Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Mwaka 2002 namsaidia kijana mdogo mpemba. Mtaji wa elfu 10 kuuza maji yale ya 50 nimekutana na dogo 2017 ni tajir anauza magar. Kwa kifup dogo kawa mchaga full mwez wa 12 tunaendaga nae moshi. Anadai alinitafuta sana. Na mimi nilimkuta analia stend pale anaomba hela ya nauli arud kwao pemba. Baba yake alishafariki yupo yeye na mdogo wake wa kike wanalelewa na baba mdogo anawatesa na amekuja dar kubahatisha. Ila amechemka. Bahat nzur cku hiyo nilitoka nae tukaenda kula nikampiga picha nilikuwaga na camera. Ni stor ndefu ila Nachojua Mungu ana sababu zake kwanini vitu hutokea.
kitali ikikupendeza simulia yote wengine wapate kujifunza
 
kitali ikikupendeza simulia yote wengine wapate cntasahau cku tunakutana. Nimetoka kuibiwa hela ya kodi ml 18 dukan mwenye frem kaja juu mbaya kabisa. Nashangaa naitwa jina halafu dogo kaenda kulipa kodi yeye kisha ndio kijitambulisha. Kumbe yeye ananikumbuka mi cmkumbuki kabisa kanenepa kawa mweupee. From there ni history mzee. Tuache tu ila Mungu ni muaminifu sana.
 
Mwaka 98 nikiwa darasa la nne pale shule ya msingi Mwananyamala Kisiwani. Siku moja tukiwa tupo mapunziko yale ya saa nne, mimi na wenzangu tulienda nyuma ya Shule kwaajili ya kununua vitu mbalimbali ili kulituliza tumbo kutokana na njaa. Nakumbuka siku hiyo nilikuwa na njaa sana hivyo nikaona ili kuituliza ninunue viazi vitamu vya kukaanga. Kipindi hicho kiazi kimoja Sh 50, kwa kuwa nilikuwa na sh 200 hivyo nikanunua viazi vitatu kisha nikabakiwa na sh 50 kwaajili ya kununua barafu la kwenda kulia darasani. Kwa bahati mbaya vile viazi vilifungwa kwenye gaazeti, na kutokana na mchuzi kuwa mwingi lile gazeti lilichanika na hatimaye viazi kuanguka chini sehemu chafu. Kutokana na njaa niliyonayo nikasimama pale huku nikifikiria niviokote ama niende darasani!!!? Wakati naendelea kiwaza namna ya kufanya akatokea mkaka hivi na kunambia dogo achana navyo hvyo chukua hii 500 ukanunie vingine. Kitendo hiki mpaka leo hakitoki kichwani mwangu na kimeniathiri kiasi kwamba ninapokuwa na niko vizuri kisha nikaona watu wanagombana kwa kudaina pesa ambayo naweza kuimudu kuilipa basi ni heli nimlipie mdaiwa kisha maisha yaendelee.

Yaani kiufupi huwa sipendi kukutana na mtu anataabika njiani, kama ninauwezo wa kumsevu huwa nafanya hvyo. Yule jamaa simkumbuki hata kwa sura.

Ila ninachoweza kukitolea ushuhuda ni kwamba ukiwa na tabia ya kusaidia watu kwenye matatizo bila kutarajia malipo, basi nawe utajikuta ukipata msaada kwenye magumu bila kutarajia ulipotokea.
Nikweli kabisa..
 
Nina mkumbuka baba yangu mlezi (mume wa mama mdogo )alinichukua kutoka kwa mama yangu nikiwa na miaka 3 akanilea na kunisomesha tena shule za gharama kubwa.Kuanzia nursey mpaka chuo kikuu. Baada tu ya kumaliza field yangu ya mwisho,mwaka wa mwisho baba akafariki.
Nina maumivu sana mpaka Leo
[emoji26][emoji26][emoji26][emoji24][emoji24]
 
Kuna sehemu nimewahi kufanya kazi 2007-2008. Boss wangu alikuwa kila siku anatusisitiza nendeni mkaongeze elimu sisi wengine tumekaribia kustaafu na akituona kila siku ni madongo tu kwamba vijana nyie hapa mnapoteza muda tu. Kuna namna alitupambania mpaka mambo ya kawa sawa na tukaondoka na kazini tuliondoka watatu kwenda kusoma. Sasa mambo yanasonga juzi napiga story na jamaa mmoja ambae ndio tulitoka wote kwamba tumpelekee yule mzee zawadi, kuja kufuatilia ili tupate namba zake tukaambiwa amefariki mwaka huu mwezi wa 6. Dah inauma sana.
 
Mimi nachokumbuka nikiwa mwanafunzi wa chuo kimoja huko mkoa wa nyanda za juu kusini.

Chuo chetu kina hospitali ya rufaa hivyo kuna mwanamke alikuja chuoni na mtoto mgongoni akiomba uongozi wa chuo umsaidie ili aweze kupata wanafunzi wa kwenda kumsaidia mwanae aweze kupata damu kwa ajili ya blood transfusion uongozi wa ulikataa.

Hapo ndipo mimi na mwenzangu ikabidi tumfuate yule mama mwenye mtoto wodini aliko na kumwambia tutakutolea damu ila tunaomba iwe siri .kiuhalisia ikawa ndo tabia yetu tunapokezana kila baada ya miezi mitatu anaenda mwingine kumtolea damu .

Mtoto wake alizaliwa na kidonda hivyo ilibidi afanyiwe skin graft na zilikuwa zinakataa zaidi ya mara 3 mara ya nne ikakubali na yule mama wa mtoto alikaa hospitali miaka miwili hadi muda anaondoka aliweza kujipatia ndugu na marafiki wengi sana hadi leo nawasiliana nae.
 
Nikiwa nakaribia kumaliza moataba wangu katika hospitali moja mkoa X.

Rafiki yangu mmoja alinitumia tangazo nimsaidie kuapply kazi katika shirika moja la afya niliweza kufanya hivyo ila na mimi nikaamua kuapply pia.

Baada ya wiki mbili niliweza kuitwa kwenye interview ila yeye hakubahatika kuitwa na nikapata kazi ile mpaka leo nafanya.

Moyo unaniuma mpaka leo sijaweza kufanya chochote kwake .najisikia vibaya nie na vi elfu 10 ninavyomtumia ila naona nina deni sana kwake.

Yeye hajapata kazj bado ila amejishikiza sehemu
 
Nikiwa nimemaliza chuo niliamua kwenda mkoa X kujifunza maisha nje na shule.

Nilibahatika kupata marafiki wengi na uzoefu wa biashara ila sikuweza kukaa sana baada ya kuamua kurudi jiji kuu kuendelea na mishe nyingine.

Ila ninachokumbuka nikiwa mkoa ule kuna mdada mmoja alitokea kunipenda na akanieleza hisia hizo mbele yangu ila kutokana uzoefu wa kuambiwa maneno hayo na wanawake kwa muda mrefu nilimpuuzia na ukizingatia nimetoka shule hata kuna muda maisha siyaelewi hivyo mapenzi kwa wakati huo hakikuwa kipaumbele hivyo sikumwambia kwa mdomo ila kwa vitendo nadhani alielewa.

Nikiwa nimerudi mjini yule dada alionyesha kila dalili za upendo ila alingonga mwamba nachokumbuka nikiwa nampango wa kufanya biashara ya kuuza viatu nilimwelekeza kiutani nikiwa nahitaji mtaji kama wa laki mbili ndani ya dk 10 kwenye simu yangu ikaingia laki 2 kutoka kwake akinisisitiza nifanye biashara niizalishe hiyo hela na nimrudishie kiukweli sikumrudishia na tukaachana kwa ugomvi.

Wema wake haukuondoka moyoni mwangu na hapa katikati nikapita na wanawake sikupata tena kama yeye ninavyoongea leo ndo mtu ninayeishi nae na ninasubilie ikimpendeza Mungu aniletee kiumbe.

Uwa namuuliza ile laki 2 bado unanidai.
 
Ni jambo la kihisia mno, jambo lililo ndani ya moyo kabisa lisilotoka na ambalo hujirudiarudia kila Mara!

Ni kuhusu wema uliowahi kutendewa na mtu baki halafu ukaahidi kimoyomoyo kumlipa lakini isiwezekane kwakuwa hujawahi kuonana naye tena au pengine keshafariki.

Nakumbwa na hiyo hali! Namkumbuka mno Dada Jamila Mazoea R.I.P alinipenda sana na kunisaidia katika mengi, lakini kabla ya kuwa na uwezo wa kulipa wema wake kwangu alitwaliwa kutoka katika maisha haya.

Nilichoweza kumsaidia ni mwaka 1993 ambapo nilikutana naye akaniomba sh mia mbili ambayo nilimpa ile ya noti kipindi hicho, baada ya siku ile sikuwahi kuonana naye mpaka mwaka 2010 nilipoenda kwake na kuambulia kuonyeshwa kaburi lake!

Bado namkumbuka dadaangu JAMILA MAZOEA na kwenye ulimwengu wa roho analifahamu hili
Brother Mshana kwanza pole nmesoma comment za huu uzi nmelia mno.......mimi ningehadisia lkn moyo wa kuyazuia machozi sina kabisa
 
Daah uzi mzuri sana binafsi nimepata kusimuliwa visa kadhaa kama hivi ila kimoja ninachokikumbuka na kilichonigusa zaidi ni hiki

Kuna mama mmoja akiwa binti huko kijijini alikuja kugongewa hodi nyumbani kwake na mtoto mmoja masikini aliyeonekana ana njaa sana

Yule mtoto alimuomba yule binti maji tu lakini yule binti alijiongeza akamletea glass ya maziwa basi yule mtoto akanywa akashukuru akaondoka

Sasa ikapita miaka mingi yule binti akawa mtu mzima akaanza sumbuliwa na maradhi ambayo ilibidi aende kwenye hospitali kubwa mjini

Kafika mjini kwenye moja ya hospitali kubwa katibiwa maradhi yake vizuri kabisa sasa imekuja bill ni kubwa na yule mama ni masikini hawezi kuilipa

Ghafla akashangaa kaja daktari akampa karatasi imeandikwa "bill yote imelipwa na ile glass ya maziwa uliyonipatia kule kijijini miaka kadhaa iliyopita"
 
Padre Adolph Makandago Mungu amtunze amenitetea Mengi seminarini kiasi cha Kukosana na Rector....Sijatimizia Matamanio yake ya Mimi kuwa mseja ila iko siku nitalipa fadhila..alini treat kama Mdog wake wa kuzaliwa..
Pengine ningefukuzwa shule muda sana
 
Brother Mshana kwanza pole nmesoma comment za huu uzi nmelia mno.......mimi ningehadisia lkn moyo wa kuyazuia machozi sina kabisa
Asante ila jaribu kuhadithia uone nafuu utakayopata.. Machozi ni tiba nzuri sana kiroho
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom