Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 92,232
- 113,610
Nakubaliana na wewe 100%.
Pamoja na mazuri yote ya Clouds kwa jamii haimaanishi watangazaji wa Clouds wote ni wazuri 100%. Usifanye majumuisho ya jumla vinginevyo mizani yako haitatenda haki.
Ninapoona watu wanasema eti Kibonde sijui anatumia ARVs, mara Kibonde sijui nini, mara Diva kafanya hivi na mashuzi mengine kama hayo huwa nakereka sana. Mimi hapa nipo kuleta uwiano tu. Sisemi kwamba hawana mabaya. Kwani ni nani huyo mwenye mazuri tu? Lakini kuwafanya Clouds kama ni watu wabaya sana kama virusi hilo nalikataa na nitawatetea bure mpaka siku nitakayovuta pumzi yangu ya mwisho.
Ingawa umesema target group yao ni hadi miaka 34 basi kuna mgongano pale wanapojiita "redio ya watu" ikimaanisha watu kwa ujumla wao.
Channel 5 wao wanajitambulisha kama Tv na.1 ya vijana, kwa hiyo wazee pale sio mahali pao.
Ila napenda kwamba umejitambulisha upande upi wewe unasimamia.
Hakuna mgongano kwenye kauli mbiu yao. Kwani hiyo age group siyo watu? Na hilo la watu wote kwa ujumla wao ni tafsiri yako tu ambayo una haki kuwa nayo. But I caution you not to be so literal on everything.