hii mada ni very touching, nina mawili ambayo nayakumbuka sana!
mwaka 2013, nakumbuka ilikuwa mwezi Disemba, nilikuwa nahamisha makazi kutokana Dar ambako nilikuwa kwa miaka mitatu kwa sababu za kimasomo kurudi kazini kwangu kusini mwa tanzania. kutokana na haraka niliyokuwa nayo nikamuomba rafiki yangu flani hivi wa ukweli niliyesoma nae primary ambaye makazi yake permanent sasa yalikuwa hapo hapo Dar anisafirishie vitu vyangu mi nikiwa nimetangulia. alilipokea hilo na akaniahidi atavituma siku ya pili tu. jioni ya siku ya pili, alinitumia ujumbe ambao ninao mpaka leo katika simu yangu kuwa amevisafirisha kupitia gari flani inayoitwa Mashallah na kwamba ameviandika jina lake vifaa vyote hivyo nikae tayari kuvipokea siku inayofuata. ilipofika asubuhi, wakati huo gari iliyobebea hivyo vifaa ipo njiani inakuja, napokea simu kuwa yule rafiki yangu amefariki baada ya kugongwa na gari wakati anarudi kutoka katika mizunguko yake mbagala.......kumbe mizunguko hiyo ni kule kuja kunisafirishia vifaa vyangu. UTUHUMIWA NINAOJIHISI SIJUI UTATOKA LINI!!!!!!! nilichanganyikiwa mno na kamwe sitasahau hili, alikuwa ni mtu mwema sana sana tangu udogo wake. nashukuru nipo pamoja na mama'ake na tunaelewana sana. maisha haya ukiyatafakari kwa kina, utabadilika na kuwa mtu mwema sana......sisi binadamu hakuna kitu!!
tukio la pili ni la kutenda wema kwa upande wangu. ilikuwa mwaka 2002 wakati nasoma huko kibaha, pwani. alikuja dada fulani hivi maeneo ya shule amefadhaika anatafuta mtu mwenye damu group o+, mimi ndo group langu hilo.. nikajitokeza, mwalimu aliniruhusu na tukaenda na yule dada Tumbi hospitali. tulitumia muda mrefu sana pale na hatimaye baada ya vipimo vya damu kukidhi haja nikaruhusiwa kudonate. nilidonate free of charge na niligundua kumbe ilikuwa kwa ajili yake mwenyewe. baada ya tukio hili alinishukuru yule dada, aliulizia jina na kidato na kuahidi angenitembelea siku moja...nilikuwa kidato cha tatu wakati huo. hakutokea hadi namaliza shule na kuondoka, sijui kilichoendelea katika tatizo lake la kiafya lakini naamini Mungu alimsaidia na kupona. najivunia tukio hili kwani nahisi ni kama kubwa kiasi kulifanya mtu!! kila la kheir dada Elizabeth (kama nakumbuka sawasawa) popote ulipo!!