Pillow talk

Pillow talk

1475261908963.jpg
guess who? Mlale salama jiandaeni kwa pillow talk
 
Naona kuna umuhimu mkubwa wa kutoa darasa kwa wadogo zetu hapa jamvini wa kike na wa kiume kwa pamoja, kwamba nini dhima ya ndoa! Nini maana ya mapenzi, privacy tuo na mipaka
Nini maana ya kuwa mwili mmoja! Nini maana ya bedroom kuitwa sehemu ya faragha, kwamba kwa jinsi unavyojisitiri na nguo hata bedroom yako iwe na limitations ya watu wanaoingia humo
Kuna mengi Tunahitaji kuyaongea kwa uwazi lakini kwa hekima na busara na heshima

mshana jr;
Jukwaa hilo ni muhimu sana hapa ila ukilianza tu ghafla wataingia viruka njia wenye kujifanya ati wamefanya utafiti kwa ku google. Ilim ya kweli ni ile uipatayo kwa mtendaji.
Leo, binti/kijana anaolewa hajui kwa nini anaifunga ndoa yake hiyo. Mwingine anadhani kwa kuwa kaoa kazi ni kumzalisha tu ka panya. Mama wakwe wengine hata hawajui kuwa mwanaye kaoa hivyo hana nafasi naye tena. Mawifi wanadhani yule ni kaka yao bado. Hii dunia ya leo ni ya hatari balaa,
 
Mkuu;
Pillow talk haitakufa ila itapungua na tatizo ni kuwa mapenzi ya kweli ni nadra saana sku hizi. Zama zile, hata ka mume ni mpiga tungi, alikuwa akiingia ndani, mamaa anampokea, anamvutia chumbani, anamvua zote halafu anamlaza kitandani. Saa nyingine zinapanda na anachafua chumba, mamaa anafuta usiku ule ule. Jamaa akiamka asubuhi mamaa kakaa kimya kama vile hakuna baya lilitokea. Jamaa anaona aibuuu na hakika akirudia sio mbaya kama hiyo. Kidogo kdogo anajirudi.
Mama wa leo, utaamka na kupiga deki weye mwenyewe na mitusi mikuubwa juu. Hiyo pillow talk itokee wapi?? Ulio waonesha hapo wamevumiliana. Mapenzi kuvumiliana ndo dawa.
Huhitaji viagra, unahitaji Pillow talk. Kitu inasimama ka mlingoti wa bendera
Hivi vitu vingine jamani muwe mnawapunguzia kero wake zenu. Badala ya kuwaza mkeo atakufanyia nini, jiulize wewe utamfanyia nini yeye kwanza. Hivi utoke huko kwenye mipombe yako, umkiss mwenzio na liharufu hilo? Kapige mswaki kwanza, tafuna na big g. Afu baba jitu zima kwa nini usinywe responsibly? Unywe hadi ujitapikie afu umshikishe mkeo matapishi yako as if unaumwa bana. Kabla hujawish mkeo akuvumilie, em wish kumpunguzia kero mkeo ili asikuvumilie sana. Mnanichosha mie khaaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom