kuwa mwelewa wewe na jaribu kufikiri mambo kwa kutumia akili yako na sio ushabiki. Tatizo sio kutangaza officially, suala ni kwamba, Marekani imeamua kutangaza kifo cha usama katika kipindi hiki ijkiwa na sababu nyingi tu, moja ni kwamba, Obama alianza kupoteza itibari yake, hivyo kwa sasa kutamnyua kisiasa na hata kumfanya aondoke katika hali ya kukalia kuti kavu.Hivi sasa karibu muongo mmoja umepita, lakini bado kuna maswali mengi ambayo bado hayajapatiwa majibu kuhusu jinsi tukio hilo lilivyopangwa na kutekelezwa, na uwezekano wa kushiriki duru za ndani za utawala wa Marekani katika tukio hilo. Hata hivyo, hakuna shaka kuwa, milipuko ya Septemba 11 na kukiri Bin Laden kuwa alishiriki katika mashambulizi hayo, kuliipa Marekani kisingizio tosha cha kuishambulia Afghanistan na kuikalia kwa mabavu, na kisha kuanzisha vita nchini Iraq. Kama Bin Laden analaumiwa kwa kusababisha vifo vya karibu watu elfu 3 katika tukio la Septemba 11, Wamarekani katika kulipiza kisasi cha tukio hilo, wamewaua moja kwa moja au katika matukio yasiyo ya moja kwa moja zaidi ya watu milioni 1 nchini Afghanistan, Iraq na hivi karibuni nchini Pakistan. Nchini Pakistan pekee, kwa kila muhanga mmoja wa tukio la Septemba 11, Wapakistan 17 wameuawa katika mashambulizi ya ndege zisizo na rubani za Marekani dhidi ya nchi hiyo. Kwa vyovyote vile, kuchelewa kuuawa Usama bin Laden ni jambo jingine lenye utata kuhusiana na kadhia hiyo. Licha ya Wamarekani kudai kuwa wana zana za kisasa kabisa za ujasusi na upelelezi, lakini imewachukua karibu miaka 10 kuweza kumuua mtu ambaye kama anavyoitwa ni 'adui hatari zaidi wa Marekani'. Ushahidi wa kuaminika unaonyesha kwamba, katika muda wote huo, makomandoo wa Marekani mara kadhaa walikaribia kumtia mbaroni kiongozi huyo wa mtandao wa al Qaida, ama katika dakika za mwisho White House na Pentagon zilitoa amri ya kusimamishwa operesheni hizo. Ni wazi kuwa Usama Bin Laden aliingia katika uwanja wa kisiasa kwa maslahi ya Marekani na hata katika kukabiliana kwake na Wamarekani mwishowe alipelekea kudhaminiwa maslahi haramu ya nchi hiyo duniani. Hivi sasa pia inaonekana kuwa hata habari za kuuawa kiongozi huyo wa al Qaida ni kwa faida ya Marekani au kwa uchache zitamsaidia Obama katika kampeni zake za uchaguzi ujao nchini humo.