Nimemfuma kaka yangu anaabudu mizimu

Nimemfuma kaka yangu anaabudu mizimu

si ajabu ibada zako wewe ndio za kipumbafu.Una uhakika gani kuwa YESU ndio yuko sahihi.Je una uhakika gani kuwa mtume Mohamedi ndio yuko sahihi?
hivi unajua wazungu walitumia dini unayoabudu wewe kutuingiza chaka tukatawaliwa?hivi unajua waarabu pamoja na kutuletea dini lakini pia walikuwa wanatufanya watumwa.
Wewe ndio unaonekana mpumbafu kile kitendo cha kwenda kujisaidia porini inaonekana hujastarabika.
Muache kaka yako unachoamini wewe sio lazima umlazimishe mtu amini
na ndio maana mimi nasemaga dini ni kama vyama vya siasa kila dini inatafuta njia ya kumuabudu mungu
Ulaniwe ewe roho itokayo kuzimu. Ingekuwa dini zililetwa kutupumbaza basi huko zilikotoka kusingekuwa na makanisa wala misikiti maana wanajua ilikuwa ni kwaajili ya kutupumbaza tu Waafrika. Lakini mbona hata wao wanazidi kuabudu inamana wazungu wanaoabudu wanajidanganya kwa kitu wanachokijua?. Mfano unajua fika kuwa dawa flani haiponyi nilidanganya wagonjwa ili wafe je wewe mtengenezaji utaendelea kunywa hiyo dawa ilihali unajua kabisa wewe ndoumetengeneza na ukinywa itakuua?.
 
Samahani sikuweza kumpiga picha angeniona.

Kweli mnaweza mkawa Familia moja mkidhani ni watu wa dini lakini Kuna mmoja yupo tofauti. Ni kaka etu wa kwanza kwenye Familia nimeshuhudia kwa macho yangu katika kipindi hiki nipo kijijini, nilipotoka kanisani ikabidi nichukue baiskel kwenda shambani lakini nilipofika shambani sikumkuta. Nikafikli labda yupo ndani ya shamba ngoja nimuangalie.

Nilipoona mzigo nyuma umenilemea niliingia polini na kidumu cha maji kwenda kuushusha, lahaulaah!

Sikuamini macho yangu ni kaka angu kabisa anainama na kuinuka huku akisujudu mti. Nikaona sio kweli ikabidi nijifiche ila nilichokishuhudia nikajua kumbe ndomambo yake sisi jumapil kila tukienda kanisani yeye huwa anasema naenda shambani kumbe ana ibada zake za kipumbavu.

Sasa najipanga namna yakuliweka wazi hili swala mbele ya baba na mama ilikusudi tusije Pata laana kizazi na kizazi mbele ya Mwenyezi Mungu
Huyo ndio anayejitambua, sio nyinyi mnaoabudu dini zilizoletwa na wageni kwenye majahazi, we huyo Mungu wa wazungu na waarabu ulishawahi kumwona?? mwacheni adumishe mila, big up kwake kaka huyo.
 
Ww ndio inawezekana ndio una ujinga mwingi kichwani,hizi dini tumeletewa na hawa waarabu na wamisionari matokeo yake tumekuja mila na desturi za mwafrika
 
Hallafu kingine sikuamini toka umezira kumalizia ile story yako nakuonaga magumashi tuu na nyuzi zako [emoji706]
 
Kwahiyo mababu zako walipoabudu mizimu ulipata laana?
Screenshot_20220606-100243.jpg
 
Samahani sikuweza kumpiga picha angeniona.

Kweli mnaweza mkawa Familia moja mkidhani ni watu wa dini lakini kuna mmoja yupo tofauti. Ni kaka etu wa kwanza kwenye Familia nimeshuhudia kwa macho yangu katika kipindi hiki nipo kijijini, nilipotoka kanisani ikabidi nichukue baiskel kwenda shambani lakini nilipofika shambani sikumkuta. Nikafikiri labda yupo ndani ya shamba ngoja nimuangalie.

Nilipoona mzigo nyuma umenilemea niliingia polini na kidumu cha maji kwenda kuushusha, lahaulaah!

Sikuamini macho yangu ni kaka angu kabisa anainama na kuinuka huku akisujudu mti. Nikaona sio kweli ikabidi nijifiche ila nilichokishuhudia nikajua kumbe ndomambo yake sisi jumapil kila tukienda kanisani yeye huwa anasema naenda shambani kumbe ana ibada zake za kipumbavu.

Sasa najipanga namna yakuliweka wazi hili swala mbele ya baba na mama ilikusudi tusije Pata laana kizazi na kizazi mbele ya Mwenyezi Mungu
Kumrekebisha mtu yeyote kwa kutumia imani asiyoiamini ni kazi bure.. Mfano, muislam kuja kunihubiria mimi Mkatoliki kuwa kula kitimoto ni dhambi unategemea tutaelewana kweli!?
 
Kumrekebisha mtu yeyote kwa kutumia imani asiyoiamini ni kazi bure.. Mfano, muislam kuja kunihubiria mimi Mkatoliki kuwa kula kitimoto ni dhambi unategemea tutaelewana kweli!?
Hapana huyu haabudu inaonekana ana mapepo inabidi apelekwe kwenye makanisa ya kilokole akaombewe hayo mapepo yaende kwenye nguruwe
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom