Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 371,741
- 861,143
- Thread starter
- #81
Maisha hutukutanisha na mengi kuanzia kuzaliwa. Makuzi kujitambua utu uzima, uzee hadi kifo.. Ni kati ya hayo mengi kuna mazuri na kuna mabaya. Kuna ya kuumiza moyo na kuna ya kuleta faraja. Kuna ya kukumbuka kwa namna ya pekee kabisa lakini pia kuna ambayo hutamani usiyakumbuke Kabisa
Kisa changu na mchunga ng'ombe Dsm Ubungo Kibo
Nitasimulia kwa vipande hivyo mtaniwia radhi
Mwanzoni mwa miaka ya tisini, nikiwa eneo tajwa nikipambana kuanza maisha nilitapeliwa kodi ya nyumba shilingi elfu 18, kodi ya miezi 6 kwa kupangishwa chumba cha mtu
Nilidhani nimepata kumbe nimepatikana kwakuwa wakati huo kodi chumba hakikuwa chini ya sh 5000.. Lakini mimi nikapatac kwa 3000 tena kina kitanda cha chuma cha BANCO na godoro lake..lakini bila foronya bila shuka
Siku ya tatu tangu kuingia makazi yangu mapya nikakutana na taharuki kubwa.. Chumba nilichopangishwa kilikuwa kimoja tu kwenye foundation ya nyumba ya vyumba vitano.. Nikakuta mtu kakaa hapo nje na mabegi na watoto wawili na mwanamke! Na ilikuwa ni saa nne usiku
Automatically hao ndio walikuwa wenye nyumba, yalitokea mengi kwa muda mchache lakini niseme tu kwamba kufika saa nne na robo usiku sikuwa na pa kulala
Nitaendelea...
Kisa changu na mchunga ng'ombe Dsm Ubungo Kibo
Nitasimulia kwa vipande hivyo mtaniwia radhi
Mwanzoni mwa miaka ya tisini, nikiwa eneo tajwa nikipambana kuanza maisha nilitapeliwa kodi ya nyumba shilingi elfu 18, kodi ya miezi 6 kwa kupangishwa chumba cha mtu
Nilidhani nimepata kumbe nimepatikana kwakuwa wakati huo kodi chumba hakikuwa chini ya sh 5000.. Lakini mimi nikapatac kwa 3000 tena kina kitanda cha chuma cha BANCO na godoro lake..lakini bila foronya bila shuka
Siku ya tatu tangu kuingia makazi yangu mapya nikakutana na taharuki kubwa.. Chumba nilichopangishwa kilikuwa kimoja tu kwenye foundation ya nyumba ya vyumba vitano.. Nikakuta mtu kakaa hapo nje na mabegi na watoto wawili na mwanamke! Na ilikuwa ni saa nne usiku
Automatically hao ndio walikuwa wenye nyumba, yalitokea mengi kwa muda mchache lakini niseme tu kwamba kufika saa nne na robo usiku sikuwa na pa kulala
Nitaendelea...