Nimepatwa na utata kidogo, sina mahali pengine pa kuuliza bila kujulikana na ninaomba ushauri wa kweli.
Pole na tatizo/mtihani/majaribu yaliyokukumba. Kwa bahati mbaya, naona majibu mengi uliyopewa yamekaa kiutani utani. Sijui km nawe uko serious kiasi gani!
Tunaambiwa kuwa ulimi ni mjumbe wa moyo. Ulimi hutoa kauli; kauli ni maneno. K/hiyo maneno hudhihirisha kilichofichwa na moyo.
Nilichojifunza kutokana na maneno yako mwenyewe ni haya:
"Uliwatolea wengi nje" k/sbb hao hawakuwa na vigezo ulivyovitaka wewe. On the contrary, huyu "mheshimiwa" anavyo vigezo hivyo. Hebu angalia lugha yako:
Nimekuwa nikiwatolea wengi nje kwa sababu najua wanachotaka ni kitu kimoja tu.
Kwanini sababu hizo hukuziona na kwa "mheshimiwa" pia? Unajuaje kuwa naye anataka hicho hicho wanachotaka wengine? Unasema:
kasema ati mke wake yuko busy sana na hawezi kusafiri mara nyingi na majaribu mengi njiani anataka awe na "mtu" ambaye anamjali n.k
Maisha hayana definition moja. Nawe ukifikwa na sababu za kutoweza kumridhisha, atafanya nini tena? Je, alitakalo yeye si lile lile ulilodai kuwatolea nje wengine? Je, ukimkubalia, huo ndio utakuwa mwisho wa hayo majaribu? Mfano ameshakuoa, na wewe ni mjamzito – huwezi kusafiri – nani atampoza na majaribu huko njiani?
Unamuangalia sana mtu kwa nje kuliko unavyomuangalia kwa ndani, na labda hili ndilo lililokufanya usidumu na mzazi mwenzako. Kumuangalia mtu kwa nje ni kuangalia, kwa mfano, mali zake, cheo chake, umashuhuri wake, and the like.
Nilimuuliza kwanini anataka kuwa nami wakati ana mke?
Kwanini hukumwambia hivi: "Siwezi kuwa nawe k/sbb unae mke" badala ya kumuuliza ulivyomuuliza? Kujiamini ndiko kunakupa msimamo, dada!
Jinsi ulivyojizuia kubaki pweke, ndivyo jinsi unavyozizuia hizo "signals" – i.e., jinsi ulivyoshindwa kujizuia, ndivyo utakavyoshindwa kuzizuia "signals".
Unajitutumua bila kufikia uamuzi hasa wa kufanya hivyo. Labda k/sbb umekosa will, know-what, and know-how, ambavyo vinakufanya ukose kujiamini na kutoa uamuzi makini. Angalia hatima ya kujitutumua kwako:
Nikajitutumua mimi mwenyewe na kwa kiasi kikubwa nimeweza kufanya mambo yangu mimi mwenyewe na maisha siyo mabaya sana.
… amekuwa akinionesha ukaribu na ukarimu katika mambo mengine na tangu wakati huo hajagusia neno lolote la mapenzi kiasi cha kuanza kumuamini na pole pole nimeanza kujikuta ninavutwa kwake. Hata hivyo sikumtumia "signal" zozote za kuashiria ninavyojisikia
Kuendelea kwako kuwa single parent ni jitihada zako za
kujitutumua tu (labda kutaka kumuonesha mzazi mwenzako kuwa unaliweza hili), lkn unaonekana hulimudu hilo. Sister, hili suala la
cold competition lipo kwa kiasi kikubwa kwa wanandoa wenye mfarakano, na nadhani ukijiweka huru utagundua kuwa nawe limekuathiri. Ni hivi: unaonekana bado unampenda mzazi mwenzako (ndio maana ukaamua kubaki "single" kwa muda wote huo), ila kuna aina fulani ya kujitoa kwako kimasomaso kumuonesha kuwa huna habari naye. Sasa umeshindwa kulivumilia hilo, ndio maana unajikuta uko njia panda.
Ulizipokea "signals" kutoka kwa "mheshimiwa" tangu awali ya kisa hiki,
… amekuwa akinionesha ukaribu na ukarimu katika mambo mengine na tangu wakati huo hajagusia neno lolote la mapenzi kiasi cha kuanza kumuamini na pole pole nimeanza kujikuta ninavutwa kwake. Hata hivyo sikumtumia "signal" zozote za kuashiria ninavyojisikia
… nawe ulizihisi hizo "signals" lkn ulikuwa ukiidanganya tu nafsi yako kuwa sizo wkt internally ulijua kuwa ndizo ila kwa hulka ya wanawake, ulikuwa ukisubiri tu muda wa ulimi wa "mheshimiwa" kudhihirisha contents za moyo wake.
K/hiyo, unaonekana kuwa jibu unalo, dada, lkn tu hujiamini, na umelileta suala hili k/sbb ya kutafuta tu kuungwa mkono kwa namna fulani. Hebu angalia "
ati ati" zako:
kasema ati mke wake yuko busy sana … amenihakikishia kuwa ati nisiwe na wasiwasi mimi na mwanangu tutaishi vizuri tu.
… na kumbe uliliona kuwa hili ni tatizo:
Sasa tatizo ni kuwa huyu bwana ana mke
… mbona bado unaendelea kutafuta ushauri?
Na hili nalo la kuliona suala lako ni muhimu lkn …
Kwa kweli, najua ni jambo la kipuuzi.
USHAURI WANGU:
· Usikurupuke kutoa jibu. Jipe muda kumchunguza na kujichunguza wewe mwenyewe km kweli ulitakalo ndilo hilo. Ukimpa jibu la haraka huenda hiyo the so-called "ndoa" ikachukua indefinite time, na hivyo kuhalalisha uhawara – hapo utakuwa umelamba "Joker".
· Suala la ukewenza linaendana na imani ya mtu. Kabla ya ushauri mwingine, hivi wewe dada ni dini gani?
· Usiangalie mambo ya nje ya mtu, km mali, cheo, umaarafu, … k/sbb hivyo huenda vikaondoka, na ukabaki unajuta. Angalia mambo ya ndani ya mtu, km uaminifu, kujali, upendo wa kweli (unconditional love), ushirikiano, uvumilivu, … kadri Alivyokujaalia Mungu. Kipimo cha kwanza ni kumwambia kuwa huwezi kutoa jibu la haraka k/sbb hukuwa na mpango wa kuolewa. Hapo utaona uvumilivu na upendo wake kwa kiasi fulani.
· Ichunguze ndoa yake.
Mengine baadae, km nitapata muda, au wengine wataendeleza.