Nisaidieni kutumia mfumo wa kupata leseni ya biashara online iitwao tausi portal

kelvin complex

JF-Expert Member
Jul 27, 2013
605
580
Habari, naomba mwenye uzoefu wa kutumia mfumo wa kupata leseni ya biashara online uitwao tausi portal unaopatikana katika tovuti ya Tamisemi, anisaidie namna ya kupata mawasiliano ya huduma kwa wateja, kwani mtandao umekuwa na changamoto ya kuchelewa kutoa control number ili kupata leseni ya biashara online, pia kila ninapojaribu kuingia kwenye account yangu unatoa message ya either bad credentials or bad gate away hali inayoashiria mfumo huu una changamoto. Nina siku zaidi ya nne tangu nijisajili lakini hali imekuwa bado changamoto

Sent from my TECNO KD6 using JamiiForums mobile app

====

Mkurugenzi wa TEHAMA, Ofisi ya Rais TAMISEMI mkoani Dodoma Erick Kitali, ameeleza kwamba mfumo mpya wa ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri ujulikanao kama Tausi utasaidia kupunguza urasimu uliokuwepo hapo awali kwenye ukusanyaji wa mapato.

Kitali alitoa tathmini hiyo wakati wa mahojiano maalum na The Chanzo yaliyofanyika ofisini kwake mjini hapa hivi karibuni kuhusu mfumo huo unaotajwa kubuniwa na wataalam wa ndani ya nchi.

Ukipewa jina la ndege huyo mzuri anayepatikana nchini Tanzania, Tausi umebuniwa baina ya kubainika uwepo wa changamoto mbalimbali kwenye mfumo uliokuwa unatumika hapo awali, ikiwa ni pamoja na uzoefu wa mlipa kodi.

“Mfumo huu utasaidia kupunguza muda, kuondoa urasimu uliokuwepo kwa baadhi ya sehemu,” Kitali alisema kwenye mahojiano hayo. “Na sehemu nyingine tulikuwa tunaambiwa kwamba kuna rushwa tumepunguza kwa sababu hukutani moja kwa moja na mwananchi.”

Pamoja na mambo mengine, mfumo wa Tausi humsaidia mteja kufanya malipo kwa kutumia VISA, MasterCard na namba ya malipo kutoka Mfumo wa Malipo wa Kielektroniki wa Serikali (GePG).

Mfumo huo pia humsaidia mteja kujihudumia mwenyewe, hali ambayo haimlazimu tena kwenda ofisi za halmashauri kuomba, au kulipia, tozo, ushuru, leseni, faini au vibali mbalimbali badala yake anaweza kufanya mwenyewe kupitia dirisha la mteja, au Taxpayer Portal.

Kabla ya ujio wa mfumo huo, Serikali ilikuwa inatumia mfumo wa LGRCIS, au Local Government Revenue Collection Information System, ambao Kitali alisema kwenye mahojiano yake na The Chanzo kwamba ulipaswa ubadilishwe ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya kiteknolojia.

Akizungumzia kuhusu namna wananchi walivyoupokea mfumo huo mpya, Kitali alisema mpaka sasa muitikio ni mkubwa.

“Kwa sababu wananchi walikuwa wanapata changamoto ya kupoteza muda mwingi sana kwenda kufuatilia huduma,” alisema. “Ule urahisi wa kufanya malipo mbalimbali ya Serikali umesaidia wananchi kuwa na muitikio mkubwa.”

“Umeongeza uaminifu kwa wananchi kwa Serikali yao kwa sababu wana uhakika na fedha wanayoilipa inakwenda moja kwa moja kwenye Serikali,” aliongeza Kitali. “Pia, mfumo huu umesaidia fedha zinazokusanywa [na halmashauri] zinapelekwa benki kwa wakati.”

 
System imekuwa na issue toka juzi tarehe 17 April 2023 mida ya saa tano na nusu mchana mpaka sasa tarehe 19 2023 bado ni changamoto na wenye system hawasemi chochote ikienda manispaa unapew majibu kuwa mtandao uko down. Nafikiri ni muda muafaka sasa waseme jambo au watoe njia mbadala ya kufanya kazi hii . Naamini kabisa lengo lilikuwa zuri ila huku tunapokwenda sio pazuri tuwe wazalendo tuisaidie serikali kupata mapato yake kwa njia zozote na kwa haraka ndiko dunia inapoelekea
 
Mfumo kama ni mpya lazima changamoto hizo ziwepo.

Nenda kwenye ofisi za Halmadhauri ulipo wakupe control namba umalize kazi.

Pole kwa usumbufu.
 
Njia mpya ya kulipia leseni za biashara. Ni jambo jema lakini ina mahitaji mengi yasiyokuwa ya msingi.Ingehitajika NIDA na Tax clearance ingetosha.

Hiyo password ina masharti kama code ya makombora ya nuclear.

Punguzeni mahitaji ili kila mtu aingie kwa urahisi.

Wilayani, Maafisa biashara ambao mliamini kazi itapungua ndio hao hao wanaowafungulia watu account.

Kumbukeni kuna watu wanaishi vijijini
 
Kwani inachukua muda gani baada ya kukamilisha mchakato wote hadi upate leseni online??
 
sijui kama ni mimi tu, kwa sasahivi watu wanaohitaji leseni za biashara, hizi za kawaida tu, wanahitaji kuapply mtandaoni, hakuna manual.

Kuna mtandao wa tausi tamisemi ambao unafanya uploads ya nyaraka na wao wakitathimini wanakurudishia jibu, unalipia na unadownload leseni yako.

Wazo lilikuwa zuri, lakini kwetu sisi ambao hatufanyi kazi halmashauri au serikalini huko, naona ni kikwazo kile kile kama cha zamani, unaweza ukafanya application ukakaa hadi wiki, bado tu wanaangalia.

Kwa mazingira ya biashara, watu wanahitaji kupata leseni haraka wafanya biashara, kucheleweshana ni kurudisha maendeleo nyuma. watu wa local government mmelogwa na kulaaniwa kwa bureaucracy, tangu enzi zile mpo manial mlihitaji tuwe tunawapa kidogo ili mharakishe mambo, hadi sasa bado mnakuwa wagumu kama mnaishi maporini.

Kwanini serikali huwa inaanzisha vitu na inashindwa kuvisimamia?
 
tausi poral, kuna swali naomba kuuliza, nikiwa approved, nikalipia zile fee za leseni, mnanitumia nyaraka ya leseni nidownload au siku hizi hakuna utaratibu wa kuweka leseni ukutani? thanks.
 
binafsi wamenijibu, nimelipia fee, ila sijui kama ukilipia watakutumia leseni udownload au siku hizi hakuna kubadinka leseni yao ukutani tena kama tulivyozoea.
 
Baada ya kuwa approved na kulipia tausi portal leseni, huwa wanatuma document ya leseni udownload au inatosha. sasa sehemu zingine za kiofisi nikienda watajuaje nimelipia leseni kama wakiihitaji?
 
tausi poral, kuna swali naomba kuuliza, nikiwa approved, nikalipia zile fee za leseni, mnanitumia nyaraka ya leseni nidownload au siku hizi hakuna utaratibu wa kuweka leseni ukutani? thanks.
Una download, mimi nime-download leseni yangu wiki iliuppita

Sent from my SM-J610F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom