Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

Nina hakika hili lilishakutokea hata wewe

So touching to me this.
Ngoja namm niweke yangu hapa mkuu, ila hii ni ya kusaidia.

Kuna mwaka nilikua manyara nasimamia shamba la miwa la bro, flani hivi, sasa baada ya miwa kukatwa ikabidi niende kiwandani pale manyara sugar kupelekwa ile miwa nikiwa nasubiri pale kwenye folen
akaja mzee hivi akanisalimia baada ya hapo akaanza kunieleza yanayomsibu.

aisee nilimuonea huruma vibaya mno akasema yy alikua ziwani ni mvuvi sasa alipata kama laki sita hivi wenzake aliokua anaishi nao walimuibia usiku alafu wakaondka maana n kile kipindi magufuli anapiga vita uvuvi Haram kwahiyo yeye pale alikua ana hela za kuondoka kabisa ila
baada ya kuibiwa akawa hana ujanja tena.

Ikabidi atembee kwa miguu kutoka magara, hadi pale kiwandani angalau aje apate kibarua pale, kufika pale hakuna anaemjua hata mmoj akajaribu kuomba kazi pale akaambiwa ahonge 150k ili apate kazi, wakati huo yy hana hata mia alivyoniona pale akawa anaomba kama ninayo hata buku nimpe ajitetee kwa muuza chakula pale ale, aisee jamaa hata kuongea alikua anashindwa kutokana na njaa m mfukoni nilikua na buku tatu ambayo niliuza miwa njian tena namm mwenyewe nilikua nina njaa ya hatari ila ilibidi tu nimpe yule mzee yote akaniuliza naww vp mbn hela unanipa yote nikamwambia mzee m narudi shamba saivi we usijali kule kuna hela ipo wala haina shida.

Huwezi amini yule mzee alitaka kulia ila nilmbembeleza sana ikabd tu aache, akasema kijana nmeomba watu wengi sana tena wengine n wenye hela ila hawajanipa ww umenipa?? Akaushika mkono wangu akaubusu. Baadae nilivyotaka kuondoka akaomba namba yangu ya sim nikampa tena niliandka kwenye karatasi maana hata simu walimuibia.
Baada ya siku kama tatu hivi akanipigia simu akaniambia kua alitumiwa nauli na ndugu zake hivyo anaenda zake kwao musoma. aliomba simu pale ili anijulishe kama ameondoka.
kiukwel nilifurahi sana kwa kunikumbuka kwake ila hakuwahi kunitafta tena mpaka Leo sjui alipoteza ile namba. Ama ilikuaj.
 
 
Nami niweke kisa changu japo ni chakawaida lakini kwangu ni moja ya tukio ninalo dumu nalo kwa kumshukuru sana Mungu kwaajili ya huyu ninaemzunguzia hapa.

Mwaka 1992 nilikua nakaa na bibi baada ya wazazi kufariki mwishoni mwa miaka ya 80.

92 hio bibi alipata shida ya macho na hakujaliwa kuona tena mpaka anakufa .

Mzazi wangu alikufa alikua ni mwanae wa mwisho 3 kufariki hivyo akawa hana msaada kwa chakula na mahitaji mengine ya kibinadamu.

Ilibidi awe ananituma mimi kuomba kwa majirani chakula, leo huku kesho kule mpaka 96 nilipopata nguvu kidogo nikawa naanza kufanya vibarua vya hapa na pale napata mia, mia mbili na wakati mwingine mia tano.

Ilitusaidia kununa mboga , kusaga mahindi, na vitu vidogo vidogo vya kutuwezesha kuishi.

Hii ilienda nikiwa nimetenga siku za kwenda shule , Jumatatu naenda jumanne naenda kibaruani jumatano shule alhamisi kibaruani ijumaa shule jumamosi kibaruani jumapili kanisani.

Kwa mfumo huo ndio nienda kupausua kokoto mahali mbali kidogo tokea asubuhi mpaka saa tisa alienipa kazi hajatokea, njaa inaniuma Sana hata kunyanyua nyundo nikashindwa, lakini mawazo yote yapo kwa yule bibi ambaye tokea jana hajala kitu na hapo alipo hawezi kusogea hata hatua moja.

Ilinibidi nitoke hapo niende kwa baba mmoja aliekuwa anatufahamu kwa lengo la kumuomba kazi yoyote hata nipate 500 tu nirudi nyumbani nikanunue chochote, bahati mbaya sikumkuta ila watoto tuu, niliwaambia shida yangu lakini hawakuwa na lakunisaidia .

Ilibidi niwaombe malimao nile maana ile njaa ilioniuma siku ile mwaka 97 mpaka leo naikumbuka.

Nilikula yake malimao nikapata nguvu kurudi nyumbani km kama 7 hivi, huku sijui itakuwaje kule nyumbani.

Lakini ile nafika tu saa 12 bibi ananiuliza nimefanikiwa chochote maana njaa inaniuma mno, chozi lilipotokea hata sijui.

Lakini nikasikia mlio wa gari yule baba akaja mpaka nyumbani ana unga sukari na mchele, hata nguo hakubadilisha alipoambiwa na watoto kwamba nimekuja na nimeomba kibarua, alishindwa kuvumilia hata kuingia ndani ilibidi aje atuletee chakula.

Hilo tukio ni moja ya matukio ambayo yananipa faraja sana kwamba Mungu yupo na nisikate tamaa hata kama jua limezama chochote kinaweza kutokea.

Nilipika kile chakula lakini nilishindwa kula ila bibi alikuala, shukrani niliompa yule baba mpaka leo sioni kama inatosha, yeye pengine aliona ni kawaida lakini mpaka sasa ni miaka 25 sasa sijasahau na sita sahau zaidi ya kushukuru na kuwa msaada kwa wengine.

Wema ni akiba ndugu zangu tena akiba isio na mfano.

Lakini pia kushukuru ni kwema mno.
Nimelia jamani, Mungu ni mwema saana.
 
Hii ilimtokea Mama yangu mkubwa, Anafanya biashara ya kuuza chakula. Siku moja katika kuhudumia wateja akakuta mteja mmoja amesahau wallet yake yenye pesa kama laki 6 hivi na chenchi, ikabidi aihifadhi ili mwenye pesa akija kuulizia ampatie pia ilikuwa imeshafika usiku na watu wengi wameshaondoka.

Anafanya biashara karibu na soko so wengi wa wateja wake ni wafanyabiashara. Kesho yake amesubiri kama kuna mtu atakuja kuulizia holaa, mara wiki mpaka inakaribia mwezi hakuna mtu amekuja kuulizia wallet.

Sasa siku moja akawa anaulizia kuhudu mteja wake mmoja ambae alikuwa anakula pale mgahawani, lakini siku hizi hamuoni tena.
Si ndio anaambiwa kwamba hee! Fulani mbona alishaacha biashara ya mtumba, alipoteza pesa zake zote za biashara kuna mahali alidondosha wallet yake na haikuwai kupatikana.

Ikabidi aombe msaada huyo mteja aitwe kama ndio yeye mwenye wallet. Kweli kuja kumuuliza maswali ni yeye mwenye pesa. Yaani mteja hakuamini alikuwa ameshakata tamaa hajui anaanzia wapi tena. Mpaka leo yaani wamekuwa kama ndugu.
 
Hii ilimtokea Mama yangu mkubwa, Anafanya biashara ya kuuza chakula. Siku moja katika kuhudumia wateja akakuta mteja mmoja amesahau wallet yake yenye pesa kama laki 6 hivi na chenchi, ikabidi aihifadhi ili mwenye pesa akija kuulizia ampatie pia ilikuwa imeshafika usiku na watu wengi wameshaondoka.

Anafanya biashara karibu na soko so wengi wa wateja wake ni wafanyabiashara. Kesho yake amesubiri kama kuna mtu atakuja kuulizia holaa, mara wiki mpaka inakaribia mwezi hakuna mtu amekuja kuulizia wallet.

Sasa siku moja akawa anaulizia kuhudu mteja wake mmoja ambae alikuwa anakula pale mgahawani, lakini siku hizi hamuoni tena.
Si ndio anaambiwa kwamba hee! Fulani mbona alishaacha biashara ya mtumba, alipoteza pesa zake zote za biashara kuna mahali alidondosha wallet yake na haikuwai kupatikana.

Ikabidi aombe msaada huyo mteja aitwe kama ndio yeye mwenye wallet. Kweli kuja kumuuliza maswali ni yeye mwenye pesa. Yaani mteja hakuamini alikuwa ameshakata tamaa hajui anaanzia wapi tena. Mpaka leo yaani wamekuwa kama ndugu.
Mama abarikiwe
 
Hii ilimtokea Mama yangu mkubwa, Anafanya biashara ya kuuza chakula. Siku moja katika kuhudumia wateja akakuta mteja mmoja amesahau wallet yake yenye pesa kama laki 6 hivi na chenchi, ikabidi aihifadhi ili mwenye pesa akija kuulizia ampatie pia ilikuwa imeshafika usiku na watu wengi wameshaondoka.

Anafanya biashara karibu na soko so wengi wa wateja wake ni wafanyabiashara. Kesho yake amesubiri kama kuna mtu atakuja kuulizia holaa, mara wiki mpaka inakaribia mwezi hakuna mtu amekuja kuulizia wallet.

Sasa siku moja akawa anaulizia kuhudu mteja wake mmoja ambae alikuwa anakula pale mgahawani, lakini siku hizi hamuoni tena.
Si ndio anaambiwa kwamba hee! Fulani mbona alishaacha biashara ya mtumba, alipoteza pesa zake zote za biashara kuna mahali alidondosha wallet yake na haikuwai kupatikana.

Ikabidi aombe msaada huyo mteja aitwe kama ndio yeye mwenye wallet. Kweli kuja kumuuliza maswali ni yeye mwenye pesa. Yaani mteja hakuamini alikuwa ameshakata tamaa hajui anaanzia wapi tena. Mpaka leo yaani wamekuwa kama ndugu.
Ikabidi aombe msaada huyo mteja aitwe kama ndio yeye mwenye wallet. Kweli kuja kumuuliza maswali ni yeye mwenye pesa. Yaani mteja hakuamini alikuwa ameshakata tamaa hajui anaanzia wapi tena. Mpaka leo yaani wamekuwa kama ndugu.[emoji173][emoji173][emoji173]
 
Hii ilimtokea Mama yangu mkubwa, Anafanya biashara ya kuuza chakula. Siku moja katika kuhudumia wateja akakuta mteja mmoja amesahau wallet yake yenye pesa kama laki 6 hivi na chenchi, ikabidi aihifadhi ili mwenye pesa akija kuulizia ampatie pia ilikuwa imeshafika usiku na watu wengi wameshaondoka.

Anafanya biashara karibu na soko so wengi wa wateja wake ni wafanyabiashara. Kesho yake amesubiri kama kuna mtu atakuja kuulizia holaa, mara wiki mpaka inakaribia mwezi hakuna mtu amekuja kuulizia wallet.

Sasa siku moja akawa anaulizia kuhudu mteja wake mmoja ambae alikuwa anakula pale mgahawani, lakini siku hizi hamuoni tena.
Si ndio anaambiwa kwamba hee! Fulani mbona alishaacha biashara ya mtumba, alipoteza pesa zake zote za biashara kuna mahali alidondosha wallet yake na haikuwai kupatikana.

Ikabidi aombe msaada huyo mteja aitwe kama ndio yeye mwenye wallet. Kweli kuja kumuuliza maswali ni yeye mwenye pesa. Yaani mteja hakuamini alikuwa ameshakata tamaa hajui anaanzia wapi tena. Mpaka leo yaani wamekuwa kama ndugu.
Ndio uzuri wa wema na dhamira iliyo njema, kila jema ufanyalo haliwi ni faida kwa mtu moja tu bali wengi , sawa na alivyo fanya huyo mama, amemrudishia tumaini huyo baba kwa kumrejeshea hela yake na kurudi kwenye biashara yake , riziki atajayo ipata itawafaidia wengi kuliko mama huyo angebaki na hio hela.
 
Ndio uzuri wa wema na dhamira iliyo njema, kila jema ufanyalo haliwi ni faida kwa mtu moja tu bali wengi , sawa na alivyo fanya huyo mama, amemrudishia tumaini huyo baba kwa kumrejeshea hela yake na kurudi kwenye biashara yake , riziki atajayo ipata itawafaidia wengi kuliko mama huyo angebaki na hio hela.
riziki atajayo ipata itawafaidia wengi kuliko mama huyo angebaki na hio hela.
 
 
Nilichoweza kumsaidia ni mwaka 1993 ambapo nilikutana naye akaniomba sh mia mbili ambayo nilimpa ile ya noti kipindi hicho, baada ya siku ile sikuwahi kuonana naye mpaka mwaka 2010 nilipoenda kwake na kuambulia kuonyeshwa kaburi lake!😭😭😭😭
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom