NYARAKA: Omar Nundu ni msafi...

NYARAKA: Omar Nundu ni msafi...

Hongereni sana nyote mlionaaccess ya nyaraka hizi maana sasa mmfenya macho yetu yaone.Muda wa ukombozi umefika.
 
Mkuu Mbona tumsikia hao kwenye wekundu ni NUSU ya bei ya hawa CCCC, hebu msihukumu kabla ya kujua mambo, iletwe proposal ya hao China Merchants nadhani ndio tutajua mbichi na mbivu, hivi hivi tutakuwa tunasema jambo tusilolijua.

Mkuu......Wizi ni Wizi tu........Uhuni ni Uhuni tu..........kuhujumu ni kuhujumu tu........HAKUNA kitu kinachoitwa kuhujumu/wizi/uhuni NUSU.............wananchi tumewapa dhamana ya uongozi hawa watu sio ili watuletee upuuzi/wizi/hujuma namna hii......halafu mijitu inayooneka imeenda shule na sifa kem kem........Waziri Nundu, Naibu wake, Katibu Mkuu wao......na maafisa wote (waliosaini barua) walioingia kwenye michongo hiyo ni wa kufukuzwa.....period.......
 
Ebanaee huyu Nundu asipojiuzuru watanzania tuandamane hadi magogoni. Hivi inakuwaje jamani? Mbona wenzetu walianzisha maandamano na wakafanikiwa kuziangusha serikali zao?
 
Katika documents zote hizi, nimeshangazwa na vitu vingi lakini kikubwa ni kimoja tu kinachosema;
Hapa ni dhahiri waziri Nundu alikuwa anataka kufaidika moja kwa moja na uwekezaji wa CMHI kwahiyo akaamua kuzungumza na hawa wachina wa CMHI peke yake bila kuwashirikisha wenzake serikalini, wizarani kwake na wizara ya fedha. Kama TICTS kuongezewa mkataba toka miaka 15 hadi 25 hatukubaliani na huo mkataba, Nundu anapata wapi guts za kuingia mkataba wa miaka 45 na wachina hawa?

Kwa ufupi tu ni kwamba hapa Nundu hawezi kupata pa kutokea pamoja na kumtupia mpira Naibu wake Mfutakamba. Kama wizara ya fedha na Bandari walikuwa wanafanya mawasiliano na Exim Bank kwa ajili ya kupata fedha za ujenzi wa gati hizo mbili, ilikuwaje waziri Nundu anafanya mawasiliano na CMHI bila kuwashirikisha wizara ya fedha??

Sasa nimefahamu kwanini waziri Nundu alikuwa anapingana na ushauri wa kamati ya POAC juu ya mawaziri kuyasimamia mashirika ya umma kwa utaratibu wa Eyes on Hands off!!

Ndugu yangu Mwita Maranya hiyo kitu ya eyes on hands off iko kwenye makaratasi tu; mawaziri wanaingilia hadi jikoni bila hivyo watakufa njaa.
 
Last edited by a moderator:
Endeleeni kumwaga nondo na mimi kesho nakuja na zangu!. Jee nani anajua hao CCCC walipatikanaje?. Jee kuna tenda yoyote ilitangazwa?!. Jee walijuaje TZ tunataka kupanua bandari?. Jee nani aliwapa kibali cha kufanya feasibility study?. Wangapi mnajua kuwa good practice ni feasibility study kufanywa na mwingine, funding kutafutwa kwa mwingine, construction company iwe nyingine na consultants ni wengine for checks and balance!. Jee ni wangapi mnajua feasibility study wanefanya hao CCCC, consultants ni wao wao CCCC wakaja na hiyo figure ya dola milioni 500 plus bila any independent verification na mkopo wakaomba hao hao CCCC kutoka Exim Bank?. Why?. Tangu lini unaomba mkopo alafu banker anakulazimisha usipofanya kazi na CCCC no mkopo!.

Mbona Mombasa wamejenga kwa 200 why sisi tujenge kwa 600?!.

Hivi mnajua kiburi na jeuri ya Mfutakamba inatoka wapi?. Mnamjua nani anampa ruhusa kwenda kuhongwa huko nje huku akimby pass boss wake?!. Nnajua aliandika recomendation ya kuifagilia CCCC na kuisubmit wapi bila kumuonyesha waziri?. Amini nawaambieni hao CCCC ni yule yule RA!. Kama Richmond tuu ila this time sio US ni China!. Hivi mnanuamini Serukamba?!. Mnaamini ni yeye ndie aliyeomba kuwa M/Kiti wa Kamati ile?. No amewekwa kama alivyo pewa ubunge!. Yeye ni remote tuu ya RA!.

Endeleeni kumwaga mboga kesho na sisi tunamwaga ugali wakose wote!. Kusema ukweli napandwa na hasira sana mpaka natamani nchi hii tungekuwa kama China, mafisadi wana kula bullets soonest possible na kusahaulika!.

Mchukua Nundu na Mfutakamba uwapime nani fisadi na nani sio!. Tatizo la ufisadi ni kubwa kuliko nilivyodhania maana mpaka humu jf vibaraka wao, wametamalaki sana!.

Mungu Ibariki Tanzania!. Nawahakikishia kama 2015 Watanzania wataamua kufanya kweli, kuna wenzetu humu humu watatafuta pa kutokea maana kwao pia ni kilio na kusaga meno!.

Mkuu Pasco jana nilikuona ulipokuwa unamshauri Mh. Nundu kabla hajaanza kuongea na waandishi wa habari.. Ungemsaidia kama ungemshauri atangaze kuachia ngazi kwanza.. Halafu baadae atoe dukuduku lake na kuweka kila kitu wazi.. Kwa kusema kile alichokisema jana watu wengi watakuwa na shaka na credibility yake.. Watakachoona ni yeye kujaribu kupambana kubaki na uwaziri..
 
kila siku wanasafiri nje kumbe nchi ishauzwa hii...nundu anamtupia mpira naibu wake
 
Mkuu Kobelo, kwenye mikataba kuna mikataba inaitwa void na voidable, mkataba ukishakuwa void unaitwa "void ab initio" wakimaanisha hakuna mkataba hivyo kila mtu inakula kwake!.

Tatizo hapa ni hawa CCCC walikujaje mpaka kupata hiyo MOU?. Ikumbukwe MOU sio contract!.

Kwani MoU iliyowekwa hapa JF ni ya CCCC au CMH?
 
ama kwa hakika watanganyika bado tunasafari ndefu sana, ikiwa viongozi wetu wanauza ardhi yetu na rasilimali zetu kwa vipande vya nguo na juice ya machungwa toka south afrika ilihali zinapatikana hata bahresa.
 
Kwa ushahidi wote huu, maamuzi ya msingi yasipochukuliwa basi nitaconfirm kuwa serikali hii inahitaji uongozi wa wananchi kwa sasa ili kurekebisha mfumo ulipo.
 
quote_icon.png
By Pasco

Endeleeni kumwaga nondo na mimi kesho nakuja na zangu!. Jee nani anajua hao CCCC walipatikanaje?. Jee kuna tenda yoyote ilitangazwa?!. Jee walijuaje TZ tunataka kupanua bandari?. Jee nani aliwapa kibali cha kufanya feasibility study?. Wangapi mnajua kuwa good practice ni feasibility study kufanywa na mwingine, funding kutafutwa kwa mwingine, construction company iwe nyingine na consultants ni wengine for checks and balance!. Jee ni wangapi mnajua feasibility study wanefanya hao CCCC, consultants ni wao wao CCCC wakaja na hiyo figure ya dola milioni 500 plus bila any independent verification na mkopo wakaomba hao hao CCCC kutoka Exim Bank?. Why?. Tangu lini unaomba mkopo alafu banker anakulazimisha usipofanya kazi na CCCC no mkopo!.

Mbona Mombasa wamejenga kwa 200 why sisi tujenge kwa 600?!.

Hivi mnajua kiburi na jeuri ya Mfutakamba inatoka wapi?. Mnamjua nani anampa ruhusa kwenda kuhongwa huko nje huku akimby pass boss wake?!. Nnajua aliandika recomendation ya kuifagilia CCCC na kuisubmit wapi bila kumuonyesha waziri?. Amini nawaambieni hao CCCC ni yule yule RA!. Kama Richmond tuu ila this time sio US ni China!. Hivi mnanuamini Serukamba?!. Mnaamini ni yeye ndie aliyeomba kuwa M/Kiti wa Kamati ile?. No amewekwa kama alivyo pewa ubunge!. Yeye ni remote tuu ya RA!.

Endeleeni kumwaga mboga kesho na sisi tunamwaga ugali wakose wote!. Kusema ukweli napandwa na hasira sana mpaka natamani nchi hii tungekuwa kama China, mafisadi wana kula bullets soonest possible na kusahaulika!.

Mchukua Nundu na Mfutakamba uwapime nani fisadi na nani sio!. Tatizo la ufisadi ni kubwa kuliko nilivyodhania maana mpaka humu jf vibaraka wao, wametamalaki sana!.

Mungu Ibariki Tanzania!. Nawahakikishia kama 2015 Watanzania wataamua kufanya kweli, kuna wenzetu humu humu watatafuta pa kutokea maana kwao pia ni kilio na kusaga meno!.

Mkuu kwanza tunasubiri doccuments na nondo za utetezi wa mambo anayoyafanya Nundu, ikiwa ni pamoja na kujiumbua kwa waandishi wa habari na kitendo cha yeye kushindwa kusema na kuwasilisha docs kwenye kamati. Lakini pili, hakuna kibaraka humu na pengine usiwe kama huyo waziri wewe ni mtu unayeheshimika sana katika jamii, usihukumu watu, humu watu wanataka data na doccuments ambazo tunasubiri za kujibu hizi zilizopo si maneno tu, ambayo yeyote anaweza kuyasema. Maneno kama "nani alimpa ruhusa kwenda kuhongwa" yanahitaji kubebwa na ushahidi wa kutosha maana ni tuhuma nzito kutolewa na Waziri dhidi ya Waziri mwenzake. Kama Mfutakamba amehongwa anastahili kushitakiwa na Nundu asaidie Takukuru (japo haina meno) kumshitaki Naibu wake na Naibu naye kama ana data (hajawahi kusema) naye asaidie dola kumshughulikia Nundu. Hapa hakuna anayebebwa katika mawaziri wala watendaji wako wa serikalini na mashirika yao yanayomeza fedha za umma kila kukicha.

Jambo linalonifurahisha ni kauli yako kwamba kuna mkono wa RA na kwamba Serukamba amewekwa madareakani na RA.... Ukweli ni kwamba kama ni mkono basi si wa RA bali ni EL ambaye ndiye mtu wa Serukamba na nimefurahi pia kusikia kutoka kwako kwamba hii kashfa ya bandari ni zaidi ya Richmond!! Kumbe Richmond ilikuwa kashfa? Kumbe EL na RA hawakuonewa kuwa ni magamba? Naona hapa tuko pamoja, na kwa kweli kama Mfutakamba na yeyote awe Nundu ama nani, wakihusika na ulaji, hakuna wa kubaki wote waondoke. Pia tusaidie kutuambia, taratibu zinasemaje Naibu Waziri ama Waziri akisafiri anamuaga nani? baada ya hapo ndio tuangalie kama kweli alikosea ama la?

Pia, nadhani Nundu asikwepe kama anataka atuambie pia na Dk. Kawambwa naye amekula fedha ili list iwe ndefu na Mkulo naye amekula kwenye hili la Bandari, hakuna kuuma maneno na wote kama wanahusika waache "wafu wazike wafu wenzao" tusimtetee mtu hapa, lakini pia tusifanye ukasuku, tumwage data na ushahidi, wa wazi. Nundu alete hapa hiyo LAPTOP yake aliyoingia nayo katika kamati akasema hana Doccuments. Tuache kushambuliana binafsi tujenge HOJA kwa HOJA, wezi wang'oke tu.
 
Hivi wakuu kwani hata mipango ya serikali kwa ajili ya maendeleo ni SIRI? mbona naona barua zote zimegongwa mihuri "secret" au ndo michezo michafu imetawala hata kwenye miradi ya maendeleo?
 
Ni ajabu kwelikweli namna mambo yanavyokwenda kwenye wizara hizi, ukiziangalia kwa makini unagundua kuwa barua hizi zinatakiwa ziwe zimetoka kwenye taasisi mbili tofauti ambazo zinafanya kazi moja (moja, ya Nundu, inaonyesha kuegemea CMHI na nyingine ya "Futakamba?" inataka mradi huo utekelezwe na CCCC na pia serikali itoe dhamana na mradi huu).

Kwa haraka haraka utaona kuwa mradi wa Nundu una unafuu zaidi kwa serikali ingawaje hakuna taarifa zinazoenyesha gharama kuweza kuthibitisha maoni yangu. Wenye taarifa za gharama za miradi hii miwili (CMHI na CCCC) watusaidie ili tuweze kuchangia tukiwa na taarifa sahihi
 
Kumbeee....sasa nimejua ni kwanini staff wa TPA wanatanua sana hapa jijini: magari ya bei mbaya, wanaburudika na whisky za bei mbaya, wanachukua vimwana vya uhakika, kwao kwenda UK na Dubai ni kama kwenda Kariakoo, kwa ujumla wanatisha kwa pesa. Miaka 45 ni ili wanao na wajukuu waendeleze matanuzi. This is too much now, bora wavuliwe gamba!
 
Kuna vitu nilikuwa sitaki kuzungumza humu: Kwanza nikufahamishe kwamba mimi nimesoma Uingereza na nimekaa huko zaidi ya miaka saba, nimefanya kazi na Wachina zaidi ya miaka kumi na ushee kwa hiyo najua Modus Operandi ya Wachina wa siku hizi, la tatu Mh.Nundu anijuhi na wala sijawahi kukutana naye; mambo mengine hayaitaji kusomea mambo ya sayansi ya roketi kutambua ni akina nani wanao pania kunufaika na mradi huu mzima by hooks and crooks wana inflate thamani ya mradi husika wanafikili hatuna akili.

Analytical mind ya kawaida tu inakudhilihishia wazi ni nani ana Uzalendo wa kweli kati ya Mh.Nundu na group lililo mkalia kooni kwa kutaka kichwa chake - hivi mzalendo wa kweli anaweza kuafiki mkataba ambao huko open ended bila kuwa na check and balance, mpaka Dogo Mnyika alipo nusuru jahazi na Mh. Nundu kuhafikiana naye, unataka kutueleza kamati hilo walikuwa awalioni!!!!!! Alafu muadishi wa post hii amekasirika as if naye anafanya kazi wizarani-WHY?

China kuna makampuni lukuki ambayo ni mahili katika mambo ya ujenzi, why pick CCCC; kampuni ambayo inazunguka zunguka tu hapa Tanzaini kufanya lobbing na ku-exploit weakness za wazalendo wasiokuwa na uaminifu - kwa nini awakai kwao wakasubiri atima ya tenda yao, some Chines are very cunning; waulize TTCL ilivyo ingizwa mkenge kwa kushikizwa na Wachina kwenda mfumo wa CDMA wakati makampuni yote ya simu nchini ni GSM.

Mwisho nataka kuwaelezeni kwamba ni mara chache ma-injinia kujihingiza katika mambo ya ajabu ajabu-wao wanalidhia kuona projects zao zina take off na kukamilika na kuona zinafanya kazi kama walivyo kuwa wanafikilia, mambo ya pesa na hujuma ni secondary kwao. Mimi namuomba Mh.JK ampe rungu Mh.Nundu a-deal na watu hawa kwa nguvu zake zote bila kuogopa mtu yeyeyote-Watanzania wengine wamekubuhu katika kufanya mambo ya fitina, uzushi na kuaribiana sifa na hii ndiyo inayofanyika katika Wazari hii, Waziri asipokuwa makini anaweza kuyumbishwa sana - chain of command aziheshimiwi hata kidogo.

Mh Nundu futilia mbali mambo ambayo unayaona hajakaa sawa na umuombe mweshimiwa Raisi afanye mabadiriko makubwa kwenye Wizara hii nyeti, asihishie hapo hata TPA wanapashwa kushughulikiwa. Nataka nimkumbushe Mh.Nundu kwamba wewe ndiye umepewa dhamana ya ku-run Wizara kwa hiyo don't you be wobbly au kuwa-controlled remotely, historia ndiyo itakuhukumu. Just read between the lines kwa huyu anayenipinga humu ndiyo utajua unakazi ya ziada-wamejipanga kweli kweli. Mungu akulinde.

Well said mkuu!
 
Nundu na wenzake wote wamenasa katika mtego mmoja,...waondoke,..hatutaki kusikia utetezi:doh:

Mwalimu alijenga berth zote 12 pesa alitoa wapi?, yaani leo nchi hii inashindwa hata kujenga hizo berth mbili tu?:A S shade:
 
Back
Top Bottom