Nitajie tarehe yako na ya mwenza wako nikwambie mpo vipi na hatima yenu, siri yake n.k

Mimi me 30/10
Yeye ke 1/1
Wewe ni Maji ya moto na yeye ni mchanga wa pwani;
Hisia zako zote kali na zenye nguvu hukaribishwa na kutulizwa hapa. Wewe ni maarufu kwa kuwa mtata sana kwenye mapenzi unagubu ambalo si rahisi kuonekana wazi lakini kadri unavyozidi kuwa na huyu mwenzio ndivyo atakavyozidi kukutuliza kwa maana ana asili ya utaratibu na kumezea mambo mengi na vile vile yeye ni mtu mzazi sana vile vile matukio yake ya kusisimua hukufanya kuwa ni mwenye kuvutiwa nae zaidi na kufanya uhusiano wenu uwe na huba ndani yake kwa maana yeye pia huvutiwa na hupenda tabia yako ya kumuonea wivu japo anaweza kukuthibitishia hilo au kisiri ambalo hili humfanya ajihisi yupo kwenye mahusiano ya kueleweka na kujihisi analindiwa mapenzi yake.
Nyote wawili mnahusiana vizuri na mnaonekana ni wenye kuwa na mtizamo mmoja linapokuja suala la kimtizamo.
kwa maana nyinyi ni wenye tamaa moja, nia moja na mtizamo mmoja mnapoingia kindoa na kuwajibika pamoja kila mtu kwa nafasi aliyopo mna nafasi kubwa ya kufanikiwa kindoa kuliko uhawara hata mafanikio ya kiuchumi kubwa tu mnatakiwa kushirikishana na kuwa wawazi kila mtu kwa mwenzio ukifanya kitu usimfiche vile vile na yeye.

Rakims
 
Mkuu Rakims;

Mimi ni mwanaume, jina langu linaanzia na herufi N, nimezaliwa tarehe 22/12.

Huyu ni mwanamke natarajia kumuoa, jina lake linaanzia na herufi W, amezaliwa tarehe 29/11.

Aminia sana mkuu!..
 
Habari zenu wana ndoa na wenye ndoto za ndoa,

Yawezekana umewahi kusikia kauli maarufu sana inasema;
"Kosea yote usikosee ndoa"

Katika thread hii nitakupa maana halisi na siri iliyojificha nyuma ya kauli hiyo hivyo ukiweza kunitajia tarehe yako na ya mwenza wako na herufi zenu za mwanzo,mchumba,mpenzi na mwanandoa nitakupa taarifa zako na zake na siri zake kimapenzi hivyo utakachojua hapa ni kitu kitakachokusaidia kuimarisha mahusiano yenu au kuyaharibu kabisa.

View attachment 2185484

Yafuatayo nitakutajia;
  • Tabia zake
  • Sehemu yake ya hisia
  • Jinsi ya kumfanya azidi kuwa karibu na wewe
  • Mtizamo wake kwako
  • Mtizamo wako kwake
  • Unachopenda akufanyie
  • Udhaifu wake
  • Na vingine vya ziada
MATOKEO:
Kwa asilimia 90 nitakayokwambia ni ya kweli kama sivyo basi kuna mmoja kati yenu alidanganya tarehe kwa mwingine,

MFANO WA KUANGALIZIWA
Ili niweze kukuangalizia vizuri andika hivi;

Mimi mwanaume Jina langu (Herufi ya kwanza);
Nimezaliwa tarehe: 14 December mwaka
Mwezi wangu Jina lake (Herufi ya kwanza)
Kazaliwa tarehe: 24 April mwaka

(Kisha unaweza kusema upande gani nikazie zaidi japo sio lazima)

MEMBER WA KWANZA
Ke 24/4 P

Me 14/12 E

Matokeo yake:

MTIZAMO WAKO KWAKE;

Wewe ni mtu mwenye tabia za maji na yeye ni mtu mwenye tabia za udongo kwa mjumuiko huu unaonyesha kabisa nyinyi kuendana ni vigumu na hata kama mnapendana vipi itakuwa dhoruba tu ndani.

Kwa mtizamo anaonekana yeye ni mtu wa kupenda utawala na ukubwa kwa kuongoza mambo/kupelekesha- ambapo wewe unaonekana sio mtu wa kupelekeshwa na hautakubali hilo.

Pia, wewe ni mtu wa kuhitaji mabadiriko,anuwai,matukio ambapo hayo humfanya yeye kujihisi tofauti na wewe kwa kuwa yeye ni mtu wa ambaye hujifanya ni mjuaje na incharge wa mambo yanavyokuwa yanakwenda katika miliki yenu na kujiona ni mtawala mzuri wa tabia za nyumbani na hujiona ni mwenye hekima na heshima na imani zaidi kuliko wewe. Yeye anakuwa ni mtu wa kutaka kufanya mambo ambayo teyari yana uhakika na kutaka kufanya mambo yenye uhakika, wakati wewe unakuwa upo teyari kufanya chochote kinachowezekana.

Na pia wewe ni mtu wa kusema chochote kinachokujia na nimtu wa kumdondoshea maneno tu randomly yanayokujia kichwani kwa fikra yako ambayo humfanya kuanza kujawa na hasira taratibu. Pia kuna tatizo la pesa katika mahusiano yenu, hiyo ni sababu wewe unataka kuzalisha pesa kwa yanayowezekana leo hali ya kuwa yeye anawaza kuhusu mambo ya kesho (ukifa unaniachaje). Mna muda mfupi sana kwenye mahusiano yenu.

MTIZAMO WAKE KWAKO:
Mapenzi yenu yanaweza kwenda kama tu ataweza kujikaza vizuri kuwa na wewe au kukuvumilia kwa maana mtizamo wake kwako wewe ni mtu ambaye huvumiliki. wote mnavutiwa zaidi kwa muonekano wa mwenzi wake, kwa tamaa zake yeye alizonazo katika kufanya tendo anakuwa anavutiwa zaidi na ufanyaji wako.

Lakini ni mtu inamuwia ugumu katika kuvumilia tabia yako ya kupepesa macho na kutizama mambo mapya(wanawake wa nje) wewe ni mtu wa kuchukulia kila jambo poa poa na rahisi rahisi inapokuja katika maswala ya mahusiano na tendo la ndoa wakati yeye ni mtu muda mwingi anataka kuwa serios kwenye mahusiano na kutawala. hali ya kuwa wewe ni mtu ambaye hutaki kutawaliwa kimapenzi na mtu yoyote hakuna baya kwenu lakini ni watu wenye kupishana mara kwa mara uhawara kwenu inakuwa ni starehe kuliko ndoa. maana mnaweza kukaa kwenye uhawara miaka ila mwezi tu ndoa ikawa ndoana.

Mahusiano yenu ya ndoa yatakuwa ni vichekesho tu.

SEHEMU ZAKE ZA HISIA:
Sehemu zake za hisia ni shingo na koo ndio maeneo ambayo kuna hisia zake kubwa za kiwazimu ikiwa;- utagusa eneo hilo,kumbusu na kutomasa eneo hilo hata kama umekaa nae basi utampandisha kwa kasi sana hisia zake na hasa ukiwa umekaa karibu nae ukawa unamgusa hapo chochote unachosema kinaingia kwenye akili yake na roho yake moja kwa moja kuhusu wewe.

Ukimbusu eneo hilo vizuri na kumng'ata kichokozi akiwa kalala chali na kwenye koo lake basi utaona maajabu. Fanya mbinu hii pia itakuongezea umaarufu kwake. Mfanyie massage hii ili kuweza kumfanya siku yake yote ajihisi yupo kwenye raha:

(1)Akiwa kalala kwa mgongo wake muwekee mitetemo kwenye shingo yake karibu na mizunguko ya masikio yake kwa kutumia vidole vyako tumia miondoko ya taratibu sana kwa maana sio punda huyu kama kina fulani huyu anataka vitu sensitive rudia hivyo hadi uone vipele vimesimama kwenye mikono yake. (Be very gentle kuzunguka sehemu ya pipe za hewa kwenye shingo vinginevyo utamniga).

(2) Kumbuka ni mtu mwenye kupenda zaidi kufanyiwa hivyo akiwa kalala kwa tumbo lake hivyo fanya hivyo hadi kukaribia eneo la muunganiko wa uti wa mgongo lakini usitoke nje ya shingo maana umeme utakatika halafu ataona unamtembezea wadudu.
Ukianza kuona vinyweleo vimesimama na vipele basi jua chini hali si shwari wacha niishie hapa na Ramadhan hii nisije nikafanya mambo magumu masaa yamebaki machache.

Ikiwa utamgusa au kumfanyia manjonjo sehemu za shingo yake basi ni mtu mwenye kupata hisia za kiwazimu na wewe ikiwa atajua kucheza na mapaja yako yako basi ataweza kukupeleka mbali sana kihisia hisia zako siwezi kukwambia sana kwa maana wewe unamtizamia yeye.

UTAMVUTIA VIPI:-
Yeye kwanza sio mtu wa papara ni mtu anapenda kama ni utafiki ama mahusiano basi yaanze taratibu kama vile unajenga nyumba mapenzi kwake anataka uanzie msingi kwanza hivyo inakutaka kuwa ni mtu mwenye subira kuweza kummudu kimapenzi na subira wewe muda mwingine ni kitu huwa,

Mbinu;
kwanza kabisa kama ndio unaanza nae basi hakikisha kuwa unakuwa ni mtu wa kwanza kumtafuta na usiende nae kwa pupa kama hujagusa katika kujifanya ni mtu mwenye subira sana basi moja kwa moja hutampata kwa maana kama ni wa dada wazamani huyu atakwambia nisubiri miezi 9 nikufikirie.

Muonyeshe kuwa upo radhi kuwepo muda wote pale anapokuwa anakuhitaji na ujionyeshe kuwa wewe ni mtundu mtundu. Yeye hupenda mtu anaekuwa taratibu taratibu na kama unaweza kumsababisha kucheka cheka basi huna muda mrefu unayoyataka utapata. Pia utaanza kumuona nae ni mtu anautundu utundu na kupenda utani utani na anapenda mtu mwenye kumvutia kwa yale anayoyafikiria akilini kwake yaani unatakiwa kujipendekeza kuuliza unataka niwe vipi?

Tabia zake za kero ndogo ndogo ni mategemeo yake uzifurahie na ujifanye kucheka anapoongea upumbavu au jambo lisilo na maana kwako.

Na kama akisema kwa utani ukajibu kwa utani basi moja kwa moja anakufungulia moyo wake na kuona hakuna mtu kama wewe duniani hapa na anaweza kukuganda kama kupe pia utani wa kimwili kama kumgusa mwili na kumminya minya ni vitu anapenda kama ni mke wako basi jaribu leo hata akinuna ukifanya hivyo anakaa sawa. Ni mtu kama unataka kumtoa basi anapendelea sehemu za hadhi ya juu kidogo na anapenda sehemu anayoenda kuwe kuna watu wanaojua nini wanafanya hasa wapishi. Mnunulie kinyaji kisichokuwa na kilevi ndio mapenzi yake kama sio mlevi lakini kama ni mtumiaji basi utakuta ni mpenzi wa wine.

Mazingira ya nyumbani ukimpikia hata chochote tu hujihisi special sana na hataskia la mtu kuhusu wewe valia mavazi ya kupika unapomuandalia chakula na hakikisha muonekano wako uwe ni safi mfanyie hivyo hata mara moja kwa mwezi utaanza kuona anatoa machozi

Ikiwa mazungumzo yanachelewa basi jitahidi asikushinde kimaongezi na wala usikwame katika kuzungumzia mnayoyapenda hasa akianza kuongelea pesa muhimu tabaka hili ni mwanamke mwenye kupenda pesa na kuigiza hajali pesa.

Pia tengeneza account mbili tatu za bank ili akitizama aone kabisa ni mtu mwenye kushughulika na mambo ya saving hata kama huna pesa atatambua ukipata utatunza.

Usihodhi mazungumzo. anapoanza kuzungumza usimkatishe na usiwe mzembe katika kutoa sifa akifanya kitu hata cha kipuuzi nyumbani,kwenye gari yake,mapambo ni watu wenye kupenda kusifiwa wanapofanya mambo madogo.

Rakims
Anza na baba na mama yako. Acha ukumbaff hapa. Utakuta wewe unaishi kwenye mahusiano mabovu ambayo ni moto. Onyesha busara na ujuzi badala ya ujinga na ukumbaff mwanangu
 
Mkuu Rakims;

Mimi ni mwanaume, jina langu linaanzia na herufi N, nimezaliwa tarehe 22/12.

Huyu ni mwanamke natarajia kumuoa, jina lake linaanzia na herufi W, amezaliwa tarehe 29/11.

Aminia sana mkuu!..
Unapendelea sana kufanya kinyume na maumbile lakini pia huna hela kenge wewe
 
Mimi me 12/2 jina S
Yeye ke 18/12 jina T
Wewe una Asili ya Upepo wa kimbunga hali ya kuwa yeye ana asili ya moto wa nyasi nyote wawili mpo vizuri kitabia za nyiota hasa ukizingatia kuwa nyota yako ni thabiti na yake ni yenye nyuso mbili yaani baina ya Mutable na fixed hii hupelekea mtizamo wenu kinyota kuwa mzuri Nyie wawili mnaendana sana katika mahusiano kiasi kwamba hata likija suala la kufanya mapenzi basi kila mtu anatarajia maandalizi makubwa kutoka kwa mwenzie kuanzia usafi na utendaji mnapofika chumbani watu wangekuwa wanawaona basi wasingesita kulipia ili kuwaona mkifanya tena na tena.
Kila mmoja kati yenu anamvutia mwenzie kiakili na mko radhi kuendana kiroho bila nyinyi kuzungumza lakini roho zenu zinakuwa zina makubaliano teyari.
Hasa ukizingatia ya kwamba wewe una mawazo ya mbali sana na ya uvumbuzi ukija kwake ni Mwenye matumaini na maono vile vile mafanikio kwenu ni rahisi sana labda kama ataingilia mtu katikati hasa pia tukirejea katika herufi ya jina lako inatawala nyota ya Samaki na ya kwake inatawala Kaa basi hapo hata negative energies zenu zipo sawa kwa maana zote zinatabia ya maji hivyo hata ugomvi ukitokea kwenu ni mwepesi sana kuzimwa na kuendeleza maelewano
Ingawa maono yako mara nyingi yanakuwa na ukweli usiopingika, hiyo haimkwazi yeye ambaye muda mwingine anaonekana mbishi kiasi kwa utundu tu na baadae anaelewa.
Nyote wawili ni watu wa watu na wenye kupendwa na watu wanaowazunguka, nyote mnapenda kutembelea maeneo mapya na mko teyari kufanya lolote lisilotabirika katika mapenzi yenu ili tu kuyakomaza japo kuwa inaweza kuwa ngumu kuelewana mwanzoni mwa mahusiano.
Kipande kizuri kuhusu nyie ni either mmoja kati yenu huwa na wivu pale ambapo mwingine anakuwa hayupo nyumbani.

Rakims
 
Anza na baba na mama yako. Acha ukumbaff hapa. Utakuta wewe unaishi kwenye mahusiano mabovu ambayo ni moto. Onyesha busara na ujuzi badala ya ujinga na ukumbaff mwanangu
Neno unakuta ni Dhana, Mkuu ikiwa nimekukwaza kuweka post hii niwie radhi lakini mlengwa ulikuwa sio wewe vile vile Jamii forum is WHERE WE DARE TO TALK OPENLY hivyo kama unakwazika na ninachokiandika pimwa kwanza akili,
*Vile vile Baba na mama wanafika vipi hapa?
Unapozungumzia busara elewa na kumbuka
"Sifa za mtu duni haonyi vitendo vyake hata umtie chupani atatoa kidole chake" ingawa unaigiza jina la hapa Jamii forum lakini ukweli wako utabaki kuwa wako tu, lisikuhadae jina la kutumia mtandaoni ukahisi Dunia haina Karma sijakudhuru kwa lolote hivyo kuna kitu nimeongea hapa kitakuja kukutesa sana baadae kiakili ukikaa ukatulia kumbuka MWANANGU as how you call me, neno likishatamkwa halirudi tena kinywani vile vile mzazi wa mwenzio ni wako tu ukisema baya kwa mzazi wa mwenzio ndivyo ulivyosema baya kwa mzazi wako.
Jitizame ulivyomjinga kiasi gani makala ya kuandika tu mtandaoni inakuumiza roho kiasi kwamba unatamani hata ningekuwa karibu ungenipiga kibao. Tafuta sehemu nzuri ya maombi ujiombee Mungu akuongoze ukae sawa mdogo wangu yasikuharibu akili maisha ya Duniani.
Nyie wenye username zaidi ya moja mnajidanganya sana na ulimwengu wa sasa.

Rakims
 
Waulize wagagnga wenzio.
Mnaoshirikiana kuharibu maisha ya watu.
Sawa mkuu nimekuelewa. mimi unaona naharibu ndio maana upo wewe unaetengeza maisha ya watu, vile vile hizi thread kama hazikufai rejea kwenye zile unazopenda kuchangia za ushoga pamoja na huyu mwenzio kule ambapo kutukana mama zenu ni bora zaidi kuliko kufuata nyota ambazo zimeumbwa ili kuwa muongozo wa kuwatoa watu kwenye kiza cha bara na baharini.

Rakims
 
Mimi mme 14/12
Yeye mke 24/02
Baina ya nyie wawili wewe ni Moto wa nyasi na yeye ni Maji ya kisima kwa maana hii yeye atavutiwa zaidi kwako kulingana na nguvu yako ya utafutaji wa maisha, na vile vile wewe utavutiwa nae zaidi kwa mtizamo wake wa kiimani na mambo ya kiroho.

Ukweli ni kwamba katika mahusiano wewe unahitaji mwenza ambaye ni kama mshkaji na yeye anahitaji mwenza ambaye ni kama mwenye ndoto za mapenzi yaani mapenzi muda wote mfano mwanaume wa ndoto zake nyote wawili hamuendani kwa maana kati yenu hakuna anaeweza kumsaidia mwenzie katika mahitaji yake

Asili yako ya roho ya uthubutu na kujitoa utakuta inakwamishwa sana na yeye ambaye ni tegemezi zaidi kwako na uoga wake pia

Yeye ambaye huwa na hisia kali sana muda wote hata kuona unamapenzi nae zaidi ya kumtaka akutimizie haja zako kingono tu, vile vile atakuona ni mtu ambaye hujatulia mambo mengi na vile ulivyo ni mtu wa kupenda uhuru basi moja kwa moja utajiwekea akilini kuwa huyu ni wa kuwa nae tu kwa muda kisha utatafuta mwingine lakini mahusiano yenu taratibu huanza kuzama mfano umemwaga maji kwenye mchanga kila mtu ataangalia uelekeo wake. ndio ndoa hizi mara nyingi watu wanakuwa pamoja ajili ya kuangalia matumizi na watoto tu lakini ni ndoana.

Rakims
 
Me 20/4/ erufi A
Ke 29/6/ erufi H
Nyote wawili mna mengi mnayoendana.

Wote ni wenye kupenda maisha ya nyumbani, wapenda hisia, na hasa kwenye kufanya mapenzi.

Wewe ni mwenye kupenda kwenda pole pole na na vile vile kupenda vitu asilia ambapo ni mvuto mkubwa kwake katika ugonjwa wake wa kuwa na mood zenye kubadirika badirika, ingawa muda mwingine kupenda kwake kuongea kwa uwazi kunakutaka wewe kuwa makini sana kutokumharibu hisia zake kwa maana ni mtu yupo kihisia zaidi na ukimuingia ndani zaidi utaona ni mtu wa kupenda kulia, yeye anataka mtu ambaye ni mwenye nguvu mwenye nyota yako kwa ajili ya kumtegemea kwa kila jambo, baadae utaona ukimtimizia atakupa uaminifu mkubwa wa mapenzi na kukwambia kila siri yake hata wanaomtaka atakuorodheshea, wewe ni mwenye kubana uchumi na kutunza vema na yeye pia ni mtu mwenye kupenda kujibana na kutunza akiba hivyo nyote wawili mna lengo moja au malengo sawa.

Masilahi yenu pamoja na matamanio yenu sawa basi huleta uhusiano mzuri wenye baraka, ukimuoa huyu hujapoteza.

Rakims
 
Mimi: 14 Feb
Wife: 04 Feb
Baina ya wawili nyie ni sawa na kidole na pete

Nyote mnakuwa ni wenye kutamaniana yaani kila mmoja ana tamaa na mwenzie, na hasa katika kufurahia ucheshi wa kila mtu na mwenzie

Uvumbuzi, maendeleo, kuvutiwa upya kusiko na kifani kwa kila mmoja kati yenu ni jambo la kawaida sana na vile vile mnafaana katika tendo na wenye kushirikiana kwa maslahi mapana

Nyote wawili kila mmoja wenu anajihusisha na yote kwa mwenzie na katika shughuli zote na urafiki pia na kushirikishana kama ni wacheza kamari basi mngecheza pamoja pia kulingana na mnavyoendana.

Mambo mengi ya kujishughulisha kwa nje mnaweza kuwa mbali katika kufanya mambo yenu lakini hilo sio tatizo kwenu. hamna kitu ambacho mnachobishana sana zaidi mwisho wake ni kukubaliana nyote mpo kibusara zaidi kuliko kihisia. mapenzi yenu hayatakuwa mazito sana lakini yatakuwa ni yakuvutia yaani hampo deep sana lakini mtu vema.

Rakims
 
Wengine username si rahisi kujua nani mwanamke nani mwanaume fafanua
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom