Hatua za kufuata ili kuacha kuvuta Sigara

Sosoma Jr

JF-Expert Member
Aug 7, 2020
312
281
HATUA ZA KUACHA KUVUTA SIGARA

Madhara ya kiafya yatokanayo na uvutaji sigara ni makubwa na yanahatarisha si tu uhai wa mvutaji bali hata na watu wengine wanaovuta moshi kutoka kwa mvutaji. Kwa upande mwingine, hakuna faida yoyote anayopata mvutaji, hivyo wavutaji wa sigara wanashauriwa waache uvutaji.

Zifuatazo ni hatua saba zilizothibitishwa zinazoweza kukusaidia kuacha uvutaji wa sigara.

1. ELEWA KWAMBA KUVUTA SIGARA NI DHAMBI DHIDI YA MWILI WAKO NA MUNGU WAKO
Zaidi ya kuharibu afya ya kimwili, sigara pia huharibu afya ya kiroho ya mvutaji. Biblia inautaja mwili wa mwanadamu kuwa ni hekalu la kiroho ambamo Mungu Roho Mtakatifu anaishi, soma katika 1 Wakorintho 6:19-20 na Warumi 12:1. Uvutaji wa sigara huharibu hekalu hilo. Roho Mtakatifu hawezi kuishi katika hekalu lililoharibika. Kwa sababu hiyo, Mungu anatuonya dhidi ya kuharibu hekalu lake. Ukijua kuwa kuvuta sigara ni dhambi, utaamua kuacha.

2. KIRI KWAMBA WEWE NI MDHAIFU NA HUWEZI KUACHA MWENYEWE
Inawezekana umehangaika sana ukijaribu kuacha kuvuta sigara. Inawezekana umetafuta msaada kwa miaka mingi kama yule mgonjwa aliyekuwa ameugua kwa muda wa miaka 38 (soma Yohana 5:5-8). Ili uweze kushinda tabia hii, kubali kwamba wewe ni dhaifu. Kiri kwamba huwezi kufanikiwa wewe mwenyewe. "Pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote." (Yohana 15:5). Kwa kukiri hivi utajikabidhi mikononi mwa Mungu Akusaidie.

3. AMINI KWAMBA JAPOKUWA WEWE NI MDHAIFU, MUNGU ANA NGUVU JAPOKUWA HUWEZI, YEYE ANA UWEZA WOTE
Tunapoamua kuweka makusudi yetu dhaifu yenye kusitasita chini ya makusudi ya Mungu, uweza wote uliomo ulimwenguni utakuwa wetu. Tukimwomba Mungu atatuwezesha kushinda tusiyoyaweza. "Nayaweza yote katika Yeye anitiaye nguvu" (Wafilipi 4:13).

4. JITOE KWA MUNGU
Ili Mungu aweze kukupa ushindi dhidi ya tabia hii ya uvutaji ni lazima ujitoe kikamilifu kwake. Mungu hawezi kukupa ushindi bila wewe kukubali kushirikiana naye. Soma 2 Wakorintho 6:2. "Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure."

5. AMINI KWAMBA SASA USHINDI NI WAKO KISHA MSHUKURU MUNGU
Baada ya kukubali na kujisalimisha kwa Mungu sasa umeshinda na umshukuru Mungu kwa kukupatia ushindi dhidi ya kuvuta sigara. "Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo." (1 Wakorintho 15:57).

6. HARIBU SIGARA ZOTE
Ili usipate tena ushawishi wa kuvuta sigara inabidi ukae mbali na sigara. Kama ulikuwa na sigara nyumbani kwako amua kuzitupa au kuziharibu zote na usibakize hata moja mahali ulipo. Jitoe kwa Mungu na umpinge shetani. "Basi mtiini Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia. Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi. Itakaseni mikono yenu, enyi wenye dhambi, na kuisafisha mioyo yenu, enyi wenye nia mbili." (Yakobo 4:7-8).

7. FUATA KANUNI ZIFUATAZO ZITAKUSAIDIA
Hata baada ya kuacha kuvuta sigara, bado kuna wakati utakuwa unajisikia hamu ya kuvuta. Zaidi ya kufuata hatua zilizotajwa hapo juu, unaweza kuchukua hatua zingine kwa ajili ya kukusaidia kuepukana na majaribu ya kuvuta sigara. Ili kuondoa hamu ya kuvuta sigara, fanya yafuatayo:
  • Unapokuwa na hamu ya kuvuta sigara, vuta pumzi taratibu kwa kina hadi hamu itakapokwisha.
  • Kunywa bilauri (glasi) 10 hadi 12 za maji kila siku kwa siku tano mfululizo.
  • Pumzika kwenye maji ya uvuguvugu katika bafu kabla ya kulala.
  • Panga kulala saa zisizopungua nane kila siku.
  • Epuka kutumia kinywaji cha kahawa au pombe.
  • Fanya mazoezi ya kutembea kwa dakika zisizopungua 30 mara mbili kwa siku.
  • Endelea kumsifu Mungu kwamba uweza wake ni mkubwa.
Imani yangu ni kuwa kama utafuata hatua hizi kwa uaminifu, Mungu atakusaidia kushinda tabia ya uvutaji wa sigara. Bwana akubariki na kukushindia.

Ewe ndugu yangu mpendwa tafuta kanisa la Waadventista wa Sabato linaloabudu siku ya jumamosi na ibada inaanza saa tatu asubuhi mpaka saa sita mchana hudhulia hapo hutajuta kamwe kwa mafunzo utakayoyapata ya kiroho na kimwili. Barikiweni nyote.
 
Habari wadau.? Kama mada inavyojieleza hapo juu mimi ni kijana wa miaka 29 ambae ni baba wa mtoto mmoja (Baba Rahma) nilijiingiza kwenye uvutaji wa sigara tangu mwaka 2017 mpka hivi sasa 2023. Kiukweli hakuna kitu ninachojilaumu na kujuta maishani kama kuingia kwenye hili kundi maana kutoka inaniwia ugum sana nimejitahid kadri niwezavyo ili niweze kuondoka kwenye uvutaji wa sigara lkn mwisho wa siku najikuta narudi tena kwenye uvutaji.

Kun kipindi kweli nakuwa na nia ya kuacha na ninakaa ata wiki bila kuvuta lakini siku nikimuona mtu anavuta ndio kama ananitamanisha na mm nivute, nitanunua na nitajisemea hii ndio mala ya mwisho kuvuta lkn waaap nitarudia tena na tena. Nimekuja hapa na kuandika huu uzi ili kuomba msaada kwa wadau anaejua njia au namna ya kuacha kuvuta sigara tafadhari anisaidie, hii tabia inanitesa sana. Nakaribisha maoni, ushauri nk...
 
Acha kujiendekeza hamna mbinu yoyote ya kuacha sigara ni maamuzi tu kwamba mimi naamua kuacha sigara ukisubiri upate mbinu trust me utavuta hiyo misigara yako hadi wakati wa kutwaliwa roho yako
 
Punguza idadi ya sigara, kama kwa siku ulikuwa unavuta 5, sasa hivi vuta 1.
Kidogo kidogo baada ya miezi mi3 kuna siku utajikuta unapitisha huvuti, ikishakuwa tabia utajikuta unaacha.

Pia acha urafiki na wavuta sigara, kaa nao mbali. Badili marafiki
 
Punguza idadi ya sigara, kama kwa siku ulikuwa unavuta 5, sasa hivi vuta 1.
Kidogo kidogo baada ya miezi mi3 kuna siku utajikuta unapitisha huvuti, ikishakuwa tabia utajikuta unaacha.

Pia acha urafiki na wavuta sigara, kaa nao mbali. Badili marafiki
Asante
 
Acha kujiendekeza hamna mbinu yoyote ya kuacha sigara ni maamuzi tu kwamba mimi naamua kuacha sigara ukisubiri upate mbinu trust me utavuta hiyo misigara yako hadi wakati wa kutwaliwa roho yako
Naiman ww hujawahi kupitia situation kama hii lkn najitahid sana somtime nakaa ata siku 4 lkn kuna alosto kaka, ila ntafanyia kazi ushauri wako
 
Screenshot_20230428-025440~2.png
 
Naiman ww hujawahi kupitia situation kama hii lkn najitahid sana somtime nakaa ata siku 4 lkn kuna alosto kaka, ila ntafanyia kazi ushauri wako [emoji1
Mimi nimevuta sigara muda mrefu niliacha 2008 nikaanza tena 2012 mpaka 2016 ndio nikaacha, sijavuta tena sigara toka mwaka huo sikutumia trick yoyote nilijiamulia tu kuwa naacha sigara ni maamuzi tu mjomba
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom