Picha: Rais Kikwete ashiriki maombolezo ya Regia Mtema

Sijaona hoja yako ya msingi hapo, hata kama msiba ni wa kitaifa lakini haiondoi UHALISIA kuwa wafiwa wakubwa ni ndugu, wakifuatiwa na CDM na kwa vile yeye alikua kiongozi mkubwa wa chama, si vibaya taratibu za KICHAMA ikiwemo kutumika bendera ya chama zikitumika katika mazishi hayo... Tsiende nje ya mada na kusababisha ubishi usio na maana hasa katika kipindi hiki cha majonzi, tushirikiane kwa pamoja bila kujali mavazi gani yanatumika kwa sababu sidhani kama nguo au bendera ya chama ina madhara katika mazingira hayo.... RIP dada Regia Mtema!!
Hicho ni kitambaa tu chenye rangi zinazofanana na bendera ya Chadema. Hata CCM makada wao wanapofariki bendera, kofia khanga zinatawala msibani. Green guard hutumika kubeba jeneza wakiwa na sare za UVCCM. Lakini kwa kuwa marehemu alikuwa Mbunge, ndo maana ataagwa ukumbi wa Karimjee, na bendera ya Taifa itafunika jeneza lake. Huu msiba ni wa KITAIFA unaoratibiwa na CHADEMA kushirikiana na BUNGE na wana ndugu.
 
Hiyo colour ya uchama ya kazi gani msibani? Haoni wenzake walivyovaa?
Miaka hamsini na Wodi zetu.........Tafakari.

wodi.jpg
 
Kwa kweli hii nimeipenda sana, tunatanguliza utaifa kwanza, katika matukio kama haya tofauti za kiitikadi tunaziweka kando na tunaungana kufanya maombolezo yanye kutukutanisha na kuwa taifa moja. Hizi ni nafasi adimu sana ambazo hutokea kutuunganisha watanzania wenye itikadi tofauti na kushirikiana kuwa kitu kimoja.

Sote pamoja na kutofautiana kiitikadi malengo ni kwa ajili ya kujenga taifa letu, kwani itikadi ni njia tofatuti tu tunazopitia tukiwa na malengo yale yale yakufikia kileleni. Na hizi tofauti zetu za kiitikadi tunapoziunganisha kwa kupishanisha kupeana awamu ni malengo ya kuchochea maendelea ya taifa si uadui.

Narudia matukio haya ni ujumbe mahsusi kwetu na njia ya kuzidi kutuunganisha na kutoa tofauti za kifikra za kuhasiniana bali kujenga mfumo wa kushindana kwa hoja ndio maendeleo tunayotaka.

Hongera viongozi wa serikali kuonyesha njia, kwani wengi wamejifunza na watazidi kujifunza mengi katika matukio kama haya licha ya simanzi nzito aliyotuachia dada yetu marehemu Regina Mtema.
Uliyo sema Ndg yangu Candid Scope ni kweli kabisa, matukio kama haya ndiyo yanayoonyesha Utanzania wetu ujamaa wetu aliotuachia Marahemu Mwl Nyerere wa kupendana. Hapo ndipo utakapo ona kuwa siasa si chuki wala uadui bali ni mwelekeo wa sera zikiwa na utofauti ili kufikia malengo ya kuleta maendeleo kwenye taifa letu!!!!!!!!! Kama viongozi wetu walioshika dola watalielewa hilo kama wanavyo onyesha Tanzania litakuwa taifa bora la kuishi!!!!!!!!!! Ni majonzi na masikitiko kwa kupoteza mpambanaji wetu dada Regia Mtema, hili ni pigo kwa Watanzania wapenda haki na pigo pia kwa upinzani kupata replacement ni vigumu. Mungu awatie nguvu na uvumilivu familia yote ya marehemu na wadau kwa ujumla!!!!!!!!!

 
Sina uhakika kama kuna kosa katika hali inanyoonekana. Picha za chadema sioni kama ni tatizo ni heshima tu kwa mbunge wake kipenzi. Ni mwakilishi wake bungeni, ni kiongozi wao. Ni heshima tu. Vazi la msiba sawa kwa walionalo na waliojiandaa kulivaa kulingana na muda wao na mahali. Vazi ni changuo la mtu na uhuru binafsi.
 
Halima Mdee, uzungu mpaka msibani au ndio maendeleo!

ivi nani kasema msibani lazima wanawake wavae Khanga. Mwacheni avae what she feels confortable bwana. Wengine hawana mazoea ya kuvaa Khanga sasa kwanini apretend msibani? I hate pretenders...
 
Mkuu, kama vichwa hivi vyote vingekuwa vinaungana kupigania haki na maslahi ya Watanzania, hakika tungekuwa mbali sana.
Kama wangeachana na kauli na vitendo vya kuonyesha 'sisi ndio wenye nchi' na kujiamualia mambo kwa maslahi binafsi na malahi ya chama kwa maana ya kuendelea kuongoza daima dumu.

Hawa, wangesimama kidete kutenda haya:
  • Watuhumiwa na washiriki wote wa wizi na uporaji wa fedha za EPA washughulikiwe, kama hakuna sheria ya kuwashughulikia vizuri, basi watunge sheria fasta
  • Fedha zote za maendeleo zinazokwenda katika Halmashauri na manispaa zinasimamiwa vyema, any poor audit report leads to dismissal of responsible people
  • Budget ya maendeleo inakuwa kubwa kuliko budget ya matumizi ya kawaida
  • TRA inabanwa mbavu kukusanya kodi
  • Vyanzo vya kodi hasa makampuni ya madini, gas na industry inzima ya hotels/appartments inapitiwa upya na mianya ya ukwepaji wa kodi unadhibitiwa ipasavyo.
  • Nchi inajikita katika Viwanda......viwanda stahiki vinafufuliwa/kuanzishwa.
  • Usafirishaji bidhaa ghafi kwenda nje unapunguzwa kwa ku-process malighafi hizo katika viwanda vyetu.
  • Importation ya vitu visivyo vya msingi unadhibitiwa - viwanda vya vitu kama maziwa ya watoto, metal fabrication - spare za magari watu waweze kununua genuine au kuchongesha katika viwanda vyetu.....n.k.
  • .....ENDELEZA MWENYEWE HAPA...
Hapo umenena kweli kamawangeshirikiana kutenda haya yote nchiyetu ingekuwa bora zaidi!!!!!!!!! Hawa walioka madarakani waache kupiga mabomu watetezi wawanyonge waonyeshe mshikamano kuokoa nchiyetu kwenye uangamivu wa kiuchumi!!!!!!!!!!

 
ri.jpg

Pichani Heche mwenyekiti wa umoja wa vijana Chadema na sare za chama msibani

Chadema ni chama makini, tunataka kuchangia mawazo kuongeza kiwango cha umakini zaidi, hivyo maoni yetu si kukiua chama ila ni kukifanya kiwe makini na mtazamo mpana na mwono mpana zaidi. Chadema kimejaa wasomi tunataka kifanye shughuli zaki kisomi kwa viongizi kuwa vinara wa kutoa mifano na wengine watafuta.

Mkuu nadhani unapoteza muda kuzungumzia mavazi ya chama msibani. Mavazi ya chama hayaepukiki hata ufanyeje.

Ni kama vile kuwashutumu wanajeshi ama polisi ama magereza kuvaa sare zao katika msiba wa askari mwenzao, tena wa cheo cha juu. Kama unadhani hiki kitu hakipo, nimeona mahali unazungumzia ustaarabu sijui ustaarabu gani huo unaoufahamu wewe peke yako wengine hawaufahamu.

Kila mara tunashuhudia misiba mbalimbali ndani na nje ya nchi, watu wakiwa wamevaa wamevalia mavazi ya nayotambulisha ufuasi ama taaluma. Ushawahi kushuhudia msiba wa jaji? umeona mavazi wanayovaa majaji wenzake? au nao hawajui ustaarabu?

Kama kuna jambo jengine la msingi unaweza kulileta tukalijadili in relation to this msiba lakini la mavazi ni kutuchosha na sort of propaganda za kiserikali kwani hata mtazamo wako ni serikali ya JK ndiyo inaongoza maombolezo wakati ukweli ni kwamba chadema ndio wanaongoza maombolezo. Tuendelee na mambo mengine mkuu achana na hii ya mavazi.
 
Sorry to say sorry, hatujafikia huko ambako mwenzetu umeshavuka uzio, sisi tupo pamoja na yaliyotokea ni ya kawaida kushirikiana katika kuomboleza na kuwatuliza wafiwa. Upande uliopo mwenzetu inatuwia vigumu kuchangamana nawe, bora urudi upande wtu tutakuwa kitu kimoja.

Jitahidi kujibu hata kama wajua ni kitanzi kwa hoja zako.
 
Tunataka Maalim Seif awaongoze CUF na wazanzibar kushiririki msiba huu mzito wa kitaifa

Chadema kwa kulazimisha mambo.
maaalim ni makamo wa kwanza wa Rais Znz na ana shughuli nyingi za kitaifa.
Pasi na shaka CUF wataongozwa na Mtatiro, Naibu wake bara.

Na Hamad Rashid atakuwepo pia. Kwani yeye anashinda pale Habari maelezo Dar

 
Halima Mdee, uzungu mpaka msibani au ndio maendeleo!

Hata mimi nimeshangaa sana. Kashindwa kufunga kitambaa kichwani hata kuvaa kanga pia!!!!.

Kweli huo ndio uzungu uzungu tu.

Je ataweza dumisha mila za waTz au ndio atapalilia uzingu Tz.

 
Yeyote aliyemsifia kikwete analazimika kujibu swali lifuatalo; UKIMKUTA SHETANI KANISANI UTASHANGILIA NA KUSHUHUDIA YA KUWA SHETANI AMEOKOKA, MAJARIBU KWISHNEHI??!!!!!!!!!!! R.I.P REGIA

Jogi Mwanadamu akimkosea Mungu ageuki shetani hapa duniani,kwa kuwa Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake hivyo, kama Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake basi kimpatacho mwanadamu baada ya kukiuka maagizo ya Mungu wake ni kugeuka kuwa mfuasi wa shetani na si Shetani,kwa kuwa unapokuwa mfuasi wa kitu unakuwa na hiari yako binafsi uache au ufuate ndio maana wanadamu tofauti na wanyama tunakitu kikubwa Mungu katupatia nacho ni utashi.

Na kikubwa Mungu hakuja duniani kwa wema pekee bali alikuja kwa wakosefu,kwa kuwa ukombozi umewekwa kwa ajili ya wakosefu,ambao ni mimi,wewe na mwingineyo yoyote hapa duniani na kipimo cha ubaya ni wema.

Kilichofanya na Mheshimiwa Rais ni chema hata kama kuna yale ambayo sisi tunaona anamakosa nayo lakini tuna nafasi pia ya sisi kupima uzuri na hatujui nafsi yake yeye kwa msiba huo anajisikia kuwajibika kwa lipi kimatendo ila jukumu ni lake yeye na mola wake nasi wengine kama binadamu wenzie tutampima kibinadamu kwa matendo yake ikiwemo hili la kuhudhulia kwenye msiba wa Binti wa Nchi ambae yeye ni Rais wake.

Siri ya Mungu juu ya kwanini haya yatokee na kwanini Jakaya audhulie msibani anayo Muumba na kwa kila mmoja wetu mioyoni mwake kama Wanadamu tulio umbwa na Mungu.Ndio maana mambo uwa hayatokei hivi hivi yanatokea kwa sababu Mungu anasababu zake.

Ndio maana mimi kuna thread niliandika humu ndani kuwa msiba wa Regia, Mungu anasababu na Watanzania [BOFYA HAYA HAPA].

Alichofanya Rais Jakaya Kikwete ndicho Mungu alichopanga, na ndio maana humu ndani kuna watu wameanza kuhoji na walitamani kuona picha ya Dk Jakaya na Dk Slaa,zikipamba kulasa za magazeti ya Watanzania,hakika hata mimi ninatamani,lakini Mungu ndie anaeujua atawakutanisha wapi na kwa sababu gani.Amepanga tumemuona Jakaya kwenye msiba,ambao wewe unaona ni shetani kaingia kanisani.

Ushauri wangu kwako uko katika picha hii ni nani hasa Shetani? Kati yako wewe ulie hoji udhulio la Rais Jakaya Kikwete ambae tunamtizama kuhudhulia kwenye msiba wa mpendwa wetu Regia Mtema akiwa kama Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mwenyekiti wa Chama cha CCM ambacho ni chama shindani cha Chadema,na kama Mtanzania wa kawaida na wewe uliyetoa kauri ya kishetani.

Kwa kuwa kialisia mtu ambae ana akili timamu na si za kiwendawazimu yani akili za kishetani, msiba uwa hauna ndugu tunajua dhahiri hilo licha ya kuupokea kwa tafsiri ya ushiriki wetu hapa duniani na mahusiano yetu na Mungu, pia tunaupokee kwa tafsiri ya tendo la kibinadamu na hasa kiafrika tunapofiwa na wenzi wetu kisha ndugu, jamaa na marafiki wakafika kuja kushiriki nasi kwenye maombolezo, jamii nzima ujisikia auheni kuwa Mungu ametwaa mwenzi wao lakini Mungu huyo huyo ametuma waja wake kuja kuwapa wafiwa matumaini mapya kwenye tukio ilo la kuondokewa na mpendwa.

Hivyo kuhudhuria kwake na wengineo wote waliodhuria na watakao hudhuria mpaka dakika ya mwisho kumfikisha mpendwa wetu Regia kwenye makazi yake ya milele.Basi kama shetani atakuwa na sura ya ubinadamu atafanana na ni yule aliyehoji watu wote wa Mungu ambao, Mungu aliwaumba kwa mfano wake,kisha kwa mfano wake huo leo kawapa dhamila ya kuwatuma waudhurie msiba wa Regia kuwafariji wafiwa mpaka kwenye kumsitili mpendwa wao huyo.

Pole sana Jogi,Mungu bado anakupenda anakupa nafasi kwa kuwa usijione umesimama, Mungu hakuja kwa wema kwa kuwa wema tayari ni wake,bali alikuja kwa wakosefu.

Ndio maana aliye mwema wake Regia Mtema kesha mchukua.
RIP Regia.
 
Back
Top Bottom