​
Katavi
2,415,000,000​
647,857,804.16​
26.83
8​
Kigoma
4,025,000,000​
1,214,720,116.91​
30.18
9​
Kilimanjaro
4,830,000,000​
3,185,000,399.14​
65.94
10​
Lindi
4,255,000,000​
2,835,639,555.47​
66.64
11​
Manyara
3,910,000,000​
1,466,267,463.30​
37.50
12​
Mara
5,405,000,000​
1,679,598,900.89​
31.07
13​
Mbeya
15,755,000,000​
3,135,586,583.36​
19.90
14​
Morogoro
14,260,000,000​
4,123,392,146.82​
28.92
15​
Mtwara
6,980,000,000​
5,154,066,461.83​
73.84
16​
Mwanza
24,610,000,000​
7,285,576,433.45​
29.60
17​
Njombe
4,715,000,000​
961,205,021.67​
20.39
18​
Pwani
18,745,000,000​
7,042,242,662.51​
37.57
19​
Rukwa
2,990,000,000​
615,364,926.44​
20.58
20​
Ruvuma
3,680,000,000​
1,063,726,227.68​
28.91
21​
Shinyanga
9,775,000,000​
2,207,507,285.58​
22.58


Na.
Mkoa
Makisio
Makusanyo
Asilimia %
22​
Simiyu
2,990,000,000​
662,068,718.96​
22.14
23​
Singida
3,680,000,000​
987,905,481.02​
26.85
24​
Songwe
3,680,000,000​
1,334,128,996.05​
36.25
25​
Tabora
4,255,000,000​
1,062,108,015.84​
24.96
26​
Tanga
12,075,000,000​
5,042,272,180.89​
41.76
Jumla
300,000,000,000
136,000,000,000.00
45.30
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 3: Mchanganuo wa Fedha za Matumizi ya Kawaida na Miradi ya Maendeleo Fungu 03 zilizopokelewa na kutumika hadi 15 Mei, 2024

Aina ya Matumizi

Bajeti iliyoidhinishwa
Kipindi cha Julai 2023 Hadi Tarehe
15 Mei, 2024
% ya Kiasi Kilichopokelewa
Kiasi
Kilichopokelewa
Kiasi
Kilichotumika
Mishahara
3,126,020,500​
2,547,154,000​
2,547,154,000​
81.48​
Matumizi Mengineyo
2,293,724,000​
1,368,568,130.63​
1,365,603,482.18​
59.67​
Mradi wa Maendeleo
3,410,000,000​
3,410,000,000​
3,329,466,879​
100​
Jumla
8,829,744,500
7,325,722,130.63
7,242,224,361.18
82.97
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 4: Fedha Zilizotokana na kuhamasisha wadau na kuchangia Utekelezajikwa Fungu 03 kwa Mwaka kuanzia Julai, 2023 hadi 15 Mei 2024
Na.
Mdau
Kiasi cha FedhaKazi zilizotekelezwa
Idadi
ya Vijiji
1.​
Jane Goodall Institute (JGI)
23,595,000
Kuandaa Mpango wa Matumizi ya Ardhi katika
Vijiji 3 vya Nyamhoza, Nyamigufa na Mkwanga katika Halmashauri ya Wilaya ya Kigoma
3​
2.​
Ngorongoro
Conservation Authority
(NCA)

220,000,000​
Uandaaji wa Mipango kina na Upimaji wa katika Vijiji vya Msomera, Saunyi na Kitwai
-​
3.​
MAKENA
25,000,000​
Uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi Vijiji 3 vya Turugeti, Kitenga na Kwisarara
katika H/Wilaya ya Tarime Mkoa wa Mara
3​
4.​
BONDE LA MAJI W1AMI
2,560,000​
Uchambuzi wa ripoti za Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 4 vya Langali, Kibangula, Nyandira na Tchezema vya Halmashauri ya Wilaya ya Mvomero pamoja na Uchapishaji wa
ripoti za Mipango hiyo
-​
5.​
Frankfurt Zoological Society
(FZS)/TANAPA -
704,973,150​
i) Uandaaji wa Mipango ya Matumizi ya Ardhi katika Vijiji 30 Wilaya za
30​



Na.
Mdau
Kiasi cha FedhaKazi zilizotekelezwaIdadi ya
Vijiji
Hifadhi ya Taifa NyerereMorogoro (6), Kisarawe (5), Tunduru (8),
Liwale (6) na Ulanga (5).
ii) Kuandaa Mipango Kina na Hati za Hakimiliki za Kimila (9,874) katika Vijiji 25 vya Wilaya 4
6.​
Ofisi ya Makamu wa Rais (VPO)
715,000,000​
Kuandaa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya vijiji 5 katika wilaya ya Wanging’ombe (1) na Sumbawanga (4), Mipango Kina ya vijiji 30 na Utoaji wa Hati za Hakimiliki za Kimila katika Wilaya 6 za Mpimbwe (1063), Mbeya (598),
Mbarali (563), Iringa (740), Wanging’ombe
(395) na Sumbawanga (1,082).
5​
7.​
UVINZA
1,200,000​
Kuchapisha vitabu vya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji vya Kashangulu, Lufubu na
Ubanda katika Halmashauri ya Wilaya ya Uvinza
-​
8.​
Benki ya
Maendeleo ya Afrika (AfDB)

927,722,500
Kuandaa Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 72 katika Wilaya za Musoma (24), Butiama (24), Shinyanga (4), Makete (16) na
Sumbawanga (4)
72​


Na.
Mdau
Kiasi cha FedhaKazi zilizotekelezwa
Idadi ya Vijiji
9.​
Halmashauri ya Wilaya ya KyerwA
0​
Kuandaa Mpango wa Matumizi ya Ardhi ya Kijiji cha Morongo
1​
10.​
Uvinza
1,200,000​
Kuchapisha vitabu vya Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji 3 vya Kashangulu, Lufubu na Ubanda katika Halmashauri ya Wilaya ya
Uvinza
11.​
TFS
53,178,000​
Uhuishaji wa mipaka ya upimaji wa Vijiji 7 katika Halmashauri ya Wilaya ya Mlele katika Vijiji vya Mgombe, Kanoge, Wachawaseme, Mtakuja, Nsekwa, Kaulolo na Kalovya
Jumla
2,776,032,50
0
114
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 5: Idadi ya Hatimiliki, Hati za Hakimiliki za Kimila, Hati za Sehemu ya Jengo, Vyeti vya Ardhi ya Vijiji, Miamala ya Hatimiliki na Nyaraka za Kisheria Zilizotolewa na Kusajiliwa Kuanzia Tarehe 01 Julai, 2023 Mpaka 15 Mei, 2024
Na.
Mkoa
Hatimiliki
Hati za Hakimiliki Za Kimila
Hati Za Sehemu Ya Jengo
Vyeti Vya Ardhi Ya Kijiji
Miamala Ya Hatimiliki Na
Nyaraka Za Kisheria
1.​
Dodoma
20,583​
1,311​
4,473​
2.​
Dar es Salaam
16,541​
324​
35,344​
3.​
Pwani
6,718​
3160​
1​
10,788​
4.​
Mwanza
5,539​
8,889​
5.​
Mbeya
4,366​
9461​
33​
2,407​
6.​
Tanga
2,859​
801​
2​
2,866​
7.​
Morogoro
2,713​
2,457​
13​
3,884​
8.​
Arusha
2,262​
1238​
1​
5,017​
9.​
Manyara
2,143​
1063​
3​
1,089​
10.​
Simiyu
1,999​
11,750​
21​
807​
11.​
Kigoma
1,829​
6008​
11​
811​
12.​
Iringa
1,790​
1,301​
8​
1,976​
13.​
Shinyanga
1,756​
4​
0​
1,996​
14.​
Njombe
1,559​
7279​
28​
1,006​
15.​
Ruvuma
1,525​
4656​
15​
1,007​
16.​
Songwe
1,514​
497​
38​
584​
17.​
Kilimanjaro
1,484​
458​
2​
2,957​


Na.
Mkoa
Hatimiliki
Hati za Hakimiliki Za Kimila
Hati Za Sehemu Ya Jengo
Vyeti Vya Ardhi Ya Kijiji
Miamala Ya Hatimiliki Na Nyaraka Za Kisheria
18.​
Mtwara
1,382​
128​
898​
19.​
Geita
1,341​
1,113​
20.​
Kagera
1,267​
269​
23​
2,900​
21.​
Mara
1,226​
207​
18​
1,433​
22.​
Tabora
1,191​
61​
62​
969​
23.​
Singida
1,010​
2,245​
6​
702​
24.​
Lindi
965​
3458​
23​
610​
25.​
Katavi
889​
24,228​
28​
412​
26.​
Rukwa
789​
4954​
26​
518​
JUMLA
87,240
86,994
324
362​
95,456
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 6: Mchanganuo wa maombi ya ardhi ya uwekezaji
Na
WawekezajiIdadi ya
Maombi
Ukubwa (Ha)
Mtaji (Usd-Mil)
1​
TIC
148​
11,189.67​
56.08​
2​
EPZ
3​
6.74​
2.87​
3​
Watanzania
65​
95.73​
-​
JUMLA
216
11,292.14
58.95
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 7: Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi Kiutawala
Na
MkoaIdadi ya Migogoro ya
Ardhi Iliyopokelewa
Idadi ya Migogoro ya Ardhi
Iliyoshughulikiwa
1​
Arusha
329​
175​
2​
Dar es Salaam
4,486​
3285​
3​
Dodoma
2,330​
1780​
4​
Geita
63​
41​
5​
Iringa
41​
31​
6​
Kagera
133​
110​
7​
Katavi
37​
37​
8​
Kigoma
34​
27​
9​
Kilimanjaro
147​
113​
10​
Lindi
102​
89​
11​
Manyara
124​
78​
12​
Mara
442​
317​
13​
Mbeya
272​
182​
14​
Morogoro
32​
24​
15​
Mtwara
92​
38​
16​
Mwanza
1,181​
111​
17​
Njombe
118​
102​
18​
Pwani
303​
238​
19​
Rukwa
106​
80​
20​
Ruvuma
146​
109​
21​
Shinyanga
62​
25​


Na
MkoaIdadi ya Migogoro ya Ardhi IliyopokelewaIdadi ya Migogoro ya Ardhi Iliyoshughulikiwa
22​
Simiyu
45​
40​
23​
Singida
30​
26​
24​
Songwe
66​
45​
25​
Tabora
627​
613​
26​
Tanga
512​
169​
JUMLA
11,860
7,885
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 8: Utatuzi wa Migogoro ya Ardhi katika Vijiji 975
NaMkoaJumlaVijiji/Mitaa Ambayo
Utekelezaji Umekamilika
Vijiji/Mitaa Ambayo
Utekelezaji Unaendelea
1​
Kigoma
33​
29​
20​
2​
Mbeya
54​
33​
19​
3​
Tanga
18​
6​
12​
4​
Arusha
116​
10​
106​
5​
Katavi
60​
41​
19​
6​
Pwani
87​
17​
70​
7​
Singida
12​
1​
18​
8​
Kagera
34​
11​
25​
9​
Tabora
98​
58​
47​
10​
1ringa
14​
4​
19​
11​
Ruvuma
38​
30​
8​
12​
Geita
39​
22​
17​
13​
Mtwara
6​
10​
2​
14​
Morogoro
81​
48​
42​
15​
Dsm
5​
2​
3​
16​
Songwe
5​
0​
5​
17​
Simiyu
45​
45​
0​
18​
Kilimanjaro
8​
10​
2​
19​
Manyara
21​
16​
5​
20​
Dodoma
40​
0​
42​
21​
Rukwa
13​
7​
6​


NaMkoaJumlaVijiji/Mitaa Ambayo Utekelezaji UmekamilikaVijiji/Mitaa Ambayo Utekelezaji Unaendelea
22​
Shinyanga
9​
5​
7​
23​
Lindi
19​
11​
14​
24​
Mwanza
23​
23​
4​
25​
Njombe
22​
0​
29​
26​
Mara
20​
12​
12​
Jumla
920
451
553
Jumla Kuu
1,004
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 9A: Malipo ya Fidia kwa Wananchi Waliopo Katika Vijiji 975
NA
ENEO
VIJIJI/MITAAKIASI (TZS)HATUA
ILIYOFIKIWA
1Mita 500 ya Hifadhi ya Bwawa la MinduMikoroshini, Mindu, Kasanga, Mkoya na
Mkwajuni
4,683,884,895.00​
Uthamini umekamilika
2Hifadhi ya Taifa RuahaMsanga, Luhanga, Kilambo, Yala na Madundasi na vitongoji 17 katika vijiji 7 vya Iwalanje, Ikanutwa, Magigiwe, Vikae, Igunda, Lualanje na
Mwanavala.
72,850,221,038.67​
Uthamini unaendelea
3Hifadhi ya Bonde la
Mto Kilombero
Wananchi 1053 katika
Kijiji cha Ngombo
7,351,097,480.46​
Uthamini
umekamilika
4Pori la Akiba MkunguneroKaya 145 katika vitongoji vya Kagera, Msumbiji, Elbenek na Ndaja katika vijiji vya
Kisondoko na Keikei
511,567,709.34​
Uthamini umekamilika
5Eneo la Ghuba ya SpekeTamau, Serengeti, Nyatwali na Kariakoo
59,516,450,405.93​
Uthamini umekamilika na
nyaraka


NA
ENEO
VIJIJI/MITAAKIASI (TZS)HATUA
ILIYOFIKIWA
zimewasilishwa
Hazina
6Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Kilimanjaro (KIA)Kijiji cha Chemka, Mtakuja, Tindigani, Samaria Kati, Majengo,
Mhula na Sanya Station
11,321,898,061.00​
Uthamini umekamilika
7Hifadhi ya Taifa ya MkomaziKitongoji cha Kimuni katika Kijiji cha Mkota
642,917,912.2​
Uthamini umekamilika
8Hifadhi ya Taifa Mahale-Uvinza- Kigoma;Wananchi 194 katika kitongoji vya Mahasa na Kabuyungu katika kijiji
cha Kalilani.
1,605,144,974.42​
Uthamini unaendelea
9Shamba la utegiKitongoji cha Kibinyongo, Mabatini, Oringa, Denga, Omuga na Shule ya Msingi
Utengi
7,727,036,577.31​
Uthamini umekamilika
10Pori la Akiba la Mpanga KipengeleJumla ya Kaya 101 (Kaya 30 katika Kitongoji cha Soliwaya
Kijiji cha Wangama; na Kaya 56 katika
1,200,000,000.00​
Uthamini unaendelea


NA
ENEO
VIJIJI/MITAAKIASI (TZS)HATUA
ILIYOFIKIWA
Kitongoji cha Mlowo na kaya 15 katika Kitongoji cha Maswagu Kijiji cha
Kigala;
11Pori Tengefu Mto
Umba
Perani, Mbuta,
Mwakijembe na Mkota
10,458,045.00​
Uthamini wa Awali
umekamilika
12Pori Tengefu Lunda MkwambiKaya 82 katika Kijiji cha Maperamengi
198,670,000.00​
Uthamini unaendelea
13Hifadhi ya Msitu
Mkuti
Kanisa la wasabato
Rungwe mpya-
53,838,381.61​
Uthamini
umekamilika
14Hifadhi ya Msitu
Mbangala
Marumba na
Mbangalambuyuni-
2,779,152,634.34​
Uthamini wa Awali
umekamilika
15Hifadhi ya Taifa
Ibanda Kyerwa
Familia 13 katika Kijiji
cha Nyakakoni
353,667,000.00​
Uthamini
umekamilika
16Hifadhi ya Taifa ArushaKaya 33 katika Kitongoji cha Momela eneo la Nasula/ Kijiji
cha Orkung’wado
626,674,753.00​
Uthamini unaendelea
17Hifadhi ya Msitu wa Kupanda Sao HILLVijiji vya Igeleke, Usokani, Kibengu, Wamimbalwe,
Mapanda, Iyegeya,
7,087,123,000.00​
Uthamini wa Awali umefanyika


NA
ENEO
VIJIJI/MITAAKIASI (TZS)HATUA ILIYOFIKIWA
Ihomasa, Mangunguli, Kitasengwa, Luhunga, Ligolofi na Ligereka-
18Hifadhi ya Msitu Mto LoasiKitongoji cha Misako katika Kijiji cha Mpasa53,000,000.00Uthamini wa awali umefanyika
Jumla Kuu
178,572,802,868.2
8
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na 9B: Mchanganuo wa maeneo yaliyolipwa fidia
NA
ENEO
VIJIJI/MITAAKIASI (TZS)HATUA ILIYOFIKIWA
1.Hifadhi ya Taifa ya SaadaniKaya 17 na
mashamba 22 katika Kitongoji cha Uvinje
376,436,839.60​
Fidia imelipwa mwezi Septemba 2023 kwa wananchi wa Kitongoji cha Uvinje (kaya 17 na mashamba 22) katika Kijiji cha Saadani ili kupisha eneo la Hifadhi
ya Taifa ya Saadani.
2.Hifadhi ya Taifa ArushaWananchi 15 ndani ya Shamba Na. 358 katika kijiji cha Orkung’wado
135,365,800.00​
Wamelipwa fidia kupitia H/Wilaya ya Meru Desemba, 2022 na kupisha eneo la Hifadhi ya Taifa
Arusha.
3Hifadhi ya Maji Mto THEMIWananchi 51 wa Kijiji cha Kivuluvulu na 42
wa Kijiji cha Olgilai
887,043,462.00​
Wananchi wamelipwa fidia na kuondoka
4Hifadhi ya Bwawa la
Farkwa
Wananchi wa
vijiji vya
7,400,700,000.00​
Wananchi wamelipwa
fidia na kuondoka


NA
ENEO
VIJIJI/MITAAKIASI (TZS)HATUA ILIYOFIKIWA
Bubutole na Mombose
5
Hifadhi ya Maji Nyakanasi​
Wananchi 6 wa Mtaa wa Nyakanasi
73,146,200.56​
Wananchi wamelipwa fidia na kuanza kuondoaka
6Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Kilimanjaro (KIA)Kijiji cha Chemka, Mtakuja, Tindigani, Samaria Kati, Majengo, Mhula
na Sanya Station
11,200,000,000.00​
Wananchi 1,666 kati
ya 1,712 wamelipwa fidia
Jumla Kuu
20,072,692,302.1
6
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 10: Uthamini wa Fidia Katika Miradi ya Kimkakati
Na.
Mradi
Mahali
1.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha ujenzi wa miundombinu ya umeme wa msongo wa 400KV kutoka
Mtwara hadi Somanga Lindi
Mtwara na Lindi
2Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha Ujenzi wa Reli ya Kisasa awamu ya tatu (SGR Lot III) kutoka Makutupora hadi
Tabora
Singida na Tabora
3.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha Ujenzi wa Reli ya Kisasa awamu ya Nne (SGR Lot IV) kutoka Tabora hadi IsakaTabora na Shinyanga
4.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha Ujenzi wa Reli ya Kisasa awamu ya Tano (SGR Lot V) kutoka Isaka hadi
Mwanza
Shinyanga na Mwanza
5.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha Ujenzi wa Miundombinu ya umeme wa kuendeshea Reli ya Kisasa
awamu ya Tano (SGR Lot V) kutoka Isaka hadi Mwanza
Shinyanga na Mwanza
6.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha Ujenzi wa Reli ya
Kisasa awamu ya Sita (SGR Lot VI) kutoka Tabora hadi Kigoma
Tabora na Kigoma
7.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha maeneo ya Hifadhi
ya Ngorongoro
Ngorongoro, Arusha
8.Uthamini wa mali za wananchi wanaozunguka Bwala la
Milala, Manispaa ya Mpanda Mkoa wa Katavi
Katavi


Na.
Mradi
Mahali
9Mradi wa ujenzi wa miundombinu ya umeme wa 220KV kutoka Geita hadi Nyakanazi KageraGeita na Kagera
10.Uthamini wa mali za wananchi ambao maeneo yao yanatwaliwa kupisha ujenzi wa miundombinu ya umeme wa 132 KV kutoka Tabora hadi KigomaTabora na Kigoma
11.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha maneo ya Hifadhi ya Taifa RuahaMbarali , Mbeya
12.Upanuzi wa Uwanja wa Ndege Musoma Mkoa wa MaraMusoma, Mara
13.Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha mradi wa ujenzi wa barabara kutoka Kahama hadi Kakola (73km)Shinyanga
14Uthamini wa mali za wananchi wanaopisha kutoka Shamba
la Serikali Utegi la ufugaji na Kilimo eneo la Rorya, Mara
Mara
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 11: Idadi ya Maeneo Yaliyotangazwa Kuendelezwa Kimji na Maeneo ya Urasimishaji Yaliyotangazwa Kuanzia Julai, 2023 hadi 15 Mei 2024
A. Maeneo Mapya Yaliyotangazwa Kuendelezwa Kimji Mwaka 2023/24
Na.
Mkoa
Na.
HalmashauriJina la Amri ya Tangazo
Namba ya Tangazo
na Tarehe
1​
Simiyu
1​
MeatuAmri Ya Kupanga Eneo La Kisesa ya Mwaka, 2023.817 of 2023 la tarehe
10/11/2023
2​
Mbeya
2​
BusokeloAmri ya Kupanga Eneo la Kikuba za Mwaka, 2024.Na. 49 la tarehe
\A26/01/2024
Amri ya Kupanga Eneo la Kifunda ya Mwaka, 2024Na. 73 la tarehe
02/02/2024
Amri ya Kupanga Eneo la Kitali ya Mwaka, 2024.Na. 74 la tarehe
02/02/2024
Amri ya Kupanga Eneo la Mbambo ya Mwaka, 2024Na. 75 la tarehe
02/02/2024
Amri ya Kupanga Eneo la Kipapa ya Mwaka 2024.Na. 78 la tarehe
02/02/2024
3​
Mbeya DCAmri ya Kupanga Eneo la Swaya ya Mwaka, 2024.Na. 50 la tarehe
26/01/2024
Amri ya Kupanga Eneo la Nsongwi za Mwaka, 2024.Na. 51 la tarehe
26/01/ 2024
Amri ya Kupanga Eneo la Ilembo ya Mwaka, 2024Na. 57 la tarehe
26/01/2024
3​
Mwanza
4​
MaguAmri ya kupanga eneo la Magu mjini ya mwaka 2023800 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Bukandwe ya mwaka 2023802 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Bujashi ya mwaka 2023803 of 2023 ya
10/11/2023


A. Maeneo Mapya Yaliyotangazwa Kuendelezwa Kimji Mwaka 2023/24
Na.Mkoa
Na.
HalmashauriJina la Amri ya Tangazo
Namba ya Tangazo
na Tarehe
Amri ya kupanga eneo la Sagani ya mwaka 2023804 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Nyigogo ya mwaka 2023808 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Ng’haya ya mwaka 2023812 of 2023 ya
10/11/2023
Amri kupanga eneo la Chabula ya mwaka 2023815 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Kisesa mwaka 2023817 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Mahaha ya mwaka 2023818 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Bujashi ya mwaka 2023822 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Kitongosima ya mwaka 2023823 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Kongolo ya mwaka 2023825 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Kabila ya mwaka 2023834 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Kahangala ya mwaka 2023835 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Nyanguge ya mwaka 2023811 of 2023 ya
10/11/2023
5​
SengeremaAmri ya kupanga eneo la Sima ya mwaka 2023806 of 2023 ya
10/11/2023


A. Maeneo Mapya Yaliyotangazwa Kuendelezwa Kimji Mwaka 2023/24
Na.
Mkoa
Na.
HalmashauriJina la Amri ya Tangazo
Namba ya Tangazo
na Tarehe
6​
MisungwiAmri ya kupanga eneo la Mwaholo ya mwaka 2023813 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Kanyelele ya mwaka 2023837 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo ia Ukiruguru ya mwaka2023805 of 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Nyang’homango ya mwaka 2023810 ya 2023 ya
10/11/2023
Amri ya kupanga eneo la Mbalika ya mwaka 2023836 of 2023 ya
10/11/2023
4​
Morogoro
7​
UlangaMavimba and Milola Planning AreaGN No. 615K ya
28/08/2023
5​
Singida
8​
ManyoniAmri ya kupanga eneo la Makutupora ya mwaka, 2023.451 of 20237/7/2023
6​
Dodoma
9​
BahiAmri ya Kupanga Eneo la Chilungulu ya Mwaka, 2023.Na. 833 la tarehe
10/11/2023
7​
Rukwa
10​
Nkasi (W)Amri ya Kupanga Eneo la Kipili ya Mwaka 2023618C of
2023,28/08/2023
11​
Sumbawanga (W)Amri ya Kupanga Eneo la Muze na Kalakala ya Mwaka 2023615X of 2023,28/08/2023
Amri ya Kupanga Eneo la Ilemba ‘A’, ‘B’ na Kaswepa28/08/2023618F of 2023,
Amri ya Kupanga Eneo la Kilyamatundu ya Mwaka 2023618I of
2025,28/08/2023
12​
Kalambo (W)Amri ya Kupanga Eneo la Msanzi ya Mwaka 2023618G of
2023,28/08/2023
Amri ya Kupanga Eneo la Mlenje ya Mwaka 2023618H of
2024,28/08/2023


B. Maeneo ya Upangaji yaliyo katika hatua za Kutangazwa
Na
MkoaNa.Halmashauri
Jinala Tangazo
1​
Lindi1Kilwa DCAmri ya kupanga eneo la Kiranjeranje ya mwaka, 2024.
2 Simiyu2Bariadi DCAmri ya Kupanga Eneo la Ibulyu ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Kasoli ya Mwaka, 2023.
Amri ya Kupanga Eneo la Masewa ya Mwaka, 2023
3BusegaAmri ya Kupanga Eneo la Lamadi ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Lukungu ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Mwabayanda ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Yitwimila A ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Yitwimila B ya Mwaka, 2023
4ItilimaAmri ya Kupanga Eneo la Budalabujiga ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Ikindilo na Ntenga ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Kinangw’eli ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Lagangabilili ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Migato na Simiyu ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Mwamigagani ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Mwaumishenu ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Nanga ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Nkoma ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Nyamalapa na Kimali ya Mwaka, 2023
5Maswa DCAmri ya Kupanga Eneo la Nguliguli ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Njiapanda ya Mwaka, 2023
6Meatu DCAmri ya Kupanga Eneo la Ipililo ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Kisesa ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Makao ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Malwilo ya Mwaka, 2023
Amri ya Kupanga Eneo la Mwaukoli ya Mwaka, 2023


C. Maeneo ya Urasimishaji Yaliyotangazwa Mwaka 2023/24
Na.Mkoa
Na.
HalmashauriJina la Amri ya Tangazo
Namba ya Tangazo
na Tarehe
1​
Mara
1​
Musoma
Manispaa
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Musoma ya Mwaka 2023.
617I of 2023 la tarehe
28/08/2023
2​
Simiyu
2​
BusegaAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kiloleli ya Mwaka 2023
615A of 2023 la
tarehe 28/08/2023
3​
ItilimaAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Nanga ya Mwaka 2023.
615B of 2023 la
tarehe 28/08/2023
4​
MaswaAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Ipilili/ (IPILILO) ya Mwaka 2023
617P of 2023 la
tarehe 28/08/2023
3​
Mbeya
5​
BusokeloAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Kandete, Kitongoji cha Kalulu ya Mwaka, 2024
Na. 69 la tarehe
02/02/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Ndembo, Kitongoji cha Itete ya Mwaka, 2024.
Na. 70 la tarehe
02/02/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo la Ikamambande, Kitongoji cha Kitungwana Butumba ya
Mwaka, 2024.
Na. 71 la tarehe 02/02/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa katika Eneo
la Mwela, Kitongoji cha Lusungo ya Mwaka, 2024
Na. 102 la tarehe
16/02/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa katika Eneo
la Kapulampunguti ya Mwaka, 2024.
Na. 103 la tarehe
16/02/2024
6​
MbaraliAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Ubaruku ya Mwaka, 2024.
Na. 66 la tarehe
02/02/ 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Mswiswi ya Mwaka, 2024.
Na. 67 la tarehe
02/02/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Mabadaga ya Mwaka, 2024.
Na. 68 la tarehe
02/02/2024
7​
Mbeya DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa katika Eneo
la Igawa ya Mwaka 2024
Na. 106 la tarehe
16/02/2024


C. Maeneo ya Urasimishaji Yaliyotangazwa Mwaka 2023/24
Na.
Mkoa
Na.
HalmashauriJina la Amri ya Tangazo
Namba ya Tangazo
na Tarehe
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Simambwe ya Mwaka, 2024
Na. 53 la tarehe
26/01/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Nsongwi Juu ya Mwaka, 2024.
Na. 54 la tarehe
26/01/ 2024
8​
Chunya DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Ifumbo ya Mwaka, 2
Na.58 la tarehe
26/01/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Bitimanyangaya ya Mwaka, 2024.
Na. 64 la tarehe
02/02/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Katika Eneo
la Chalangwa ya Mwaka, 2024.
Na.52 la tarehe
26/01/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa katika Eneo
la Sangambi ya Mwaka, 2024.
Na.104 la tarehe
16/02/2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa katika Eneo
la Ifiga ya Mwaka, 2024.
Na. 101 la tarehe
16/02/2024
4
Tabora​
9​
Tabora
Manispaa
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Mabatini ya Mwaka 2023.
617Y of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Usule ya Mwaka 2023
615C of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Mchichani ya Mwaka 2023.
615N of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kizigo ya Mwaka 2023.
615O of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Rufita ya Mwaka 2023.
615R of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Mtakuja ya Mwaka 2023.
615Y of 2023 tarehe
28/08/2023


C. Maeneo ya Urasimishaji Yaliyotangazwa Mwaka 2023/24
Na.MkoaNa.HalmashauriJina la Amri ya Tangazo
Namba ya Tangazo
na Tarehe
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Usengi ya Mwaka 2023.
615Z of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Mpepo ya Mwaka 2023.
616Z of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kijiweni ya Mwaka 2023.
617A of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kazaroho ya Mwaka 2023.
617C of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kipalapala ya Mwaka 2023.
617G of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kidatu ‘B’ ya Mwaka 2023.
617H of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kidatu ‘A’ ya Mwaka 2023.
617R of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Ikindwa ya Mwaka 2023.
617S of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Lwanzari ya Mwaka 2023.
617T of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Chang’ombe ya Mwaka 2023.
617U of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kwihala ya Mwaka 2023.
617V of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Kombamasai ya Mwaka 2023.
617W of 2023 tarehe
28/08/2023
Amri ya kupanga eneo la Mbalika ya mwaka 2023836 of 2023 ya
10/11/2023


C. Maeneo ya Urasimishaji Yaliyotangazwa Mwaka 2023/24
Na.
Mkoa
Na.
HalmashauriJina la Amri ya Tangazo
Namba ya Tangazo
na Tarehe
5​
Morogo
ro
10​
UlangaMavimba and Milola Planning AreaGN No. 615K ya
8/08/2023
6​
Rukwa​
11​
Sumbawnga
Manispaa
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyo pangwa Eneo la Izia
ya Mwaka 2023
615V of
2023,28/08/2023
12​
Nkasi (W)Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyo pangwa Eneo la Kabwe Asilia na sehemu ya Kabwe Camp na Udachi ya
Mwaka 2023
615W of 2023,28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Itete,
Mtakuja na Kamwanda ya Mwaka 2023
617D of
2023,28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Chala ‘A’, ‘B’, na ‘C’ ya mwaka 2023
617F of
2023,28/08/2023
13​
Sumbawanga
(W)
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Muze
na Kalakala
617B of
2023,28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa ya Eneo la
Ilemba ‘A’, ‘B’, na Kaswepa
618L of
2026,28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa ya Mtowisa
‘A’ na Mtowisa ‘B’
618Q of
2028,28/08/2023
14​
Kalambo (W)Amri ya Kurasimsiha makazi Yasiyopangwa Eneo la
Santamaria, Namlangwa na Matai ‘B’
618P of
2027,28/08/2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la
Mtakuja ya Mwaka 2023.
615 of 2023,
28/08/2023


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
1Dar es salaam
1​
Kinondoni MCAmri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka, 2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka, 2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka, 2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka, 2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka, 2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.
Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka, 2023
Amri ya kurasimisha makazi yasiyopangwa eneo la Viwanda Mbezi ya mwaka,
2023
2
Simiyu​
2​
ItilimaAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Budalabujiga ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ikindilo ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Inalo ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kinangw’eli ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Laini ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Lugulu ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Migato ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwamapalala ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwamigagani ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nanga ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nkoma ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nyamalapa ya Mwaka,
2023
3​
Bariadi TCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Bunamhala Chuoni ya
Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Bunamhala ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ditima ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Giriku ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Guduwi ya Mwaka, 2023


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Isanga ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kilulu ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mahaha ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mbiti ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwakibuga ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwamhuba ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ngw’angw’ali ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nyakabindi ya Mwaka,
2023
4​
Bariadi DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Byuna ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Dutwa ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Gasuma ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Gilya ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ibulyu ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Igegu na Igegu Mashariki
ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kasoli ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kilalo ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Masewa ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Matongo ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwasinasi ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwasubuya ya Mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ngulyatiya Mwaka, 2023


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.
Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nkindwabiye na Songambele ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nkololo ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nyamswa ya Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sapiwi ya Mwaka, 2023
5​
Bariadi TCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Old-Maswa ya Mwaka,
2023
3
Kigoma​
6​
Kasulu TCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Heru juu ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kabanga Mlinda na
Kiduguda ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kanazi, Ngoma, Nyangwe,
Migogwe, Nyakabondo, Luzilampene na Tabilugu ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kidyama, Nyachijima na
Nyarumanga ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mudyanda ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Muhunga, Kanyika,
Lugongo na Labilo ya mwaka, 2022
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mgandazi, Murufiti A,
Murufiti B, Murufiti Kati, Nyamigombero A, Nyamigombero B ya mwaka, 2022
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nyansha, Kilombero na
Nyantare ya mwaka, 2022
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mnanila, Nyangunge, Mnanila, Mwikungu, Nyumbingwa A, Nyumbingwa B na Tumaini ya mwaka,
2022
7​
Ujiji MCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Bushabani ya mwaka,
2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Businde ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kagera ya mwaka, 2023


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.
Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kisingirima ya mwaka, 2022
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kibirizi ya mwaka, 2022
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kitongoni ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Majengo ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwenge ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Rubuga ya mwaka, 2023
8​
Kibondi DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Malagarasi ya mwaka,
2023
9​
Kasulu DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Makere ya mwaka, 2023
4
Dodoma​
10​
Dodoma CCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nzasa ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mhanga ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Azimio ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Chamwino ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Gawaye ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Chisichili ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Hombolo makulu ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kangarima ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Msisi ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Zepisa ‘A’ ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Zepisa ‘B’ ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ipala ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Itumbi ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Iwelewele ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kawawa ya mwaka, 2024


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.MkoaNa.Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kusenha ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Makutopora ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mazengo ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mapinduzi Mbabala ya
Mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mphusu Mbabala ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwongozo Mbabala ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nguji ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mlangwa ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Muungano Chahwa ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Muungano Matumbulu ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwinyi ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwongozo - Matumbulu ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwongozo - Chahwa ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nyemihanga ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sabasaba - Mpunguzi ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sokoine - Zuzu ya mwaka,
2024


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sokoine - Ipala ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ukombozi - Ipala ya
mwaka, 2024
11​
Dodoma CCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nzasa ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mhanga ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Azimio ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Chamwino ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Gawaye ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Chisichili ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Hombolo makulu ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kangarima ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Msisi ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Zepisa ‘A’ ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Zepisa ‘B’ ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ipala ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Itumbi ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Iwelewele ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kawawa ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kusenha ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Makutopora ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mazengo ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mapinduzi Mbabala ya
Mwaka, 2023


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.
Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mphusu Mbabala ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwongozo Mbabala ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nguji ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mlangwa ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Muungano Chahwa ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Muungano Matumbulu ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwinyi ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwongozo - Matumbulu ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mwongozo - Chahwa ya
mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Nyemihanga ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sabasaba - Mpunguzi ya mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sokoine - Zuzu ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sokoine - Ipala ya mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Ukombozi - Ipala ya mwaka, 2024
5
Njombe​
12​
Njombe DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kidegembye ya Mwaka,
2024


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.
Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Matembwe ya Mwaka, 2024.
13​
MaketeAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kitulo - Mnadani ya
Mwaka, 2024.
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Lupila - Mnadani ya
Mwaka, 2024.
6​
Tabora​
14​
Urambo DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa eneo la Kariakoo ya Tabora ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa eneo la Azimio ya mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa eneo la Bombamzinga manne ya
mwaka, 2023
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa eneo la Kigamboni ya mwaka, 2023
7​
Kilimanja
ro
15​
Moshi MCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Arabika ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kalimani ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Katanini ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la KDC ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kigongoni ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kwa - Komba ya Mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Langoni ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Magereza ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Matindigani ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mjimpya ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mjimwema ya Mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Msufini ya Mwaka, 2024


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Rauya ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Relini ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sokoni njoro ya Mwaka,
2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Viwandani ya Mwaka, 2024
16​
Moshi DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Bogini ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Chekeleni ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Faru ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kameti ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Karamsingi ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kariwa ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kindi, Sambarai, Kisiwani,
Miembeni, Bomani na Mvuleni ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Koresa ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Korini Kusini ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Longuo ‘A’ ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mabogini ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mabungo ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Majengo - Kimochi ya
Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Makuyuni ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mtakuja ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Muungano, Maendeleo na
mjimpya ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mvuleni ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Njiapanda Mashariki ya
Mwaka, 2024


D. Maeneo ya Urasimishaji yaliyo hatua za Kutangazwa
Na.
Mkoa
Na.
Halmashauri
Jinala Tangazo
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Oria ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sango ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Shabaha ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Uchira ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Uparo ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Yamumakaa ya Mwaka, 2024
17​
Hai DCAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Bomang’ombe ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kimashuku ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Mungushi ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Rundugaiya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kwa Sadala ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Sanya - Station ya Mwaka, 2024
Amri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Shirinjoro ya Mwaka, 2024
8
Tabora​
18​
Tabora ManispaaAmri ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo la Kariakoo Ya Mwaka 2024
Amri Ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo La Azimio - Isevya, 2024
Amri Ya Kurasimisha Makazi Yasiyopangwa Eneo La Bombamzinga Ya Mwaka 2024
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 12: Vipande vya Ardhi Vilivyorasimishwa Kimkoa kuanzia Julai, 2023 Hadi 15 Mei 2024


Na.

Mkoa
Idadi ya Mchoro ya Urasimishaji Makazi
Idadi ya Viwanja vya Urasimishaji
Viliyoidhinishwa
1​
Arusha
26​
4,519​
2​
Dar es Salaam
104​
65,570​
3​
Dodoma
118​
39,161​
4​
Geita
39​
16,404​
5​
Iringa
17​
2,497​
6​
Kagera
3​
1,165​
7​
Katavi
15​
3,491​
8​
Kigoma
18​
9,746​
9​
Kilimanjaro
25​
11,840​
10​
Lindi
4​
1,896​
11​
Manyara
3​
1,352​
12​
Mara
12​
3,630​
13​
Mbeya
17​
3,854​
14​
Morogoro
8​
1,816​
15​
Mtwara
2​
1,164​
16​
Mwanza
25​
7,823​
17​
Njombe
16​
6,079​
18​
Pwani
30​
38,245​
19​
Rukwa
7​
981​
20​
Ruvuma
2​
939​
21​
Shinyanga
8​
5,157​
22​
Simiyu
8​
3,461​
23​
Singida
2​
1,835​
24​
Songwe
7​
1,421​
25​
Tabora
13​
3,378​
Jumla
529
237,424
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 13: Viwanja na Mashamba Vilivyoidhinishwa
Kimkoa kuanzia Julai, 2023 hadi 15 Mei 2024

NaMkoaHalmashauriIdadi ya
Viwanja
Idadi ya
Mashamba



1​



Dodoma
Dodoma Jiji
24424​
135​
Chamwino
1049​
52​
Mpwapwa
56​
0​
Kondoa Mji
32​
0​
Kondoa Dc
0​
0​
Bahi
39​
2​
Chemba
2743​
0​
Kongwa
2418​
0​
Jumla
30761
189



2​



Kigoma
Kigoma Ujiji
2,103​
3​
Kigoma
1,003​
7​
Kasulu
4​
4​
Kasulu Mji
4,287​
1​
Kibondo
1,413​
0​
Kakonko
7​
0​
Buhigwe
18​
11​
Uvinza
1,542​
79​
Jumla
10,377
105



3​



Mbeya
Mbeya Jiji
3,484​
0​
Chunya
155​
0​
Mbalali
395​
54​
Busokelo
5​
2​
Mbeya
269​
0​
Rungwe
71​
3​
Kyela
3,946​
0​
Jumla
8,325
59


4​


Songwe
Mbozi
1,005​
4​
Tunduma Tc
2,512​
6​
Ileje
7​
1​
Momba
26​
0​
Songwe
440​
16​
Jumla
3,990
27


5​


Iringa
Iringa Mc
1,362​
0​
Mafinga Tc
1,404​
0​
Iringa
619​
4​
Kilolo
359​
6​
Mufindi
603​
0​
Jumla
4,347
10

6​

Njombe
Njombe Tc
2,489​
0​
Njombe
807​
0​
Makambako Tc
1,008​
0​
Wanging'ombe
453​
0​

NaMkoaHalmashauriIdadi ya
Viwanja
Idadi ya
Mashamba
Ludewa
5,411​
0​
Makete
354​
7​
Jumla
10,522
7


7​


Katavi
Mpanda Mc
3,925​
0​
Tanganyika
98​
103​
Nsimbo
392​
0​
Mlele
163​
0​
Mpimbwe
102​
0​
Jumla
4,680
103



8​



Lindi
Lindi Mc
4,572​
0​
Mtama
441​
0​
Liwale
505​
0​
Kilwa
615​
0​
Nachingwea
1,476​
6​
Ruangwa
30​
0​
Jumla
7,639
6



9​



Arusha
Arusha Jiji
1,375​
0​
Longido
67​
0​
Arusha
1,098​
18​
Meru
889​
3​
Karatu
260​
1​
Monduli
244​
3​
Ngorongoro
170​
0​
Jumla
4,103
25




10




Mara
Musoma Mc
1,737​
0​
Musoma
12​
0​
Tarime Tc
2,312​
0​
Butiama
2,051​
3​
Rorya
4,364​
0​
Bunda Tc
695​
0​
Bunda
53​
0​
Serengeti
0​
0​
Tarime
12​
0​
Jumla
11,236
3


11


Dsm
Ilala
2,251​
0​
Kigamboni
5,884​
0​
Kinondoni
1,934​
0​
Temeke
1,664​
0​
Ubungo
5,007​
0​
Jumla
16,740
0


12


Geita
Geita Mji
2,764​
0​
Geita
121​
0​
Chato
3,704​
0​
Bukombe
140​
0​
Mbogwe
873​
0​

NaMkoaHalmashauriIdadi ya
Viwanja
Idadi ya
Mashamba
Nyang'hwale
2​
Jumla
7,604
0



13



Simiyu
Bariadi Tc
3,797​
0​
Bariadi Tc
4,750​
0​
Busega
306​
0​
Itilima
16​
0​
Meatu
78​
0​
Maswa
0​
Jumla
8,947
0



14



Mwanza
Nyamagana
4,440​
0​
Ilemela
1,648​
0​
Misungwi
2,716​
0​
Magu
1,375​
0​
Kwimba
109​
0​
Sengerema
83​
0​
Ukerewe
417​
3​
Buchosa
52​
0​
Jumla
10,840
3


15


Rukwa
Sumbawanga
Mc

978​

0​
Sumbawanga
1,077​
3​
Kalambo
268​
0​
Nkasi
4​
3​
Jumla
2,327
6




16




Mtwara
Mtwara Mc
1,408​
0​
Mtwara
823​
2​
Nanyamba
9​
0​
Tandahimba
0​
0​
Newala Tc
0​
0​
Newala
0​
0​
Masasi Tc
18​
0​
Masasi
7​
0​
Nanyumbu
18​
0​
Jumla
2,283
2



17



Ruvuma
Songea Mc
2,724​
0​
Nyasa
277​
0​
Mbinga
335​
0​
Mbinga Tc
1,671​
7​
Songea
122​
1​
Madaba
607​
3​
Namtumbo
256​
0​
Tunduru
247​
4​
Jumla
6,239
15
18ManyaraBabati Tc
15​
0​
Babati
2,627​
0​

NaMkoaHalmashauriIdadi ya
Viwanja
Idadi ya
Mashamba
Hanang'
1,013​
0​
Kiteto
1​
5​
Mbulu
43​
0​
Mbulu Tc
729​
0​
Simanjiro
5​
43​
Jumla
4,433
48



19



Singida
Singida Tc
7,547​
0​
Singida
10​
17​
Ikungi
538​
3​
Manyoni
1,345​
18​
Itigi
412​
0​
Iramba
1,474​
6​
Mkalama
2​
13​
Jumla
11,328
57



20



Tabora
Tabora Mc
546​
0​
Nzega Tc
17​
0​
Nzega
40​
0​
Uyui
2​
0​
Urambo
62​
0​
Kaliua
622​
0​
Sikonge
113​
0​
Igunga
1,523​
0​
Jumla
2,925
0




21




Morogoro
Morogoro Mc
16,353​
0​
Morogoro
2,307​
8​
Ifakara Tc
1,432​
0​
Kilosa
81​
40​
Mvomero
1,271​
102​
Gairo
35​
0​
Ulanga
7​
0​
Malinyi
0​
0​
Mlimba
2​
0​
Jumla
21,488
150



22



Kagera
Karagwe
89​
4​
Misenyi
141​
6​
Kyerwa
102​
1​
Muleba
23​
3​
Ngara
63​
0​
Bukoba
567​
11​
Bukoba Mc
171​
0​
Biharamlo
47​
0​
Jumla
1,203
25

23
Shinyan gaShinyanga Mc
3,112​
0​
Kahama Mc
1,324​
0​
Shinyanga
24​
1​

NaMkoaHalmashauriIdadi ya ViwanjaIdadi ya Mashamba
Msalala
365​
0​
Kishapu
399​
0​
Ushetu
1,215​
0​
Jumla
6,439
1



24



Kilimanj aro
Moshi Mc
303​
0​
Moshi
753​
2​
Siha
18​
2​
Hai
1,608​
4​
Rombo
1,068​
6​
Same
18​
1​
Mwanga
0​
0​
Jumla
3,768
15




25




Pwani
Bagamoyo
6,416​
0​
Chalinze
5,282​
29​
Kibaha Tc
3,137​
0​
Kibaha
2,222​
0​
Kibiti
34​
0​
Kisarawe
616​
33​
Mkuranga
2,121​
2​
Rufiji
30​
2​
Mafia
72​
0​
Jumla
19,930
66





26





TANGA
Tanga Cc
2,030​
0​
Korogwe Tc
831​
0​
Korogwe
29​
8​
Handeni Tc
456​
3,893​
Handeni
1,965​
0​
Muheza
23​
0​
Lushoto
17​
0​
Bumbuli
11​
0​
Pangani
310​
0​
Mkinga
21​
0​
Kilindi
1,274​
1,784​
Jumla
6,967
5,685
Jumla Kuu249,340
7,559
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 14: Idadi ya Vijiji Vilivyohakikiwa na Kupimwa
Kimkoa Kuanzia Julai, 2023 hadi 15 Mei 2024

Na.Mkoa
Idadi ya Vijiji Vilivyohakikiwa
Mipaka
Idadi ya Vijiji Vipya
Vilivyopimwa
Jumla ya Vijiji Vilivyohakikiwa
na Kupimwa
1Dodoma
13​
5​
18​
2Kigoma
8​
4​
12​
3Mbeya
11​
5​
16​
4Songwe
14​
7​
21​
5Iringa
14​
7​
21​
6Njombe
38​
1​
39​
7Katavi
18​
8​
26​
8Lindi
26​
21​
47​
9Arusha
0​
0​
0​
10Mara
57​
10​
67​
11Dsm
0​
0​
0​
12Geita
0​
0​
0​
13Simiyu
34​
23​
57​
14Mwanza
24​
6​
30​
15Rukwa
24​
51​
75​
16Mtwara
0​
0​
0​
17Ruvuma
31​
14​
45​

Na.Mkoa
Idadi ya Vijiji Vilivyohakikiwa Mipaka
Idadi ya Vijiji Vipya Vilivyopimwa
Jumla ya Vijiji Vilivyohakikiwa na Kupimwa
18Manyara
0​
0​
0​
19Singida066
20Tabora4876124
21Morogoro516
22Kagera32032
23Shinyang a9716
24Kilimanja ro000
25Pwani000
26Tanga691584
Jumla475267742
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 15: Hali ya Urejeshaji wa Fedha Zilizokopeshwa Kwa Halmashauri Kwa Ajili ya Utekelezaji wa Miradi ya Kupanga, Kupima na Kumilikisha Ardhi (KKK) kuanzia Mwaka 2021/22 hadi 15 Mei 2024
(i) Halmashauri zilizokamilisha Marejesho kwa 100%
Na.
HalmashauriMkopoMarejesho
1​
Moshi DC
233,200,000​
233,200,000​
2​
Mwanza Jiji
800,000,000​
800,000,000​
3​
Meru DC
1,650,000,000​
1,650,000,000​
4​
Morogoro
Manispaa
1,000,000,000​
1,000,000,000​
5​
Ifakara Mji
200,000,000​
200,000,000​
6​
Geita DC
600,000,000​
600,000,000​
7​
Bariadi TC
79,750,000​
79,750,000​
8​
Mbozi DC
495,000,000​
495,000,000​
9​
Ilemela
Manispaa
3,589,774,000​
3,589,774,000​
10​
Tunduma
TC
543,000,000​
543,000,000​
11​
Songwe DC
450,000,000​
450,000,000​
12​
Kaliua DC
100,000,000​
100,000,000​

13​
Ofisi ya
Ardhi Mkoa wa Iringa

450,000,000​

581,318,714​
14​
Kigamboni
Manispaa
1,500,000,000​
1,500,000,000​
JUMLA
11,690,724,000
11,822,042,714

(ii) Halmashauri zilizorejesha sehemu ya fedha

Na

Halmashau ri

Mkopo

Fedha zilizorejeshwa
Kiasi ambacho hakijarejeshw
a

Asilimi a
1​
Rhombo DC
1,060,000,000​
838,000,000​
240,000,000​
79​
2​
Kibaha TC
1,588,000,000​
1,218,156,528​
369,843,472​
77​
3​
Kilosa DC
200,000,000​
150,000,000​
50,000,000​
75​
4​
Mbeya Jiji
2,000,000,000​
1,500,000,000​
500,000,000​
75​
5​
Bunda TC
493,989,000​
370,410,330​
123,989,000​
75​
6​
Njombe TC
700,000,000​
507,000,000​
193,000,000​
72​
7​
Mbeya DC
584,000,000​
400,000,000​
184,000,000​
68​
8​
Makambak o TC
683,300,000​
410,000,000​
273,300,000​
60​
9​
Musoma Manispaa
250,000,000​
120,000,000​
120,000,000​
48​
10​
Meatu DC
93,500,000​
45,000,000​
48,500,000​
48​
11​
Mtwara Manispaa
1,679,450,000​
800,000,000​
879,450,000​
48​
12​
Sumbawan
ga DC
47,630,000​
20,000,000​
27,630,000​
47​
13​
Tabora Manispaa
885,000,000​
360,726,252​
524,273,748​
41​
14​
Tarime TC
560,000,000​
216,355,000​
343,645,000​
39​
15​
Mbulu DC
162,500,000​
60,000,000​
152,500,000​
37​
16​
Ushetu DC
259,850,000​
87,892,300​
172,157,700​
34​
17​
Butiama DC
297,000,000​
105,245,500​
191,754,500​
35​
18​
Morogoro
DC
865,210,000​
310,000,000​
555,210,000​
32​
19​
Babati TC
250,000,000​
80,117,091​
169,882,909​
32​
20​
Chalinze DC
2,500,000,000​
800,000,000​
1,700,000,000​
32​
21​
Tanga Jiji
400,000,000​
107,306,000​
292,694,000​
27​
22​
Dodoma Jiji
3,000,000,000​
810,062,115​
2,189,937,885​
27​
23​
Uyui DC
100,000,000​
27,205,000​
72,795,000​
27​
24​
Babati DC
125,000,000​
32,000,000​
93,000,000​
26​
25​
Mbinga TC
330,000,000​
77,106,758​
252,893,242​
23​
26​
Ileje DC
432,319,000​
100,000,000​
332,319,000​
23​
27​
Ludewa DC
405,000,000​
89,000,000​
316,000,000​
22​

(ii) Halmashauri zilizorejesha sehemu ya fedha

Na

Halmashau ri

Mkopo

Fedha zilizorejeshwa
Kiasi ambacho hakijarejeshw
a

Asilimi a
28​
Buchosa DC
327,000,000​
52,000,000​
275,000,000​
16​
29​
Maswa DC
850,000,000​
140,000,000​
710,000,000​
16​
30​
Rorya DC1,000,000,000
150,000,000​
850,000,000​
15​
31​
Kishapu DC
882,000,000​
124,080,955.5
0​
757,919,045​
14​
32​
Msalala DC1,609,500,000
202,171,000​
1,407,329,000​
13​
33​
Ikungi DC
598,226,000​
71,000,000​
527,226,000​
12​
34​
Lushoto DC
208,000,000​
22,360,596​
185,639,404​
11​
35​
Chamwino DC
300,000,000​
30,000,000​
270,000,000​
10​
36​
Hanang’ DC
187,500,000​
14,120,000​
173,380,000​
8​
37​
Manyoni DC1,520,770,000
100,000,000​
1,420,000,000​
7​
38​
Mbulu TC
455,000,000​
30,000,000​
425,000,000​
7​
39​
Korogwe TC
80,000,000​
5,075,000​
74,925,000​
6​
40​
Shinyanga DC
900,000,000​
49,647,482​
850,352,518​
6​
41​
Korogwe DC
240,000,000​
12,880,000​
227,120,000​
5​
42​
Lindi Manispaa1,600,000,000
8,730,000​
1,591,270,000​
1​
JUMLA
30,709,744,0
00
10,653,647,9
08
20,113,936,4
23
(iii) Halmashauri ambazo hazijarejesha fedha
NaHalmashauriMkopoFedha zilizorejeshwaKiasi ambacho hakijarejeshwa
Asilimia
1​
Musoma DC
200,000,000​
0​
200,000,000​
0​
2​
Shinyanga Manispaa1,055,000,000
0​
1,055,000,000​
0​
JUML
A
1,255,000,000
0
1,255,000,000
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 16: Idadi ya Vijiji Vilivyoandaliwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi, Vilivyopimwa Mipaka, Vilivyoandaliwa Vyeti vya Ardhi Katika Wilaya 21 Zinazotekeleza Mradi wa Uboreshaji wa Usalama wa Milki za Ardhi (LTIP) Kwa Kipindi cha Julai 2023 hadi 15 Mei 2024.
Na.
Halmashaur iMipaka ya Vijiji
Vyeti vya Ardhi ya
Kijiji
Mipango ya Matumizi ya Ardhi ya Vijiji
1​
Chamwino
8​
9​
64
2​
Chunya
3​
4​
21
3​
Handeni
7​
7​
35
4​
Kaliua
38​
38​
53
5​
Kilindi
29​
25​
35
6​
Kilwa
18​
25​
48
7​
Ludewa
0​
0​
31
8​
Makete
5​
7​
19
9​
Maswa
41​
41​
62
10​
Mbinga
33​
33​
64
11​
Mkinga
24​
0​
41
12​
Mufindi
11​
0​
45
13​
Mvomero
16​
14​
48
14​
Ngara
22​
22​
38
15​
Nkasi
32​
11​
50
16​
Rorya
12​
0​
45
17​
Ruangwa
26​
16​
30
18​
Songwe
28​
15​
38
19​
Tanganyika
17​
17​
10
20​
Uyui
37​
36​
56
21​
Iramba
0​
0​
10
Jumla
407
320
843
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jewali Na. 17: Ukarabati wa Majengo na Nyumba za Shirika la Nyumba la Taifa Kimkoa
Na.
Mikoa
Idadi ya Majengo ya kukarabatiIdadi Majengo Yaliyokamilika Kukarabatiwa
Idadi ya Sehemu (Nyumba) za kupangisha zilizokamika
kukarabatiwa
Majengo yanayoendelea kukarabatiwa
Idadi ya Sehemu (Nyumba) za kupangisha zinazoendelea
kukarabatiwa
1​
Upanga
24​
21​
304​
3​
28​
2​
DSM Metropolitan
15​
9​
84​
6​
56​
3​
Iringa
9​
9​
166​
3​
0​
4​
Katavi
1​
1​
10​
0​
0​
5​
Singida
3​
3​
28​
0​
0​
6​
Temeke
3​
2​
18​
1​
10​
7​
Kilimanjaro
15​
5​
183​
10​
26​
8​
Nbeya
6​
6​
137​
0​
0​
9​
Dodoma
2​
2​
46​
0​
0​
10​
Ruvuma
1​
1​
4​
0​
0​
11​
Mwanza
15​
15​
193​
0​
0​
12​
Morogoro
2​
2​
46​
0​
0​
13​
Arusha
30​
10​
220​
20​
82​
14​
Kinondoni
3​
3​
55​
0​
0​
15​
Ilala
31​
24​
507​
10​
63​
16​
Tabora
5​
4​
91​
1​
10​
17​
Lindi
13​
4​
38​
9​
83​
18​
Kagera
14​
14​
225​
0​
0​
19​
Tanga
20​
17​
357​
7​
27​
20​
Mtwara
13​
6​
55​
13​
66​
21​
Shinyanga
5​
5​
115​
0​
0​
22​
Mara
10​
10​
94​
0​
0​
23​
Kigoma
8​
8​
135​
0​
0​
Jumla
248
181
3111
83
451
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 18: Idadi ya Vijiji Vilivyoandaliwa Mipango ya Matumizi ya Ardhi kwa Kipindi cha Julai, 2023 hadi 15 Mei 2024
NaMkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
1MaraTarimeKitenga, Kwisarara, Turugeti
3​
NLUPC & H/W
TARIME/MAKENA​
ButiamaRyamagubo, Songora, Nyarukoru,
24​
NLUPC & ZORED​
Nyanza, Nyabikwabi, Nyamikoma,
Tonyo, Bisumwa, Busegwe,
Kyamajoje, Nyakiswa, Bumangi,
Kizaru, Bisarye, Nyasirori, Kwigutu,
Mwibagi, Kwisaro, Ryamisanga,
Kitasakwa, Buswahili, Kongoto,
Kamgendi, Kirumi.
MusomaKigera, Kwikuba, Maneke,
24​
NLUPC & ZORED​
Mmahare, Kasoma, Chumwi,
Mabuimerafuru, Lyasembe,
Buanga, Rusoli, Kwikerege,
Butata, Bwasi, Kome, Bugunda,
Bujaga, Bugwema, Musanja,
Kaburabura, Masinono,
Makojo, Makojo, Chitale,
Chimati, Busungu.
RoryaIkoma, Kogaja, Panyakoo,
Ng’ope, Ochuna, Nyamasanda,
20​
NLUPC​


NaMkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
Nyamusi, Roche, Chereche,
Tatwe, Burere, Irienyi, Oliyo,
Kwibuse, Kuruya, Nyambiwe,
Kirogo, Rabuor, Makongro,
Radienya.
BundaBukama, Kiloreri, Kambubu,
16​
NLUPC​
Sikilo, Mugara, Mwiruruma,
Isanju, Nyarugoma,
Mumagunga, Namhura,
Chingulubila, Kasahunga,
Nakatuba, Karukekere,
Namalebe, Neruma
2ShinyangaShinyangaWelezo, Nsalala, Nshishundo,
Mwamkanga,
4​
NLUPC & ZORED​
Amani, Mwiseme, Sayu, Nzoza,
12​
NLUPC​
Mwakatola, Mwaduntu,
Shilabela, Mwamadilanha,
Bulambila, Ng’hama,
Mwang’osha, Kituli, Mwamalogo,
Mwaluka
UshetuNsunga, Mliza, Nhimbo,
20​
NLUPC​
Ngokolo, Mhulidede, Mhuge,
Kabanga, Bulima, Itumbo,


NaMkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
Itumbili, Iwilo, Igalula, Chibiso,
Nshimba, Kigwa, Mbuta, Sofi, Igunda, Bunasani, Ilemve
3SingidaSingidaMvae, Kinyeto, Mgori, Munkhola, Sughana, Unyampanda, Mughunga, Lamba, Ghata, Mughamo, Mpipiti, Ughandi A, Ughandi B, Mwarufyu, Mjughuda, Msimihi, Mwachambia, Merya, Ikhanoda,
Msange.
20​
NLUPC​
4KigomaKigoma VijijiniMkwanga, Nyamhoza,
Nyabigufa
3​
NLUPC & JGI​
KibondoBusuzu, Kisongwe
2​
NLUPC​
5KageraKyerwaMurongo
1​
NLUPC, H/W KYERWA & KIKAGATI- POWER
Co LTD​
6MorogoroMorogoroKichangani, Gomero,
Nyarutanga, Mnganzi, Magogoni, Kongwa.
6​
NLUPC, FZS & TANAPA​
UlangaChilongola, Euga, Gombe,
Nkongo, Mzelezi
5​
NLUPC, FZS & TANAPA​


NaMkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
7LindiLiwaleNdunyungu, Mitawa,
Ngorongopa, Mpengere, Lubaba, Nambinda
6​
NLUPC, FZS & TANAPA​
RuangwaChiundu, Namkatila,
Nandandala, Namkonjela, Mkaranga, Nandanda, Mbecha, Chilangalile, Likwachu,
Nambiranje, Nanjaru,
Chikwale, Chikoko, Mibure, Nanganga, Litama.
16​
NLUPC​
8RuvumaTunduruNgapa, Mnazimmoja, Chawisi, Muhuwesi, Jaribuni, Ligunga,
Liwangula, Matemanga,
8​
NLUPC, FZS & TANAPA​
Chingulungulu, Msagula, Majimaji, Chalinze, Magomeni, Namiungo, Mnenje, Nammanga, Mchengamoto, Mkowela, Tanga, Namatanda, Tinginya, Imani, Pachanne, Misufini, Kazamoyo,
Nangolombe, Mitwana,
Mnazimmoja, Twendembele, Amani
20​
NLUPC​


NaMkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
9PwaniKisaraweKihare, Koresa, Kwala,
Mafumbi, Cholesamvula
5​
NLUPC, FZS & TANAPA​
10NjombeMaketeUkange, Mbalatse, Ukwama,
Ihanga
4​
NLUPC​
Kijyombo, Igumbilo, Malanduku, Lupila, Ilungu, Lupombwe, Ipepo, Udilu, Masisiwe, Maliwa Ikete,
Ilevelo, Ihela, Usagatikwa, Utweve, Igolwa
16​
NLUPC & ZORED​
Wanging’ombeMapogoro
1​
NLUPC & VPO​
LudewaLihagule, Kingole, Liughai, Kimelembe, Nkomang’ombe, Ilela, Ngelenge, Mbongo, Luana, Mbwila, Mholo, Mfalasi, Kiyombo, Mkiu, Lupande,
Lupanga.
16​
NLUPC​
11TangaKilindiSaunyi
1​
NLUPC​
12TaboraIgungaMbutu, Ganyawa, Ibutamisuzi, Kidalu, Jogohya, Kining’inila, Hindishi, Mwanyagula, Iyogelo, Mwamashimba, Chagana, Mtungulu, Igoweko, Mwina,
Buhekela, Mwamashinga,
20​
NLUPC​


Na
MkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
Mwamala, Ntobo, Imalilo,
Matinje.
13​
DodomaKondoaKalamba Juu, Kalamba chini
2​
NLUPC​
14​
MbeyaRungweSuma, Nditi
2​
NLUPC​
15MwanzaMaguLubugu, Bubinza, Kisamba, Misungwi, Sayaka, Kitongo, Kayenze B, Chandulu, Bugatu, Salama, Kisesa B, Mwamanga,
Mwabulenga, Ng’washepi, Nhobola, Igombe, Langi, Itandula,
18​
NLUPC​
BuchosaMgogo, Isenyi, Luhiza, Chanika, Bugoro, Nyachitale, Kabanga, Nyakasasa, Nyamisiwi, Buhama, Nyamkolechilwa, Nyakabanga, Nyagalamila, Igwanzozu,
Mwamanyili, Lumeya, Bilulumo, Kisisa, Humulumo, Kasela, Lusolelo, Kamisa, Isegeng’he, Luharanyonga
24​
NLUPC​
16​
RukwaSumbawangaIlembo, Kilembo, Lusaka, Mulombo, Kapewa, Kaoze,
Msanda Muungano A, Liwelyamvula, Mshani, Msanda
12​
NLUPC​


NaMkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
Muungano B, Lyanza, Nankanga C.
Kazi, Itela, Mkunda, Katonto
4​
NLUPC & ZORED​
Nankanga, Kapenta, Nsanga, Mkusi
4​
NLUPC & VPO​
JUMLA
339
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 19: Idadi ya migogoro ya Ardhi ya vijiji iliyotatuliwa na Tume Katika Halmashauri za wilaya 20 kwa Kipindi cha Julai, 2023 hadi 15 Mei 2024

Na
MkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
1MaraTarimeKitenga, Turugeti, Gamasala, Keisangula, Tagare, Kimusu, Mtagacha, Muriba, Nyantira,
Nyakalima, Komarera, Nyansicha
12​
NLUPC​
ButiamaSongora, Nyarukoru, Nyanza, Nyamikoma, Tonyo, Bisumwa,
Busegwe, Kyamajoje, Nyakiswa, Kitasakwa, Kirumi, Kigori, Nyakanga.
13​
NLUPC​
MusomaKigera, Mmahare, Kasoma, Chumwi,
Butata, Bujaga, Musanja, Kaburabura.
8​
NLUPC​
RoryaChereche, Burere, Oliyo, Kwibuse,
Nyambiwe, Kirogo, Rabuor, Radienya, Malasibora.
9​
NLUPC​
BundaBukama, Chingulubila.
2​
NLUPC​
2ShinyangaShinyangaMwiseme, Mwakatola, Shilabela, Mwamadilanha, Bulambila, Ng’hama,
Mwang’osha, Mwamalogo, Mwaluka.
9​
NLUPC​
UshetuMliza, Ngokolo, Mhulidede, Kabanga,
Igunda.
5​
NLUPC​
3​
SingidaSingidaMvae, Sughana, Unyampanda, Lamba,
Ghata, Mughamo, Mwarufyu,
12​
NLUPC​


Na
MkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
Mwachambia, Msikii, Mwighanji,
Munkola, Mugunga
4​
KigomaKigomaNyamhoza, Nyabigufa
2​
NLUPC & JGI​
5​
MorogoroMorogoroKichangani, Gomero, Kongwa, Kisaki
Kituoni, Tulo
5​
NLUPC
6LindiLiwaleMitawa, Ngorongopa, Mpengere,
Lubaba
4​
NLUPC
RuangwaChiundu, Mbecha, Nanjaru, Chikwale,
Mchenga, Mihewe.
6​
NLUPC
7​
RuvumaTunduruNgapa, Mnazimmoja, Chawisi, Muhuwesi, Jaribuni, Ligunga, Liwangula, Matemanga, Chingulungulu, Msagula, Majimaji, Chalinze, Magomeni, Namiungo, Mnenje, Nammanga, Mchengamoto, Mkowela, Tanga, Namatanda, Tinginya, Imani, Pachanne, Misufini, Kazamoyo, Nangolombe, Mitwana, Mnazimmoja, Twendembele, Mtangashari, Sautimoja,
Amani
32​
NLUPC
8​
NjombeMaketeUkange, Mbalatse, Ukwama, Ihanga,
Kijyombo, Igumbilo, Malanduku, Lupila, Ilungu, Lupombwe, Ipepo,
24​
NLUPC


Na
MkoaH/Wilaya
Kijiji
Idadi
Mwezeshaji
Udilu, Masisiwe, Maliwa Ikete, Ilevelo, Ihela, Usagatikwa, Utweve, Igolwa, Makangalawe, Ilindiwe, Mago, Ikonda
LudewaKiyombo, Lupanga, Mkiu, Utilili
4​
NLUPC​
9​
TaboraIgungaMbutu, Ganyawa, Mwamashimba, Mwina, Buhekela, Mwamala, Ntobo, Imalilo, Matinje, Mwanyalali10
NLUPC​
13MwanzaMaguLubugu, Bubinza, Kisamba, Misungwi,
Sayaka, Kitongo, Bugatu, Salama, Mwamanga, Mwabulenga, Inonelo
11
NLUPC​
BuchosaMgogo, Luhiza, Chanika, Bugoro, Kabanga, Nyakasasa, Nyamisiwi, Nyakabanga, Mwamanyili, Kisisa, Humulumo, Lusolelo, Luharanyonga13
NLUPC​
14​
RukwaSumbawangaMsanda Muungano A, Liwelyamvula, Msanda Muungano B, Lyanza, Nankanga C, Nankanga, Kapenta, Nsanga, Mkusi, Ngomeni.10
NLUPC​
15​
KataviMpimbweNtibili, Igalukilo, Ikulwe
3​
NLUPC​
Jumla194
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024

Jedwali Na. 20: Idadi Halisi ya Mahitaji ya Watumishi na Upungufu wa Watumishi hadi kufikia 15 Mei 2024
Na.
Idara
Mahitaji
Watumishi Waliopo
Upungufu wa Watumishi
Watumishi Waliopo Makao
Makuu
Watumishi Waliopo Ofisi za Ardhi Mkoa
na Halmashauri

1​
Utawala na Rasilimaliwatu
336​

241​

95​

107​

134​

2​
Uhasibu na
Fedha

81​

34​

47​

21​

13​

3​
Sera na
Mipango

29​

15​

14​

15​

0​

4​
Ukaguzi wa
Ndani

19​

6​

13​

6​

0​
5​
TEHAMA
47​
21​
26​
10​
11​

6​
Menejimenti ya Ardhi na
Maendeleo

952​

686​

266​

20​

666​

7​
Upimaji na
Ramani

1,117​

612​

505​

33​

579​

8​
Maendeleo ya
Makazi

1,117​

329​

788​

30​

299​

9​
Mabaraza ya
Ardhi na

817​

170​

647​

9​

161​


Na.
Idara
Mahitaji
Watumishi Waliopo
Upungufu wa Watumishi
Watumishi Waliopo Makao Makuu
Watumishi Waliopo Ofisi za Ardhi Mkoa na Halmashauri
Nyumba ya Wilaya
10​
Uthamini
343​
214​
129​
12​
202​
11​
Usajili wa Hati
101​
35​
66​
4​
31​

12​
Ununuzi na Ugavi
20​

17​

3​

13​

4​

13​
Huduma za Kisheria
19​

6​

13​

6​

0​

14​
Kitengo cha Milki
20​

4​

16​

2​

2​

15​
Mawasiliano Serikalini
10​

5​

5​

5​

0​
JUMLA
5028
2395
2633
293
2102
Chanzo: Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, 2024


67












156



157
 

Attachments

  • 24_05_2024%20Hotuba%20ya%20Bajeti%20ya%20Wizara%20ya%20Ardhi%20.pdf
    3 MB · Views: 2
Back
Top Bottom