Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,741
- 861,138
- Thread starter
- #101
ila usiku mmoja wenye giza nilitumiwa meseji na namba ngeni ya kuwa rafiki yako amefariki akiwa South africaKisa cha pili
Nikiwa chuo mwaka wa pili katika chuo nilichokuwepo kulikuwa na utaratibu wa kuomba field katika mtandao wa chuo then unaenda kufanya mafunzo ya vitendo yaani field , katika kufanya hivyo nikapata sehemu niliyotaraji
Ila baada ya huo mtandao kufungwa nikawa nimebadilisha mawazo kuwa niende sehemu nyingine hii kutokana na msukumo wa marafiki na pia kupunguza gharama za usafiri
Basi chuo kilikuwa na utaratibu ikiwa mtandao umefungwa na unahitaji kubadili kituo cha mafunzo inakubidi utafute kituo mwenyewe kwa kwenda kuonana na wakuu wa idara wa hiyo sehemu unataka kwenda uwaombe kufanya field hapo wakikubali wakupe barua , hiyo barua umpatie msimamizi wako wa field
Alafu uende sehemu uliyoomba kwenye mtandao ukutane na mkuu wa hiyo department umueleze kuwa hautaweza kufanyia hapo field sababu ya kuwa unaenda kwingine
Ofcourse nilifanya hivyo ila bahati mbaya sehemu ya kwanza ya field niliyoomba , mkuu wa hiyo department aliniplease sana kuwa ana uhitaji sana na watu wa fani yangu hivyo hakubaliani na maamuzi yangu
Ujana maji ya moto , mimi nikaona ananizingua ikiwa tayari nishamaliza wajibu wangu , hivyo field ilipoanza kwa muda wake mimi nikawa naenda zangu sehemu ya pili nilipoomba kwa mdomo
Later on coordinator wa field ananipigia simu kwanini sijauhudhuria kwenye field nikamueleza kuwa nipo sehemu fulani na barua nishatuma , akasema ikiwa nataka hivyo niende nimalizane na mkuu wa idara wa sehemu niliyoomba mwanzo then anipe barua pia ya kuridhia mimi kutofanya field kwake .
Hilo nilijua lisingewezekana hivyo njia pekee niliandika barua mwenyewe na nikaanza kuusaka muhuri wa ile department kupitia watu wangu wa karibu , badae nikaupata
Nikaenda Temeke nikachonga muhuri wa ile department then nikaupiga kwenye barua nikamtumia coordinator (utoto )
Siku ya assessment coordinator anasema ulinidanganya mbona mkuu wa department ya kule mwanzo hakuwahi kukuona ? Hivyo uliforge muhuri
Nikaona hili ni zali nikakubali kosa ila nikahitaji tuyamalize akakaza
Hivyo field ikaishia pale , tumerudi chuo nasubili what's up mara napigwa na barua ya kikao cha nidhamu
Siku naenda kwenye kikao nakutana na pannel ya madaktari na maprofesa wote wananisikiliza mimi huku nje polisi wananisubili .
After five hours ya kikao , hukumu inatoka kwa upande wa chuo sitakiwi chuo nimedisco na pia nakabidhiwa kwa askari ili waendelee na uchunguzi .
Ni hapo Mungu anamleta profesa mmoja anaikataa hukumu huku akihitaji sababu za yule mkuu wa department kunikatalia mimi kwenda sehemu nyingine hivyo haoni kama kuna sababu ya mimi kudisco na kutoendelea na masomo
Mara pannel yote iko kimya hakuna anayesema chochote , mara mtoa hukumu anauliza wangapi hawakubaliani na hiyo hukumu , bado yule profesa anakuwa upande wangu .
Inapangwa kikao siku nyingine , ni hapo mimi nakabidhiwa kwa askari ila sifiki nao mbali tukiwa njiani wanasimamishwa na gari la profesa aliyenitetea kwenye mataa ya fire hapo kariakoo , anawaomba tuyamalize mimi niwe huru
Note :sikuwa na undugu wowote na yule mzee wala sikuwa chini yake darasani maana hakuwepo kwenye fani yangu
Sikujua ni kiasi gani alitoa ila naambiwa dogo kuwa makini sana , nashuka kwenye difenda napanda kwenye hilux , narudishwa chuo mpaka chumba namba 16 , kwenye ofisi ya huyu mzee anaitaka historia yangu mbali na shule nampa historia anasema toka hapo mimi ni mwanaye .
Kesi iliisha kimya kimya maana sikuitwa tena nikaendelea na masomo
Profesa mawasiliano yaliendelea vizuri japo nilikuja kupoteza simu hivyo ikanichukua muda kidogo kupata namba yake maana alihama chuo na kwenda South africa,,ila usiku mmoja wenye giza nilitumiwa meseji na namba ngeni ya kuwa rafiki yako amefariki akiwa South africa
Inaniuma sana maana sina fadhila niliyolipa kwake hasa alivyonipambania
Kila nikiwaza naumia sana , nimebaki na picha za ukumbusho tu
Bahati mbaya hakuwa na mtoto wala mke
Na hakuletwa hapa Tanzania alizikwa huko
South africa
Natamani hata nilione kaburi lake , niseme asante kwa zile fadhila zake
Kila nikisikia story za chuo basi moyo umkumbuka mzee profesa na machozi hayakawii.
Inaniuma sana maana sina fadhila niliyolipa kwake hasa alivyonipambania
Kila nikiwaza naumia sana , nimebaki na picha za ukumbusho tu
Bahati mbaya hakuwa na mtoto wala mke
Na hakuletwa hapa Tanzania alizikwa huko
South africa
Natamani hata nilione kaburi lake , niseme asante kwa zile fadhila zake [emoji2827][emoji24]