Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Nini Hatma ya Upinzani Tanzania?

Wakuu macho_mdiliko na Rwabugiri nawapa asante kwa maoni yenu. Kama kuna kitu kinachonikera kikweli kweli ni misimamo na maoni ya watu kama MwanaFaslsafa1. MwanaFalsafa1 anadai kuwa CCM ina nguvu kubwa vijijini na ndiyo maana ni rahisi sana kwao kushinda iwe kwenye ubunge au uraisi, je kwa nini wameweza kushinda nafasi zote za Ubunge mjini Dar es Salaam. Kwa nini yeye MwanaFalsafa1 licha ya kuwa na uelewa kuliko hao wa vijijini bado anakaa pembeni na eti kuwashauri wengine namna ya kuiondoa CCM.

Yaonekana
MwanaFalsafa1 anaridhika na uongozi wa CCM nchini uliojaa ubabaishaji, ufisadi na ulaghai wa kiwango cha juu na kama ni hivyo kwa nini ashauri namna ya kuiondoa CCM ? Na kama haridhiki na hali hii kwa nini akae pembeni kusubiri watanzania wengine (yeye anawaita wapinzani lakini mimi nawaita wazalendo wenye uchungu na taifa lao) ndio walikomboe taifa ? Kama ni unafiki, hapa MwanaFalsafa1 anaonyesha kiwango cha juu kabisa kama walivyo wengi wanaotetea status quo.

MwanaFalsafa1 anatetea kuwa wizi peke yake hauwezi kuwanyima wazalendo ushindi lakini anasahau kuwa huo wizi ni sera ya CCM inayolindwa na dola. Hiyo asilimia 80% ni idadi ya walioweza kupiga kura kama ilivyotangazwa na dola kwa mdomo wa kinachoitwa tume ya uchaguzi. Je, ni asilimia ngapi ya watanzania walinyimwa fursa ya kupiga kura ama kwa shahada zao kununuliwa, vitisho vya dola, rushwa, wizi, udanganyifu, ulaghai na uzembe wa wasimamizi wanaoteuliwa na CCM.

Tuache kudanganyana hapa, ama umepiga kambi kwenye bonde la kashfa na harufu ya uvundo si tatizo tena kwako au uko kando na unakerwa na hiyo harufu kiasi cha kusogea mbali.
MwanaFalsafa1 ameamua kulifanya hilo bonde kuwa makao yake ya kudumu na kwa kuwa katiba inalinda kuwepo kwa bonde haoni kasoro yoyote na kuwepo kwake. NI lini tutakuwa wakweli kwa nafsi zetu na kutambua nguvu halisi alizonazo hili zimwi la CCM. Kila siku tunashuhudia haya mambo hadi kwa jirani zetu lakini hatujifunzi, tuna nini ?



Huu ni ulaghai - CCM ingetaka kuona upinzani wenye nguvu, hivi sasa tungekuwa na katiba mpya, tume huru ya uchaguzi na dola inayofanya kazi bila uonevu, upendeleo na kwa maelekezo ya CCM. Kwa hali hiyo vitendo tulivyovishuhudia Busanda havingepata nafasi.
MwanaFalsafa1, unajua hatari ya kila chama kuunda kikosi cha vijana,
je, umesikia walichokuwa wanafanya vijana wa CCM huko Busanda ?


Ndiyo maana nikasema kila mpenda maendeleo awe mwana-CCM au la ata penda kuona upinzani ukiendelea hapo umeshindwaje kuelewa? Sasa kama CCM hawaja fanya hivyo ndiyo maana nikasema mwana-CCM MPENDA MAENDELEO.

Acha kumisquote watu Mag3. Wapi nimesema kikosi cha vijana? Mimi naongelea umoja wa vijana ambao wata jiunga na mchakato wa siasa. Mimi nime ongelea vijana wenye vipaji kushirikishwa kwenye siasa sasa wewe hiyo kikosi cha vijana umetoa wapi? Soma vizuri uelewe hapa umeboa kabisa kwa sababu hauja fikiri kabla ya kuandika.

Baadhi ya mambo kwenye post yako umeandika bila kutafakari. it is obvious you wrote with passion rather than ration.
 
Kila mwaka kabla ya Uchaguzi mkuu kuna kuwa na chaguzi ndogo za serikali za mitaa. Je huko wapinzani wanafanyaje?

Kwa maoni yangu serikali za mitaa ziko more directly involved na wananchi kwa maana hiyo upinzani ungefanya vizuri kwenye chaguzi ndogo isingesaidia kupalilia njia kwa ajili ya uchaguzi mkuu? Ukiangalia uchaguzi wa Busanda CCM ilikuwa ina viongozi wengi wa serikali za mitaa iliyo wasaidia kuwa fikia wananchi wengi zaidi je nayo hii haita wasaidia wapinzani?

Kuwa na viongozi wengi kwenye serikali za mitaa kumeisaidia sana kufikisha ujumbe kwa wananchi wa kawaida ambao kwao kuwaona wabunge wao au viongozi wengine ni nadra.

Mimi naona upinzani unaweza kujijenga kwa kuanzia chini kwanza mpaka kwenda juu badala ya kukazania tu uraisi, ubunge na udiwani.

Mwaka huu kuna chaguzi ndogo je viongozi hawa watasaidiaje vyama vyao kwenye uchaguzi wa mwakani?
 
Kaka Es:

Sikujua kama na wewe ni propagandist, nimekuzoea zaidi kama protaganist ama walau propoundist!

Maandiko yako umeyavika ukada na umeshindwa kutazama pande mbili za shilingi. Ukienda Karatu ukawasomea maneno hayo, watakunyooshea vidole vya macho kama walivyofanya kwa mkapa(joke)

Najua wewe unaingia baadhi ya vikao vya CCM, kwa hiyo unajua hofu ya chama chako kuhusu upinzani kinyume na unachotaka kusema hapa.

Si vyama vyote 18 vi sawa. Vingine ni TUMAINI JIPYA, na vingine ni AIBU kwa Taifa. Tuko katika chekecheke hivi sasa.

Kaa karibu na Kaka yako Lowasa, utajua jinsi anavyoiona CHADEMA kama nightmare kwa ndoto zake za kifisadi.

Ufisadi wa CCM si sawa na udhaifu wa upinzani-na kubwa zaidi ni kuwa vipo vyama vinavyoongezeka nguvu kila kukicha.

Toa mifano ya allegation zako kuwa kuna vyama ambavyo badala ya kuwa kwenye kampeni vijijini wakati wa uchaguzi wako kwenye JF.

Pigia chapuo CUF chambelecho cha divided attention. Lakini jua kwamba watu makini wako focused. Wanajua adui wa kumlenga ni yupi na alengwe vipi kwa kutumia silaha gani.

Ipo siku utakumbuka haya maneno, hata kama nimeyaandika kwa uchache wa hoja.

Upo udhaifu katika upinzani;lakini zipo nguvu zinazoonekana na kuu kuliko yote ni kwamba uko mwelekeo uliyo bayana katika baadhi ya vyama na sehemu ya wanasiasa wa KIZAZI KIPYA.

Kuwa wakala wa mabadiliko unayotaka kuyaona kaka- bahari ni muunganiko wa matone madogo madogo ya maji. Kama kila mpenda mageuzi akitimiza wajibu wake, udhaifu ulioko katika upinzani utazidi kutoweka na nguvu inayoongezeka itatamalaki.

Time kills, Time Heals, Time Tells.

Mdogo wako,

JJ


Mkuu, umesema ukweli, maana kuna watu wengine wanaongea kwa sababu tu ya ukada wao, maana udhaifu wa vyama vya upinzani pia hufanya hivyo kuwa na serikali dhaifu, kama wao wanasema upinzania ni dhaifu tukubali pia CCM ni dhaifu na serikali pia, Maana msingi mizuri huwa ina pressure kubwa kwa serikali, wewe n MIMI ndio tunaweza kuchangia kwa vyama kuwa dhaifu
 
Gazeti la Tanzania Daima la jana Jumapili freemedia limekuja na habari hiyo baada ya Mgombea wa CUF huko Mbeya Vijijini kujiunga na Chadema.

Mgombea huyu wa CUF BWANA DAudi MPONZI alipata kura zaidi ya elfu kumi kwenye uchaguzi mdogo wa jimbo la Mbeya vijijini akishindana na mchungaji Mwanjali wa CCM,MGOMBEA WA CHADEMA alitolewa kwenye kinyanganyiro hicho baada ya kutokujua kujaza fomu za uchaguzi huku akidai ni mwanasheria.sasa atagombea Daudi Mponzi au Mwanasheria asiyejua kujaza fomu 2010?

Wimbi la Chadema kuwazoa au kuwachukua watendaji wa CUF limekuwa kubwa baada ya aliyekuwa katibu mkuu msaidizi wa CUF kwa Tanzania Bara kujiunga na Chadema,tayari katibu wa wilaya na mkoa wa Kagera kama sikosei wamejiunga na Chadema.hii ina maana Lwakatare alikuwa ni nguzo kubwa ya CUF?

Mchukia Ufisadi naomba utupe habari kwani inapokuja habari za Lwakatare unazijua vyema kama Field marshal ES na habari za Kilango.
 
Its now the time opposition parties in Tanzania to think far away than staying in this dumping house of taking members from one party to another but without having any success in the election competition. My advice to them is that they dont have to dream for presidential post or even more MPs posts in 2010 if they will keep on their Chademas or TLPs or CUFs etc. Simply because they dont have that influence to the people particularly in rural areas where the country situated and not in big cities where no one has time to go and line up during election time.

Please wake oppostion parties learn from Kenya and somewhere else in Africa and the world in large.
 
Unajua kama wewe ni kiongozi na maarufu basi ujue kuna watu nao wanakinyemelea pale ulipo ,hivyo akiondoka mmoja wale wanaonyemelea na kukodolea macho huwa wapo tayari kurithi cheo chako ,kwa hivyo basi mtaji si kiongozi mtaji ni watu wanaokiunga mkono Chama chao,ikiwa hao wataondoka basi tunaweza kusema CUF inaporomoka ,ila kumbuka tu hawa wanaoondoka jana na leo si wa mwanzo ,watu wanakufa na wengine kuzaliwa.
 
Unajua kama wewe ni kiongozi na maarufu basi ujue kuna watu nao wanakinyemelea pale ulipo ,hivyo akiondoka mmoja wale wanaonyemelea na kukodolea macho huwa wapo tayari kurithi cheo chako ,kwa hivyo basi mtaji si kiongozi mtaji ni watu wanaokiunga mkono Chama chao,ikiwa hao wataondoka basi tunaweza kusema CUF inaporomoka ,ila kumbuka tu hawa wanaoondoka jana na leo si wa mwanzo ,watu wanakufa na wengine kuzaliwa.

mwiba.
kama hamuendi kupiga kampeni Mbeya unategemea hao wafuasi watabaki?watazaliwa vipya wanachama wapya bila kampeni na mipango?
 
Mkandara.
Huku ndiko kugombea ukoko wa chungu kama ulivyosema.
 
Hivi karibuni mh Lipumba alisema "
Hivi sasa CUF haipambani na chama tawala pekee bali hata chama kimoja cha upinzani – Chadema hivi sasa kinajikusanyia wimbi wa wanachama na hata kuwa ni chama kinachopambana kwa karibu na CCM katika chaguzi. Hilo limejidhihirisha katika uchaguzi wa Tarime, Busanda na hata uchaguzi uliofanyika hivi karibuni wa Biharamulo" jee kupambana na Chadema nini kukiimarisha Chama au kukua chama (CUF)
 
Kama Umetaka kutoka kihivyomsawa,lakini anayepambana na Chadema ni Lyatonga Mrema mzee wa Kiraracha,kumbuka kule B/muro alinukuliwa akisema'kama hamtamchagua mgombea wa chama changu cha TLP basi chagueni mgombea wa CCM na msithubutu kumchagua mgombea wa Chadema kwani ni watu wenye fujo,vurugu na hawajuhi siasa'.Kumbuka CUF hawakusimamisha mgombea kule B/muro.
 
Ukweli unabaki kuwa CHADEMA ni Chama Makini na wenye mikakati imara sana kuliko vyote na ni tishio kwa CCM
 
Hivi karibuni mh Lipumba alisema "
Hivi sasa CUF haipambani na chama tawala pekee bali hata chama kimoja cha upinzani – Chadema hivi sasa kinajikusanyia wimbi wa wanachama na hata kuwa ni chama kinachopambana kwa karibu na CCM katika chaguzi. Hilo limejidhihirisha katika uchaguzi wa Tarime, Busanda na hata uchaguzi uliofanyika hivi karibuni wa Biharamulo" jee kupambana na Chadema nini kukiimarisha Chama au kukua chama (CUF)


TX umeingia sijui juzi hapa ama leo .Unadandia hoja tu na umejawa na udini na KAFU wako .Ongea hoja za maana wacheni kutupotezea muda na hoja za hovyo hovyo .Hii mada yako iko hapa tayari .Moderator futa hii bwana.
 
Hatma yake ni kupatikana watu makini kutoka CCM kujiunga nao kama ilivyotokea kwa KANU huko Kenya.Hapo CCM inaweza kung'olewa,zaidi ni wapinzani kuongeza viti vya upinzani Bungeni.
 
huwezi kulinganisha hali ya vyama vingi wakati wa uhuru na muda huu, mazingira ni tofauti sana kipindi hicho in the 1960s tulikuwa tunaongelea zaidi ujinga, maradhi na umasikini muda huu ni ufisadi tu so hizi ni area mbili za tofauti kiasi.

Naweza kuhitimisha kwa kusema kuwa upinzani tanzania upo on the right truck ukiondoa hivyo vyama vidogovidogo vya daftarini. Jamani ni wazi kazi ya upinzani katika ishu nzito kama epa , meremeta, deep green tungeyajuaje lets be open and frank.

Mungu ibariki tanzania tusaidie rasilimali zetu kwaajili ya watoto wetu na amani yetu daima.
 
Mchukia Ufisadi naomba utupe habari kwani inapokuja habari za Lwakatare unazijua vyema kama Field marshal ES na habari za Kilango.

- Yaani kama na wewe unavyozijua habari za Mzee Mengi na Mwakyembe, au unataka kukikimbia kivuli chako mkuu kwamba ukiwa Kanda2 basi hufahamiki?

- By the way, nilitaka kuleta salam tu kwamba Mama Kilango ni mzima wa afya njema, alifanyiwa operation ndogo sana ambayo hakutaka hata watoto wake waijue, lakini ikawa nje ya her control habari ikatoka, ndio kwanza amemaliza Degree yake ya Uchumi hapa Open University na sasa anajitayarisha kwa kuanza Masters pia,

- Jimboni kwake hakuna hata harufu ya Upinzani mzito kisiasa, kwa hiyo ameamua kuwa ni bora tu aunganishe na Masters badala ya kuhangaika kukimbia jimboni kila wakati kama wengine, unajua ukiwatumikia wananchi kwa kila ulichonacho, wananchi wanazo akili za kujua mwanzo na mwisho wa uwezo wako kiuongozi, hivyo unakuwa huna sababu ya kukosa usingizi uchaguzi unapokaribia, na hii ni changamoto nzito sana hii kwa wabunge wetu, kwamba watumikie wananchi hutakuwa na sababu ya kulia lia kwamba mafisadi wanamtayarisha mtu kukutoa.

Otherwise, tupo pamoja sana wakuu, ingawa niko nyuma sana na threads humu maana nimepata nafasi kuanzia jana kuingia baada ya kuwa off yaani likizo ya muda ambayo bado inaendelea, lakini naona bado moto upo pale pale kuacha tu nonsense za hapa na pale ambazo ni za kawaida kwenye demokrasia makini kama hii ya JF.

Idumu JF na Mungu Aibariki Tanzania.

Respect and Out.

Kamanda FMES!
 
Kuja kuwa na upinzani wa dhati tanzania hii itachukua miaka mingi sana! Chaguzi ndogo tu vyama vinanaza kugombana, do u think wanaweza kuungana na kuleta upinzani wa kweli na kuing'oa sisi M ( Mafisadi)? Ni ndoto kabisa.
 
Mara kadhaa nimeona wapenzi/washabiki/wanachama wa CUF wakikishambulia CHADEMA kuliko vyama vingine ikiwemo hata CCM!

Mfano mzuri ni uchaguzi mdogo wa Mbeya Vijini ambapo CUF kiliweka pingamizi dhidi ya mgombea wa CHADEMA, Shitambala. Pamoja na mgombea huyo kujitoa bado CUF kiliendelea kukilaumu CHADEMA ambacho kilikuwa nje kuliko CCM ambayo walibaki nayo kuchuana. Humu JF tumeona thread zikidai kuwa CUF ina sifa kadhaa ukilinganisha na CHADEMA! Sijui kwa nini walinganishe na CHADEMA badala ya TLP, NCCR, etc?

Swali la kujiuliza: Hivi CUF ni chama cha upinzani kwa CHADEMA tu?
 
Mashabiki wenyewe wa CUF kina maralia Sugu, wala ndio maana hasa hawajui nani ni nani katika siasa za nyumbani, hakika mtu akiisha kuwa mwana CUF kuna mambo natilia shaka juu ya uelewa wake.
 
mashabiki wenyewe wa CUF kina maralia Sugu, wala ndio maana hasa hawajui nani ni nani katika siasa za nyumbani, hakika mtu akiisha kuwa mwana CUF kuna mambo natilia shaka juu ya uelewa wake.
Kwa nini unatilia mashaka kuhusu wanaCUF ndugu?
 
CUF ni CCM B, ndo maana inatumiwa na kufadhiliwa kiiangushe CHADEMA
 
Back
Top Bottom