Nyerere Alifanya Makosa Makubwa...

Nyerere Alifanya Makosa Makubwa...


Sasa Jirani yetu KENYA chini ya MZEE JOMO KENYATTA alikuwa na MISINGI MAALUMU YA KUONGOZA? kumbuka kulikuwa na Mwanaukombozi kwa JINA LA DEDAN KIMATHI aliyekuwa na uhamasisho mkubwa kudai ARDHI yao iliyochukuliwa na MABEBERU wa kizungu ndio walioanzisha MAU MAU WAR; Kenyatta akapandikizwa

Kenya ikapata uhuru sababu ya Huyo Jamaa na Land Issue, Lakini Kenyatta land kidogo aliyopewa na wazungu aligawana na vizito wenzake wachache; wengine akawapa vibaraka Dedan Kimadhi akafa bila ARDHI

Kwa Nyerere Tanganyika ilitawaliwa na Wakoloni wawili MJERUMANI halafu MWINGEREZA wakati wa MWINGEREZA hakuwa anaijali sana Tanganyika na Maendeleo yake alikuwa anajua iko siku ataikosa atanyangány´wa kwahiyo pamoja na Tanganyika kuwa na Utajiri haikuendelezwa

Tanganyika ilikuwa na Makabila MENGI; DINI KIBAO;

Kwanza ukiangalia katika MAKABILA; Ni Mengi zaidi ya 250 lakini kuna 5 ambayo ni Makubwa na yana Machief na hayo pia yameendelea kielimu na yana mifumo bora sana ya ELIMU ukilinganisha na MAKABILA MENGINE

PILI DINI kulikuwa na Dini kuu kusema kuu ni Maana well established nchini ambazo zilikuwa tayari zina SHULE kuanzia PRIMARY HADI VYUO VYA UALIMU... Ukiangalia Shule za Utawala wa Mkoloni ambaye ni Mwingereza zilikuwa hazina huo mkondo Murua kama hizo shule za dini ni dini kama ya ROMAN CATHOLICS

LUGHA kwasababu ya makabila kibao. ingekuwa vigumu sana kuwasiliana kwenye nchi kubwa kama Tanganyika; South Africa hawana Makabila mengi kama sisi lakini wana 7 official national languages

ÆÆÆÆ Sasa Nyerere alipochukua UHURU kwanza alipendekeza LUGHA ya TAIFA kuwa KISWAHILI hivyo basi kila mtu lazima awe anaongea na ni lugha inayoongelewa Maeneo ya Pwani; kwahiyo haina mwenyewe... Pili kwasababu ya VYAMA VYA USHIRIKA enzi hizo vilikuwa na NGUVU kwa UPANDE wa hayo MAKABILA MAKUBWA akavunja Uongozi wa MILA --- Machief na Watemi wakaondolewa hii ilisaidia sana, sababu enzi hizo walikuwa na sauti kuliko hata Governor wa kikoloni sasa kama wangeachwa nchi ingekuwa labda bado Marais wanabadilishana toka Makabila Makubwa pekee... tusingeona Nyerere, Mkapa, Mwinyi na Kikwete wote toka Makabila Madogo wakiiongoza nchi hii...

Nyerere alitaifisha shule nyingi tu za DINI ili wanafunzi waweze kusoma bure elim ya msingi na walifanikiwa.... na UNAPOSEMA KUWA NYERERE ALIWEKWA MADARAKANI ni only yeye??? kwasababu alikuwa na watoto 9 watoto wake wooote walisome elimu ya Tanganyika hawakusomea ELIMU iliyokuwa inatolewa na SHULE za DINI. Watoto wake hawana Ma-Ph.D na hawafanyi kazi kwenye hizo kampuni zilizomuweka baba yao madarakani

Mwl Nyerere ni wa BUTIAMA; yeye na hao wanae hawakujenga International Airport Butiama; International PORT; au kupafanya BUTIAMA INTERNATIONAL FREE TRADE ZONE... Nyerere hakuwajengea Mahekalu wanae MBEZI BEACH; sasa kama kweli hao waliomweka madarakani walimtakia mema kwanini waliiacha familia yake OMBA OMBA???

Hakuna hata visenti USWISI kama wengine? Sasa kweli ni misingi gani Imara hadi leo unataka aiweke?

THE BEST PEDAGOGIST He did AZIMIO LA ARUSHA... lakini kila mtu aliyekua chini yake aliichambua kidogo kidogo kwasababu hawakulipenda...

wakaondoa nguzo 5 za uongozi, sasa ukaona viongozi wanamiliki makampuni na wanaingia nayo maofisini mwao; wanaajiri wake zao, wanauziana Majumba, hawakuishia hapo ikaishia kuwa it is not a police state... unaingiza madawa ya kulevya... wewe ni tajiri, wanaua viwanda wananchi wanakosa kazi kwahiyo ndio wateja wa hayo madawa ya kulevya

Lakini Mnaogopa kulaumiana.... Mnamkimbilia Mwl. Nyerere oh alikuwa akiendeshwa na waliomweka MADARAKANI!!! kweli hamuoni AIBU???

&&& Yaani ni kwanini Mwarabu wa Furniture Center katupiwa KEMIKALI...??? na nani kaenda kumuangalia South Africa --- Rais Kikwete... watu hawamuongelei vizuri huyo jamaa... ni jinsi anavyo operate jijini Dar...

Lakini wote mwafunga Macho.... Mwamwangalia Nyerere ati????

Mkuu una moyo wa chuma, wewe unaweza hata ukajitolea muda wako kuandika aya ndeeefu kuwapa somo ng'ombe. Keep it up mkuu labda wataelewa.
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.

Vyema sana....

Tatizo si lipo kwenye msingi?!? Sasa ili kuondoa tatizo, inatupasa kubomoa nyumba nzima kabisa, ili tuanze upya. Tuweke msingi mpya, utakaokuwa imara kwa miaka 200 ijayo.

Heko kwa kufikiria kwa upana.

Cc: ZeMarcopolo
 
Last edited by a moderator:
Usimrithishe mtoto mali....

mpe elimu....

hapo chacha ndipo baba alipokosea

Oh! Hivi si ni Mwalimu aliyetaifisha shule za kidini ili watoto wote hadi wa kiislamu na dini zote wasome?

Sasa, ulitaka afanyeje zaidi ya hivyo katika kipindi chake? Literacy rate unafahamu ilikuwaje? Na sasa ipoje?
 
nonsense!
Alishawaambia mchukue mazuri mnayoyaona mabaya muyaache
Tatizo udini unawasumbua, na mtavuna mnachopanda!!
The creator never sleep nor slumber
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.

FaizaFoxy kwanini waliomfuatia hawakurekebisha makosa hayo? Sasa naona CCM na nyie vijana wa CCM mnaacha kurekebisha makosa hayo mmebaki kushupalia ni nani aliyeyafanya.
Huko ni sawa na kuanguka kisha uendelee kukaa hapohapo chini ulipoangukia.
Hii thread yako ni ya kijinga kuliko thread nyingine yeyote.
Emmancipate urself from mental slavery
 
Last edited by a moderator:
How many people had access to right information?

Kulikuwa na magazeti mangapi? Yalikuwa yanamilikiwa na nani?

Usiposikia kitu haimaanishi kuwa hakipo, wake up...

HIZI HOJA ZINANIKERA NA ZINANIUDHI! Hivi unalinganisha kipindi cha Nyerere hasusani katika access to information na kipndi kipi katika taifa au taifa lipi? Hivi unajua Digital DATA Systems zimekuwepo duniani tangu lini? Je unajua TV za Rangi kwa matumizi ya nyumbani kwa nchi kama Uingereza imeanza lini? Information Technology duniani imezuka pengine tuseme gafla kabisa. Mataifa makubwa yalikuwa na hali iliyofanana sana na ya kwetu wakati wa Nyerere miaka ya 50 na 60.

Hoja yangu - kudhani kwamba kipindi cha Nyerere kulikuwa na kunyimwa access to information, kulikuwa hakuna magazeti utitiri kama tulio nao leo ni kushindwa kujua historia! Tena historia ya wakati wetu. Tumeona mabadiliko makubwa kwenye teknolojia ya habari hasa magazeti miaka ya 80 na 90. Uingereza magazeti ya aina ya Kiu (kama mirror, the sun ) ni magazeti yaliyoanza miaka hio mwishoni wa 70 na mwanzoni 80, sembuse Tanzania! Lakini ufahamu Tanzania tumeruka kwenye IT, tuko mbali kuliko hata Mwingereza kwa kuwa tu hatukuwa na haja ya kupitia hatua za awali za technolojia, tumerukia advanced steps.

HOJA KWA Mpuuzi Faiza: Si kweli Taifa letu Halikuwekewa misingi mizuri! Kinyume kabisa misingi ile tumeivunja, tumeitupilia mbali! Mataifa mengi Afrika yanatuonea wivu kwa mwanzo wetu uliyokuwa mzuri na wanatushangaa tulikojipeleka. Nyerere alifanya kazi kubwa na hata literacy level (kujua kusoma na kuandika) miaka ya 70 ilikuwa zaidi ya 85% ikiwa ni pamoja na miapngo thabiti kama elimu ya Ngumbaru iliyowawezesha wazee ambao hawakuwa wamekwenda shule kuweza kurudi na kufundishwa na kujua kusoma na kuandika (mama yangu alifaidi hili na katika umri wake wa miaka 86 anaweza bado kusoma na kuandika ingawaj polepole sana). Faiza mtoto mpe ELIMU sio pesa- ndio urithi tosha kabisa. Nyerere alitupa ELIMU!
 
  • Thanks
Reactions: ral
How many people had access to right information?

Kulikuwa na magazeti mangapi? Yalikuwa yanamilikiwa na nani?

Usiposikia kitu haimaanishi kuwa hakipo, wake up...
Ni kweli hakukuwa na vyombo binafsi vya habari, lakini vichache vilivyokuwepo vya umma vilifanya kazi kwa uwazi na ubora mara mia moja ya huu utitiri wa sasa wa vyombo binafsi na umma ambavyo karibu vyote vimesheheni makanjanja na wachumia tumbo kuganga njaa!
Kibaya zaidi ni vyombo vya umma kama TBC, Habari leo na Daily News vimepoteza kabisa haiba na vinafanya kazi kama misukule ya wezi, wauza 'unga', majangiri na wahalifu waliosheheni katika ngazi zote za chama tawala CCM!
Kwa hiyo ni wazi, serikali ya awamu ya kwanza chini ya Nyerere ilikuwa 'more transparent' kuliko awamu hizi za mavuvuzela na wala rushwa hata za kuhongwa suruwali, shati na tai.
Wananchi walikuwa na shauku ya dhati kusikiliza na kusoma habari toka vyombo rasmi vilivyokuwa vikimilikiwa na serikali kuliko ilivyo leo!
Ni katika enzi za Nyerere tu hata mwalimu wa kawaida wa shule ya msingi, seremala na mkulima wa kawaida waliweza kupata fursa ya kuchaguliwa kuwa viongozi hadi ngazi za ubunge. Tena ni katika utawala wake tu viongozi walimaliza utumishi wao na kurejea kama wananchi wa kawaida na si leo ambapo sifa ya mtu kuchaguliwa hata ujumbe wa shina ni kuwa na fedha bila kujali zimepatikanaje; na wanaoukwaa uongozi ndani ya chama huondoka wakiwa matajiri na kama wameuaga umasikini hata kwa ngazi za chini kama udiwani na Uenyekiti wa chama wilayani!
Wengi wanaomsakama Mwalimu wanafanya hivyo kwa msukumo wa chuki za kiitikadi; na idadi kubwa miongoni mwao kama faizafox ama walikuwa wadogo wakati wa utawala wake (kwa maana wameokoteza porojo za mitaani na kwenye vijiwe tu) au ( kwa wale wenye zaidi ya miaka 50 sasa) walipambana naye walipojaribu kufanya yanayofanywa na CCM hii ya sasa ambapo kila uhalifu ni 'ruksa'.
 
Mamndenyi said:
Mmezoea kudhulumu. Sheria gani ulitaka wewe. Nyerere aliandika katiba bila wasomi wengi imeongoza nchi hadi leo. Nchi imejaza wasomi lakini mmeshindwa hata kuedit katiba ili muweke hiyo misingi ya hizo sharia zako unazotaka.
Labda kwa sababu wasomi wa siku hizi hawatumii mabavu katika kukilinda kile wanachokiandika.
 
Kajifunze kuandika Kiingereza ndio uje nikuelewe una maanisha nini.

Huo ndio msingi uliowekwa na Nyerere. Hujuwi Kiingereza na nna uhakika hata Kiswahili hukijui.

Hapa ndio unadhihirisha ujinga wako. Kwani hapa ulileta mada ya Kiingereza bora na kibaya au ulikuwa unamzungumzia mtu Adili? Unaumwa kichwani wewe, jibu hoja, habari za Kiingereza achana nazo.
 
Hauna akili wala hujui kilichokufikisha hapo ulipo wewe uliyesoma bure na umeshindwa kufanya kitu chochote unamlaumu nyerere aliyepokea nchi ikiwa haina wasomi wakusaidiana naye. Hata watoto wako siku moja watakukana kuwa na mzazi mbumbumbu kama wewe copy chama
Mamndenyi
Hebu niulizie kwa huyu Red Giant ni kiongozi gani aliyemuona yeye amefaa sana maana naona matatioz ya kiuchumi ya nchi za kiafrika yanafanana na ukiangalia kwa undani watanzania tuna nafuu; pamoja na kulalamika eti Nyerere aliacha msingi mbovu lakini bado hatujaachwa sana; kwenye theory za uchumi sio kila ulichoinvest leo unakivuna kesho matunda mengine yanaonekana baada ya miaka 30
 
Last edited by a moderator:
chama pitia hapa ona wanaweza kuinua mdomo na vidole eti mwalimu alikosea.

Bado hawajesema nani aliyepatia maana tumeshapata maraisi 3 baada ya Nyerere; hizi ni chuki za kizandiki ukitaka kujua Nyerere alipatia mpaka leo hakuna raisi hata mmoja aliyethubutu kumsema Nyerere vibaya; zaidi kumpongeza; sasa hawa wafua chupi wasikuumize kichwa!
 
Nchi hii ilikosa misingi ya kuifikisha ipasapo ilipokabidhiwa madaraka ya kujiendesha yenyewe. Kumbuka, hatukupewa Uhuru, kwani mwaka 1961 tulikuwa hatutawaliwi.

Aliyeshindwa kuweka hiyo misingi imara ni Julius Kmabarage Nyerere. Jee, tumlaumu kwa kuwa alikuwa hana uzoefu wa kuongoza? au tumlaumu kwa kuwa alikuwa akiendeshwa na waliomuweka madarakani?

Nyerere alishindwa kuweka misingi imara na ndio maana kila alichokifanya nchini kikashindwa au alikuwa hajui kuwa kila alifanyalo ni kosa mbeleni? alikuwa hana muono?

Tujadili.

Mama FaizaFoxy
Kama hiyo misingi iliyoachwa ilikuwa mibaya kinasubiriwa nini kuivunja ili ijengwe misingi mipya? sasa hawa wenye maono wamefanya kipi cha ajabu; hivi baba yako akikuachia nyumba mbovu isio na msingi imara utaendelea kuitumia au utavunja na kujenga nyumba yenye msingi unaoutaka wewe?
 
Last edited by a moderator:
Wewe mwanamke FaizaFoxy nimpumbavu unaendeshwa na kuwashwa na udini! chuki za kijinga
zisizo na base wala misingi yoyote zaidi ya unafiki na ufedhuli kufanya uchochezi watu waanze malumbano yasiyo natija.[/QUOTE]

kaka wewe umesema ukweli. Hii hoja imejaa udini tu. Na laiti angejua kama kuna watu wanapaswa kumshukuru mwl Nyerere ni waislam. Kwani alitaifisha shule nyingi sana za mission za kikristu kuwa za kitaifa kitu ambacho kimesaidia hata waislamu msome. Maana kabla ya hapo wengine hawakusoma kwasababu shule karibu zote zilikua za dini ya kikristu
 
Last edited by a moderator:
Ukitaka kujua kuwa Mwalimu hakuna na marafiki angalia jinsi familia yake ilivyoachwa na mfumo hivi sasa. Hivi unadhani Nyerere angekuwa na marafiki mtu kama mama Maria Nyerere angeweza kudhurumiwa kiwanja?

Madingi wengi walioiga mfano wa Mwalimu wamestaafu hawana marafiki na wanaishi maisha magumu baada ya kutoka kwenye nafasi zao. Huo ndio ukweli wenyewe.
Si walikuwa wakilipwa mishahara kwa kazi walizokuwa wakizifanya? tena mikubwa sana kutokana na wakati wao!

Sasa kama walizembea katika matumizi yao kwa nini kodi ya Mtanzania asiyetimiza hata milo miwili kwa siku itumike kushughulikia upatikanaji wa kiwanja cha mtoto wa nyerere?

Tena kuna aliyemtaka waziri Taibajuka atumie muda wa kazi yake inayolipwa na mlipa kodi kushughulikia suala la kiwanja cha mtoto wa nyerere!
 
Nadhani mkuu una nafasi kubwa tu ya kusaidia nchi hii kutoka hapa ulipo. Katiba inakuruhusu kugombea hata uraisi ukatekelza maono yako. Sioni faida ya kumhukumu mtu aliyeondoka madarakani miaka 20 iliyopita. Marekani imejengwa ma maraisi mbalaimabli wala sio raisi mmoja. Huku kunaitwa kutojiamini kusingizia kuwa makosa yako ni sababu ya mtu fulani

Kidzude,

Hoja yako ni nyepesi sana mtu yeyote kwako anayekosoa na kuhoji utawala wa Nyerere unataka agombee urais, hii ni forum wanajadiliwa wengi tu kwa mazuri na mabaya yao.

Mkuu hata hao marais wa Marekani unaowatolea mifano kila mmoja anajadiliwa kwa kipindi chake.
 
Last edited by a moderator:
Nyerere kuwa Mtakatifu hivi karibuni wakina Fox wataombewa watoke mapepo ya udini, zambi ya umimi, ubaguzi na kudhuru mwili wa binadamu wenzio. Kuondoa kabisa kisiwa hatari cha waroho wa madaraka , kinyongo na atawaombea Maccm yaache kuingiza sembe kutafuta fedha za 2015
 
Kama nyerere alifanya makosa basi tuyarekebishe. Kwanini tulaumiane? Watz hatuipendi nchi yet Bali tunapenda vyama vyetu vya siasa.
Mama FaizaFoxy
Kama hiyo misingi iliyoachwa ilikuwa mibaya kinasubiriwa nini kuivunja ili ijengwe misingi mipya? sasa hawa wenye maono wamefanya kipi cha ajabu; hivi baba yako akikuachia nyumba mbovu isio na msingi imara utaendelea kuitumia au utavunja na kujenga nyumba yenye msingi unaoutaka wewe?
 
Last edited by a moderator:
Nyerere aliachia nchi mwaka 1985. Ni miaka 28 imepita mpaka sasa hivi. Alikuwa kiongozi wa nchi hii tangu mwaka 1961 au twaweza sema 1962. Kwa maana hiyo aliongoza kwa miaka 23. Sasa kama alifanya makosa kwa miaka 23, hawa waliomfuata wameshindwaje kuyarekebisha kwa hii miaka 28? Mnatumwa kumchafua huyu mzee bure na dhambi hii itawanyoosha in the future. Amewatunzia raslimali zenu na mpaka sasa mnazigawa bure kwa wageni na bado hatuoni mnachofanya. Kwa kuwa kama ni mabarabara yote mnakopa na mwisho wa siku ni sisi walipaji. Acheni kumnyanyasa huyu mzee. So far mnaenjoy amani ambayo ni matunda ya akili na busara zake. Stop it please.

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
sasa
hayo mapungufu unayotaka tuyataje na kufafanua(bila shaka unayajua) kwa
kuwa mwl hatunaye tena una maoni gani ili turudishe nchi yetu kwenye
mstari?
 
Hivi tangu uhuru si CCM ndo iko madarakani hadi sasa? Mnaanza kumsingizia marehemu? Kwani yeye ndo ameuza rasilimali za nchi? Yeye ndo anaua tembo? Yeye ndo amewaambia muuze unga? Yeye ndo amewaambia mtumwagie tindikali? Mtung'oe meno? Msafirishe wanyama hai? Mfiche pesa uswisi? Mnalaaniwe wenyewe kwa kulitafuta taifa chili lililokuwa na rasilimali tele.


(QUOTE=Ritz;7318548]Kidzude,

Hoja yako ni nyepesi sana mtu yeyote kwako anayekosoa na kuhoji utawala wa Nyerere unataka agombee urais, hii ni forum wanajadiliwa wengi tu kwa mazuri na mabaya yao.

Mkuu hata hao marais wa Marekani unaowatolea mifano kila mmoja anajadiliwa kwa kipindi chake.[/QUOTE]
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom