Nimepigwa zongo wakati nikila chakula

Nimepigwa zongo wakati nikila chakula

Ni uchawi tumbo linajaa hewa na hupati choo wala hujambi
Hiyo ni moja ya aina za zongo, ziko aina kibao. Ni style fulani ya kuchezeana hivi. Kuna dogo mmoja alipigwa ya homa kama malaria hivi, ilikuwa siku ya msiba wa baba yake. Ilikuwa Korogwe. Wazee wakamchana fagio lenye mate akapona. Mara nyingi hupigana wanaofahamiana kiasi,na hasa ukiwa mgeni.
 
Mkuu nitumie hilo ZONGO tumalize ubishi

Knowledge yangu ndogo kwenye medical field nitaitumia nitapona bila hayo mazingaumbwe yenu ya kichawi

Sent using Jamii Forums mobile app
Nilishakwambia kuwa mie sio mtaalamu wa hayo mambo sasa iweje tena unaniambia nikutumie hilo zongo ambalo hauliewi?

Kama unahisi kuwa watu wakiwa hawana uelewa na jambo ndiyo husingizia uchawi basi pia isingewezekana kwa watu hao wakawa na ufumbuzi wa hilo jambo ambalo hawalielewi, mfano hilo zongo ambalo hawalielewi lakini wanajua tiba zake na hatuoni mtu kwenda hospitali kudai anaumwa zongo.

Ndiyo maana nakushangaa unapotoa hitimisho wakati hata haujui hilo zongo ni nini.
 
Hamna maelezo ya kitaalam kweli kuhusiana na hiyo hali?

Sent using Jamii Forums mobile app
Ushaambiwa ni ugonjwa unaosabaishwa kimazingara kwa kutumia macho, Tumbo linajaa gas, unakosa hamu ya kula kazi ni kucheua tu na wakati mwingine kujamba, tumbo linakuwa kubwa na gumu na wakati mwingine likiandamana na maumivu, wakati mwingine unaweza kosa choo kubwa hata siku tatu.
 
Ninahitaji msaada wa kitaalamu juu ya hili tatizo kwani linanisumbua sana na pia linaweza kumpata mtu bila kujua kwani huwa katika mazingira usiyoweza kuyaona kwa macho.

Hivyo kwa mtu yeyote anayefaamu kautaalamu kakutegua afanye kweli kuokoa jahazi. Siku hizi kila kona ni mawindoni

Sent using Jamii Forums mobile app
Tafuta matunda yanaitwa ndulele yachome , mvuke jifukishe nao. Au majivu yake jipake.
 
Mnaweza kuniona niwapatie hiyo dawa ya zongo kwa jina rahisi tunaita makata
 
Ni uchawi tumbo linajaa hewa na hupati choo wala hujambi
Dawa yake ndogo sana. Lipake Tumbo mafuta ya nguruwe kisha sugua tumbo na sabuni ya magadi pamoja na maji ya ubuguvugu. Hutaliona LIVE ila wakati linatoka utahisi umeshika vimawe vidogo au changarawe kama umetupiwa na mwanamke
 
Dah! Na kiwango changu chote cha ufahamu sijaweza kuelewa uzi huu unazungumzia nini. Naona wenzangu mmeelewa naomba mnisaidie kufafanua.
Huu uzi unahusu watu wenye elimu ndogo kuanzia std 7 tena ambao wanaishi uswahilini
Ila wewe uliyesoma ST FRANSIACO UK na ukija likizo unafikia kwa wazazi wako Masaki huwezi kuelewa kitu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom