Nimewapiga wachawi—kipigo cha mbwa koko!

Nimewapiga wachawi—kipigo cha mbwa koko!

Kama hukubaliani na andiko hilo. Na hili je?
Luka 10:17–19
Ndipo wale sabini waliporudi kwa furaha, wakisema, Bwana, hata pepo wanatutii kwa jina lako. Akawaambia, Nilimwona Shetani, akianguka kutoka mbinguni kama umeme. Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru.

Hapo wanaposema "wanatutii kwa Jina lako," ni nani anaambiwa kama si Yesu?
Aliyesema "nimewapa amri ya kukanyaga nyoka" ni nani kama si Yesu?

Wewe kama unabishi, acha sisi tuendelee kulitumia Jina la Yesu kuyachapa mapepo.

Huyo aliyeandika ni Luka na yeye ameanza Luka1;1 kuandika kuwa hizo ni hadithi alizosikia kwa watu mitaani akaamua kumwandikia Theophilus , si wewe wala Mimi . Pia Hao waliozichapisha wanasema hakuna uthibitisho wa Luka kuandika hizo hadithi ndio ikaandikwa Injili Kama alivyotuhadithia Luka.
Usifikiri kuwa nakataa Mimi Tu Laa! ni Hao waliochapisha hizo biblia ndio wanasema hivyo. Siye Mimi. Ukitaka ushahidi wa biblia nitakuwekea
 
MKUU 🤣🤣

Sawa tunaamini katika KRISTO lakini kuna vitu sio shetani wala nini ni mwili wako tu ndio unayafanya hayo kaka.

Kuna kitu kinaitwa "KUPARALAIZ USINGIZINI" hii inatokana vitu vifuatavyo.
1. Kulala vibaya - umejikunjakunja

2. Oxygen debt - washa feni elekeza upande mwingie yaan upepo usikuguse dorect acha hewa iwepo ndani inazurula

3. Mazingira unayolala yaangalie pia.

UKIONA BADO YAPO BASI PIGA GOTI ITA YESU AJE AOKOE JAHAZI.
Isome vizuri hiyo sayansi ya Sleep Paralysis utaona jinsi ilivyo feki. Wenye SP huwa wanasema wanasikia sauti ya watu wanatembea, au wanaona mtu yuko karibu na kitanda. Sasa wanasayansi wanakubaliana na hizo shuhuda lakini waambie wa-prove kisayansi kama wataweza. Mapepo huwezi kuyaona kwa zana za kisayansi.
 
Huyo aliyeandika ni Luka na yeye ameanza Luka1;1 kuandika kuwa hizo ni hadithi alizosikia kwa watu mitaani akaamua kumwandikia Theophilus , si wewe wala Mimi . Pia Hao waliozichapisha wanasema hakuna uthibitisho wa Luka kuandika hizo hadithi ndio ikaandikwa Injili Kama alivyotuhadithia Luka.
Usifikiri kuwa nakataa Mimi Tu Laa! ni Hao waliochapisha hizo biblia ndio wanasema hivyo. Siye Mimi. Ukitaka ushahidi wa biblia nitakuwekea
Wewe una lako jambo. Hadithi unazosikia mtaani zinaweza kuwafanya vipofu wakaona, viziwi wakasikia, viwete wakatembea? Jina la Yesu ndilo linalotenda hayo. Na mimi nimeshuhudia miujiza mingi kwa kutamka Jina la Yesu. Hivyo sielewi unachobisha ni nini. Kama wewe unaona Biblia ni hadithi endelea kuamini hivyo lakini mimi nimefaidi mengi kwa kuamini kuwa Biblia ni Neno la Mungu lililo hai.
 
Babu yako alipamban na huyo shetani kamshindwa hajawahi kumuua na wewe unapambana nae utamshindwa hadi mjukuu wako itakua hivyo hivyo
Shetani ni kama nzi tu. Tunamshinda kirahisi sana kwa kutamka Jina la Yesu. Kazi yetu ni kumfukuza anapotuijia. Ila kwakuwa yuko kama nzi ukimfukuza baada ya muda anarudi tena. Akirudi hatuchoki tunamfukuza tena. Ni mwendo huohuo mpaka Yesu atkapordi. Hatutakiwi kumuua. Kwanza hafi kwa sababu ni roho. Ila saa yake ya kutupwa motoni inakuja, na moto umeishaandaliwa kwa ajili yake.
 
Hiyo ni Sleep paralysis inatokana haswa na mtindo mbovu wa maisha.

Kutokuwa na utaratibu maalumu wa kula, Uchovu mwingi, Stress, Kulala chali na kuchelewa kulala ni moja ya visababishi.
😆😆😆😆
 
Ushahidi gani tena unaotaka zaidi ya ushuhuda huu nilioandika katika uzi huu? Kama Yesu angekuwa hajaagiza tutumie Jina lake unafikiri hao wachawi wangekimbia? Si wangeninyonga?
Wacha kujipakazia , mchawi gani akujie wewe ili apate nini kwako ? Umeshiba maharage mengi na ugali usiku , gesi imekujaa unakuja kutumwagia upepo JF, Yesu haäwezi kuwaambia watu watumie jina lake. Huo ni ushirikina
 
Hii ni habari ya kweli kabisa. Uongo mimi nauchukia kama ukoma.

Kama huamini kuna wachawi, sikiliza vizuri: Hivi majuzi, walikuja usiku, muda mfupi baada ya mimi kujilaza kitandani. Wakaanza kunikandamiza kwa nguvu sana. Mgandamizo ulikuwa mzito, utafikiri mtu ameweka juu yangu mifuko mitano yenye saruji. Sio mzaha, nakwambia.

Sijawahi kuhisi uzito huo kamwe. Haraka sana nilitambua ni wachawi wanaotumiwa na mapepo kujaribu kunidhuru. Nikaanza kuwakemea kwa Jina la Yesu - kwa sauti ndogo, lakini yenye mamlaka watoke na kuniachia. Instantly, waliniacha na mgandamizo ule ukatoweka. Jina la Yesu lina nguvu sana. Ukilitamka, wachawi wanapigwa kipigo kikali sana na kukimbia. Hii ni mojawapo ya faida za kuokoka. Unatembea kifua mbele bila kuogopa wachawi.

Yakobo 4:7-10
"Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili. Huzunikeni, na muomboleze, na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni. Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua."
Kawaida watu wengi walio okoka wanakuwa wamepitia mambo mengi sana mpaka kufikia kuokoka, wengi wao wanakuwa wamechoka kujiuza mitaani na mitandaoni na wengine wanakimbia uchawi wa kifamilia. Wewe mwenzetu ulikimbia nini mpaka kuokoka?
 
Hii ni habari ya kweli kabisa. Uongo mimi nauchukia kama ukoma.

Kama huamini kuna wachawi, sikiliza vizuri: Hivi majuzi, walikuja usiku, muda mfupi baada ya mimi kujilaza kitandani. Wakaanza kunikandamiza kwa nguvu sana. Mgandamizo ulikuwa mzito, utafikiri mtu ameweka juu yangu mifuko mitano yenye saruji. Sio mzaha, nakwambia.

Sijawahi kuhisi uzito huo kamwe. Haraka sana nilitambua ni wachawi wanaotumiwa na mapepo kujaribu kunidhuru. Nikaanza kuwakemea kwa Jina la Yesu - kwa sauti ndogo, lakini yenye mamlaka watoke na kuniachia. Instantly, waliniacha na mgandamizo ule ukatoweka. Jina la Yesu lina nguvu sana. Ukilitamka, wachawi wanapigwa kipigo kikali sana na kukimbia. Hii ni mojawapo ya faida za kuokoka. Unatembea kifua mbele bila kuogopa wachawi.

Yakobo 4:7-10
"Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili. Huzunikeni, na muomboleze, na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni. Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua."
Huo nao ni uvhswo
 
Hii ni habari ya kweli kabisa. Uongo mimi nauchukia kama ukoma.

Kama huamini kuna wachawi, sikiliza vizuri: Hivi majuzi, walikuja usiku, muda mfupi baada ya mimi kujilaza kitandani. Wakaanza kunikandamiza kwa nguvu sana. Mgandamizo ulikuwa mzito, utafikiri mtu ameweka juu yangu mifuko mitano yenye saruji. Sio mzaha, nakwambia.

Sijawahi kuhisi uzito huo kamwe. Haraka sana nilitambua ni wachawi wanaotumiwa na mapepo kujaribu kunidhuru. Nikaanza kuwakemea kwa Jina la Yesu - kwa sauti ndogo, lakini yenye mamlaka watoke na kuniachia. Instantly, waliniacha na mgandamizo ule ukatoweka. Jina la Yesu lina nguvu sana. Ukilitamka, wachawi wanapigwa kipigo kikali sana na kukimbia. Hii ni mojawapo ya faida za kuokoka. Unatembea kifua mbele bila kuogopa wachawi.

Yakobo 4:7-10
"Basi mtiini Mungu. Mpingeni ibilisi, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia. Itakaseni mikono yenu ninyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu ninyi wenye nia mbili. Huzunikeni, na muomboleze, na kulia. Kicheko chenu na kigeuzwe kuwa kuomboleza, na furaha yenu kuwa huzuni. Jinyenyekezeni mbele za Bwana, naye atawainua."
Ni kuongoka sio kuokoka.
 
Unawezaje kuthibitisha kuwa huyo Roho wa Mungu unayedai anakufunulia si mawazo yako tu au hisia zako potofu?

Unajuaje kama huo ni udanganyifu wa nafsi tu?
Kwanini kila mkristo akishindwa kujibu swali anakimbilia kusema mpaka uwe na roho ndiyo utaelewa?

Kwanini lazima niamini kwanza ndipo nipate majibu na siyo nipate majibu kwanza ili niweze kuamini?
Achana na mental health people mkuu hapa utakesha kubishana na machizi...corrupted minds all in the name of religion ..
 
Marko 16: 17
Na ishara hizi zitafuatana na hao waaminio; kwa jina langu watatoa pepo; watasema kwa lugha mpya;

Aya hizo ni uzushi ,aya yako sasa inatambulika ulimwenguni kote kuwa "imeingizwa" baadaye na Kanisa na matoleo yote ya hivi karibuni ya Biblia, kama vile Revised Standard Version the New Revised Standard Version, New American Standard Bible, New English Bible, Phillips Modern English Bible ... nk. wote wameifuta aya hii katika biblia zao .

Bila ya kujali. Kwa nini hii? Mfasiri wa maandiko Benjamin Wilson anatoa maelezo yafuatayo kwa kitendo hiki katika "Emphatic Diaglott" yake. Bwana Wilson anasema:

"Maandiko haya yanayohusu ushuhuda wa mbinguni hayamo katika hati yoyote ya Kigiriki ambayo iliandikwa mapema zaidi ya karne ya kumi na tano.

Haijatajwa na yeyote kati ya waandishi wa kikanisa; si na baba yeyote wa mapema wa Kilatini hata wakati masomo ambayo walishughulikia kwa kawaida yangewaongoza kukata rufaa kwa mamlaka yake. Kwa hivyo ni dhahiri kuwa ni ya uwongo."
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom