Kang nimezoea kukusoma kule kwenye jukwaa ka sayansi na teknolojia.
Hebu niambie kwa utaalamu wako yawezekana kweli nyumba yenye ungo (dish) ikaelezwa kwamba haina mawasiliano ya internet na ikashindikana kuwa na simu?.
Na jee kwa kutumia dish Osama angeweza kuongoza mtandao wa Alqaida na kuweka mafaili yake kwenye kabati pale Abbottabad?.
Kama kweli Osama alikuwa bado hai, na hii operation yao ilimfikia na kumuua basi bado maelezo wanayotoa yanakinzana.
Lakini tuchukulie alikuwa Osama waliyempata na kumuua. Ni wazi alijua anatafutwa na lazima alijua kuwa US wanashuku kuwa yuko Pakistan..vipi ataweka kumbukumbu "za operations zake" ambazo anajua zitawa-expose wapambe wake siku akikamatwa?
Kama alikuwa ni msiri, hakutumia simu wala internet, messeges zilitumwa hand to hand...hili haliingii akilini.
Lakini katika maelezo waliyotoa walisema alipigwa risasi ya kichwani,utosini na kifua ni...lakini katika account nyengine walisema alipotokewa na SEALS alikimbilia ndani na wao walihofia kuwa anaenda kuchukua silaha au bomu na wao ndio walimtwanga risasi..sasa mtu anaekimbia anakupa mgongo!!! sio kifua au uso...au alikuwa anakimbia reverse style!!??