Nimepigwa zongo wakati nikila chakula

Nimepigwa zongo wakati nikila chakula

Nilihisi utakuwa Arusha wana huo mchezo balaa,nliteseka sana kipindi cha nyuma nkaenda kupewa dawa na baba mmoja hivi wa Kiarusha,ndo nkapona
Duhh....[emoji45] [emoji45] [emoji45]
 
Hyo kitu wataalam wake wapo Tarime na Sirari,wao huiita voucher so, labda kama unae ndugu au jamaa Wa mazingira hayo anaweza kukusaidia lakn hata Umasaini wataalam Wa hyo kitu wapo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Dawa ya zongo ipo upareni bana...inatwa dawa ya jiwe pia wenyeji huiita makata japo si jina rasmi sana..ni ya unga wa chumvichumvi ina kaukakasi fulanihivi..wasiliana na watu wa upareni watakusaidia.
Au ogea maji yaliyochanjwa na matunda ya ndulele weka kama matunda 6 hivi koroga kwa nguvu hadi itoe povu jingi kisha ogea hayo maji kwisha kazi..
 
Dawa ya zongo ipo upareni bana...inatwa dawa ya jiwe pia wenyeji huiita makata japo si jina rasmi sana..ni ya unga wa chumvichumvi ina kaukakasi fulanihivi..wasiliana na watu wa upareni watakusaidia.
Au ogea maji yaliyochanjwa na matunda ya ndulele weka kama matunda 6 hivi koroga kwa nguvu hadi itoe povu jingi kisha ogea hayo maji kwisha kazi..
du!
 
Ingependeza kama ningepata maelezo mazuri kutoka kwako

Mara nyingi ninaposikia habari zenye utata kama hizi ( uchawi) kutoka kwa mtu huwa ana refer to 3rd person yeye huwa hana

Either nilisimuliwa au kuna mtu alishuhudia

Sent using Jamii Forums mobile app
Mi sio mtaalamu wa haya mambo na ndiyo maana nikakwambia uende tanga kwenye wataalamu,ila tatizo ushaanza kupinga jambo ambalo bado hata hujalielewa vizuri unafikiri itakuaje?
 
Dawa ya zongo ipo upareni bana...inatwa dawa ya jiwe pia wenyeji huiita makata japo si jina rasmi sana..ni ya unga wa chumvichumvi ina kaukakasi fulanihivi..wasiliana na watu wa upareni watakusaidia.
Au ogea maji yaliyochanjwa na matunda ya ndulele weka kama matunda 6 hivi koroga kwa nguvu hadi itoe povu jingi kisha ogea hayo maji kwisha kazi..

magadi hayo baba, achukue yale magadi ya mawe asage alambe
 
Zongo nijuavyo ni aina ya uchawi uletao madhara kupitia macho...yaani mtu mwenye aina hii ya nguvu za kichawi anapokuangalia hususani unapokuwa unakula kitu(baada ya kula tumbo linaweza kuuma au kuharisha,kujaa gesi n.k) au umeshika chakula ambacho hakijapikwa halafu ukaenda kukipika kinaweza kisiive kwa wakati kama ulivyozoea.mf.kny masherehe vyakula vilivyoko jikoni vinaweza pigwa zongo mkashangaa mnapika lakini pido au ndizi haziivi kabisa yani.
Watu wengi wenye aina hii ya uchawi huwa hawajijui kama wanao ila jamii inawajua kuwa wanamadhara katika maeneo hayo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom