NYARAKA: Omar Nundu ni msafi...

NYARAKA: Omar Nundu ni msafi...

Hivi inawezekana JK kwake habari nzito ni kwenda kuzika a Dead body Bingu wa Mutharika kuliko hii, bado siamini kama JK pamoja na udhaifu wake mwingi bado atakuwa amefanya kosa hili.

Si unakumbuka ile ya Kanumba, kuna safari aliahisrisha tena
 
Hizi barua hazimsafishi Nundu bali inaonyesha kuwa alikuwa ana kaurafiki haramu na hii kampuni ya China Merchants Holdings nje ya njia zinazokubalika yaani kiofisi maana hawa wanaonekana hawafuati njia sahihi zinazotakiwa kufuatwa na kampuni bali wanatumia kiongozi mla rushwa/mlafi kama Omar Nundu kuipiga bao kampuni ya China Communications construction Ltd ambayo tayari proposal yake imekubalika na imeshapata fedha toka Exim Bank China! Sasa sijui ni punda gani anaweza kuacha mradi ulioiva namna hiyo wa China Cummunications Construction Ltd akaenda kwa huu wa China Merchants Holdings ambao haujasema ni kiasi gani ita-finance huo mradi na kwa riba kiasi gani! hapa simply hii barua inaonyesha jinsi mawaziri wetu vilaza walivyo tayari ku-take risky decisions na ku-subotage miradi mikubwa ya maendeleo ili mradi tu wamehakikishiwa kushibishwa matumbo yao na miradi fake inayokosa transparency bali kupitia kwa vimemo viinavyoweza kui-cost nchi kama mikataba ya umeme ta Tanesco! Omar Nundu lazma ajiuzulu manina.....!

umeandika kichuki chuki mno bila kuzingatia hoja za msingi.
 
hizi barua hazimsafishi nundu bali inaonyesha kuwa alikuwa ana kaurafiki haramu na hii kampuni ya china merchants holdings nje ya njia zinazokubalika yaani kiofisi maana hawa wanaonekana hawafuati njia sahihi zinazotakiwa kufuatwa na kampuni bali wanatumia kiongozi mla rushwa/mlafi kama omar nundu kuipiga bao kampuni ya china communications construction ltd ambayo tayari proposal yake imekubalika na imeshapata fedha toka exim bank china! Sasa sijui ni punda gani anaweza kuacha mradi ulioiva namna hiyo wa china cummunications construction ltd akaenda kwa huu wa china merchants holdings ambao haujasema ni kiasi gani ita-finance huo mradi na kwa riba kiasi gani! Hapa simply hii barua inaonyesha jinsi mawaziri wetu vilaza walivyo tayari ku-take risky decisions na ku-subotage miradi mikubwa ya maendeleo ili mradi tu wamehakikishiwa kushibishwa matumbo yao na miradi fake inayokosa transparency bali kupitia kwa vimemo viinavyoweza kui-cost nchi kama mikataba ya umeme ta tanesco! Omar nundu lazma ajiuzulu manina.....!

hatuwezi kutaka mtu ajiuzulu kwa sababu tunataka ajiuzulu. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kipi bora? Cccc mradi wao ni zaidi ya b500 na hao wengine ni kama b300. Sasa ata kama nundu anapata chochote atakuwa ameokoa kiasi gani?
 
Habari inasikitisha tuu, yeye alikuwa wapi kumlipua naibu wake kabla ya sakata hili? Wote ni walewale hawezi kujitoa kabisa, Kuhusu uwezo Kuchagua kwa urafiki nafasi za kiutendaji zina madhala

hajamlipua ila ameeleza ukweli kwamba hakuna ujanja ujanja ktk hii skendo bali utaratibu umefuatwa
 
Nundu hachomoki hapa, amepata hasira baada ya wajanja Chambo na Mfutakamba kumzunguka, ukitaka kumjua Chambo muulize Magufuli, alitoa sharti la Chambo kutoka ujenzi kabla ya kuingia ofisini ndo akapelekwa kwa Nundu, Chambo ni kati ya Mkatibu bilionea hapa Tz tena kwa kupitia hio mikataba fake au ya ufisadi.

Hakuna cha nini hapo, hii wizara lazima isafishwe, kuanzia katibu, naibu na Nundu mwenyewe.
 
Sijapenda habari za kutoa bandari rehani kwa miaka 45.
Aisee hii kali. Maana hata miaka hamsini ijayo ya uhuru bado hawa jamaa watakuwa manamiliki hizi gati mbili na Wakati huo Malindi na Mombasa port zitakuwa kali sana na ktuacha sisi hatuna kitu kabisa. Wenyewe hawa hawajali mradi wachukue chao sasa hivi bomu litakuja kuwapasikia wajukuu zao.
 
huu ndio mwisho wa CCM! CCM inafikia mwisho, inakufa kabisa na itabaki historia. CCM haifai watanzania, chonde chonde watz tuikatae CCM

sasa hapa CCM inaingiaje mkuu?kosa la wawili watatu sio kosa la chama chote..mwenyekiti wa chama lazima alishughulikie ili swala na watu watawajibishwa na chama kitasonga mbele zaidi.
 
Katika documents zote hizi, nimeshangazwa na vitu vingi lakini kikubwa ni kimoja tu kinachosema;
Party A, hereby exclusively engages party B to develop berths no.13 and 14 of Dar es salaam port on a 45 years BOOT(Build, Own, Operate and transfer) basis ["the project"]
Hapa ni dhahiri waziri Nundu alikuwa anataka kufaidika moja kwa moja na uwekezaji wa CMHI kwahiyo akaamua kuzungumza na hawa wachina wa CMHI peke yake bila kuwashirikisha wenzake serikalini, wizarani kwake na wizara ya fedha. Kama TICTS kuongezewa mkataba toka miaka 15 hadi 25 hatukubaliani na huo mkataba, Nundu anapata wapi guts za kuingia mkataba wa miaka 45 na wachina hawa?

Kwa ufupi tu ni kwamba hapa Nundu hawezi kupata pa kutokea pamoja na kumtupia mpira Naibu wake Mfutakamba. Kama wizara ya fedha na Bandari walikuwa wanafanya mawasiliano na Exim Bank kwa ajili ya kupata fedha za ujenzi wa gati hizo mbili, ilikuwaje waziri Nundu anafanya mawasiliano na CMHI bila kuwashirikisha wizara ya fedha??

Sasa nimefahamu kwanini waziri Nundu alikuwa anapingana na ushauri wa kamati ya POAC juu ya mawaziri kuyasimamia mashirika ya umma kwa utaratibu wa Eyes on Hands off!!
 
hatuwezi kutaka mtu ajiuzulu kwa sababu tunataka ajiuzulu. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kipi bora? Cccc mradi wao ni zaidi ya b500 na hao wengine ni kama b300. Sasa ata kama nundu anapata chochote atakuwa ameokoa kiasi gani?
Mkuu mpingauonevu,

Nakubaliana na wewe. Tuna ugonjwa mmoja waTanzania, kuhukumu kwa kutumia mahakama ya magazeti. Watu hawataki kusikia kitu kingine zaidi ya waziri kujiuzulu.

Hatuwezi kutumi mass ku-determine haki ya mtu. Waziri Nundu ni msafi, nimejiridhisha hivyo. Maelezo yake yamethibiti hivyo,ushahidi unaonesha hivyo. Kwa nini mnataka kuaminisha kila mtu ku-rely kwenye taarifa za magazetini na wanasiasa uchwara,wasioweza kujenga hoja juu ya misingi ya haki na uadilifu.

Hakuna mantiki ya Waziri Nundu kujiuzulu, hana kosa la kumfanya ajiuzulu. Wengine siwezi kuwasemea. Haki lazima ifuatwe hata kama anayepewa hatumpendi.
 
Kwa nini hizi nyaraka zimegongwa mhuri wa SECRET? Serikali inaficha nini wakati wananchi ndio watalipa huo mkopo?
 
quote_icon.png
By Geza Ulole

Hizi barua hazimsafishi Nundu bali inaonyesha kuwa alikuwa ana kaurafiki haramu na hii kampuni ya China Merchants Holdings nje ya njia zinazokubalika yaani kiofisi maana hawa wanaonekana hawafuati njia sahihi zinazotakiwa kufuatwa na kampuni bali wanatumia kiongozi mla rushwa/mlafi kama Omar Nundu kuipiga bao kampuni ya China Communications construction Ltd ambayo tayari proposal yake imekubalika na imeshapata fedha toka Exim Bank China! Sasa sijui ni punda gani anaweza kuacha mradi ulioiva namna hiyo wa China Cummunications Construction Ltd akaenda kwa huu wa China Merchants Holdings ambao haujasema ni kiasi gani ita-finance huo mradi na kwa riba kiasi gani! hapa simply hii barua inaonyesha jinsi mawaziri wetu vilaza walivyo tayari ku-take risky decisions na ku-subotage miradi mikubwa ya maendeleo ili mradi tu wamehakikishiwa kushibishwa matumbo yao na miradi fake inayokosa transparency bali kupitia kwa vimemo viinavyoweza kui-cost nchi kama mikataba ya umeme ta Tanesco! Omar Nundu lazma ajiuzulu manina.....!
umeandika kichuki chuki mno bila kuzingatia hoja za msingi.

Mkuu Tamuchungu,
Nakubaliana na wewe. Tuna ugonjwa mmoja waTanzania, kuhukumu kwa kutumia mahakama ya magazeti. Watu hawataki kusikia kitu kingine zaidi ya waziri kujiuzulu. Hatuwezi kutumia mass ku-determine haki ya mtu.

Waziri Nundu ni msafi, nimejiridhisha hivyo. Maelezo yake yamethibiti hivyo, ushahidi unaonesha hivyo. Kwa nini mnataka kuaminisha kila mtu ku-reply kwenye taarifa za magazetini na wanasiasa uchwara, wasioweza kujenga hoja juu ya misingi ya haki na uadilifu kuliko maelezo ya mtu tunayemtuhumu?.

Hakuna mantiki ya Waziri Nundu kujiuzulu, hana kosa la kumfanya ajiuzulu. Wengine siwezi kuwasemea. Haki lazima ifuatwe hata kama anayepewa hatumpendi.
 
hoja ya zitto itasikilizwa Mchana baada ya Hoja ya Kamati za Kilimo na Maliasili...
 
hatuwezi kutaka mtu ajiuzulu kwa sababu tunataka ajiuzulu. Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Kipi bora? Cccc mradi wao ni zaidi ya b500 na hao wengine ni kama b300. Sasa ata kama nundu anapata chochote atakuwa ameokoa kiasi gani?

Usilolojua sawa na usiku wa giza!!

Nundu anajaribu kuhalalisha ujinga, hiyo bei anayosema imetoka wapi? Nani amefanya upembuzi? Hiyo ni zuga ili kuvuruga huo mradi na ndio lengo lake. Hizi docs zinaonyesha jinsi alivyojikanyaga! Aliwaambia waandishi kwamba hajaileta hiyo Chinese Merchant, hapa tunaona walivyo na mahusiano binafsi! Alisema wizara yake haijahusishwa kwenye mkopo wa Exim, hapa tunaona wizara yake ilivyohusika!!

Kibaya zaidi ni jinsi alivyokuwa akiwapa siri hao Wachina wake!! Wachina wake wanazungumzia barua ya Wizara ya Fedha na wanaonyesha kutaka wenzao waondolewe!! Hapa anawezaje kujiona yeye msafi?

Tusiwe wavivu tutafakari Nundu ni mwizi na amekula rushwa ndio maana anataka kuaminisha umma kwamba wenzake wote wamekula!! Kama anatuhumu Naibu kula kwa mradi wa 2008 wakati ameingia 2010, yeye anasalimika vipi na mradi mpya?
 
Huyu nundu hakwepi hili baada ya kuona project imesaniwa na hakupewa 10% ndo anaanza kuzungumza kuwa kampuni zishindanishwe upya.

Kwanza kuna ugomvi kati yake na naibu wake mfutakamba yote haya ni ulafi wa 10%, pia he isn't competent kuongoza hii wizara na pengine wizara, jimbo lake huko kalitekeleza aondoke fisadi mkubwa, kama ndo alivyopanga kufanya wizi na aliyemteua basi washindwe na wewe aliyekupa barua umpigie debe hovyo.

Hizi barua huwa watz wakizihitaji wanasema ni siri za serikali ila kwa sababu amekosa pakuchomokea anazitoa ili mumsaidie shame up on...
 
Mkuu Tamuchungu,
Nakubaliana na wewe. Tuna ugonjwa mmoja waTanzania, kuhukumu kwa kutumia mahakama ya magazeti. Watu hawataki kusikia kitu kingine zaidi ya waziri kujiuzulu. Hatuwezi kutumia mass ku-determine haki ya mtu. Waziri Nundu ni msafi,nimejiridhisha hivyo. Maelezo yake yamethibiti hivyo,ushahidi unaonesha hivyo. Kwa nini mnataka kuaminisha kila mtu ku-rely kwenye taarifa za magazetini na wanasiasa uchwara,wasioweza kujenga hoja juu ya misingi ya haki na uadilifu kuliko maelezo ya mtu tunayemtuhumu?. Hakuna mantiki ya Waziri Nundu kujiuzulu, hana kosa la kumfanya ajiuzulu. Wengine siwezi kuwasemea. Haki lazima ifuatwe hata kama anayepewa hatumpendi.

We soma nyaraka uelewe, hapa hakuna cha magazeti, Nundu ndiye anataka kutumia magazeti kujinusuru. Ameshindwa kujitetea katika Bunge, na Kamatu ya Bunge, ameshindwa kuongoza Wizara hadi anatofautiana na Bodi za mashirika yake, ameshindwa hata kujieleza anaanza kutuhumu kiila mtu! Huyo Nundu hafai anajikanyaga tu! Soma kwa makini utaona
 
Back
Top Bottom