Wakuu hii picha inasambazwa kwa kasi sana mtandaoni leo inasemekana kuwa Padre Kitima na John Heche walikutana na kufanya mazungumzo Januari 06, 2025. Je, ni kweli?
i
- Tunachokijua
- Kumekuwapo na picha inayosambazwa mtandaoni ikiambatana na taarifa inayoeleza kuwa January 6, 2026 padre Charles Kitima katibu wa baraza la maaskofu katoliki Tanzania (TEC) alikutana na Makamu Mwenyekiti wa Chama cha demokrasia na maendeleo (CHADEMA) John Heche na walifanya mazungumzo yaliyoanza saa 5:05 asubuhi na kumalizika saa 7:17 mchana.
Aidha taarifa hiyo iliongeza kuwa katika kikao hicho, John Heche alimpa mrejesho wa mipango ya CHADEMA kwa mwaka 2026, kubwa zaidi likiwa maombi ya fedha yaliyowasilishwa na John Mnyika na Amani Golugwa kwa lengo la kutekeleza mikakati yao ya mwaka huu.
Je, ni upi uhalisia wa picha na taarifa hiyo?
JamiiCheck imefuatilia na kujiridhisha kuwa picha hiyo si halisi.
Aidha kwa kutumia nyenzo za kidigitali imebainika kuwa picha hiyo haijarekodiwa kwa camera bali imetengenezwa kwa kutumia programu ya kuhariri Picha inayoitwa Photoshop.
Kadhalika picha imebainika kuwa na viashiria vya Akili unde hasa katika eneo la uso jambo linaloonesha kuhusika kwa teknolojia ya Akili unde kutengeneza picha husika.
John Heche makamu mwenyekiti CHADEMA alitafutwa kuzungumzia picha na taarifa hiyo amesema:
Kwanza si kweli kwamba hiyo picha imepigwa jana (Januari 7, 2026), kwa kuwa mimi sipo Dar es Salaam na sijaonana na Padre Kitima muda mrefu, nadhani tangu ashambuliwe nilionana naye mara moja tu kumpa pole.
Pia, mimi kukutana na Kitima hata kama ingekuwa kweli tumekutana kuna tatizo gani kwani? Huyo ni Mwalimu wangu, amenifundisha, hivyo kukutana naye na kuzungumza naye wala siyo tatizo na nimeshakutana naye mara nyingi tu.
Kuhusu hiyo picha kama ni halisi au la kwa kweli sikumbuki, kama ni picha halisi basi ina takribani miaka 10, kama sijakosea ilipigwa nilipokuwa nimeshinda Ubunge au nilienda kumtembelea, nasema hivyo sababu nimekutana mara kadhaa na Padre Kitima katika mazingira ya kukaa na kunywa chai.”
Akaendelea “Hata ukitazama uso wangu wa sasa na huo unaoonekana kwenye picha kuna utofauti, haupo hivyo. Kwa hiyo sikumbuki kama ni picha ya kweli au imetengenezwa.”