Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Kisa cha pili
Nikiwa chuo mwaka wa pili katika chuo nilichokuwepo kulikuwa na utaratibu wa kuomba field katika mtandao wa chuo then unaenda kufanya mafunzo ya vitendo yaani field , katika kufanya hivyo nikapata sehemu niliyotaraji

Ila baada ya huo mtandao kufungwa nikawa nimebadilisha mawazo kuwa niende sehemu nyingine hii kutokana na msukumo wa marafiki na pia kupunguza gharama za usafiri

Basi chuo kilikuwa na utaratibu ikiwa mtandao umefungwa na unahitaji kubadili kituo cha mafunzo inakubidi utafute kituo mwenyewe kwa kwenda kuonana na wakuu wa idara wa hiyo sehemu unataka kwenda uwaombe kufanya field hapo wakikubali wakupe barua , hiyo barua umpatie msimamizi wako wa field

Alafu uende sehemu uliyoomba kwenye mtandao ukutane na mkuu wa hiyo department umueleze kuwa hautaweza kufanyia hapo field sababu ya kuwa unaenda kwingine

Ofcourse nilifanya hivyo ila bahati mbaya sehemu ya kwanza ya field niliyoomba , mkuu wa hiyo department aliniplease sana kuwa ana uhitaji sana na watu wa fani yangu hivyo hakubaliani na maamuzi yangu

Ujana maji ya moto , mimi nikaona ananizingua ikiwa tayari nishamaliza wajibu wangu , hivyo field ilipoanza kwa muda wake mimi nikawa naenda zangu sehemu ya pili nilipoomba kwa mdomo

Later on coordinator wa field ananipigia simu kwanini sijauhudhuria kwenye field nikamueleza kuwa nipo sehemu fulani na barua nishatuma , akasema ikiwa nataka hivyo niende nimalizane na mkuu wa idara wa sehemu niliyoomba mwanzo then anipe barua pia ya kuridhia mimi kutofanya field kwake .

Hilo nilijua lisingewezekana hivyo njia pekee niliandika barua mwenyewe na nikaanza kuusaka muhuri wa ile department kupitia watu wangu wa karibu , badae nikaupata

Nikaenda Temeke nikachonga muhuri wa ile department then nikaupiga kwenye barua nikamtumia coordinator (utoto )

Siku ya assessment coordinator anasema ulinidanganya mbona mkuu wa department ya kule mwanzo hakuwahi kukuona ? Hivyo uliforge muhuri

Nikaona hili ni zali nikakubali kosa ila nikahitaji tuyamalize akakaza

Hivyo field ikaishia pale , tumerudi chuo nasubili what's up mara napigwa na barua ya kikao cha nidhamu
Siku naenda kwenye kikao nakutana na pannel ya madaktari na maprofesa wote wananisikiliza mimi huku nje polisi wananisubili .

After five hours ya kikao , hukumu inatoka kwa upande wa chuo sitakiwi chuo nimedisco na pia nakabidhiwa kwa askari ili waendelee na uchunguzi .

Ni hapo Mungu anamleta profesa mmoja anaikataa hukumu huku akihitaji sababu za yule mkuu wa department kunikatalia mimi kwenda sehemu nyingine hivyo haoni kama kuna sababu ya mimi kudisco na kutoendelea na masomo

Mara pannel yote iko kimya hakuna anayesema chochote , mara mtoa hukumu anauliza wangapi hawakubaliani na hiyo hukumu , bado yule profesa anakuwa upande wangu .

Inapangwa kikao siku nyingine , ni hapo mimi nakabidhiwa kwa askari ila sifiki nao mbali tukiwa njiani wanasimamishwa na gari la profesa aliyenitetea kwenye mataa ya fire hapo kariakoo , anawaomba tuyamalize mimi niwe huru

Note :sikuwa na undugu wowote na yule mzee wala sikuwa chini yake darasani maana hakuwepo kwenye fani yangu

Sikujua ni kiasi gani alitoa ila naambiwa dogo kuwa makini sana , nashuka kwenye difenda napanda kwenye hilux , narudishwa chuo mpaka chumba namba 16 , kwenye ofisi ya huyu mzee anaitaka historia yangu mbali na shule nampa historia anasema toka hapo mimi ni mwanaye .

Kesi iliisha kimya kimya maana sikuitwa tena nikaendelea na masomo

Profesa mawasiliano yaliendelea vizuri japo nilikuja kupoteza simu hivyo ikanichukua muda kidogo kupata namba yake maana alihama chuo na kwenda South africa,,ila usiku mmoja wenye giza nilitumiwa meseji na namba ngeni ya kuwa rafiki yako amefariki akiwa South africa

Inaniuma sana maana sina fadhila niliyolipa kwake hasa alivyonipambania
Kila nikiwaza naumia sana , nimebaki na picha za ukumbusho tu

Bahati mbaya hakuwa na mtoto wala mke
Na hakuletwa hapa Tanzania alizikwa huko
South africa
Natamani hata nilione kaburi lake , niseme asante kwa zile fadhila zake

Kila nikisikia story za chuo basi moyo umkumbuka mzee profesa na machozi hayakawii.
ila usiku mmoja wenye giza nilitumiwa meseji na namba ngeni ya kuwa rafiki yako amefariki akiwa South africa

Inaniuma sana maana sina fadhila niliyolipa kwake hasa alivyonipambania
Kila nikiwaza naumia sana , nimebaki na picha za ukumbusho tu

Bahati mbaya hakuwa na mtoto wala mke
Na hakuletwa hapa Tanzania alizikwa huko
South africa
Natamani hata nilione kaburi lake , niseme asante kwa zile fadhila zake [emoji2827][emoji24]
 
Mkuu duuuuh! Umenigusa sana,
Kuna kaka mmoja (mkubwa sana kwangu) ni engineer wa mabarabara kama sikusei namtafuta japo nitamke neno Asante tu!

What he did in my life made me who I am today! Kibaya zaid sikuwah hata kulijua vizur jina lake (kitu kama BURHANI MUSSA kama sijakosea) nakumbuka sura tu ndo Huwa hainitoki, ndani ya siku 5 tu hardly 5 alibadilisha historia nzima ya maisha yangu!
Jaman ni hadithi ndefu, ila huyu kaka namtafuta mno, hadi mme wangu ameona aanze kunisaidia!
Tuletee kisa
 
Mshana Jr umeandika vitu vingi mno vinavyoleta matokeo chanya kwa kila anae soma, iwe kwa comment au thread.

Kwa namna ya pekee umekua msaada kwa kila mmoja wetu kwa angle tofauti tofauti hapa jamii forum.

Hii nayo ni mada inayogusa hisia za za watu kwa wema walio wahi kufanyiwa na kutamani kurudisha shukrani, kawaida yetu sisi binadamu huwa tunasahau, lakini kuna vitu tunafanyiwa na kufanya ambavyo pamoja na udhaifu wetu wa kibinadamu wa kusahau huwa hatusahau moja kwa moja. Tunapo kutana na mada kama hizi tukumbuka na kushukuru.

Siku zote Mungu ndie anaetusaidia kupitia kwa watu mbali mbali, so tunapo rudisha shukrani ni moja kwa moja tunamrudishia Mungu shukrani.

Kwa hiyo ndugu mshana hiki unachofanya ni zaidi ya utumishi na amini Mungu hatakupungukia kama sio wewe basi uzao wako wote.na binafsi nakuombea iwe hivyo.

Zaidi ndugu mshana kwa vile unavyo wasilisha hapa jukwaani inaonyesha ni mtu uliepitia mengi sana ya kuinuka na kuanguka, asante kwa yale uliojaliwa kutushirikisha, kwa aina ya teknolojia tulio nayo hata dumu na kudumu na yatafaidia kwa kiasi kikubwa kizazi kijacho.

Haikupendezi ndugu mshana kuandika kitabu kihusucho maisha yako ,ushuhuda ulio nao utaenea kwingi na utawainua wengi mno .

Yote ya yote Mungu awe nawe kwa kila hali.
 
Mshana Jr umeandika vitu vingi mno vinavyoleta matokeo chanya kwa kila anae soma, iwe kwa comment au thread.

Kwa namna ya pekee umekua msaada kwa kila mmoja wetu kwa angle tofauti tofauti hapa jamii forum.

Hii nayo ni mada inayogusa hisia za za watu kwa wema walio wahi kufanyiwa na kutamani kurudisha shukrani, kawaida yetu sisi binadamu huwa tunasahau, lakini kuna vitu tunafanyiwa na kufanya ambavyo pamoja na udhaifu wetu wa kibina6 wa kusahau huwa hatusahau moja kwa moja. Tunapo kutana na mada kama hizi tukumbuka na kushukuru.

Siku zote Mungu ndie anaetusaidia kupitia kwa watu mbali mbali, so tunapo rudisha shukrani ni moja kwa moja tunamrudishia Mungu shukrani.

Kwa hiyo ndugu mshana hiki unachofanya ni zaidi ya utumishi na amini Mungu hatakupungukia kama sio wewe basi uzao wako wote.na binafsi nakuombea iwe hivyo.

Zaidi ndugu mshana kwa vile unavyo wasilisha hapa jukwaani inaonyesha ni mtu uliepitia mengi sana ya kuinuka na kuanguka, asante kwa yale uliojaliwa kutushirikisha, kwa aina ya teknolojia tulio nayo hata dumu na kudumu na yatafaidia kwa kiasi kikubwa kizazi kijacho.

Haikupendezi ndugu mshana kuandika kitabu kihusucho maisha yako ,ushuhuda ulio nao utaenea kwingi na utawainua wengi mno .

Yote ya yote Mungu awe nawe kwa kila hali.
Kwa hiyo ndugu mshana hiki unachofanya ni zaidi ya utumishi na amini Mungu hatakupungukia kama sio wewe basi uzao wako wote.na binafsi nakuombea iwe hivyo.[emoji1752][emoji1545][emoji2827]

Napokea kwa unyenyekevu mkuu mkuu Pendaelli kikubwa tuombeane afya na maisha mengi mema[emoji2827][emoji1752][emoji1545]
 
Nami niweke kisa changu japo ni chakawaida lakini kwangu ni moja ya tukio ninalo dumu nalo kwa kumshukuru sana Mungu kwaajili ya huyu ninaemzunguzia hapa.

Mwaka 1992 nilikua nakaa na bibi baada ya wazazi kufariki mwishoni mwa miaka ya 80.

92 hio bibi alipata shida ya macho na hakujaliwa kuona tena mpaka anakufa .

Mzazi wangu alikufa alikua ni mwanae wa mwisho 3 kufariki hivyo akawa hana msaada kwa chakula na mahitaji mengine ya kibinadamu.

Ilibidi awe ananituma mimi kuomba kwa majirani chakula, leo huku kesho kule mpaka 96 nilipopata nguvu kidogo nikawa naanza kufanya vibarua vya hapa na pale napata mia, mia mbili na wakati mwingine mia tano.

Ilitusaidia kununa mboga , kusaga mahindi, na vitu vidogo vidogo vya kutuwezesha kuishi.

Hii ilienda nikiwa nimetenga siku za kwenda shule , Jumatatu naenda jumanne naenda kibaruani jumatano shule alhamisi kibaruani ijumaa shule jumamosi kibaruani jumapili kanisani.

Kwa mfumo huo ndio nienda kupausua kokoto mahali mbali kidogo tokea asubuhi mpaka saa tisa alienipa kazi hajatokea, njaa inaniuma Sana hata kunyanyua nyundo nikashindwa, lakini mawazo yote yapo kwa yule bibi ambaye tokea jana hajala kitu na hapo alipo hawezi kusogea hata hatua moja.

Ilinibidi nitoke hapo niende kwa baba mmoja aliekuwa anatufahamu kwa lengo la kumuomba kazi yoyote hata nipate 500 tu nirudi nyumbani nikanunue chochote, bahati mbaya sikumkuta ila watoto tuu, niliwaambia shida yangu lakini hawakuwa na lakunisaidia .

Ilibidi niwaombe malimao nile maana ile njaa ilioniuma siku ile mwaka 97 mpaka leo naikumbuka.

Nilikula yake malimao nikapata nguvu kurudi nyumbani km kama 7 hivi, huku sijui itakuwaje kule nyumbani.

Lakini ile nafika tu saa 12 bibi ananiuliza nimefanikiwa chochote maana njaa inaniuma mno, chozi lilipotokea hata sijui.

Lakini nikasikia mlio wa gari yule baba akaja mpaka nyumbani ana unga sukari na mchele, hata nguo hakubadilisha alipoambiwa na watoto kwamba nimekuja na nimeomba kibarua, alishindwa kuvumilia hata kuingia ndani ilibidi aje atuletee chakula.

Hilo tukio ni moja ya matukio ambayo yananipa faraja sana kwamba Mungu yupo na nisikate tamaa hata kama jua limezama chochote kinaweza kutokea.

Nilipika kile chakula lakini nilishindwa kula ila bibi alikuala, shukrani niliompa yule baba mpaka leo sioni kama inatosha, yeye pengine aliona ni kawaida lakini mpaka sasa ni miaka 25 sasa sijasahau na sita sahau zaidi ya kushukuru na kuwa msaada kwa wengine.

Wema ni akiba ndugu zangu tena akiba isio na mfano.

Lakini pia kushukuru ni kwema mno.
 
U
Nami niweke kisa changu japo ni chakawaida lakini kwangu ni moja ya tukio ninalo dumu nalo kwa kumshukuru sana Mungu kwaajili ya huyu ninaemzunguzia hapa.

Mwaka 1992 nilikua nakaa na bibi baada ya wazazi kufariki mwishoni mwa miaka ya 80.

92 hio bibi alipata shida ya macho na hakujaliwa kuona tena mpaka anakufa .

Mzazi wangu alikufa alikua ni mwanae wa mwisho 3 kufariki hivyo akawa hana msaada kwa chakula na mahitaji mengine ya kibinadamu.

Ilibidi awe ananituma mimi kuomba kwa majirani chakula, leo huku kesho kule mpaka 96 nilipopata nguvu kidogo nikawa naanza kufanya vibarua vya hapa na pale napata mia, mia mbili na wakati mwingine mia tano.

Ilitusaidia kununa mboga , kusaga mahindi, na vitu vidogo vidogo vya kutuwezesha kuishi.

Hii ilienda nikiwa nimetenga siku za kwenda shule , Jumatatu naenda jumanne naenda kibaruani jumatano shule alhamisi kibaruani ijumaa shule jumamosi kibaruani jumapili kanisani.

Kwa mfumo huo ndio nienda kupausua kokoto mahali mbali kidogo tokea asubuhi mpaka saa tisa alienipa kazi hajatokea, njaa inaniuma Sana hata kunyanyua nyundo nikashindwa, lakini mawazo yote yapo kwa yule bibi ambaye tokea jana hajala kitu na hapo alipo hawezi kusogea hata hatua moja.

Ilinibidi nitoke hapo niende kwa baba mmoja aliekuwa anatufahamu kwa lengo la kumuomba kazi yoyote hata nipate 500 tu nirudi nyumbani nikanunue chochote, bahati mbaya sikumkuta ila watoto tuu, niliwaambia shida yangu lakini hawakuwa na lakunisaidia .

Ilibidi niwaombe malimao nile maana ile njaa ilioniuma siku ile mwaka 97 mpaka leo naikumbuka.

Nilikula yake malimao nikapata nguvu kurudi nyumbani km kama 7 hivi, huku sijui itakuwaje kule nyumbani.

Lakini ile nafika tu saa 12 bibi ananiuliza nimefanikiwa chochote maana njaa inaniuma mno, chozi lilipotokea hata sijui.

Lakini nikasikia mlio wa gari yule baba akaja mpaka nyumbani ana unga sukari na mchele, hata nguo hakubadilisha alipoambiwa na watoto kwamba nimekuja na nimeomba kibarua, alishindwa kuvumilia hata kuingia ndani ilibidi aje atuletee chakula.

Hilo tukio ni moja ya matukio ambayo yananipa faraja sana kwamba Mungu yupo na nisikate tamaa hata kama jua limezama chochote kinaweza kutokea.

Nilipika kile chakula lakini nilishindwa kula ila bibi alikuala, shukrani niliompa yule baba mpaka leo sioni kama inatosha, yeye pengine aliona ni kawaida lakini mpaka sasa ni miaka 25 sasa sijasahau na sita sahau zaidi ya kushukuru na kuwa msaada kwa wengine.

Wema ni akiba ndugu zangu tena akiba isio na mfano.

Lakini pia kushukuru ni kwema mno.
Umeniliza
 
Nami niweke kisa changu japo ni chakawaida lakini kwangu ni moja ya tukio ninalo dumu nalo kwa kumshukuru sana Mungu kwaajili ya huyu ninaemzunguzia hapa.

Mwaka 1992 nilikua nakaa na bibi baada ya wazazi kufariki mwishoni mwa miaka ya 80.

92 hio bibi alipata shida ya macho na hakujaliwa kuona tena mpaka anakufa .

Mzazi wangu alikufa alikua ni mwanae wa mwisho 3 kufariki hivyo akawa hana msaada kwa chakula na mahitaji mengine ya kibinadamu.

Ilibidi awe ananituma mimi kuomba kwa majirani chakula, leo huku kesho kule mpaka 96 nilipopata nguvu kidogo nikawa naanza kufanya vibarua vya hapa na pale napata mia, mia mbili na wakati mwingine mia tano.

Ilitusaidia kununa mboga , kusaga mahindi, na vitu vidogo vidogo vya kutuwezesha kuishi.

Hii ilienda nikiwa nimetenga siku za kwenda shule , Jumatatu naenda jumanne naenda kibaruani jumatano shule alhamisi kibaruani ijumaa shule jumamosi kibaruani jumapili kanisani.

Kwa mfumo huo ndio nienda kupausua kokoto mahali mbali kidogo tokea asubuhi mpaka saa tisa alienipa kazi hajatokea, njaa inaniuma Sana hata kunyanyua nyundo nikashindwa, lakini mawazo yote yapo kwa yule bibi ambaye tokea jana hajala kitu na hapo alipo hawezi kusogea hata hatua moja.

Ilinibidi nitoke hapo niende kwa baba mmoja aliekuwa anatufahamu kwa lengo la kumuomba kazi yoyote hata nipate 500 tu nirudi nyumbani nikanunue chochote, bahati mbaya sikumkuta ila watoto tuu, niliwaambia shida yangu lakini hawakuwa na lakunisaidia .

Ilibidi niwaombe malimao nile maana ile njaa ilioniuma siku ile mwaka 97 mpaka leo naikumbuka.

Nilikula yake malimao nikapata nguvu kurudi nyumbani km kama 7 hivi, huku sijui itakuwaje kule nyumbani.

Lakini ile nafika tu saa 12 bibi ananiuliza nimefanikiwa chochote maana njaa inaniuma mno, chozi lilipotokea hata sijui.

Lakini nikasikia mlio wa gari yule baba akaja mpaka nyumbani ana unga sukari na mchele, hata nguo hakubadilisha alipoambiwa na watoto kwamba nimekuja na nimeomba kibarua, alishindwa kuvumilia hata kuingia ndani ilibidi aje atuletee chakula.

Hilo tukio ni moja ya matukio ambayo yananipa faraja sana kwamba Mungu yupo na nisikate tamaa hata kama jua limezama chochote kinaweza kutokea.

Nilipika kile chakula lakini nilishindwa kula ila bibi alikuala, shukrani niliompa yule baba mpaka leo sioni kama inatosha, yeye pengine aliona ni kawaida lakini mpaka sasa ni miaka 25 sasa sijasahau na sita sahau zaidi ya kushukuru na kuwa msaada kwa wengine.

Wema ni akiba ndugu zangu tena akiba isio na mfano.

Lakini pia kushukuru ni kwema mno.
Dah . very touching aisee.. Maisha yetu haya hapa duniani yamebeba siri nyingi na mambo ya kushangaza mno
Kuna wakati nayatazama haya maisha na kutamani kila kitu kingekuwa tofauti
Hakuna wabaya dunia imejaa wema
Hakuna simanzi dunia imejaa furaha
Hakuna kuumia bali kila mahali ni faraja
Hakuna kulia, hakuna kufa ujanani nknk
 
Mie niliyotendewa mazuri na watu ni mengi sana. Ila huwa najitahidi sana nami nirudishe fadhila kwao na nikishindwa basi hata kwa watu wengine.
Ajabu ni kwamba anayetenda huwa anaona kitu cha kawaida sana ila anayetendewa ndio hukumbuka sana.
Mfano wa kisa kidogo mie kuna jamaa mmoja wa nyumbani amewahi kuniongezea sh 200 mwaka 2003 ili nipate chakula na mfukoni nilikuwa na sh 300 tu huwa sisahau mpaka leo. Hata nikimkumbusha na kumshukuru basi hubaki anacheka tu kwakuwa yeye aliona ni jambo dogo.

Binafsi kuna jambo nimewahi kutenda kwa jamaa mmoja ambaye mpaka sasa navuna mengi kutoka kwake kama dua, shukrani na hata kunitembelea kunijulia hali. Hii ilikuwa mwaka 2012 mwishoni nikiwa Dom nafanya kazi na kampuni fulani. Kazi ambazo tulikuwa tunafanya zilikuwa za shift na msalahi mazuri sana. Siku hiyo nilikuwa off ya siku 4 na naelekea Dar na Kimbinyiko kama kawaida. Nakumbuka nimefika Gairo napigiwa simu namba mpya nikapokea jamaa akajitambulisha naitwa fulani (sijawahi kumfahamu) nimepewa namba yako na mlinzi hapa getini nina shida kubwa ya kutafuta kazi. Nikamuuliza elimu yake akasema form IV na VETA ile grade ya juu. Nilimuuliza maswali matatu tu nikagundua huyu anatufaa (kumbuka sijawahi kumuona) nikamwambia subiri niongee na Boss wangu hapo. Nikampigia Boss nikampamba vizuri sana akasema mruhusu aje. Basi nikampigia jamaa nikamwambia mpe mlinzi nikamwambia mlinzi mpeleke kwa fulani (Boss). Alivyofika kule Boss akamwambia nimepata taarifa zako akamuuliza umekuja na vyeti vyako jamaa akavitoa. Baada ya hapo jamaa akala kibarua Baada ya kurudi kutoka Dar jamaa ndio nikafahamiana nae. Kiukweli jamaa alikuwa the best kazini kuliko kawaida.
Project ilivyokuja kuisha pale ile kampuni ikamaliza mkataba na serikali na sisi wote tukamaliza mkataba ila jamaa aliendelea nao wakaenda Rwanda [emoji1206] kwenye Project nyingine. Jamaa alipiga pesa akajenga Dom pale na kafungua ofisi yake ya hardware palepale baada ya project ya Rwanda kuisha.

Jamaa hunikumbuka sana na ajabu kwakwe ni vile nilimsaidia wakati hatujawahi kufahamiana hata siku moja na mpaka akaja kutoboa.
 
Mkuu tuma tena maana hazifunguki
Tusome hapa sote
IMG_20220919_171837.jpg
IMG_20220919_171845.jpg
IMG_20220919_171853.jpg
IMG_20220919_171901.jpg
 
Dah . very touching aisee.. Maisha yetu haya hapa duniani yamebeba siri nyingi na mambo ya kushangaza mno
Kuna wakati nayatazama haya maisha na kutamani kila kitu kingekuwa tofauti
Hakuna wabaya dunia imejaa wema
Hakuna simanzi dunia imejaa furaha
Hakuna kuumia bali kila mahali ni faraja
Hakuna kulia, hakuna kufa ujanani nknk
Naam brother, hata hivyo bado dunia ni nzuri na watu wazuri bado wapo, ingawa kwa uchache sana ubinafsi unatutesa.
 
Mkuu duuuuh! Umenigusa sana,
Kuna kaka mmoja (mkubwa sana kwangu) ni engineer wa mabarabara kama sikusei namtafuta japo nitamke neno Asante tu!

What he did in my life made me who I am today! Kibaya zaid sikuwah hata kulijua vizur jina lake (kitu kama BURHANI MUSSA kama sijakosea) nakumbuka sura tu ndo Huwa hainitoki, ndani ya siku 5 tu hardly 5 alibadilisha historia nzima ya maisha yangu!
Jaman ni hadithi ndefu, ila huyu kaka namtafuta mno, hadi mme wangu ameona aanze kunisaidia!
unatafuta dyudyu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom