Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Nikiwa nimemaliza chuo niliamua kwenda mkoa X kujifunza maisha nje na shule.

Nilibahatika kupata marafiki wengi na uzoefu wa biashara ila sikuweza kukaa sana baada ya kuamua kurudi jiji kuu kuendelea na mishe nyingine.

Ila ninachokumbuka nikiwa mkoa ule kuna mdada mmoja alitokea kunipenda na akanieleza hisia hizo mbele yangu ila kutokana uzoefu wa kuambiwa maneno hayo na wanawake kwa muda mrefu nilimpuuzia na ukizingatia nimetoka shule hata kuna muda maisha siyaelewi hivyo mapenzi kwa wakati huo hakikuwa kipaumbele hivyo sikumwambia kwa mdomo ila kwa vitendo nadhani alielewa.

Nikiwa nimerudi mjini yule dada alionyesha kila dalili za upendo ila alingonga mwamba nachokumbuka nikiwa nampango wa kufanya biashara ya kuuza viatu nilimwelekeza kiutani nikiwa nahitaji mtaji kama wa laki mbili ndani ya dk 10 kwenye simu yangu ikaingia laki 2 kutoka kwake akinisisitiza nifanye biashara niizalishe hiyo hela na nimrudishie kiukweli sikumrudishia na tukaachana kwa ugomvi.

Wema wake haukuondoka moyoni mwangu na hapa katikati nikapita na wanawake sikupata tena kama yeye ninavyoongea leo ndo mtu ninayeishi nae na ninasubilie ikimpendeza Mungu aniletee kiumbe.

Uwa namuuliza ile laki 2 bado unanidai.
Wema wake haukuondoka moyoni mwangu na hapa katikati nikapita na wanawake sikupata tena kama yeye ninavyoongea leo ndo mtu ninayeishi nae na ninasubilie ikimpendeza Mungu aniletee kiumbe.

Uwa namuuliza ile laki 2 bado unanidai[emoji1787]
 
Daah uzi mzuri sana binafsi nimepata kusimuliwa visa kadhaa kama hivi ila kimoja ninachokikumbuka na kilichonigusa zaidi ni hiki

Kuna mama mmoja akiwa binti huko kijijini alikuja kugongewa hodi nyumbani kwake na mtoto mmoja masikini aliyeonekana ana njaa sana

Yule mtoto alimuomba yule binti maji tu lakini yule binti alijiongeza akamletea glass ya maziwa basi yule mtoto akanywa akashukuru akaondoka

Sasa ikapita miaka mingi yule binti akawa mtu mzima akaanza sumbuliwa na maradhi ambayo ilibidi aende kwenye hospitali kubwa mjini

Kafika mjini kwenye moja ya hospitali kubwa katibiwa maradhi yake vizuri kabisa sasa imekuja bill ni kubwa na yule mama ni masikini hawezi kuilipa

Ghafla akashangaa kaja daktari akampa karatasi imeandikwa "bill yote imelipwa na ile glass ya maziwa uliyonipatia kule kijijini miaka kadhaa iliyopita"
Ghafla akashangaa kaja daktari akampa karatasi imeandikwa "bill yote imelipwa na ile glass ya maziwa uliyonipatia kule kijijini miaka kadhaa iliyopita"[emoji3064][emoji2827]

Mungu wangu[emoji848]
 
Padre Adolph Makandago Mungu amtunze amenitetea Mengi seminarini kiasi cha Kukosana na Rector....Sijatimizia Matamanio yake ya Mimi kuwa mseja ila iko siku nitalipa fadhila..alini treat kama Mdog wake wa kuzaliwa..
Pengine ningefukuzwa shule muda sana
Jitahidi utimize hii nadhiri ili uwe huru
 
Kuna watu dunia hapa Mungu awape maisha marefu.

Mwaka huu mwezi wa tano nikiwa natoka kwenye mishe zangu niko na pikipiki langu kuna jamaaa hata sijui alinigonga vip kwa nyuma na pikipiki lake nilipata ajali mbaya sana nilizimia pale sikua naelewa kitu chochote nimekuja kuzinduka niko hosptali sielewi hata nimefika vip hapo hosptali ..inshort nilikua km naona ni ndoto baada ya kupata hudum na akili yangu kukaa sawa ikabidi niulize nimefika vip pale.

Ndio yule doctar akasema pumzika kwanza ila nikawa namsisitza sana aniambie ni nn kimetokea mpaka mm nimefika hapo ndo akaniambia kuna watu wamekuleta hapa na gari umepata ajali na walifanikiwa kupata simu yako wamewapigia watu ulio andika jina kaka wamewapata ..kaka zako wanakuja.

Mm roho ikatulia maana nikua siko sawa plus nilikua na maumivu makali sana mwilini nimekuja kupata nafuu sasa ndo nikapata mkanda mzima.

Nilipo pata ajari watu walikua wanapita tu na magari wakiogopa kunibeba maana nilikua natokwa na dam nyingi sana mwilini kwa hiyo wakawa wanasema nitachafua gari lakin kuna huyo bro wala simjui mpaka sasa ndo alikubali kunibeba kwenye gali lake docta anasema gar lake siti ya nyuma nilichafua sana na dam na bado huyo ndo aliitumia simu yangu ndogo ambayo vibaka hawakuniibia maana simu kubwa na hela waliiba pale ndo aliitumia kuwapigia ndugu .Docta anasema jamaa alikataa kuacha no yake akasema mm shida yangu ni huyu dogo afike sehemu apate huduma.
Brooo popote ulipo Mungu akuongezee na akupe Afya njema ww na kizazi chako [emoji2972]
 
Kuna watu dunia hapa Mungu awape maisha marefu.

Mwaka huu mwezi wa tano nikiwa natoka kwenye mishe zangu niko na pikipiki langu kuna jamaaa hata sijui alinigonga vip kwa nyuma na pikipiki lake nilipata ajali mbaya sana nilizimia pale sikua naelewa kitu chochote nimekuja kuzinduka niko hosptali sielewi hata nimefika vip hapo hosptali ..inshort nilikua km naona ni ndoto baada ya kupata hudum na akili yangu kukaa sawa ikabidi niulize nimefika vip pale.

Ndio yule doctar akasema pumzika kwanza ila nikawa namsisitza sana aniambie ni nn kimetokea mpaka mm nimefika hapo ndo akaniambia kuna watu wamekuleta hapa na gari umepata ajali na walifanikiwa kupata simu yako wamewapigia watu ulio andika jina kaka wamewapata ..kaka zako wanakuja.

Mm roho ikatulia maana nikua siko sawa plus nilikua na maumivu makali sana mwilini nimekuja kupata nafuu sasa ndo nikapata mkanda mzima.

Nilipo pata ajari watu walikua wanapita tu na magari wakiogopa kunibeba maana nilikua natokwa na dam nyingi sana mwilini kwa hiyo wakawa wanasema nitachafua gari lakin kuna huyo bro wala simjui mpaka sasa ndo alikubali kunibeba kwenye gali lake docta anasema gar lake siti ya nyuma nilichafua sana na dam na bado huyo ndo aliitumia simu yangu ndogo ambayo vibaka hawakuniibia maana simu kubwa na hela waliiba pale ndo aliitumia kuwapigia ndugu .Docta anasema jamaa alikataa kuacha no yake akasema mm shida yangu ni huyu dogo afike sehemu apate huduma.
Brooo popote ulipo Mungu akuongezee na akupe Afya njema ww na kizazi chako [emoji2972]
Pole sana unaendeleaje sasa?
 
Nakumbuka miaka ya 90 mwanzoni tukiwa tunaishi Keko National maarufu kama mabembeani. Nikiwa nasoma nursery ya kanisa katoliki Keko Mwanga, tulikuwa na tabia kipindi cha mvua mnavua viatu na kuanza kuchezea madimwi ya maji, kumbe nilikanyaga chupa na ilinikata unyayo mzima ila sikuwa nasikia maumivu mie naendelea kutembea tuu uku nikiacha alama za damu chini.

Bahati nzuri mama mmoja aliniona, alinibeba kunipeleka hospitali then baada ya matibabu alinipeleka hadi nyumbani kwetu baada ya kumuelekeza. Huwa nikiona alama ya kovu mguuni huwa namkumbuka sana kwa wema wake kwangu. Sikuweza kumjua hadi hii leo
 
Nakumbuka siku moja jioni ya saa 1 nilimsindikiza rafiki yangu mahali alikuwa na kikao cha chakula cha jioni hoteli flani.
Nilipofika karibu na hiyo hotel nili park pembeni ya barabara kuu ili kumshusha.

Wakati nimesimama kuna gari iliingia road kwa speed sana kutokea ile hotel na kuivaa pikipiki ambayo ilimbeba binti flani wa umri wa miaka 23.

Jamaa alupoona ameginga alikimbia sana lkn kuna pikipiki ilimkimbiza kwenda kusoma namba.

Mimi na yule rafiki yangu tulielekea kwenye eneo walipogongwa wale watu na binti alikuwa na hali mbaya yaani anarusha miguu kama vile anakata roho.

Kwasababu mimi nilipark karibu na tukio kuna raia walifikiri kuwa gari yangu ndio imewaginga lkn kuna watu wakasema aliyegonga amekimbia.

Watu wakaanza kushikiniza nimbebe haraka kuwahi hospital lakini niliwaambia wasubirie nitoe taarifa polisi ili yasijekunigeukia mimi


Baada ya kutoa ripoti polisi ndipo nikaomba msaada wa kumbeba kwani kwa alivyokuwa ilikuwa inaogopesha kulihitajika umakini kumbeba...cha ajabu watu wote wakawa wanarudi nyuma kukwepa kumbeba.

Nikajikuta ninashout kuwa mmejaa bure hamna msaada mnachonga tu hapa.
Nilimshika jamaa mmoja kwa nguvu...njoo tumbebe pamoja na yule rafiki yangu.

Kweli tukambeba na tukaondoka wote na watatu na mgonjwa wa 4 lkn dereva boda hakuumia sana na aliposikia tunaenda polisi badala ya kupanda gari alikimbia.

Polisi tukapewa pf3 na kuelekea hospital.
Nilipofika nikapewa gharama nikalipia na kuhakikisha amewekewa drip na mengine yakaendelea.

Kilichosaidia zaidi yule jamaa niliyemlazimisha kubeba na tukaenda naye alikuwa anamfahamu kwa sura na alimfahamu rafiki yake flani.
Ndipo akaanza kupiga simu mtaani kwao hadi rafiki yake akaja.

Muda huo ilishafika saa 7 usiku nikawaaga rafiki zake na kuwaachia namba kuwa watanijulisha maendeleo.

Baada ya miezi 8 nilipokea simu toka huyo binti.

Akajitambulisha kuwa; kaka mimi naitwa Given.
Tarehe flani nilipata ajali na nilipopona niliambiwa kuwa ulifanyika msaada mkubwa sana kwangu.

Plz naomba nikufahamu.
Kweli tulipanga na tukaona, binti alinishukuru mnoo.

Akawa ananipigia kila mara.
Kuna wakati nikao ana kila dalili ya kunipa shukrani na alianza kutamka; kaka kama inawezekana iwe.......[emoji849]

Wazee wa Cuba mtanielewa.
Ndipo taratibu nikampotezea kwani nilimsaidia sio kwa kusudi lolote bali niliona kuwa nilifanyika mkono wa Mungu kwa kutoa msaada na nisije kubeba utukufu wa Mungu nikaadhibiwa.

Given popote ulipo uishi maisha marefu mdogo wangu
 
Nakumbuka siku moja jioni ya saa 1 nilimsindikiza rafiki yangu mahali alikuwa na kikao cha chakula cha jioni hoteli flani.
Nilipofika karibu na hiyo hotel nili park pembeni ya barabara kuu ili kumshusha.

Wakati nimesimama kuna gari iliingia road kwa speed sana kutokea ile hotel na kuivaa pikipiki ambayo ilimbeba binti flani wa umri wa miaka 23.
Kwani nilimsaidia sio kwa kusudi lolote bali niliona kuwa nilifanyika mkono wa Mungu kwa kutoa msaada na nisije kubeba utukufu wa Mungu nikaadhibiwa.[emoji1752][emoji1545]
 
Hii stori imeniumiza sana...Mungu atusaidie tuwakumbuke yatima na wasiojiweza..Mungu ambariki sana huyo baba
Nami niweke kisa changu japo ni chakawaida lakini kwangu ni moja ya tukio ninalo dumu nalo kwa kumshukuru sana Mungu kwaajili ya huyu ninaemzunguzia hapa.

Mwaka 1992 nilikua nakaa na bibi baada ya wazazi kufariki mwishoni mwa miaka ya 80.

92 hio bibi alipata shida ya macho na hakujaliwa kuona tena mpaka anakufa .

Mzazi wangu alikufa alikua ni mwanae wa mwisho 3 kufariki hivyo akawa hana msaada kwa chakula na mahitaji mengine ya kibinadamu.

Ilibidi awe ananituma mimi kuomba kwa majirani chakula, leo huku kesho kule mpaka 96 nilipopata nguvu kidogo nikawa naanza kufanya vibarua vya hapa na pale napata mia, mia mbili na wakati mwingine mia tano.

Ilitusaidia kununa mboga , kusaga mahindi, na vitu vidogo vidogo vya kutuwezesha kuishi.

Hii ilienda nikiwa nimetenga siku za kwenda shule , Jumatatu naenda jumanne naenda kibaruani jumatano shule alhamisi kibaruani ijumaa shule jumamosi kibaruani jumapili kanisani.

Kwa mfumo huo ndio nienda kupausua kokoto mahali mbali kidogo tokea asubuhi mpaka saa tisa alienipa kazi hajatokea, njaa inaniuma Sana hata kunyanyua nyundo nikashindwa, lakini mawazo yote yapo kwa yule bibi ambaye tokea jana hajala kitu na hapo alipo hawezi kusogea hata hatua moja.

Ilinibidi nitoke hapo niende kwa baba mmoja aliekuwa anatufahamu kwa lengo la kumuomba kazi yoyote hata nipate 500 tu nirudi nyumbani nikanunue chochote, bahati mbaya sikumkuta ila watoto tuu, niliwaambia shida yangu lakini hawakuwa na lakunisaidia .

Ilibidi niwaombe malimao nile maana ile njaa ilioniuma siku ile mwaka 97 mpaka leo naikumbuka.

Nilikula yake malimao nikapata nguvu kurudi nyumbani km kama 7 hivi, huku sijui itakuwaje kule nyumbani.

Lakini ile nafika tu saa 12 bibi ananiuliza nimefanikiwa chochote maana njaa inaniuma mno, chozi lilipotokea hata sijui.

Lakini nikasikia mlio wa gari yule baba akaja mpaka nyumbani ana unga sukari na mchele, hata nguo hakubadilisha alipoambiwa na watoto kwamba nimekuja na nimeomba kibarua, alishindwa kuvumilia hata kuingia ndani ilibidi aje atuletee chakula.

Hilo tukio ni moja ya matukio ambayo yananipa faraja sana kwamba Mungu yupo na nisikate tamaa hata kama jua limezama chochote kinaweza kutokea.

Nilipika kile chakula lakini nilishindwa kula ila bibi alikuala, shukrani niliompa yule baba mpaka leo sioni kama inatosha, yeye pengine aliona ni kawaida lakini mpaka sasa ni miaka 25 sasa sijasahau na sita sahau zaidi ya kushukuru na kuwa msaada kwa wengine.

Wema ni akiba ndugu zangu tena akiba isio na mfano.

Lakini pia kushukuru ni kwema mno.
 
Mimi nachokumbuka nikiwa mwanafunzi wa chuo kimoja huko mkoa wa nyanda za juu kusini.

Chuo chetu kina hospitali ya rufaa hivyo kuna mwanamke alikuja chuoni na mtoto mgongoni akiomba uongozi wa chuo umsaidie ili aweze kupata wanafunzi wa kwenda kumsaidia mwanae aweze kupata damu kwa ajili ya blood transfusion uongozi wa ulikataa.

Hapo ndipo mimi na mwenzangu ikabidi tumfuate yule mama mwenye mtoto wodini aliko na kumwambia tutakutolea damu ila tunaomba iwe siri .kiuhalisia ikawa ndo tabia yetu tunapokezana kila baada ya miezi mitatu anaenda mwingine kumtolea damu .

Mtoto wake alizaliwa na kidonda hivyo ilibidi afanyiwe skin graft na zilikuwa zinakataa zaidi ya mara 3 mara ya nne ikakubali na yule mama wa mtoto alikaa hospitali miaka miwili hadi muda anaondoka aliweza kujipatia ndugu na marafiki wengi sana hadi leo nawasiliana nae.
Safi sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom