Hata hapa hapa bongo, Ukiwa mbunge tu
Automatically unakabidhiwa diplomatic passport ambayo unaenda nchi zaid ya 50 bila visa.
Hukaguliwi hovyo airport za kimataifa,
Automatically utapitia v.i.p gate na kukaa v.i.p lounge Kila airport uendayo
Na baadhi ya nchi zinatoa upendeleo kabisa WA kiKodi kwny forodha ukinunua bidhaa kwao,
wkt uku bongo ndo kabsaa haulipi Kodi,kila upoagiza bidhaa zako nje ya nchi
Ndo maana UKIJICHANGANYA kwenye 18 za wanasiasa, wako radhi ata wakuue Ila sio kuuachia ubunge wao
Wakiuchoka ubunge wanarithishana TU kwenye familia zao.
Kamwe Huwezi shindana na mbunge kubadilisha magari, yeye halipi ushuru,ila Wewe utalipia
Huwezi shindana na mbunge biashara ya mabasi, Basi mpya ya mil 198, Ushuru wake Ni mil 210. Jumla ni mil 408.
Wewe unaiwazia mil 408, yeye anaiwazia mil 198, Kwa Basi lile lile. Hamlingani kabisa.
Utawapakiza abiria wako Basi chakavu Hadi wakuchoke, wakati mbunge wako anabadilisha Basi jipya Kila baada ya miez 3 .
UBUNGE WAO NDO KULA YAO