Hivi Watanzania tumekuwaje? Huyu bwana tunajua ana inda na Tz kwasababu ya kichapo cha M23 na uwepo wake kule DRC.
Tunajua ana inda na kauli ya JK na tunajua ni dereva wa CoW kwa nia ile ile
Hana jema analoweza kuongelea kuhusu nchi yetu
Hatusimami kwa U-CCM au UKAWA , tunaangalia masilahi mapana ya taifa.
Anaposema ata 'hit hard kwa JK' haa maana kwa JK kama mtu, ana maana kwa Tz.
Jirani mwema anapaswa kukaa kimya kwa wakati huu. Ndivyo tuliyokaa kimya chaguzi za nchi jirani.
Kenya walipopata matatizo tuliweza kuwaweka pamoja kwasababu kila mmoja alikuwa na trust nasi
Leo Museveni akiibuka na lake, Uhuru na lake, Nkurunzinza na lake juu ya Tz hatuoni tatizo?
Hivi PK amesema kwa nia njema kweli! angalieni anaweza kutupa uchafu ilimradi tuvurugane arudi DRC
Mambo yetu yanatuhusu wenyewe, PK aendelee na kubadili katiba atawale kama chief, hatuhusu
Hadi hapa amefanikiwa maana hatujadili hatma yetu tunamjadili PK ! who's PK kwetu?
Huyu PK anaweza kusema tukamsikiliza kweli!