ipogolo
JF-Expert Member
- Aug 15, 2011
- 6,275
- 5,961
Hicho ni kitambaa tu chenye rangi zinazofanana na bendera ya Chadema. Hata CCM makada wao wanapofariki bendera, kofia khanga zinatawala msibani. Green guard hutumika kubeba jeneza wakiwa na sare za UVCCM. Lakini kwa kuwa marehemu alikuwa Mbunge, ndo maana ataagwa ukumbi wa Karimjee, na bendera ya Taifa itafunika jeneza lake. Huu msiba ni wa KITAIFA unaoratibiwa na CHADEMA kushirikiana na BUNGE na wana ndugu.Sijaona hoja yako ya msingi hapo, hata kama msiba ni wa kitaifa lakini haiondoi UHALISIA kuwa wafiwa wakubwa ni ndugu, wakifuatiwa na CDM na kwa vile yeye alikua kiongozi mkubwa wa chama, si vibaya taratibu za KICHAMA ikiwemo kutumika bendera ya chama zikitumika katika mazishi hayo... Tsiende nje ya mada na kusababisha ubishi usio na maana hasa katika kipindi hiki cha majonzi, tushirikiane kwa pamoja bila kujali mavazi gani yanatumika kwa sababu sidhani kama nguo au bendera ya chama ina madhara katika mazingira hayo.... RIP dada Regia Mtema!!