Single mother ananing'ang'ania

Single mother ananing'ang'ania

Nonji

Member
Joined
Nov 22, 2017
Posts
29
Reaction score
26
Habari wana jamii,
Mimi ni mume wa mke mmoja na kutokana mambo ya kazi Sikai na familia yangu mkoa mmoja hapo ni mikoa ya jirani kidogo kama mwendo wa masaa manne kwenda.

Maisha haya nimeyaanza muda kidogo tangu 2022 lakini nimekuwa nikijaribu kujicontrol kuepuka vishawishi vya kuingia kwenye mahusiano na wanawake wengine. Ila mwaka jana wakati nafanya shopping ya familia kwa ajili ya Christmas nilikutana na binti mmoja miaka kama 28 ana mtoto mmoja wa kiume wa miaka tisa.

Aliniuzia nguo akiwa ananichagulia kwa kuangalia picha za wahusika na kunishauri nguo za kuchukua.

Sasa tukajikuta tumebadilishana namba za simu na mawasiliano yakaanza na sasa naona anataka mahusiano ya kimapenzi na anasumbua kwelikweli. Anadai alipewa mimba 2016 na mwalimu wake na akamkataa.

Wakuu mimi kama mwanaume mnavyojua kuna kaudhaifu ketu ila sasa nafsi mbili zinapata vita kali sana kwangu moja unataka nyingine inapinga na sababu kubwa ni kwamba simfahamu vizuri na katika maelezo yake kuna mengine yananitia shaka lakini bado hatujaanza mahusiano ya kimapenzi bado tuliwahi kuongea kuhusu kwenda kupima ndipo tuanze lakini kila kukicha napata mgogoro wa nafsi inayopinga kesho yake napata mgogoro wa nafsi inayotaka kuingia kwenye haya mahusiano.

Ebu kwa uzoefu wenu nipeni ushauri hapa ili niamue kusuka au kunyoa ninyi mnajua mengi na mnaona mbali pia maisha kusaidiana.
 
Achana naye, ukizidiwa muite mkeo masaa manne sio mbali na hapo!
Ni limalaya tu dada lisimalize akili zako kwamba masaa manne kuna umbali gani kwenda kwa mkewe na kurudi kazini kila siku ?
Watu wanasafiri masaa mpaka kumi na mbili daily ili abaki karibu na familia yake alafu pajamas kamoja kanalalamika kuhusu masaa manne kumkwepa shetani like serious ?
 
Ni limalaya tu dada lisimalize akili zako kwamba masaa manne kuna umbali gani kwenda kwa mkewe na kurudi kazini kila siku ?
Watu wanasafiri masaa mpaka kumi na mbili daily ili abaki karibu na familia yake alafu pajamas kamoja kanalalamika kuhusu masaa manne kumkwepa shetani like serious ?
Sio malaya bwana huoni anaumiza kichwa kwa dem mmoja? Malaya hanaga muda wa kufikiri anatia tu kila anayejipitisha!

Ila wanaume, eti singo maza ananing’ang’ania! My pride can’t🤭
coz wtf😫
 
Hapa utapata kila aina ya ushauri kwa watu wengi tu ambao wala huwajui but at the end maisha ni yako na utabaki peke yako,

Kua makini sana usije ukaharibu maisha yako kwa starehe au tamaa ya madakika tu,
respect ur wife and be honest.
 
Habari wana jamii,
Mimi ni mume wa mke mmoja na kutokana mambo ya kazi Sikai na familia yangu mkoa mmoja hapo ni mikoa ya jirani kidogo kama mwendo wa masaa manne kwenda.

Maisha haya nimeyaanza muda kidogo tangu 2022 lakini nimekuwa nikijaribu kujicontrol kuepuka vishawishi vya kuingia kwenye mahusiano na wanawake wengine. Ila mwaka jana wakati nafanya shopping ya familia kwa ajili ya Christmas nilikutana na binti mmoja miaka kama 28 ana mtoto mmoja wa kiume wa miaka tisa.

Aliniuzia nguo akiwa ananichagulia kwa kuangalia picha za wahusika na kunishauri nguo za kuchukua.

Sasa tukajikuta tumebadilishana namba za simu na mawasiliano yakaanza na sasa naona anataka mahusiano ya kimapenzi na anasumbua kwelikweli. Anadai alipewa mimba 2016 na mwalimu wake na akamkataa.

Wakuu mimi kama mwanaume mnavyojua kuna kaudhaifu ketu ila sasa nafsi mbili zinapata vita kali sana kwangu moja unataka nyingine inapinga na sababu kubwa ni kwamba simfahamu vizuri na katika maelezo yake kuna mengine yananitia shaka lakini bado hatujaanza mahusiano ya kimapenzi bado tuliwahi kuongea kuhusu kwenda kupima ndipo tuanze lakini kila kukicha napata mgogoro wa nafsi inayopinga kesho yake napata mgogoro wa nafsi inayotaka kuingia kwenye haya mahusiano.

Ebu kwa uzoefu wenu nipeni ushauri hapa ili niamue kusuka au kunyoa ninyi mnajua mengi na mnaona mbali pia maisha kusaidiana.
Mkuu,

Ukiaa naye huyo kimapenzi uwe naye kwa lengo la kumuoa na kabla ya kuwa naye umshirikishe mke wako na familia yako, hususan mke wako akukubalie.

Vinginevyo, utajiingiza kwenye majaribu, migogoro, kung'ang'aniwa, na gharama bila sababu ya msingi.

Listen to a brother who knows.
 
Hapa utapata kila aina ya ushauri kwa watu wengi tu ambao wala huwajui but at the end maisha ni yako na utabaki peke yako,

Kua makini sana usije ukaharibu maisha yako kwa starehe au tamaa ya madakika tu,
respect ur wife and be honest.
mkanganyiko huohuo wa nafsi inayo mwambia fanya, usifanye ataupata na huku kwa kupewa majibu yote mawili 😁😁😁

all in all achague sahihi zaidi
 
Mkuu,

Ukiaa naye huyo kimapenzi uwe naye kwa lengo la kumuoa na kabla ya kuwa naye umshirikishe mke wako na familia yako, hususan mke wako akukubalie.

Vinginevyo, utajiingiza kwenye majaribu, migogoro, kung'ang'aniwa, na gharama bila sababu ya msingi.

Listen to a brother who knows.
Hiyo ni ngumu! Hiyo vita itabidi mpatanishi awe karibu sana na well informed 😂 😂 😂
 
Kataa zinaa. Utakwenda jehanamu kama utaendelea na hayo mawazo yako maovu kichwani.
 
Back
Top Bottom