Paul Kagame umeongea ukweli hataki unafiki!

Paul Kagame umeongea ukweli hataki unafiki!

DRC nayo ina bahari
Kiongozi bora ni yule anayeweza ku-utilize resources alizonazo na sio yule anayeshindwa kufanya hiki au kile kwa kisingizio kwamba nchi haina natural resources! Ni sawa mtoto kilaza wa masikini anayesingiziwa kutofika chuo kikuu kwa sababu baba ake sio Bakhresa!
 
Kiongozi bora ni yule anayeweza ku-utilize resources alizonazo na sio yule anayeshindwa kufanya hiki au kile kwa kisingizio kwamba nchi haina natural resources! Ni sawa mtoto kilaza wa masikini anayesingiziwa kutofika chuo kikuu kwa sababu baba ake sio Bakhresa!

Natamani nikujibu ila i am quite sure hata wewe mwenyewe ukisoma ulichokiandika kamwe hautajielewa, unataka kuzungumzia nini?! Yaani pointi yako haswa ni nini?
 
Kuwa muelewa, au hadi utafuniwe kama mtoto ndio umeze?

Ndio nitafunie nimeze!! I never stop asking question because its from them that i get pure knowledge!! Wewe ulitaka nijifanye kuelewa hata kama sijaelewa?
 
hebu engage ubongo kidogo!
Miaka 50 ya uhuru ccm imeweza kuleta umaskini!
Lakini uhuru na demokrasia havijaletwa na ccm!
kama vitu vizuri katika nchi vinazuka tu bila ya kuletwa na yeyote, nadhani na vibaya pia huzuka tu!
so tusiwasikilize wale zero wenu wakiilalamikia ccm kuwa ndio chanzo cha matatizo!
Hizi shida zimekuja tu kama jinsi raha zinavyozuka tu!

2kimo very hopeless mshkaji wangu, hebu ona hata aibu kijana
 
Last edited by a moderator:
Nisome vizuri Chakaza... Membe nimeandika Halmashauri kuu na sio Kamati Kuu! Kamati Kuu ni ile ambako majina yasiyozidi matano yanafika na kupatikana matatu yanayofika Mkutano Mkuu! Hebu tukumbushane, baada ya majina 5 kuingia Kamati Kuu, kumbukumbu zangu zinaoenesha ambao waliingia Halmashauri Kuu ni Migiro, Amina na Pombe!

Hata hivyo kuna kitu nimesahau hapa au kinanichanganya! Katiba yao inaonesha majina yasiuopungua matano ndiyo yanatoka Kamati ya Maadili na Usalama kuingia Kamati Kuu... from Kamati Kuu majina yanaingia Halmashauri na kikao cha mwisho Mkutano Mkuu. Sasa ikiwa majina yanatoka Kamati Kuu na kuingia Halmashauri Kuu... hapa kumbukumbu zimenitoka! Pale Kamati Kuu si yanachujwa kuingia Halmashauri Kuu? Kumbukumbu zangu hapa ndo majina ya Makamba na Membe yaliishia na matatu yakaingia Halmashauri Kuu! Sasa ikiwa Mkutano Mkuu yanaenda majina matatu, hapa Halmashauri Kuu ni nini kinafanyika ikiwa napo yaliingia majina matatu kutoka Kamati Kuu!
Iko hivi chige, majina yote ya walioomba yanatakiwa yaingizwe Kamati Kuu na watu wahojiwe, hilo halikufanyika na ugomvi wao ndipo ulipoanzia baada ya kusema kamati ya maadili imewakata na kubakisha watano ili wapate baraka za kupelekwa Halmashauri kuu. Hivyo majina yaliyopelekwa Halmashauri kuu ni Membe,January, Magufuli,Migiro na Amina.
Hapo ndio yanatoka matatu kwenda mkutano mkuu, na yakatoka ya Magufuli,Migiro na Amina.
 
Last edited by a moderator:
Iko hivi chige, majina yote ya walioomba yanatakiwa yaingizwe Kamati Kuu na watu wahojiwe, hilo halikufanyika na ugomvi wao ndipo ulipoanzia baada ya kusema kamati ya maadili imewakata na kubakisha watano ili wapate baraka za kupelekwa Halmashauri kuu. Hivyo majina yaliyopelekwa Halmashauri kuu ni Membe,January, Magufuli,Migiro na Amina.
Hapo ndio yanatoka matatu kwenda mkutano mkuu, na yakatoka ya Magufuli,Migiro na Amina.
Hapana Chakaza, usisikilize propaganda za akina Kingunge ingawaje kwako ni muhimu kwa kuwa ni UKAWA! Katiba ya CCM inasema Kamati Kuu itapokea majina yasiyopungua matano kutoka Kamati ya Maadili na Usalama! Wakati nakupa hilo dokezo, ngoja nikutafutie screenshot ya Katiba ya CCM!
 
Hapana Chakaza, usisikilize propaganda za akina Kingunge ingawaje kwako ni muhimu kwa kuwa ni UKAWA! Katiba ya CCM inasema Kamati Kuu itapokea majina yasiyopungua matano kutoka Kamati ya Maadili na Usalama! Wakati nakupa hilo dokezo, ngoja nikutafutie screenshot ya Katiba ya CCM!
Kazi za kutumwa zinatufanya tusiwe na uwezo kukamilisha tunachosema! Anyway, nimeipitia tena katiba ya CCM. Kwa kifupi, kuna mkanganyo kidogo ambao bila shaka unatokana na nguvu iliyonayo Kamati ya Maadili na Usalama ambayo haijataja kazi zake kwenye katiba zaidi ya kutaja uwepo wake kwenye Ibara ya 107 (23).

Katika pekua pekua, nikakuta kumbe, according to Mwananchi, kazi za Kamati ya Maadili na Usalama zimetajwa kwenye Kanuni za Uongozi na Maadili, toleo la 2012 kifungu cha 4(ii). Unfortunately, sijui hizi kanuni zinapatikana wapi tena nakumbuka siku za nyuma nilizitafuta sana lakini sikuzipata! Lakini Mwananchi wanaojua ni wapi wamezipata hizo kanuni wanasema:
"…wanachama wanaogombea uongozi ambao uteuzi wao hufanywa na vikao vya kitaifa, watachunguzwa kwanza uadilifu wao na chombo cha maadili cha CCM kwa ushirikiano na vyanzo vingine.
....................................
Ikiwa mwanachama hakupendekezwa kwa sababu ya kukiuka Katiba ya CCM, Kanuni za CCM na sheria ya nchi, hatakuwa na haki ya kukata rufaa kwa mtu yeyote au kikao chochote. Lakini ikiwa mwanachama atakataliwa kugombea kwa sababu ya madhambi yake katika chama, basi ni wajibu wa Kamati ya Usalama na Maadili kumjulisha makosa yaliyomnyima haki ya kugombea, naye anaweza kukata rufaa kwa mujibu wa haki zake kikatiba.
On the other hand, wakati kazi za Kamati ya Maadili hazijaoneshwa kwenye katiba zaidi ya kuwepo kwenye kanuni, moja ya kazi za Kamati Kuu kwenye hili suala zinaishia tu kusema: 109 (6)Unapofika wakati wa Uchaguzi Kamati Kuu ya Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa itashughulikia mambo yafuatayo:-
(b) Kufikiria na kutoa mapendekezo yake kwa Halmashauri Kuu ya CCM ya Taifa juu majina ya Wanachama wasiozidi watano wanaoomba kugombea kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Hivyo basi, kwa maoni yangu nadhani mkakati wa kumkata Lowassa ulianza mwaka 2012 lakini wafuasi wake wakachelewa kuliona! Walichelewa kuliona kwa sababu, wakati wao walikuwa na imani kwamba EL ana timu yake kwenye Kamati Kuu, katiba yao wenyewe haijasema popote kwamba itajadili majina ya wagombea WOTE bali itapendekeza majina yasiyozidi matano!

Wakati katiba haijasema popote kwamba Kamati Kuu itajadili majina yote ya wagombea, kanuni zinasema majina ya wagombea yataanza kwanza kujadiliwa na Kamati ya Maadili na Usalama na kutoka hapo; wapo ambao hawatapendekezwa na hawatakata rufaa popote lakini pia wapo ambao hawatapendekezwa na kupewa haki ya kukata rufaa!! Haki ya kukata au kutokata rufaa itategemea na "makosa" watakayokukuta nao Kamati ya Maadili!!! Sasa endapo Timu Lowassa (CCM) wangekuwa makini, since 2012 wangegundua kwamba kuna watu wameandaliwa kupelekwa Qibla na wakishapelekwa; hakuna kukata rufaa!!!
 
Kuwa muelewa, au hadi utafuniwe kama mtoto ndio umeze?

Ndio nitafunie nimeze!! I never stop asking question because its from them that i get pure knowledge!! Wewe ulitaka nijifanye kuelewa hata kama sijaelewa?

Kama unajua huna meno ya kutafuta kwanini uwe jeuri?
 
"Preaching about Democracy is one thing but Practising it is another thing! As East African Countries members we are witnessing whats going on in Tanzania as they are heading to their General Election;

So we are curiously looking forward seeing our best friend and the Presiding Chairman of our Community proving to us how Democracy is Practically adhered in Tanzania so as to differentiate himself from either me or Nkurunzinza!"

Kagame, Paul

SOURCE DW

Well said Mr. President
 
anaizungumzia Tanzania et kwa vile Kikwete ni chairman anamwacha kumzungumzia Museven anavyong'ang'ania madaraka miaka 30 sasa.
 
Kwa mtu yoyote mwenye akli hawezi kushabikia mambo ya Kagame, Kagame ni hatari kwa ustawi wa taifa letu, kuna mengi yamejificha nyuma ya huyu mtu, usishadadie kisa anamfavour mtusi mwenzake EL. Yapo mengi usiyoyaelewa, kinachokuponza ni uhaba wako wa information. kagame ni hatari tena hatari sana kwa nchi yetu.
Naomba nisaidie hizo information ambazo nina uhaba nazo bro.
 
Hivi Watanzania tumekuwaje? Huyu bwana tunajua ana inda na Tz kwasababu ya kichapo cha M23 na uwepo wake kule DRC.

Tunajua ana inda na kauli ya JK na tunajua ni dereva wa CoW kwa nia ile ile
Hana jema analoweza kuongelea kuhusu nchi yetu

Hatusimami kwa U-CCM au UKAWA , tunaangalia masilahi mapana ya taifa.

Anaposema ata 'hit hard kwa JK' haa maana kwa JK kama mtu, ana maana kwa Tz.

Jirani mwema anapaswa kukaa kimya kwa wakati huu. Ndivyo tuliyokaa kimya chaguzi za nchi jirani.

Kenya walipopata matatizo tuliweza kuwaweka pamoja kwasababu kila mmoja alikuwa na trust nasi

Leo Museveni akiibuka na lake, Uhuru na lake, Nkurunzinza na lake juu ya Tz hatuoni tatizo?

Hivi PK amesema kwa nia njema kweli! angalieni anaweza kutupa uchafu ilimradi tuvurugane arudi DRC

Mambo yetu yanatuhusu wenyewe, PK aendelee na kubadili katiba atawale kama chief, hatuhusu

Hadi hapa amefanikiwa maana hatujadili hatma yetu tunamjadili PK ! who's PK kwetu?

Huyu PK anaweza kusema tukamsikiliza kweli!

Kuna jambo moja tu dogo ccm inatakiwa wafanye. km wanataka kumuaibisha kagame wakubali ufanyike uchaguzi wa kidemokrasia.
ACHA POROJO ZSIZO NA MAANA YOYOTE!
WATZ WANATAKA MABADIRIKO KUANZIA KESHO
 
Akili za bavicha hizi, hamia rwanda basi ...

ccm mnakazi ndogo tu. Ili kumuaibisha KAGAME kubalini ufanyike uchaguzi wa kidemokrasia.
WTZ WANATAKA MABADIRIKO
 
Back
Top Bottom